Rafiki yangu kanipa kesi, kisa nimemsaidia mtoto wake mwenyewe

Rafiki yangu kanipa kesi, kisa nimemsaidia mtoto wake mwenyewe

Na hapa kuna sheria zinazofanana na nyumban mkuu. Lakini hapa tulipo mtu kukutumia watu waje kuchukua roho yako ni sekunde tu.

So hii inanifanya nikubaliane na ushauri wa rafiki yetu kutukutanisha na kuliongelea swala hilo mbele yake. Maybe he will do something better to his son.
Dah umetangaza vita na huyo mkongo walivyo wachawi sasa, huyo mtoto anateseka sana
 
Ningekuwa mimi ningepiga ngumi kali sana huyo jamaa tena ningempasua ili aende polisi alafu tukifika polisi ndo kila kitu kitajulikana hapo ningeelezea sababu ya mimi kufanya hivyo ni kwa maslahi ya mtoto ningeomba watuhumiwa tuwe wawili mm na mke wa jamaa kama vp aitwe mtoto atoe ushahidi kama vp haujachelewa subiri siku huyo mama wa kambo anamtesa mwambie wife wako arekodi video kwa siri alafu we nenda kakate ufunue huyo mama lazima akimbilie polisi huko unakwenda kumwaga ushahidi hata kama utakaa ndani usijari haizidi masaa 24 mkeo aende polisi awape ela ya blashi na awaonyeshe ushahidi utakuwa umemsaidia sana huyo dogo vinginevyo dogo ataendelea kutubu kwa huyo mama wa kambo.
 
Wewe nae mjinga, kuongea na mshikaji wako kuhusu hali ya mtoto wake huwezi, ila kumnunulia nguo mtoto wake na kupeleka umeweza, la kwanza ni rahisi kuliko la pili.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Jirani na hapa nnapoishi mimi kuna home boy fulani ambae tumetokea kuzoeana, kushauriana na hata sometimes kutembeleana. Tulitokea kujuana nae miezi 6 iliyopita baada ya yeye na familia yake kuhamia hapa. Kwa Tanzania ni mzaliwa wa Kinondoni, wakati mimi mzaliwa wa Magomeni Dar es salaam, hivyo tunaishi kama ndugu.

Kabla ya kuishi na mke alie nae sasa hivi, alikuwa ashaoa mke wake wa kwanza ambae alizaa nae mtoto mmoja wa kiume. Lakini kwa bahati mbaya mkewe alifariki miaka 3 iliyopita na kuacha mtoto huyo akiwa na umri wa miaka 4.

Baada ya mkewe kufariki, mwamba hakuchelewa, akakutana na huyu mkongo, akatangaza ndoa na kuanza maisha mapya (kumbuka hapo jamaa alikuwa na mtoto wa miaka 4), baadae na mkongo akamletea mtoto mungine wa kike, so jumla jamaa ana watoto wawili. Maisha yao huko walipokuwa haswa kwa upande wa mtoto wa kambo sijui yalikuaje, ila baada ya kuhamia jirani yetu na kufahamiana na jamaa, ndo nikaanza kuona mateso anayopitia mtoto.

Japo imezoeleka kuona mama wa kambo wengi ni makatili, lakini huyu aisee ni zaidi ya shetani. Hana chembe ya huruma, utu wala ubinadam. Anaweza kumpa mtoto adhabu ya kuweka miguu juu (ukutani) mikono chini (mfano wa sarakasi) kwa muda mrefu zaidi, bila kushusha miguu chini, na akishusha anakula kipondo ambacho anatakiwa kupigwa mwizi huko polisi.

Yote tisa, kumi ni pale anapomshindisha na njaa, alafu akigundua kuwa alikuja kwangu na wenzake (watoto wangu) akala, basi atachokutana nacho atajuta ni kwanini alimpoteza mama yake akiwa bado mdogo. Atapigwa, atapewa adhabu ya kuweka miguu juu, na kushindishwa na njaa.

Kila nlipotaka kumwambia jamaa kuhusu mateso anayopitia mwanae, moyo ulisita, nisije kuharibu ndoa ya watu au kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto mwenyewe. So niliamua kushona mdomo wangu tu kama sijui kinachoendelea.

