Rafiki yangu kanipa kesi, kisa nimemsaidia mtoto wake mwenyewe

Rafiki yangu kanipa kesi, kisa nimemsaidia mtoto wake mwenyewe

Ningekuwa mimi ningepiga ngumi kali sana huyo jamaa tena ningempasua ili aende polisi alafu tukifika polisi ndo kila kitu kitajulikana hapo ningeelezea sababu ya mimi kufanya hivyo ni kwa maslahi ya mtoto ningeomba watuhumiwa tuwe wawili mm na mke wa jamaa kama vp aitwe mtoto atoe ushahidi kama vp haujachelewa subiri siku huyo mama wa kambo anamtesa mwambie wife wako arekodi video kwa siri alafu we nenda kakate ufunue huyo mama lazima akimbilie polisi huko unakwenda kumwaga ushahidi hata kama utakaa ndani usijari haizidi masaa 24 mkeo aende polisi awape ela ya blashi na awaonyeshe ushahidi utakuwa umemsaidia sana huyo dogo vinginevyo dogo ataendelea kutubu kwa huyo mama wa kambo.
Nimecheka sana 🤣🤣🤣
 
Ingekuwa saivi ninge-report kwenye vyombo husika na mtoto ningemsaidia kulingana na mahitaji yake.
Ila mpaka saivi sijajua yule mama alikumbwa na nini mpaka amfanyie mtoto wake wa kuzaa unyama ule.
Mungu awarehemu wote maana wametangulia mbele za haki.
Basi kama na yeye ametangulia huenda wamekutana na sasa ana kesi ya kuijibu roho ya huyo mtoto kwa kuisababisha itoke kabla ya wakati wake.

Mungu mjuzi wa yote atamhukumu kila mtu sawa na uzito wa kosa lake. Ila huyo mama alizingua, labda alihisi akimchukua mwanae ndo atapendwa zaidi na mumewe.
 
Ningekuwa mimi ningepiga ngumi kali sana huyo jamaa tena ningempasua ili aende polisi alafu tukifika polisi ndo kila kitu kitajulikana hapo ningeelezea sababu ya mimi kufanya hivyo ni kwa maslahi ya mtoto ningeomba watuhumiwa tuwe wawili mm na mke wa jamaa kama vp aitwe mtoto atoe ushahidi kama vp haujachelewa subiri siku huyo mama wa kambo anamtesa mwambie wife wako arekodi video kwa siri alafu we nenda kakate ufunue huyo mama lazima akimbilie polisi huko unakwenda kumwaga ushahidi hata kama utakaa ndani usijari haizidi masaa 24 mkeo aende polisi awape ela ya blashi na awaonyeshe ushahidi utakuwa umemsaidia sana huyo dogo vinginevyo dogo ataendelea kutubu kwa huyo mama wa kambo.
Mtoto akikukana utafanyaje? Kuna matukio mtoto katestify uongo kwa maelekezo ya wazazi mhusika anajikuta kwenye aibu. Anadanganywa na vi icecream na vipipi unashangaa mtoto anakuwa upande wa wazazi wake unaingia aibu.

Mshkaji alitakiwa awasiliane na baba mtoto ambae ni rafiki yake na amueleze kuwa kuna mzigo atampa shemeji.

Sasa ananunua zawadi, anampelekea mke wa rafiki yake huku rafiki yake hana habari ilihali anajua kabisa mkewe ana roho mbaya.

Na wanawake walivyosmart akijua bado mnamfatilia na akataka kuharibu zaidi hii miezi kadhaa mtoto anaweza pendwa kinafiki, siku mnamuita huyo rafiki yenu anawaona wote mnamtamani mkewe.
 
Uchawi upo lkn sikuona njia nyingine ya kumsaidia huyu mtoto zaidi ya hii niliyofanya mkuu au wewe unaonaje?
Hukujipanga vizuri, huyo ungempangia mkakati na kumdhibiti asingekuwa na hiyo jeuri kabisa ya kuleta uchonganishi, hapo ndo utaona kwanini inasisitizwa akili katika kuishi na mwanamke, sasa umejiongezea mlima wa kutatua huo mgogoro
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Jirani na hapa nnapoishi mimi kuna home boy fulani ambae tumetokea kuzoeana, kushauriana na hata sometimes kutembeleana. Tulitokea kujuana nae miezi 6 iliyopita baada ya yeye na familia yake kuhamia hapa. Kwa Tanzania ni mzaliwa wa Kinondoni, wakati mimi mzaliwa wa Magomeni Dar es salaam, hivyo tunaishi kama ndugu.

