Radi iliyopiga juzi Dar imeacha hasara ya kutosha

Radi iliyopiga juzi Dar imeacha hasara ya kutosha

pole ila huo ndio mwanzo tu itaungua hadi nyumba kwa ubahili wa kuweka vitu vya bei nafuu
Mkuu hapo kitu gani ni cha bei nafuu kilichopelekea TV kuungua baada ya radi kupiga. Maana kwenye wiring sikufanya ya kuungaunga ila bado radi imefanya yake
 
Udongo

Umesema Udongo ni kipitishi kizuri cha umeme. Ukitumia tofali za kuchoma kama nyaya za umeme,taa itawaka?

Mfano ukaunganisha betri mbili na tofali moja la kuchoma kisha glopu ukakamilisha circuit,glopu itawaka? Circuit yenye glopu,waya,betri mbili. Ukaamua ufanye tofali kama betri la tatu. Umeme utapita na glopu kuwaka?
Kuna mtu anatumia sign ya COMMON SENSE IS NOT COMMON, we ukiangalia udongo na tofali la kuchoma vinafanana?
 
Mkuu hapo kitu gani ni cha bei nafuu kilichopelekea TV kuungua baada ya radi kupiga. Maana kwenye wiring sikufanya ya kuungaunga ila bado radi imefanya yake
Hiyo TV guard yako ni bei nafuu, kawaida haitakiwi kuwaka kwa sekunde 90 baada ya umeme kurudi kama ulizima , we unasema umeme haukuwa low voltage kwa hiyo ikaunguza TV. lakini OG bila kujali umeme ni low au High inatakiwa kusubiri mda huo ndio iruhusu umeme kupta.
 
Juzi jumamosi mida ya asubuhi mvua ilinyesha Dar na around saa tatu hivi ikapiga radi moja kubwa sana kwa wanaokaa pande za goba, mbezi,tegeta A, Msumi, Makabe etc. wataelewa ninachosema.

Radi ambayo ilipelekea umeme kukatika kwa dakika chache tu ila tayari ilikua imeshafanya uharibifu kwenye vifaa vya umeme nikiwemo mimi na majirani kadhaa tuliounguliwa TV. Binafsi natumiaga fridge guard kwenye TV lakini ngoma haikusaidia sababu haikua low voltage.

Nimekaa Dar muda sijakutana na hali hii maana ilikua ni radi ya level ya zile konki za kanda ya kigoma, katavi na Rukwa.

Nimetoka dukani kwa mangi mitaa ya huku nimekuta jamaa wengine nao wanaongelea kuunguliwa TV sababu ya ile radi. Kuna muhanga mwingine humu?
True,
Siku za nyuma pia nilishuhudia radi mpka nikakumbuka BUKOBA

KULE RADI ZINAPIGA MCHANA JUA LINAWAKA
 
Best earth rod nunua copper wire 6mm, uvue gamba suka yako kwa size ya kutosha, hii unakuwa na uhakika maana za kununua unaweza pewa feki kwa bei ya og
 
Mkuu hapo kitu gani ni cha bei nafuu kilichopelekea TV kuungua baada ya radi kupiga. Maana kwenye wiring sikufanya ya kuungaunga ila bado radi imefanya yake
huwez ukawa na vifaa og alafu radi izingue
 
Hiyo TV guard yako ni bei nafuu, kawaida haitakiwi kuwaka kwa sekunde 90 baada ya umeme kurudi kama ulizima , we unasema umeme haukuwa low voltage kwa hiyo ikaunguza TV. lakini OG bila kujali umeme ni low au High inatakiwa kusubiri mda huo ndio iruhusu umeme kupta.
Mkuu fridge guard na power stabilizer huwa zinalinda kifaa dhidi ya low voltage, sio high voltage. Ndio maana umeme ukipungua itasubiri hadi urudi sawa ndio inaruhusu umeme upite. Ikiwa high voltage haizuii na hapo kifaa kinaweza ungua kama ilivyotokea radi. Unless kuna guard na stabilizer mpya za majuzi zinazolinda dhidi ya high voltage, sanasana socket breaker ndio inasaidia kwenye high voltage kwa kujizima
 
Kuna mtu anatumia sign ya COMMON SENSE IS NOT COMMON, we ukiangalia udongo na tofali la kuchoma vinafanana?
Kwahiyo tofali la kuchoma sio kipitishi kizuri cha umeme ila udongo ni kipitishi kizuri cha umeme?
 