Huyu mama mwanzoni alianza kuwa karibu na mke wangu, kutokana na ukaribu uliopo mimi na mumewe. Lakini alipogundua kwamba mke wangu huwa na tabia ya kumpa chakula mtoto anaeteswa, na sometimes kumpa hela pamoja na watoto wangu ili wanunue vitu vidogo vidogo vya kula, basi yule mama wa kambo akakata mawasiliano na mke wangu, na madam nae akampotezea kwa kufuata ule msema wa "akunyimae kunde, anakupunguzia kuja...m..ba.

Mtoto bado mdogo (miaka 7) kumweleza baba yake anashindwa, na mama huwa hampi nafasi ya kumsogelea baba yake akae nae mwenyewe. Halaf mtoto nguo, na viatu vimemuishia mpaka aibu naona mimi.

Juzi alhamisi nikaona upuuzi, wakati natoka mihangaikoni kwangu nikaingia dukani nikanunua nguo suruali 5, T'shirt 5, mashati mawili, jacket za baridi 3, viatu pea 3 na sandroz pea 1. Nikaenda mpaka kwa home boy nikamkabidhi mkewe nikamwambia kuwa zile nguo na viatu nilikuwa nimemnunulia mwanangu, lakin kwa bahati mbaya nimekuta havimtoshi, so ndomaana nikaona nimpe yeye ambae vinaonekana kumtosha, alaf mimi nitaenda na mtoto wangu town nikamnunulie vingine. Yule mama akapokea, lkn ni kwa shingo upande (kumbuka ni shemej yangu) halaf sina ugomvi nae yeye wala mumewe. So hakuwa na nguvu ya kukataa uso kwa uso.

Kumbe na yeye jana alienda town, akanunua nguo zake kadhaa, na kuja nazo nyumban kwa malengo yake binafsi. Usiku mumewe alipofika akaanza kumwambia kuwa mimi nimekuwa nikimtongoza na kumtaka kimapenzi muda mrefu bila mafanikio, na kwamba nilifikia hadi hatua ya kumnunulia yeye na mtoto (wa kambo) nguo ili anikubali, lakini bado alinikwepa na kuchukua tu nguo ili aje amuonesha (mumewe) nk.

Home boy alipotaka ushahidi yule mama akaenda kutoa zile nguo alizoenda kununua jana town, akajumlisha na zile nilizopeleka kwa ajili ya kumpa mtoto wa kambo anaeteseka. Aisee sijui jamaa alikuwa katika hali gani usiku ule na sijui alilalaje.

Asubuhi naona home boy anakuja nyumban bila salam anaanza kunibwatukia mbele ya mke wangu na watoto wangu. Namuuliza tatizo nini, anabwaga zile nguo mbele yangu na kusema eti ashajua kila kitu kuhusu mpango wangu wa kumtongoza mkewe.

Eti natongoza kishamba sana kwa kukimbilia kuhonga nguo. Yani nikashindwa kumuelewa vizuri, mpaka alipofafanua kwamba nilikuwa namtongoza mkewe, nilipoona hakubaliani na mimi ndo nikaenda town kununua vijinguo vya kumlaghai ili nimpate kiurahisi nk.

Nikataka kutumia ukaribu wetu kumueleza kile kinachoendelea katika familia yake mpaka mimi kufikia hatua ya kununua zile nguo za mtoto wake, lakini bingwa hakunielewa, akawa mtata mwisho nikamuacha aongee akichoka aamue mwenyewe anachotaka kufanya.

Baada ya kuona lengo lake la kunichafua mbele ya familia yangu limefeli akaondoka akidai kuanzia leo mimi na yeye ni maadui. Nisimjue, asinijue, nisiende kwake, na hatokuja kwangu, kila mtu aangalie maisha yake, nikamwambia poa.

Kwa bahati nzuri mke wangu anajua kila kinachoendelea, so ile complain ya kumtongoza mkewe haikumuingia akilini.

Namuonea huruma sana home boy, ni kama mapenzi yamemfanya asifatilie kinachoendelea katika nyumba yake. Damu yake inateswa, na sisi tunaosaidia tunaonekana wabaya. Mateso anayopitia yule mtoto hakuna mtu yoyote mwenye huruma hapa JF anaweza kuyaona akayavumilia.

