Rais amefanya ziara Kisarawe na kuzindua Mradi mkubwa wa Maji Wilayani humo

Rais amefanya ziara Kisarawe na kuzindua Mradi mkubwa wa Maji Wilayani humo

Nachelea kuandika haya lakini ndio ukweli kukujibu wewe mpenda kukashifu watu.

Kiongozi Mkuu, aliyejijengea sifa hadi kuaminika na jamii ya ndani na kimataifa, analewa chakari hadi kuanguka na kuumia kifundo cha mguu (siyo kuvunjika), mnajitokeza kumtetea wakati hamkuwepo kwenye tukio, tuwape majina gani!

Si yeye, wala dereva wake, wamejitokeza hadharani kuelezea mkasa wote. Kwa tabia yake, ingekuwa kweli ameshambuliwa, kwa sababu za kisiasa, kama ambavyo mnadai, hakika asingekuwa kimya hadi sasa. Rejea taarifa yake kwa vyombo vya habari kuhusu kushambuliwa Lissu kwa risasi alivyoishutumu Serikali, lakini leo shambulio dhidi yake anakaa kimya!

Hamkisaidii chama kwa kufukua fukua majungu na kuanzisha uzushi wa kashfa dhidi ya Serikali na viongozi wake. Huo ni mtaji hasi wa kisiasa. Wapiga kura, naamini, wanahitaji kusikia Sera na Mikakati ya maendeleo mbadala kuwaondoa katika hali waliyo nayo kwa sasa, kuelekea kwenye neema.

WAKATI NDIO HUU BADILIKENI KIFIKRA NA MITAZAMO, tunapoelekea Uchaguzi Mkuu. Hizo fikra na mawazo yenu waachieni watoto wa chekechea.
Majungu, kashifa, matusi nk, kwa viongozi na serikali, siyo sawa!! Hayafai kwa Mbowe wala wapinzani pia! Hata Wewe hustahili kukashifiwa wala kutukanwa! Wanadamu wote ni Sawa, hivyo nakushauri, ishi kwa mfano, usimkataze G Sam kutukana, kukashifu na majungu, wakati unafanya hayo hayo kwa Mbowe na CHADEMA!
 
Kuna mambo hapo nimeyaelewa.
1. Leo hajashikana mikono na watu (Ujumbe wangu kuhusu mwenendo wa COVID 19 nchini unaanza kumuingia)
2. Mama yetu mpendwa hatimaye ametengamaa na leo yupo pembeni.

3. Nadhani DC atakuwa kwa mbali kidogo maana kwenye mapokezi sijamuona

4. Wakuu wote wa vyombo vya ulinzi wapo yani IGP na CDF hapo sijaelewa wao na mradi wa maji vinahusiana nini!

Povu ruksa kwa wale watetezi wa wanyonge!

Walau anaanza kuona umuhimu wa kujikinga na COVID 19 na naamini atahimiza wananchi wajikinge na kuvaa barakoa. Vinginevyo atakuwa sehemu ya dhambi za vifo!
 
Umerudia ulichokiandika mkuu? Hivi huwa hata nafsi haziwasuti kuandika uongo mkubwa hivo? Acha Mungu aitwe Mungu maana ni yeye pekee mtoa haki.
 
Mradi wa kuzinduliwa na waziri tu lakini Mkubwa anang'ang'ania ili apige na kampeni humo humo !
 
Halafu mwendawazimu asimame aseme anataka anamtaka Membe kwa lipi au ile mipasho!
 
Mradi w kuzinduliwa na waziri tu lakini Mkubwa anang'ang'ania ili apige na kampeni humo humo !

Mradi wa 10b unaenda kupigiwa kampeni na rais! Nilidhani ni mradi wa 100b+, kumbe ni kama hiyo hela aliyopata Laizer? Hiyo inaitwa kufanya siasa kwenye kila kitu.
 
Halafu mwendawazimu asimame aseme anataka anamtaka Membe kwa lipi au ile mipasho!

Hata kama mimi sio mpenzi wa Membe, kwani hata yeye akiwa rais atashindwa kuagiza shilingi 10b zijenga mradi wa maji?
 