Kabla ya kuishi na mke alie nae sasa hivi, alikuwa ashaoa mke wake wa kwanza ambae alizaa nae mtoto mmoja wa kiume. Lakini kwa bahati mbaya mkewe alifariki miaka 3 iliyopita na kuacha mtoto huyo akiwa na umri wa miaka 4.

Baada ya mkewe kufariki, mwamba hakuchelewa, akakutana na huyu mkongo, akatangaza ndoa na kuanza maisha mapya (kumbuka hapo jamaa alikuwa na mtoto wa miaka 4), baadae na mkongo akamletea mtoto mungine wa kike, so jumla jamaa ana watoto wawili. Maisha yao huko walipokuwa haswa kwa upande wa mtoto wa kambo sijui yalikuaje, ila baada ya kuhamia jirani yetu na kufahamiana na jamaa, ndo nikaanza kuona mateso anayopitia mtoto.

Japo imezoeleka kuona mama wa kambo wengi ni makatili, lakini huyu aisee ni zaidi ya shetani. Hana chembe ya huruma, utu wala ubinadam. Anaweza kumpa mtoto adhabu ya kuweka miguu juu (ukutani) mikono chini (mfano wa sarakasi) kwa muda mrefu zaidi, bila kushusha miguu chini, na akishusha anakula kipondo ambacho anatakiwa kupigwa mwizi huko polisi.

Yote tisa, kumi ni pale anapomshindisha na njaa, alafu akigundua kuwa alikuja kwangu na wenzake (watoto wangu) akala, basi atachokutana nacho atajuta ni kwanini alimpoteza mama yake akiwa bado mdogo. Atapigwa, atapewa adhabu ya kuweka miguu juu, na kushindishwa na njaa.

Kila nlipotaka kumwambia jamaa kuhusu mateso anayopitia mwanae, moyo ulisita, nisije kuharibu ndoa ya watu au kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto mwenyewe. So niliamua kushona mdomo wangu tu kama sijui kinachoendelea.

Huyu mama mwanzoni alianza kuwa karibu na mke wangu, kutokana na ukaribu uliopo mimi na mumewe. Lakini alipogundua kwamba mke wangu huwa na tabia ya kumpa chakula mtoto anaeteswa, na sometimes kumpa hela pamoja na watoto wangu ili wanunue vitu vidogo vidogo vya kula, basi yule mama wa kambo akakata mawasiliano na mke wangu, na madam nae akampotezea kwa kufuata ule msema wa "akunyimae kunde, anakupunguzia kuja...m..ba.

Mtoto bado mdogo (miaka 7) kumweleza baba yake anashindwa, na mama huwa hampi nafasi ya kumsogelea baba yake akae nae mwenyewe. Halaf mtoto nguo, na viatu vimemuishia mpaka aibu naona mimi.

Juzi alhamisi nikaona upuuzi, wakati natoka mihangaikoni kwangu nikaingia dukani nikanunua nguo suruali 5, T'shirt 5, mashati mawili, jacket za baridi 3, viatu pea 3 na sandroz pea 1. Nikaenda mpaka kwa home boy nikamkabidhi mkewe nikamwambia kuwa zile nguo na viatu nilikuwa nimemnunulia mwanangu, lakin kwa bahati mbaya nimekuta havimtoshi, so ndomaana nikaona nimpe yeye ambae vinaonekana kumtosha, alaf mimi nitaenda na mtoto wangu town nikamnunulie vingine. Yule mama akapokea, lkn ni kwa shingo upande (kumbuka ni shemej yangu) halaf sina ugomvi nae yeye wala mumewe. So hakuwa na nguvu ya kukataa uso kwa uso.

