Kufanya au kupiga punyeto, ni tendo la kutomasa sehemu zako mwenyewe za siri ili kujisisimua kimapenzi.
Kwa hivyo katika kupiga punyeto hamna hofu ya kuambukizwa magonjwa yanayosambazwa kupitia ngono, kwani haimshirikishi mtu mwengine.
Punyeto ni toshelezo kamili la kimapenzi kama utatumia njia mbali mbali za kujitomosa na kujipa papasa ya kujistarehesha.
Hakuna mtu anayezaliwa akijua jinsi mwili wake unavyoitikia msisimko wa kimapenzi. Inakubidi kujifunza kwa majaribio salama.
Na, kwa vile kila mtu yuko tofauti, njia nyengine ya kujua jinsi unavyoweza kumstarehesha mpenzi wako, ni kujifunza kutoka kwako mwenyewe.
Shughulika zaidi na sehemu ambazo zinasisimka kwa urahisi.
Unaweza kufikia kilele cha starehe yako kwa kuitomasa tomasa **** au kisimi, lakini kutakupa hamu kubwa na ashiki, na kufikia kutoshelezwa vya kutosha, kama utapapasa pia sehemu nyenginezo za mwili wako.
KWA NINI PUNYETO HUONEKANA KUWA MAKOSA?
Msimamo wa dini nyingi na watu wengi ni kuwa punyeto ni dhambi, mwiko, jambo lililokatazwa, jambo lisilokubalika kabisa.
Lakini wanasanyansi wanasema ni jambo salama kiafya na dhana zilizopo kulihusu, ni imani za kibinafsi na chaguo la mtu.
Wanaume wengi na wanawake hupiga punyeto maishani mwao, kwa sababu huwafanya wakajisikia vizuri na huondoa dhiki za mihemko ya kimapenzi bila kujiingiza katika ngono na mtu mwengine.
Pia hofu ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa, ikiwemo virusi vya HIV ni kichocheo tosha kinachopelekea baadhi ya watu kupiga punyeto.
FAIDA ZA KUPIGA PUNYETO.
1)Kuujua mwili wako na kujiamini zaidi linapokuja swala la kungonoka(fanya mapenzi)
2)Kuongezeka kwa hamu ya kufanya mapenzi kwa vile utakuwa unajua utamu wake.
3)Kujua "vipele vyako viliko".
4)Kutokuusaulisha mwili wako ikiwa uko nje ya uhusiano au umeamua kuwa single kwa muda.
5)Kuepuka mimba na maambukizo ya virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine.
Hizi ni baadhi tu ya faida zipo faida nyingi.
Pamoja na faida hizo vivle tukiangalia upande mwingine wa shilingi tunayaona haya hapa chini.
MADHARA YA KUPIGA PUNYETO.
Ifahamike kuwa kuna watu wengi sana wanatumia mikono yao kujichua katika sehemu nyeti, Jambo hili linamadhara makubwa sana kwa binaadamu, Jambo hili kwa lugha ya kiingereza wanaliita Masturbution, ni kitendo cha mwanaume kujisugua tupu zake.
Wanaume wengi sana wanatumia mikono mikavu kujisaga, jambo hili huwafanya waharibu mishipa ya fahamu inayounganisha uume na mfumo uliopo kwenye ubongo. Uharibifu huu humfanya mwanaume apoteze msisimko wa kujamiiana au hata akiupata humfanya ashidwe kufikisha hisia zake kisawasawa khasa akikutana na mwenza wake ambaye sehemu zake nyeti ni laini sana tofauti na mikono alozoea kujichua nayo.
Jambo jingine hatari linalo mkabili mpiga Punyeto ni upotevu wa hisia wakati wa kujichua kwa mfano ili afike kwenye kilele lazima akuze hisia zake kwa kiwango cha juu, pengine kupita ukweli halisi ataokutana nao pindi atakapokuwa na mwanamke faraghani.
Mpiga Punyeto hajitoshelezi mpaka amlete kwenye hisia mrembo kama Miss World kisha amvike utundu wa kimahaba ampe manjonjo hadi mwenyewe atosheke, kwa namna hii mwanaume mwenye kufanya mazoea ya kufanya hisia za wanawake warembo ambao hawezi kuwapata kwa hali halisi anapokutana na kina Mwafulani wa mtaani tena sio mtundu kimapenzi, hapo kamwe hawezi kusisimka mwili na hivyo kujikuta Uume wake husimama kwa kiwango cha chini sana.
Madhara mengine yanayopatikana ndani ya kitendo hiki ni kuumwa sana na kichwa, mgongo, kupoteza nguvu za mwili na macho, madhara mengine makubwa khasa mwanamme anaejichua mara mbili au tatu kwa siku ni kushidwa kuzalisha, hii inatokana na kukosekana kwa mbegu komavu za kiume kwenye mfuko wa uzazi.