Mkuu fridge guard na power stabilizer huwa zinalinda kifaa dhidi ya low voltage, sio high voltage. Ndio maana umeme ukipungua itasubiri hadi urudi sawa ndio inaruhusu umeme upite. Ikiwa high voltage haizuii na hapo kifaa kinaweza ungua kama ilivyotokea radi. Unless kuna guard na stabilizer mpya za majuzi zinazolinda dhidi ya high voltage
Ndio maana nikakwambia hicho ndio kimekuponza, mie nimenunua fridge guard hata umeme ukiwa level ukiwasha unasubiri 90 seconds ndio ina kick in. Kawaida ya fridge haitaki mshituko wa umeme maana inatumia moja kwa moja ndio maana guard yake inatakiwa iwe na delay ikitokea umeme umecheza isiwake moja kwa moja. Unatumia fridge guard ya mchongo.
 
Juzi jumamosi mida ya asubuhi mvua ilinyesha Dar na around saa tatu hivi ikapiga radi moja kubwa sana kwa wanaokaa pande za goba, mbezi,tegeta A, Msumi, Makabe etc. wataelewa ninachosema.

Radi ambayo ilipelekea umeme kukatika kwa dakika chache tu ila tayari ilikua imeshafanya uharibifu kwenye vifaa vya umeme nikiwemo mimi na majirani kadhaa tuliounguliwa TV. Binafsi natumiaga fridge guard kwenye TV lakini ngoma haikusaidia sababu haikua low voltage.

Nimekaa Dar muda sijakutana na hali hii maana ilikua ni radi ya level ya zile konki za kanda ya kigoma, katavi na Rukwa.

Nimetoka dukani kwa mangi mitaa ya huku nimekuta jamaa wengine nao wanaongelea kuunguliwa TV sababu ya ile radi. Kuna muhanga mwingine humu?
Goba imeshakuwa kama marangu tu, ukitembea hatua Tano unakutana na Manka
 
Sasa kwanini huo umeme unaozidi wakati wa radi, Tanesco wasiwe wanaucollect na kuutunza ukatumika kipindi cha mgao, kuliko kupotea ardhini.??
umeme wa radi hauwezi kuvunwa mkuu na hakuna mtaalamu anayeweza pima megawatts zake
 
Mkuu fridge guard na power stabilizer huwa zinalinda kifaa dhidi ya low voltage, sio high voltage. Ndio maana umeme ukipungua itasubiri hadi urudi sawa ndio inaruhusu umeme upite. Ikiwa high voltage haizuii na hapo kifaa kinaweza ungua kama ilivyotokea radi. Unless kuna guard na stabilizer mpya za majuzi zinazolinda dhidi ya high voltage
Siku nyingine zingatia factor muhimu ndio maana hatutumii stabilizer kwenye fridge ikawepo fridge guard. Pia uelewe tofauti stabilizer umeme ukiwa chini inauboost uendelee kutumia, kuna buck-boost conveter ndani yake umeme hata ukizidi inaurudisha level.
 