Kumbe na yeye jana alienda town, akanunua nguo zake kadhaa, na kuja nazo nyumban kwa malengo yake binafsi. Usiku mumewe alipofika akaanza kumwambia kuwa mimi nimekuwa nikimtongoza na kumtaka kimapenzi muda mrefu bila mafanikio, na kwamba nilifikia hadi hatua ya kumnunulia yeye na mtoto (wa kambo) nguo ili anikubali, lakini bado alinikwepa na kuchukua tu nguo ili aje amuonesha (mumewe) nk.

Home boy alipotaka ushahidi yule mama akaenda kutoa zile nguo alizoenda kununua jana town, akajumlisha na zile nilizopeleka kwa ajili ya kumpa mtoto wa kambo anaeteseka. Aisee sijui jamaa alikuwa katika hali gani usiku ule na sijui alilalaje.

Asubuhi naona home boy anakuja nyumban bila salam anaanza kunibwatukia mbele ya mke wangu na watoto wangu. Namuuliza tatizo nini, anabwaga zile nguo mbele yangu na kusema eti ashajua kila kitu kuhusu mpango wangu wa kumtongoza mkewe.

Eti natongoza kishamba sana kwa kukimbilia kuhonga nguo. Yani nikashindwa kumuelewa vizuri, mpaka alipofafanua kwamba nilikuwa namtongoza mkewe, nilipoona hakubaliani na mimi ndo nikaenda town kununua vijinguo vya kumlaghai ili nimpate kiurahisi nk.

Nikataka kutumia ukaribu wetu kumueleza kile kinachoendelea katika familia yake mpaka mimi kufikia hatua ya kununua zile nguo za mtoto wake, lakini bingwa hakunielewa, akawa mtata mwisho nikamuacha aongee akichoka aamue mwenyewe anachotaka kufanya.

Baada ya kuona lengo lake la kunichafua mbele ya familia yangu limefeli akaondoka akidai kuanzia leo mimi na yeye ni maadui. Nisimjue, asinijue, nisiende kwake, na hatokuja kwangu, kila mtu aangalie maisha yake, nikamwambia poa.

Kwa bahati nzuri mke wangu anajua kila kinachoendelea, so ile complain ya kumtongoza mkewe haikumuingia akilini.

Namuonea huruma sana home boy, ni kama mapenzi yamemfanya asifatilie kinachoendelea katika nyumba yake. Damu yake inateswa, na sisi tunaosaidia tunaonekana wabaya. Mateso anayopitia yule mtoto hakuna mtu yoyote mwenye huruma hapa JF anaweza kuyaona akayavumilia.

Nilikuwa na mpango wa kwenda ku report swala hili katika mamlaka husika, lakini kuna rafiki yetu (mimi na yeye) amesema nisubiri kwanza jamaa hasira ziishe hata week 1 au 2, halafu aite kikao kati yangu na home boy kwa ajili ya maridhiano, halaf hapo kwenye kikao ndo nitumie chance hiyo kumueleza home boy kile kinachoendelea katika familia yake, na sababu ya mimi kumpelekea yule mtoto zile nguo na viatu.

Huyu rafiki mimi nimemuelewa, lkn sielewi ni vipi mpaka leo jamaa haoni kuwa mtoto wake anateseka hata kwa muonekano tu wa macho. Ama kweli tenda wema uende zako. Na sio kila mwenye macho huona kilichopo mbele yake. Jamaa haoni na hasikii.

Dah...


CHAI
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Jirani na hapa nnapoishi mimi kuna home boy fulani ambae tumetokea kuzoeana, kushauriana na hata sometimes kutembeleana. Tulitokea kujuana nae miezi 6 iliyopita baada ya yeye na familia yake kuhamia hapa. Kwa Tanzania ni mzaliwa wa Kinondoni, wakati mimi mzaliwa wa Magomeni Dar es salaam, hivyo tunaishi kama ndugu.

Kabla ya kuishi na mke alie nae sasa hivi, alikuwa ashaoa mke wake wa kwanza ambae alizaa nae mtoto mmoja wa kiume. Lakini kwa bahati mbaya mkewe alifariki miaka 3 iliyopita na kuacha mtoto huyo akiwa na umri wa miaka 4.