Hii yote madhara ya hapa duniani lakini kwa Mungu ni mwisho wa hisabu kwani ''Amelaaniwa mtumiaji mkono kwa kujisugua uume wake (Punyeto)
Kujichua kwa kutumia sanamu a.k.a Dildos kunaweza sababisha kusamburuka kwa nyama za nyeti zako(inategemea na aina ya sanamu), kupoteza hisia za uume halisi kutokana na kuzoea "dubwana" hizo, kifo kutokana na "shock" ikiwa unatumia ya umeme, vilevile saratani ikiwa unatumia vilainishio ili kurahisisha "dubwana a.k.a toy a.k.a Dildo" kuingia.
kujichua kupita kiasi kunaweza kusababisha kupoteza hisia uume halisi.
NAMNA YA KUACHA KUPIGA PUNYETO
Baada ya kuangalia madhara yanayosababishwa na kupiga punyeto nilipokea simu nyingi ambazo zilitaka pia niongelee suluhisho au jinsi gani mtu anaweza kuacha punyeto kabisa. Punyeto kama tulivyoongea ni tatizo la kitabia na linaweza kudhibitika kabisa kama matatizo mengine yeyote.
FANYA YAFUATAYO....
Acha kuangalia video za ponograph: video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.
Epuka kukaa nyumbani peke yako; mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine.
Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata hasa madogo madogo kama uchovu mkubwa, kuumwa kichwa na kusahau sana hii itakupa moyo wa kuendelea kutopiga punyeto.
Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema ivoivo, kama unaacha acha mara moja.
Tafuta mpenzi kama huna kabisa: ukiwa na mpenzi madhara ya punyeto kama kupungukiwa nguvu za kiume yatakufanya uache kabisa kwani ukiendelea utaaibika siku moja pale uume utakaposhindwa kusimama kabisa mkiwa faragha chumbani na pia utapata nafasi ya kushiriki tendo la ndoa hivyo kuacha kabisa punyeto. pia unaweza kumshirkisha mwenzi wako tatizo lako ili akusaidie kuacha.
Anza mazoezi na jishughulishe na mambo mengine:hii itakufanya ue bize na mambo mengine na utumie mda wako mwingi huko, pia mazoezi ya jioni yatakufanya uchoke na kushindwa kufikiria kupiga punyeto wakati wa kwenda kulala
Uzoefu unaonyesha, mtu anayepiga punyeto, hata kama ameathiriwa na tatizo la punyeto kwa kiwango gani, endapo atafanikiwa kutopiga punyeto kwa muda wa siku arobaini mfululizo, mtu huyo hatopiga tena punyeto katika siku zote za maisha yake kwani tayari mtu huyo atakuwa amerudia katika hali yake ya kuto kuwa addicted tena na upigaji punyeto, na atalichukia kabisa hata jina la tendo hilo achilia mbali tendo lenyewe.
MAELEZO ZAIDI........
Pia ileleweke kuwa Sio rahisi kwa mtu aliyekuwa addicted na punyeto kustahimili kujizuia kupiga punyeto kwa muda wa siku arobaini mfululizo. Anaweza kujizuia kupiga punyeto kwa siku mbili lakini baada ya hapo ataendelea tena na mchezo wako.
JARIBU PIA DAWA HII....
PILIPILI
Pilipili inayo hitajika hapa ni yoyote ile ili mradi iwe kali sana, ( Ila inayopendekezwa ni pilipili mbuzi ama pilipili kichaa, pilipili hoho haihusiki hapa ).
MATUMIZI
Kwanza kabla ya kujua matumizi ni vyema ukatambua muda ambao huwa unapiga punyeto (Mara nyingi huwa ni asubuhi baada ya kuamka,wakati wa kuoga ama usiku kabla ya kulala ).
Chukua pilipili zako, zipasulie kwenye viganja vya vidole vyako na kujipakaza katika viganja vya vidole vyako. Unaweza kutumia pilipili moja kwa kila kiganja, na kwa kila muda ambao huwa unapiga punyeto lakini unaruhusiwa kujipakaza zaidi ya pilipili moja.
Ukishajipaka pilipili kwenye viganja vya vidole vyako, moja kwa moja unakuwa umekwisha jilazimisha kutokufanya punyeto, kwa sababu ukipiga punyeto kwa viganja ambavyo vina pilipili utawashwa sana wala hautaweza kufurahia tendo hilo.
JAMBO LA KUZINGATIA : Hakikisha unakuwa na walau pilipili mbili mpaka nne kila unapokuwa katika maeneo ambayo yanaweza kukuchochea kufanya punyeto.
UFANISI WA DAWA HII : Dawa hii inawafaa wale tu ambao wamedhamiria kutoka mioyoni mwao kuacha kufanya punyeto. Kwa wale ambao hawajadhamiria haitaweza kuwasaidia.