Nachelea kuandika haya lakini ndio ukweli kukujibu wewe mpenda kukashifu watu.
Kiongozi Mkuu, aliyejijengea sifa hadi kuaminika na jamii ya ndani na kimataifa, analewa chakari hadi kuanguka na kuumia kifundo cha mguu (siyo kuvunjika), mnajitokeza kumtetea wakati hamkuwepo kwenye tukio, tuwape majina gani!
Si yeye, wala dereva wake, wamejitokeza hadharani kuelezea mkasa wote. Kwa tabia yake, ingekuwa kweli ameshambuliwa, kwa sababu za kisiasa, kama ambavyo mnadai, hakika asingekuwa kimya hadi sasa. Rejea taarifa yake kwa vyombo vya habari kuhusu kushambuliwa Lissu kwa risasi alivyoishutumu Serikali, lakini leo shambulio dhidi yake anakaa kimya!
Hamkisaidii chama kwa kufukua fukua majungu na kuanzisha uzushi wa kashfa dhidi ya Serikali na viongozi wake. Huo ni mtaji hasi wa kisiasa. Wapiga kura, naamini, wanahitaji kusikia Sera na Mikakati ya maendeleo mbadala kuwaondoa katika hali waliyo nayo kwa sasa, kuelekea kwenye neema.
WAKATI NDIO HUU BADILIKENI KIFIKRA NA MITAZAMO, tunapoelekea Uchaguzi Mkuu. Hizo fikra na mawazo yenu waachieni watoto wa chekechea.