Baada ya mkewe kufariki, mwamba hakuchelewa, akakutana na huyu mkongo, akatangaza ndoa na kuanza maisha mapya (kumbuka hapo jamaa alikuwa na mtoto wa miaka 4), baadae na mkongo akamletea mtoto mungine wa kike, so jumla jamaa ana watoto wawili. Maisha yao huko walipokuwa haswa kwa upande wa mtoto wa kambo sijui yalikuaje, ila baada ya kuhamia jirani yetu na kufahamiana na jamaa, ndo nikaanza kuona mateso anayopitia mtoto.

Japo imezoeleka kuona mama wa kambo wengi ni makatili, lakini huyu aisee ni zaidi ya shetani. Hana chembe ya huruma, utu wala ubinadam. Anaweza kumpa mtoto adhabu ya kuweka miguu juu (ukutani) mikono chini (mfano wa sarakasi) kwa muda mrefu zaidi, bila kushusha miguu chini, na akishusha anakula kipondo ambacho anatakiwa kupigwa mwizi huko polisi.

Yote tisa, kumi ni pale anapomshindisha na njaa, alafu akigundua kuwa alikuja kwangu na wenzake (watoto wangu) akala, basi atachokutana nacho atajuta ni kwanini alimpoteza mama yake akiwa bado mdogo. Atapigwa, atapewa adhabu ya kuweka miguu juu, na kushindishwa na njaa.

Kila nlipotaka kumwambia jamaa kuhusu mateso anayopitia mwanae, moyo ulisita, nisije kuharibu ndoa ya watu au kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto mwenyewe. So niliamua kushona mdomo wangu tu kama sijui kinachoendelea.

Huyu mama mwanzoni alianza kuwa karibu na mke wangu, kutokana na ukaribu uliopo mimi na mumewe. Lakini alipogundua kwamba mke wangu huwa na tabia ya kumpa chakula mtoto anaeteswa, na sometimes kumpa hela pamoja na watoto wangu ili wanunue vitu vidogo vidogo vya kula, basi yule mama wa kambo akakata mawasiliano na mke wangu, na madam nae akampotezea kwa kufuata ule msema wa "akunyimae kunde, anakupunguzia kuja...m..ba.

Mtoto bado mdogo (miaka 7) kumweleza baba yake anashindwa, na mama huwa hampi nafasi ya kumsogelea baba yake akae nae mwenyewe. Halaf mtoto nguo, na viatu vimemuishia mpaka aibu naona mimi.

Juzi alhamisi nikaona upuuzi, wakati natoka mihangaikoni kwangu nikaingia dukani nikanunua nguo suruali 5, T'shirt 5, mashati mawili, jacket za baridi 3, viatu pea 3 na sandroz pea 1. Nikaenda mpaka kwa home boy nikamkabidhi mkewe nikamwambia kuwa zile nguo na viatu nilikuwa nimemnunulia mwanangu, lakin kwa bahati mbaya nimekuta havimtoshi, so ndomaana nikaona nimpe yeye ambae vinaonekana kumtosha, alaf mimi nitaenda na mtoto wangu town nikamnunulie vingine. Yule mama akapokea, lkn ni kwa shingo upande (kumbuka ni shemej yangu) halaf sina ugomvi nae yeye wala mumewe. So hakuwa na nguvu ya kukataa uso kwa uso.

Kumbe na yeye jana alienda town, akanunua nguo zake kadhaa, na kuja nazo nyumban kwa malengo yake binafsi. Usiku mumewe alipofika akaanza kumwambia kuwa mimi nimekuwa nikimtongoza na kumtaka kimapenzi muda mrefu bila mafanikio, na kwamba nilifikia hadi hatua ya kumnunulia yeye na mtoto (wa kambo) nguo ili anikubali, lakini bado alinikwepa na kuchukua tu nguo ili aje amuonesha (mumewe) nk.

Home boy alipotaka ushahidi yule mama akaenda kutoa zile nguo alizoenda kununua jana town, akajumlisha na zile nilizopeleka kwa ajili ya kumpa mtoto wa kambo anaeteseka. Aisee sijui jamaa alikuwa katika hali gani usiku ule na sijui alilalaje.