Nilikuwa na mpango wa kwenda ku report swala hili katika mamlaka husika, lakini kuna rafiki yetu (mimi na yeye) amesema nisubiri kwanza jamaa hasira ziishe hata week 1 au 2, halafu aite kikao kati yangu na home boy kwa ajili ya maridhiano, halaf hapo kwenye kikao ndo nitumie chance hiyo kumueleza home boy kile kinachoendelea katika familia yake, na sababu ya mimi kumpelekea yule mtoto zile nguo na viatu.

Huyu rafiki mimi nimemuelewa, lkn sielewi ni vipi mpaka leo jamaa haoni kuwa mtoto wake anateseka hata kwa muonekano tu wa macho. Ama kweli tenda wema uende zako. Na sio kila mwenye macho huona kilichopo mbele yake. Jamaa haoni na hasikii.

Dah...
Pole sana pia pole kwa huyo mtoto.
Hili la mtoto linanikumbusha maumivu sijui kwanini mpaka saivi namkumbuka yule mtoto.
Kwa kifupi yule mtoto alikufa kutokana na mateso ya mama yake mzazi.
Huyo mama alikuja kuolewa na mzee mmoja mtaani kwetu akiwa na mtoto huyo. Ila alipo zaa mtoto mwingine na mume wake mpya akaanza kumyima chakula na kumpiga sana mtoto kwa kukadilia mtoto alikuwa na miaka kama minne au mitano.
Wana Mtaa walivyo jua hivyo wakaanza kumpa chakula ila mama yake akaanza kuwatukana na kuanza kumfungia mtoto ndani, baada ya mtoto kutokuonekana kwa muda wakamuuliza akasema wamempeleka kwa baba yake lakini haikuwa hivyo.
Mwisho woto wa lika lake wakamuona na kutoa taarifa ndipo wana Mtaa wakaenda kumtoa mtoto kwa nguvu kupitia mwenyekiti wa mtaa ila walikuwa wemechelewa mtoto alikuwa tayari kadhoofika.
mtoto baada ya miezi kazaa akaaga Dunia, sijui kilicho endelea kisheria maana nilikuwa nina kama miaka kumi wakati ule ila baba wa kambo na mama aliendelea kudunda mtaani.
 
Popote alipo, Gwajima ni mfano tu wa authority areport tu kwa child protection services huyo mtoto ana haki ya kuwa mtoto na kukua kwa wazazi wake km watoto wengine na kama Hawako responsible wapo wanaoweza
Ni kweli mkuu, sheria za hapa kama mzazi ameshindwa kumlea mtoto wake basi amkabidhi kwa mamlaka wamsaidie kulea. Lakini sasa sina uhakika kama baba mtoto anajua kinachoendelea kwa mtoto wake.

Nangoja jamaa akitukutanisha nae nimwambie kila kitu kinachoendelea kwa mwanae. Halaf akishupaza shingo, ndo niangalie njia nyingine za kisheria za ku deal nae.
 
Pole sana pia pole kwa huyo mtoto.
Hili la mtoto linanikumbusha maumivu sijui kwanini mpaka saivi namkumbuka yule mtoto.
Kwa kifupi yule mtoto alikufa kutokana na mateso ya mama yake mzazi.
Huyo mama alikuja kuolewa na mzee mmoja mtaani kwetu akiwa na mtoto huyo. Ila alipo zaa mtoto mwingine na mume wake mpya akaanza kumyima chakula na kumpiga sana mtoto kwa kukadilia mtoto alikuwa na miaka kama minne au mitano.
Wana Mtaa walivyo jua hivyo wakaanza kumpa chakula ila mama yake akaanza kuwatukana na kuanza kumfungia mtoto ndani, baada ya mtoto kutokuonekana kwa muda wakamuuliza akasema wamempeleka kwa baba yake lakini haikuwa hivyo.
Mwisho woto wa lika lake wakamuona na kutoa taarifa ndipo wana Mtaa wakaenda kumtoa mtoto kwa nguvu kupitia mwenyekiti wa mtaa ila walikuwa wemechelewa mtoto alikuwa tayari kadhoofika.
mtoto baada ya miezi kazaa akaaga Dunia, sijui kilicho endelea kisheria maana nilikuwa nina kama miaka kumi wakati ule ila baba wa kambo na mama aliendelea kudunda mtaani.
Dah aisee inaumiza sana kuona binadam mwenzako, tena malaika asiejua chochote akiteswa na mtu ambae ana dhamana ya kumlea na kumtunza. Huu unyama sijui utaisha lini. Halaf upo kila mahali.
 