Halafu mwendawazimu asimame aseme anataka anamtaka Membe kwa lipi au ile mipasho!
Kazi Imeishia Kisarawe
Baadaye October
Tunachukua, Tunaweka, Was a!!!
Mafiga Matatu Haa ,Tupate Rais, Mbunge, Diwani
😀😁

Tanzania Ni Tajiri Sana
 
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, Leo Atafanya Ziara Wilayani Kisarawe Kuzindua Mradi Mkubwa Wa Maji. Ambao Utawanufaisha Wakazi Wa Kisarawe Hadi Maeneo Ya Ukonga, Pugu

Bila Shaka Tutaaambiwa Mapya Mengi Kuhusu Maendeleo Ya Nchi Yetu. Pia Wakazi Wa Pembezoni Mwa Barabara Atakayopita Wategemee Neema, Hata Mradi Hautapita Kijiji Chochote Bila Wananchi Kupata Maji

Chanzo Cha Taarifa, TBC
===


Katika tukio hilo la ukaguzi wa Mradi wa maji Wilayani Kisarawe Rais Magufuli alifika eneo la tukio moja kwa moja na kisha kusikiliza malelezo ya kina na mtaalamu ya namna mradi huu utakavyofanya kazi na maeneo ambayo mradi huo utafanya utahudumu.

Aidha, baada ya kupokea maelezo hayo Rais Magufuli moja kwa moja amelekea katika kuzindua rasmi mradi huo ikiwa pamoja na kujaribu namna maji yanavyotoka katika mradi huo.

Mwisho, Rais Magufuli alipiga picha ya pamoja na na viongozi na Wakandarasi wa mradi huo na kuondoka kuelekea uwanja wa Mkutano.

Hivi Jokate yuko wapi vile?
 
Umerudia ulichokiandika mkuu? Hivi huwa hata nafsi haziwasuti kuandika uongo mkubwa hivo? Acha Mungu aitwe Mungu maana ni yeye pekee mtoa haki.
Ukweli unabaki ukweli na uwongo hujitenga. Haipendezi katu kudanganya umma ili kupata huruma yao iwe mtaji wa kisiasa.

Mimi kama mimi sipendezwi na nachukia kusikia uwongo na kashfa za kizushi dhidi ya utawala. Kama kuna makosa yanatendwa yakosolewe kwa lugha ya kistaarabu siyo inayotumiwa na viongozi wa upinzani na wafuasi wao wa kwenye mitndao ya kijamii. Humu wamo wengi tu, na wamegeuza JF kijiwe cha kushindana uzushi, uwongo na matusi. Hakuna shaka yoyote wanafuata nyao za viongozi wao.

Mada KUU ni kuhusu ufunguzi wa mradi wa maji, kumtua mama ndoo kichwani. Mjadala unabadilishwa kuwa matusi, tena ya nguoni, dhidi ya viongozi. Nisingenyamaza ikabidi nami niwatolee uvivu kwa kuwakumbusha kitendo cha aibu na fedheha alichokifanya Kiongozi wao Mkuu, wampambae kwa jina la MWAMBA.
 
Kuna mambo hapo nimeyaelewa.
1. Leo hajashikana mikono na watu (Ujumbe wangu kuhusu mwenendo wa COVID 19 nchini unaanza kumuingia)
2. Mama yetu mpendwa hatimaye ametengamaa na leo yupo pembeni.

3. Nadhani DC atakuwa kwa mbali kidogo maana kwenye mapokezi sijamuona

4. Wakuu wote wa vyombo vya ulinzi wapo yani IGP na CDF hapo sijaelewa wao na mradi wa maji vinahusiana nini!

Povu ruksa kwa wale watetezi wa wanyonge!

Walau anaanza kuona umuhimu wa kujikinga na COVID 19 na naamini atahimiza wananchi wajikinge na kuvaa barakoa. Vinginevyo atakuwa sehemu ya dhambi za vifo!
Wewe jamaa na hiyo COVID 19 yako!! COVID haiishi karibuni mzee, na watu hawawezi kuacha kufanya shughuli za kiuchumi zaidi ya mwaka sababu ya hayo Mafua.
 
Back
Top Bottom