Asubuhi naona home boy anakuja nyumban bila salam anaanza kunibwatukia mbele ya mke wangu na watoto wangu. Namuuliza tatizo nini, anabwaga zile nguo mbele yangu na kusema eti ashajua kila kitu kuhusu mpango wangu wa kumtongoza mkewe.

Eti natongoza kishamba sana kwa kukimbilia kuhonga nguo. Yani nikashindwa kumuelewa vizuri, mpaka alipofafanua kwamba nilikuwa namtongoza mkewe, nilipoona hakubaliani na mimi ndo nikaenda town kununua vijinguo vya kumlaghai ili nimpate kiurahisi nk.

Nikataka kutumia ukaribu wetu kumueleza kile kinachoendelea katika familia yake mpaka mimi kufikia hatua ya kununua zile nguo za mtoto wake, lakini bingwa hakunielewa, akawa mtata mwisho nikamuacha aongee akichoka aamue mwenyewe anachotaka kufanya.

Baada ya kuona lengo lake la kunichafua mbele ya familia yangu limefeli akaondoka akidai kuanzia leo mimi na yeye ni maadui. Nisimjue, asinijue, nisiende kwake, na hatokuja kwangu, kila mtu aangalie maisha yake, nikamwambia poa.

Kwa bahati nzuri mke wangu anajua kila kinachoendelea, so ile complain ya kumtongoza mkewe haikumuingia akilini.

Namuonea huruma sana home boy, ni kama mapenzi yamemfanya asifatilie kinachoendelea katika nyumba yake. Damu yake inateswa, na sisi tunaosaidia tunaonekana wabaya. Mateso anayopitia yule mtoto hakuna mtu yoyote mwenye huruma hapa JF anaweza kuyaona akayavumilia.

Nilikuwa na mpango wa kwenda ku report swala hili katika mamlaka husika, lakini kuna rafiki yetu (mimi na yeye) amesema nisubiri kwanza jamaa hasira ziishe hata week 1 au 2, halafu aite kikao kati yangu na home boy kwa ajili ya maridhiano, halaf hapo kwenye kikao ndo nitumie chance hiyo kumueleza home boy kile kinachoendelea katika familia yake, na sababu ya mimi kumpelekea yule mtoto zile nguo na viatu.

Huyu rafiki mimi nimemuelewa, lkn sielewi ni vipi mpaka leo jamaa haoni kuwa mtoto wake anateseka hata kwa muonekano tu wa macho. Ama kweli tenda wema uende zako. Na sio kila mwenye macho huona kilichopo mbele yake. Jamaa haoni na hasikii.

Dah...
Wewe nae jau acha kujipa umuhimu kwenye maisha ya watu pmbav.
 
Nimesikitishwa sana na jambo hili.
Zingatia ushauri uliotolewa na baadhi ya wadau hapo juu, hasa kuona uwezekano wa kulifikisha suala hili kwa Dkt. Gwajima D . Japo ni ngazi ya mbali, lakini naamini ni namna rahisi na ya haraka kupata msaada.
I wish hata ndugu upande wa Mama Mzazi wa Mtoto wangefahamu madhila anayopitia Mtoto wa Marehemu ndugu yao, na kuchukua hatua muafaka za kumsaidia.
Dk Gwajima hausiki hapa jamaa anaishi South
 
Kuna wanawake hata shetani hua anakuja kujifunza roho mbaya kwao .Kuna jirani mtoto wake aliteswa aliumizwa na mama wa kambo ambaye nae ana watoto wawili amekuja nao kwa mmewe huyu jirani.Yaan hawa watoto wake ndo wamekua kama nyumba yao wao ni kula bata tu.Sisi majirani hatukutaka kuharibu ndoa ya jirani .. wanawake zetu walifanya kikao wakaja na jawabu la kumtafuta bibi wa mtoto upande wa mama yake na wakafanikiwa mtoto kachukuliwa na bibi yake sasa jirani analea dam si yake watoto wa kufikia wakati damu yake iko kwa bibi mzaa mama.Yule mwanamke hata salam yake hua naitikia tu ila nikimuona hua naona kama nimekutana na Msaidizi wa shetani.Mungu awalaani wote mnaotesa watoto na laana hii iwakumbe mpate magonjwa ya kuwatesa hadi mjinyee shenzi nyie ...
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Jirani na hapa nnapoishi mimi kuna home boy fulani ambae tumetokea kuzoeana, kushauriana na hata sometimes kutembeleana. Tulitokea kujuana nae miezi 6 iliyopita baada ya yeye na familia yake kuhamia hapa. Kwa Tanzania ni mzaliwa wa Kinondoni, wakati mimi mzaliwa wa Magomeni Dar es salaam, hivyo tunaishi kama ndugu.