In fact baba wa mtoto anajua kabisa kinachoendelea, utafanya nae kikao atakujibu majibu ya shombo utapata hasira na unaweza kumiss opportunity ya kumsaidia huyo mtoto! Hakafu kumchukua mtoto video clip wkt anaadhibiwa ni unethical na illegal! Tena kupost ndio balaa zaidi! Usijipe kazi isiyokuhusu wape wahusika kazi yao, tenda wema uende zako
Shukran sana mkuu kwa ushauri wako 🙏
 
Aisee, pole sana. Ni kawaida kuwa hata wema una gharama zake (maumivu)
Zingatia ushauri wa mtu wa 3 (rafiki yenu), naamini Mungu atamfungua macho na atajua ukweli. Sasa hapo aibu kwake; sijui atakuombaje msamaha!
Nahisi atajiona mjinga, na mpumbavu sana kwa kunitusi mtu ambae napigania uhai wa mtoto wake. Ilitakiwa aje aniulize kiume ili kuujua ukweli kabla ya kukimbilia kuropoka mbele ya watu.
 
Dah aisee inaumiza sana kuona binadam mwenzako, tena malaika asiejua chochote akiteswa na mtu ambae ana dhamana ya kumlea na kumtunza. Huu unyama sijui utaisha lini. Halaf upo kila mahali.
Ingekuwa saivi ninge-report kwenye vyombo husika na mtoto ningemsaidia kulingana na mahitaji yake.
Ila mpaka saivi sijajua yule mama alikumbwa na nini mpaka amfanyie mtoto wake wa kuzaa unyama ule.
Mungu awarehemu wote maana wametangulia mbele za haki.
 
Nahisi atajiona mjinga, na mpumbavu sana kwa kunitusi mtu ambae napigania uhai wa mtoto wake. Ilitakiwa aje aniulize kiume ili kuujua ukweli kabla ya kukimbilia kuropoka mbele ya watu.
Hawezi kujiona mjinga ,maana hajui na kashapigwa rimbwata,haelewi chochote.Dawa aburuzwe ustawi wa jamii tu
 
Ulichokosea ni kuzunguka sana kumjulisha mwamba juu ya hali ya mtoto wake, au basi tumia mamlaka za kiserikali waambie wasikutaje tu.

Una lengo zuri lakini unashindwa lifanyia kazi sawa sawa, fikiria kama jamaa angekuwa na silaha ya moto si angekuja kumiminia risasi za kutosha ufe kijinga Mkuu.?

Kuna mambo bora uka nyooka kiongozi usipite kona kona sio nzuri izo
Ni kweli hapo ndo nilipokosea, ila nilihisi kama ningemwambia labda jamaa asingenielewa na pengine angemuuliza mkewe na kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto. So nikaona mimi kama mzazi ambae nina watoto kama huyu nifanye kile ninachoona kinafaa kimya kimya.

Kwa bahati mbaya ndo hivyo nimejiletea janga kubwa kwa jamaa.
 
Mama wa kambo wengi wana roho ya chuma. Why umtese mtoto wenzio. Next time unamchoma ustawi wa jamii wa deal naye perpendicularly.
Mtu anashindwa kufikiria kwamba anapotesa watoto wa mwenzake, na yeye kesho akifa pia wa kwake watateswa. Sijui wanakuaga na akili na moyo gani hawa viumbe.
 
Fanya hivyo mkuu...ripoti haraka ustawi wa jamii huyo mama sio
Huyu ni mshenzi na muuaji. Halaf huenda ni lichawi na lishirikina, cause haiwezekani mpaka leo mshikaji hajashtuka tu kama mwanae anateswa. Inafikirisha.
 
Back
Top Bottom