kwahiyo alivyosafiri hajamkaimisha mtu madaraka yakuongoza nchi?.anatembea namadaraka ya uonhozi wa nchi hadi nje ya nchi?.Kama ni hivyo mmmmmh
sio madaraka tu na mamlaka Kamili ya Urais ndio maana anapokelewa kwa heshima na salute ya utii na heshima ya Rais huko aliko.
Anakasimisha nadharia tu,
kwamba ndugu yangu Makamu wa rais, ninasafiri kidogo ninakwenda nitarudi kaeni salama.
Ikiwa kuna jambo lisilo la kawaida msisite kunishirikisha na kuniarifu niwaelekeze cha kufanya.
CDF, big up sana nakuaminia, IGP unafanya kazi nzuri,endelea nenda nao taratibu siasa ndivyo ilivyo. Lazima wakulalamikie na wakulaumu sana.
Waziri mkuu na naibu waziri mkuu, tafadhali mtamuarifu speaker natoka kidogo. Endeleeni kuchapa kazi mkayasimamie tuliyokubaliana..
Jaji mkuu, mwende mkafanye kazi ya kusimamia haki kwa weledi. Nikirudi kuna jambo nahitaj tuliweke sawa. Tutafanya kikao kidogo.
Haya jaman mimi nakwenda.........
Kisha mama anaingia kwenye gari kuelekea uwanja wa ndege kukwea pipa huyo ughaibuni.
Kwenye ofisi yake sasa ndani ya BOING, anamuita Zuhura Yunusi na katibu Mkuu kiongozi,
Hebu ñjooni na lile faili la mapendekezo ya teuzi za wakuu wa wilaya na Wakurugenzi. Kazi inaendelea.....
Hadi anafika Dubai tayari pdf la teuzi lipo tayari na Zuhura yunusi kaisha upload na kuliposti katika kila page ya ikulu........
vivyohivyo wakat wa kurud nyumbani kazi inaendelea......