Kabla ya kuishi na mke alie nae sasa hivi, alikuwa ashaoa mke wake wa kwanza ambae alizaa nae mtoto mmoja wa kiume. Lakini kwa bahati mbaya mkewe alifariki miaka 3 iliyopita na kuacha mtoto huyo akiwa na umri wa miaka 4.

Baada ya mkewe kufariki, mwamba hakuchelewa, akakutana na huyu mkongo, akatangaza ndoa na kuanza maisha mapya (kumbuka hapo jamaa alikuwa na mtoto wa miaka 4), baadae na mkongo akamletea mtoto mungine wa kike, so jumla jamaa ana watoto wawili. Maisha yao huko walipokuwa haswa kwa upande wa mtoto wa kambo sijui yalikuaje, ila baada ya kuhamia jirani yetu na kufahamiana na jamaa, ndo nikaanza kuona mateso anayopitia mtoto.

Japo imezoeleka kuona mama wa kambo wengi ni makatili, lakini huyu aisee ni zaidi ya shetani. Hana chembe ya huruma, utu wala ubinadam. Anaweza kumpa mtoto adhabu ya kuweka miguu juu (ukutani) mikono chini (mfano wa sarakasi) kwa muda mrefu zaidi, bila kushusha miguu chini, na akishusha anakula kipondo ambacho anatakiwa kupigwa mwizi huko polisi.

Yote tisa, kumi ni pale anapomshindisha na njaa, alafu akigundua kuwa alikuja kwangu na wenzake (watoto wangu) akala, basi atachokutana nacho atajuta ni kwanini alimpoteza mama yake akiwa bado mdogo. Atapigwa, atapewa adhabu ya kuweka miguu juu, na kushindishwa na njaa.

Kila nlipotaka kumwambia jamaa kuhusu mateso anayopitia mwanae, moyo ulisita, nisije kuharibu ndoa ya watu au kusababisha matatizo zaidi kwa mtoto mwenyewe. So niliamua kushona mdomo wangu tu kama sijui kinachoendelea.

Huyu mama mwanzoni alianza kuwa karibu na mke wangu, kutokana na ukaribu uliopo mimi na mumewe. Lakini alipogundua kwamba mke wangu huwa na tabia ya kumpa chakula mtoto anaeteswa, na sometimes kumpa hela pamoja na watoto wangu ili wanunue vitu vidogo vidogo vya kula, basi yule mama wa kambo akakata mawasiliano na mke wangu, na madam nae akampotezea kwa kufuata ule msema wa "akunyimae kunde, anakupunguzia kuja...m..ba.

Mtoto bado mdogo (miaka 7) kumweleza baba yake anashindwa, na mama huwa hampi nafasi ya kumsogelea baba yake akae nae mwenyewe. Halaf mtoto nguo, na viatu vimemuishia mpaka aibu naona mimi.

Juzi alhamisi nikaona upuuzi, wakati natoka mihangaikoni kwangu nikaingia dukani nikanunua nguo suruali 5, T'shirt 5, mashati mawili, jacket za baridi 3, viatu pea 3 na sandroz pea 1. Nikaenda mpaka kwa home boy nikamkabidhi mkewe nikamwambia kuwa zile nguo na viatu nilikuwa nimemnunulia mwanangu, lakin kwa bahati mbaya nimekuta havimtoshi, so ndomaana nikaona nimpe yeye ambae vinaonekana kumtosha, alaf mimi nitaenda na mtoto wangu town nikamnunulie vingine. Yule mama akapokea, lkn ni kwa shingo upande (kumbuka ni shemej yangu) halaf sina ugomvi nae yeye wala mumewe. So hakuwa na nguvu ya kukataa uso kwa uso.