Attachments

  • fg.png
    fg.png
    20.4 KB · Views: 4
Mkuu fridge guard na power stabilizer huwa zinalinda kifaa dhidi ya low voltage, sio high voltage. Ndio maana umeme ukipungua itasubiri hadi urudi sawa ndio inaruhusu umeme upite. Ikiwa high voltage haizuii na hapo kifaa kinaweza ungua kama ilivyotokea radi. Unless kuna guard na stabilizer mpya za majuzi zinazolinda dhidi ya high voltage

Kwahiyo tofali la kuchoma sio kipitishi kizuri cha umeme ila udongo ni kipitishi kizuri cha umeme?
inachofanya udongo uruhusu umeme kupita n ule umaji maji ndani yake ukiwa mkavu umeme haupiti
 
Siku nyingine zingatia factor muhimu ndio maana hatutumii stabilizer kwenye fridge ikawepo fridge guard. Pia uelewe tofauti stabilizer umeme ukiwa chini inauboost uendelee kutumia, kuna buck-boost conveter ndani yake umeme hata ukizidi inaurudisha level.
Ndicho nilichokuambia kuwa hizi fridge guard zinalinda vifaa dhidi ya umeme wa low voltage ambao unaunguzaga sana vitu pia, ila hazilindi dhidi ya high voltage, unless kuna za kisasa zaidi zimetoka majuzi
 
Mkuu toa ushauri Earthrod ipi inashauriwa kwa mziki wa radi za Rukwa maana nipo kwenye ujenzi eneo ambalo radi kwakweli ndio kama nyumbani kwake.
Huko radi nyingi ni za kiutamaduni, mnatengeneza radi zenu wenyewe.
 
Kifaa kinacholinda mfumo wako wa umeme dhidi ya Radi ni aina hizi mbili za circuit breaker
1. Residual Current Circuit Breaker (RCCB)
2. Residual Current Device (RCD)
Radi (lightning) inapopiga circuit breaker hizi hu trip (huzima mfumo wote wa umeme), hivi ndio inavyolinda sakiti yako.
Note; binafsi naikubali RCCB kampuni ya EUROTRIX.

Kazi ya earthing system ni;

1. Kumlinda mtu asipigwe na shock ya umeme.
Mfano. Waya wenye umeme (live wire) unapogusa bati la friji, maana ake mtu akigusa lile bati la friji atapigwa na shock ya umeme, badala yake sasa endapo mfumo wako ukiwa na earthing basi umeme wote uliovuja kwenye bati la friji hupelekwa chini ya ardhi, hivyo basi hata mtu akigusa lile bati hatapigwa na shock ya umeme kwa maana umeme tayari unaelekea chini.

2. Kulinda kifaa kisiungue dhidi ya umeme unaovuja.
Mfano. Kama umeme utavuja, yaani waya ukagusa bati la friji kama hujafanya earthing kwenye sakiti yako basi kuna uwezekano wa friji lako kuungua endapo waya mwingine wenye potential tofauti ukagusa bati hilo la friji, endapo utafanya earthing basi umeme wote hupelekwa chini na friji lako litabaki salama.

Note; Earthing system hailindi kifaa dhidi ya Radi (lightning)
Uko sawa lakin kama earthing system haiko vizur hiyo circut breaker itachelewa kusensi kwa haraka hence unaunguza vitu kwahiyo huwa vinategemeana earthing system na circuit breaker
 
Juzi jumamosi mida ya asubuhi mvua ilinyesha Dar na around saa tatu hivi ikapiga radi moja kubwa sana kwa wanaokaa pande za goba, mbezi,tegeta A, Msumi, Makabe etc. wataelewa ninachosema.

Radi ambayo ilipelekea umeme kukatika kwa dakika chache tu ila tayari ilikua imeshafanya uharibifu kwenye vifaa vya umeme nikiwemo mimi na majirani kadhaa tuliounguliwa TV. Binafsi natumiaga fridge guard kwenye TV lakini ngoma haikusaidia sababu haikua low voltage.

Nimekaa Dar muda sijakutana na hali hii maana ilikua ni radi ya level ya zile konki za kanda ya kigoma, katavi na Rukwa.

Nimetoka dukani kwa mangi mitaa ya huku nimekuta jamaa wengine nao wanaongelea kuunguliwa TV sababu ya ile radi. Kuna muhanga mwingine humu?
radi inapiga thena umeme unaunguza vyombo? Maana yake Radi iliongeza voltage za umeme?
 
Back
Top Bottom