butron
JF-Expert Member
- Jun 3, 2013
- 5,640
- 7,943
Haikufaa Tanzanite kutuinua kiuchumi,itakuwa gesi?Ni wapi Duniani Tanzanite inapatikana zaidi ya Tanzania?Leo hii Tanzania tungekuwa tunauza gesi yetu Ulaya kwa bei ya juuu baada ya Urusi kususiwa.[emoji24][emoji24]
Tazama hiyo ni nchi ya Qatar
Kabla ya kugundua gesi mwaka 2002 uchumi wao ulikuwa dola bilioni 19 tu, baada ya kugundua gesi uchumi wao leo ni dola bilioni 220.
View attachment 2465599
Hii imeniuma sana kwa kuwa Magufuli alitupa kwenye pipa la taka mradi wetu wa gesi.
Akadanganya kuwa gesi yetu imetwaliwa na mabeberu, sasa kama ilitwaliwa aliwezaje kuisimamisha?
Na kama alikuwa Waziri mwandamizi kwenye serikali ya Kikwete kwa nini hakulisema hilo au hata kujiuzulu kuokoa gesi isiende kwa mabeberu?
Samia anawezaje ku negotiate mkataba ya gesi na nchi nyingine hivi sasa?
Kama haitoshi tuna Ng'ombe kibao lakini tunaagiza jozi za viatu kwa wasio na Ng'ombe!
"Haikufaa rangi,itafaa chokaa Mkuu"
Mwacheni Jiwe apumzike jamani,tumechoka na propaganda uchwara dhidi yake!