Kumbe na yeye jana alienda town, akanunua nguo zake kadhaa, na kuja nazo nyumban kwa malengo yake binafsi. Usiku mumewe alipofika akaanza kumwambia kuwa mimi nimekuwa nikimtongoza na kumtaka kimapenzi muda mrefu bila mafanikio, na kwamba nilifikia hadi hatua ya kumnunulia yeye na mtoto (wa kambo) nguo ili anikubali, lakini bado alinikwepa na kuchukua tu nguo ili aje amuonesha (mumewe) nk.

Home boy alipotaka ushahidi yule mama akaenda kutoa zile nguo alizoenda kununua jana town, akajumlisha na zile nilizopeleka kwa ajili ya kumpa mtoto wa kambo anaeteseka. Aisee sijui jamaa alikuwa katika hali gani usiku ule na sijui alilalaje.

Asubuhi naona home boy anakuja nyumban bila salam anaanza kunibwatukia mbele ya mke wangu na watoto wangu. Namuuliza tatizo nini, anabwaga zile nguo mbele yangu na kusema eti ashajua kila kitu kuhusu mpango wangu wa kumtongoza mkewe.

Eti natongoza kishamba sana kwa kukimbilia kuhonga nguo. Yani nikashindwa kumuelewa vizuri, mpaka alipofafanua kwamba nilikuwa namtongoza mkewe, nilipoona hakubaliani na mimi ndo nikaenda town kununua vijinguo vya kumlaghai ili nimpate kiurahisi nk.

Nikataka kutumia ukaribu wetu kumueleza kile kinachoendelea katika familia yake mpaka mimi kufikia hatua ya kununua zile nguo za mtoto wake, lakini bingwa hakunielewa, akawa mtata mwisho nikamuacha aongee akichoka aamue mwenyewe anachotaka kufanya.

Baada ya kuona lengo lake la kunichafua mbele ya familia yangu limefeli akaondoka akidai kuanzia leo mimi na yeye ni maadui. Nisimjue, asinijue, nisiende kwake, na hatokuja kwangu, kila mtu aangalie maisha yake, nikamwambia poa.

Kwa bahati nzuri mke wangu anajua kila kinachoendelea, so ile complain ya kumtongoza mkewe haikumuingia akilini.

Namuonea huruma sana home boy, ni kama mapenzi yamemfanya asifatilie kinachoendelea katika nyumba yake. Damu yake inateswa, na sisi tunaosaidia tunaonekana wabaya. Mateso anayopitia yule mtoto hakuna mtu yoyote mwenye huruma hapa JF anaweza kuyaona akayavumilia.

Nilikuwa na mpango wa kwenda ku report swala hili katika mamlaka husika, lakini kuna rafiki yetu (mimi na yeye) amesema nisubiri kwanza jamaa hasira ziishe hata week 1 au 2, halafu aite kikao kati yangu na home boy kwa ajili ya maridhiano, halaf hapo kwenye kikao ndo nitumie chance hiyo kumueleza home boy kile kinachoendelea katika familia yake, na sababu ya mimi kumpelekea yule mtoto zile nguo na viatu.

Huyu rafiki mimi nimemuelewa, lkn sielewi ni vipi mpaka leo jamaa haoni kuwa mtoto wake anateseka hata kwa muonekano tu wa macho. Ama kweli tenda wema uende zako. Na sio kila mwenye macho huona kilichopo mbele yake. Jamaa haoni na hasikii.

Dah...
Hukutakiwa kuingilia mambo ya watu, ungeenda tu kutoa taarifa ustawi wa jamii, then wewe unaendelea na mambo yako.
 
Mtu anashindwa kufikiria kwamba anapotesa watoto wa mwenzake, na yeye kesho akifa pia wa kwake watateswa. Sijui wanakuaga na akili na moyo gani hawa viumbe.
Huwa wanawaza ya leo sio kesho ndo maana wana roho za kikatili. Kiukweli mtu anayemtesa mtoto wa kambo huwa simuelewi.
 
Back
Top Bottom