Rais Magufuli atekeleza agizo la Makonda la ukaguzi wa silaha, apeleka bunduki zake

Rais Magufuli atekeleza agizo la Makonda la ukaguzi wa silaha, apeleka bunduki zake

Yaani sasa kulikuwa na haja gani ya Rais kupiga picha na kusambaza huku akionyesha hadharani silaha anayomiliki?

Hivi ni Ulimbukeni au ni kujisahau tu?

Ashauriwe maana sioni kama utetezi wa Kuwa anaonyesha mfano mwema utakuwa na maana.
 
Good..!

Atangaze na kuhakikiwa mali zake, ili kuwahamisisha viongozi wengine pia.
 
Lengo litakuwa kuhamasisha wamiliki wa silaha kuhakiki silaha zao kama alivyoagiza RC.
 
Japokuwa huwa sikubaliani na mambo mengi ya Jpm ila sioni shida kwa kutokea katika picha na huo mkwaju. Raisi ni kiongozi wetu ambaye anatuonyesha mfano wa kutii mamlaka za serikali na bastola inakaa kiunoni na sio mfukoni au kwenye mkoba!!!
Na mwisho kuipeleka silaha yake kukaguliwa haina maana kwamba anatembea nayo kila siku au hana imani na wanaomlinda,inawezekana alishaimiliki kabla hata hajakuwa presidaa.

NB, pelekeni mikwaju yenu kwa ukaguzi ndugu.
sawa, tutapeleka . mkuu kaanza nasi tufate,
 
Niliwahi kusema, kama unataka uwe mpinzani kwenye serikali ya Rais Magufuli lazima kwanza uvae ujinga ili uwe kama kituko kifikra au uwe mpumbavu.

Kuna baadhi ya watu hawafahamu kuwa vyombo vya habari vimekuwa embedded Ikulu na kwa maana hiyo kila anachokifanya Rais kwenye public kinakuwa kwenye media. Hii ni age ya Information technology na wananchi wanapaswa kuhabarishwa anachokifanya Rais kama citizen number one and public figure.

Kuna wengine hawafahamu kuwa ni marufuku kisheria kubeba silaha ya mtu mwingine au kumpa mtu mwingine akubebee silaha yako.

Baadhi ya watu wamekosa madhaifu ya Rais Magufuli na wanachokifanya kwa sasa ni kupiga kelele za kijinga.

We jamaa ulivyo na akili mbovu hata kama Rais akifanya madudu gani utayageuza kuwa sifa nzuri!

Uliwahi kuskia wapi Amiri Jeshi Mkuu anakaguliwa chochote achilia mbali silaha?kama yeye akikaguliwa inamaanisha kuna Rais mwingine aliye juu yake ambaye hamuamini.
 
Hii hata kama sifa imezidi.SIjawahi kuona toka enzi za JKN mpaka Kikwete,Rais kuwa na silaha.Walinzi wote wale ikulu.Au yuko first kutumia kuliko walinzi wake??Imenipa shida,nadhani hata walinzi wake itakuwa imewapa shida kumuelewa.


Na mimi nashangaa kwa nini unashangaa Rais ana silaha, hivi unajua kulenga shabaha ni hobby?
 
Yaani sasa kulikuwa na haja gani ya Rais kupiga picha na kusambaza huku akionyesha hadharani silaha anayomiliki?

Hivi ni Ulimbukeni au ni kujisahau tu?

Ashauriwe maana sioni kama utetezi wa Kuwa anaonyesha mfano mwema utakuwa na maana.


Raisi Magufuli ni ngazi nyingine kabisa simple minds hamuwezi kumuelewa, kila anachokifanya kimeshapigiwa hesabu na anajua kwa nini anafanya alivyofanya, rejea alichokisema Mkuu wa Mkoa wa Dar ni kwamba wana Dar wote wenye silaha wazipeleke kuzihakiki sasa basi kama raisi wa nchi amepeleka silaha kuhakikiwa, wewe ni nani hata usipeleke silaha yako? go figure...!
 
We jamaa ulivyo na akili mbovu hata kama Rais akifanya madudu gani utayageuza kuwa sifa nzuri!

Uliwahi kuskia wapi Amiri Jeshi Mkuu anakaguliwa chochote achilia mbali silaha?kama yeye akikaguliwa inamaanisha kuna Rais mwingine aliye juu yake ambaye hamuamini.
Kwani alipewa silaha zake kama Amiri Jeshi Mkuu.

Kwani mpaka usikie sehemu nyingine wamefanya ili na wewe ufanye suala lolote? Hizi akili na fikra za copy & paste hazina nafasi katika ulimwengu wa ubunifu.

Wewe vipi?
 
Kwa yote, nampenda Magufuli kwa kuwa ataanzisha utamaduni mpya: wa kutii sheria kwa wote. Ingekuwa ni hao waliopita, usingemwona yeyote. Walikuwa wakiwaonesha wananchi kuwa wao wako juu ya sheria. Mbaya sana.
 
Kwani alipewa silaha zake kama Amiri Jeshi Mkuu.

Kwani mpaka usikie sehemu nyingine ndio ufanye suala lolote? Hizi ni skili za copy & paste.

Wewe vipi?
Tatzo lako huelewi...limetilewa tangazo kwamba silaha zote lazma zihakikiwe UPYA ndani ya siku 90 sasa raisi amefanya loss gani kuhakiki silaha zake
 
Back
Top Bottom