Rais Magufuli atekeleza agizo la Makonda la ukaguzi wa silaha, apeleka bunduki zake

Rais Magufuli atekeleza agizo la Makonda la ukaguzi wa silaha, apeleka bunduki zake

Rais Magufuli leo atekeleza agizo la Mkuu wa mkoa la kuwasilisha silaha jeshi la Polisi kwa ajili ya ukaguzi.

Amewataka wananchi wote wanaomiliki silaha katika jiji la Dar kujitokeza kuhakiki silaha zao kama alivyoagiza mkuu wa mkoa.

View attachment 331523 View attachment 331522
View attachment 331524 View attachment 331525 View attachment 331526
Naona sasa watu wakiitwa ikulu lazima watetemeke baada ya kuona jinsi anavyoweza kuhandle hizo silaha..

But seriously sipendi guns real, fake or even toys.
 
Haaa haaaa watu media wana kazi sana safari hii duh,hongera JPM wewe ni mfano wa kuigwa imebidi niseme eti haaa haa...!
 
Rais Dr. J P Magufuli amewapiga dongo Polisi waoga kupitia kwa Kamanda Sirro leo ikulu. Rais alipoongea machache mara baada ya kuhakiki silaha yake amesema ni aibu kwa polisi kunyang'anywa silaha wakati wanazo silaha za kujihami, ni aibu kuona askari ambaye alikuwa na silaha anakwenda kwa Rpc AKIWA MZIMA kutoa taarifa kwamba ameibiwa silaha. Miezi kadhaa hapo nyuma tulisikia vituo vya polisi vya Ikwiriri na staki shari vikivamiwa na majambazi na silaha kuibiwa. Kauli hii ni dongo la wazi kwa matukio yale.
HAPA KAZI TU ni wakati sasa polisi kupambana na sio kuchungulia na kukimbia.
 
Rais John Magufuli amekwenda kuhakiki silaha zake kwa Jeshi LA Polisi. Akiwa mbele ya Kamanda Simon Siro alichomoa bastola yake kiunoni na kuweka mezani.

Hiki ni kituko cha mwaka, Rais ambaye ni raia namba moja mwenye ulinzi mkali kuliko wananchi wote bado anatembea na bastola kiunoni!?

Je, hawaamini walinzi wake? Sasa sisi wananchi wa chini huku tunahakikishiwaje usalama wetu ikiwa rais wetu hana uhakika?

Inawezekana alitaka kutoa mfano kwa watu wengine, lakini hii imemharibia.

Issue hiyo angewapa wasaidizi wake tu wakamsaidia kuhakiki.

Ndio tabia za vijana siku hizi wakinunua bastola wanaringishiana wakiwa bar. Ni ushamba tu.

Inadhihirisha pia tabia ya watawala was CCM kuamini katika mabavu tu. Hata kule bungeni wapinzani wakitoa hoja na kutaka majibu ya serikali, Spika anaita Polisi ndani kuwapiga. Kwenye uchaguzi wanategemea nguvu zabkijeshi tu, sio mapenzi ya wananchi.

Mwisho sasa nchi inageuka kuwa ya kibabe tu.

Ile nchi tuliyokuwa tukiita kisiwa cha amani haipo tena, watu waliishi kwa kuaminiana na kupendana.

Sasa ni mwendo was bastola tu.
 
I don't get it that Rais anatembea na silaha wakati anao walinzi wanaomzunguka muda wote wakiwa na silaha za kumlinda?
Mkuu hili hata mimi limenishangaza.
Yawezekana hatembei nayo huenda alikuwa akiimiliki toka zamani,
Lakini je, kwanini mara baada ya kula kiapo taratibu zisimlazimishe kuirejesha kwa vyombo vya ulinzi labda mpaka hapo atakapostaafu??
 
bd7b3008feca96a774d4097bf6da5697.jpg
 
Hope alitakiwa kuirudisha.Imenipa shida kidogo kwamba hawaamini walinzi wake.Halafu mbona lisilaha lenye kubwa mno.
Nimeshangaa aisee, dubwana hiloo kama la medani vilee
 
Nadhani silaha alikuwa nazo tangu kabla hajawa rais. Suala ni kuwa kuna umuhimu wa kuendelea kutembea nazo hadi kipindi hiki ambapo kazungukwa Na walinzi kila kona??


silaha co lazima atembee nayo, Bali inawwza kukaa hats homu. bt ulinzi binafsi stl ni muhimu. huwez ukawategemea bodigad asilimia 200
 
Hapo nakubaliana naye!
15639043, member: 307869"]Hapo nakubaliana naye![/QUOTE]
Brother acha utani. Mijambazi imewazidi firepower mara zaidi ya kumi kwa idadi na uimara wa zana hapo hakuna ujanja zaidi ya strategic retreat ikifatiliwa na Sprint ya Usain Bolt.
 
Hivi hiyo silaha iliyo kaguliwa ni ya nani ?? Nani mwingine alipaswa kubeba silaha yenye usajili wa mtu mwingine ??
Kutembea na silaha na kumiliki silaha ni jambo moja ??

Bastola inatakiwa ikae wapi kama tatizo ni yeye kuichomeka kiunoni ??

Hilo zoezi la uhakiki likiisha mnajuaje kwamba ataendelea kukaa na silaha kiunoni ? Au atarudisha panapotakiwa iwepo ??
 
nadhani gizi alinunua kabla ya kuwa raisi,, sasa katimiza wajibu tu wakwenda kuzihakiki kama agizo la mkuu wa mkoa alivyotangaza ,....
Rais yuko juu ya sheria, sasa yee kaenda kutii sheria ipi?
Hata hivyo sidhani kama kulikuwa na ulazima wa yeye kufanya hivyo.
Hasa kitendo cha kuonesha silaha hadharani na mapicha juu juu
 
Back
Top Bottom