Rais Magufuli: Mshahara wangu kwa Mwezi ni Sh. Milioni 9.5. Nitatoa salary slip...

Rais Magufuli: Mshahara wangu kwa Mwezi ni Sh. Milioni 9.5. Nitatoa salary slip...

Mkuu, hapana jamaa ana logic, mishahara matumizi yake ni kukidhi gharama za maisha ya kila siku ambazo tayari zinabebwa na bajeti ya kila mwaka. Katiba pia imemhakikishia kuishi hata baada ya kuongoza, sasa mshahara wa nini???
Ili ujue uzito wa kazi yake na anastahili zaidi ya huo mshahara, watu wenye njaa wanamlalamikia wao kuwa wana njaa, wakulima wanamlalamikia yeye kuhusu mazao, vijana wanamlalamikia yeye kuhusu ajira, wagonjwa kulala chini wanamlalamikia yeye, pesa kupotea ktk mzunguko watu wanamlalamikia yeye, nk.
Unajua kwa nini hawa watu wote wanamlalamikia yeye? Ana majukumu mazito zaidi ya udhaniavyo.
 
Hata mie nahisi hivyo.....!

Tatizo la wengi wetu tunatoa tu maoni bila hata kujiuliza katiba yetu na sheria zetu zinasemaje.......! Hivi ukimlipa rais 400,000 unadhani atamwajibishaje yule anayelipwa 15,000,000? Na je, wastaafu wenzake wataishije? Sometimes we need to think and re-think before we comment, unless we believe that our comments are non-sense, so material less.....
Unajua mkuu, kwanza kufikiri ina-cost energy, pili wengi wetu humu akili zimeamia kwenye vidole, hivyo wazia zitoke vidoleni ziende kwenye cpu kichwani inakuwa kazi kweli...😉
 
Duh, aisee, comrade, na wewe nakupa pole...ila you may have a point labda wewe itikadi zako ni za 'classical communism'. On a serious note, comrade, hivi Rais afanye nini mpaka mikakati yake ya kuijenga nchi hii,( ya kurudisha nidhamu katika jamii, ya kuwajibika, ya kufuata sheria, ya kuhakikisha kuwa kila mtu anakula kwa jasho lake, ya kuhakikisha kuwa raslimali za taifa hili watanzania wote wanafaidi) inakubalika na watanzania kama ninyi? What should the Presient do?! Kwanini mnakuwa hivi? Yaani sisi watanzania tumekuwa ni watu wa kulalamika kwa kila kitu. Wengine wanasema haya Rais ataje mshahara wake, amewatajia, lakini wako wanaoona haijatosha kwani walidhani Rais anapokea pengine milioni 100 au zaidi kwa mwezi, kwa hiyo wanasema hizo milioni 9.5 ni nyingi apunguziwe hadi zifikie 400,000/- kwa mwezi kwani eti anakula bure, sijui nini bure, etc. Yaani sisi watanzania ni watu wa ajabu, hata malaika hawezi kutawala nchi hii.
mkuu binafsi sipingani na jitihada za rais, namkubali sana magufuli, linapo kuja swala la mshahara kwa mtu kama rais sioni ni wa nini,kwasababu tunapo mpa kila hitaji lake mpaka kiwembe au wa kumkata kucha kabisa tukamlipa ili kumuwezesha afanye shughuli zake kwa wepesi, ukiongeza malipo ya mshahara kwa kutaja kiasi chochote sioni kama nirealistic.
 
Baada ya watu kutaka kujua yeye anapokea sh.ngapi awapigia simu clouds tv na kujibu swali hilo kuwa yeye anapokea sh.9.500.000 kwa mwezi na akimaliza likizo atatoa ufafanuzi wote

Source clouds Tv
Fools Day ----sikukuu ya wajinga 1/4/2016 mradi taarifa itolewe kabla ya saa nne asubuhi.
 
..wanaweza kwenda bungeni wakatunga sheria inayoruhusu kufunguza mshahara wa Raisi pamoja na Mafao ya viongozi wakuu wastaafu.

..Kama Hilo litachukua muda basi Raisi awaombe wazee wastaafu wakubali kupunguziwa Mafao Yao ili waisaidie serikali kubana matumizi.

Hawawezi kulitungia sheria; ni mpaka wabadili Katiba. Na mchakato wa kubadili Katiba sidhani kama utakuwa rahisi kivile kwa jambo moja isipokuwa kama wanataka kufanya kwa ujumla
 
mkuu binafsi sipingani na jitihada za rais, namkubali sana magufuli, linapo kuja swala la mshahara kwa mtu kama rais sioni ni wa nini,kwasababu tunapo mpa kila hitaji lake mpaka kiwembe au wa kumkata kucha kabisa tukamlipa ili kumuwezesha afanye shughuli zake kwa wepesi, ukiongeza malipo ya mshahara kwa kutaja kiasi chochote sioni kama nirealistic.
Tuzipage na akili zetu nafasi za kufikiri jamani.
 
Ili ujue uzito wa kazi yake na anastahili zaidi ya huo mshahara, watu wenye njaa wanamlalamikia wao kuwa wana njaa, wakulima wanamlalamikia yeye kuhusu mazao, vijana wanamlalamikia yeye kuhusu ajira, wagonjwa kulala chini wanamlalamikia yeye, pesa kupotea ktk mzunguko watu wanamlalamikia yeye, nk.
Unajua kwa nini hawa watu wote wanamlalamikia yeye? Ana majukumu mazito zaidi ya udhaniavyo.
ndugu ukumbuke huyu mtu tunamuwezesha kwa kila kitu ili apate urahisi wa kazi zake hata za binafsi, ukitaja kiasi hicho kuwa ndo mshahara wake hautakuwa realistic.
 
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametaja mshahara wake kuwa ni Tsh mil 9.5, huku akiahidi atatoa Salary slip zake punde akitoka mapumzikoni Chato.

Hiyo imetokea wakati wa kipindi cha magazeti leo tarehe 01/04/2016 ambapo watangazaji walisoma habari iliyoandikwa na gazeti la nipashe kuwa Zitto na Lissu waomba ataje Mshahara wake na ukatwe kodi.

Wakiwa katika mjadala huo, walipokea taarifa kuwa Rais kawasikia na katuma taarifa ofisi za Clouds kujuza mshahara wake kuwa ni mil 9.5 na atatoa stakabadhi zake akirudi Dar.

Huo ndio mshahara alioukuta na hata Rais Kikwete alikuwa akilipwa kiasi hicho pia.

Chanzo: Clouds 360 Asubuhi hii.
Duuh mbona mdogo sana!!!!
wengine mbona tunaambiwa wanalipwa mil 36.
ina maana ni mabosi wa raisi?
 
ndugu ukumbuke huyu mtu tunamuwezesha kwa kila kitu ili apate urahisi wa kazi zake hata za binafsi, ukitaja kiasi hicho kuwa ndo mshahara wake hautakuwa realistic.
Wewe unaweza fanya kazi bila kulipwa? Sio yeye tu anayewezeshwa, hata majeneral wa jeshi wamewezeshwa.
Kwa hiyo akitaka jenga nyumba ya mama yake na nyumba ya baba yake unamwezeshaje?
 
Sio mbaya maana amepunguza maneno maneno ya Akina Kabwela na Tundu Maneno. Hivi kwenye ule mpango ya kupunguza posho kwa wabunge Tundu Maneno alikuwa upande gani!!!!!
 
Wewe unaweza fanya kazi bila kulipwa? Sio yeye tu anayewezeshwa, hata majeneral wa jeshi wamewezeshwa.
Kwa hiyo akitaka jenga nyumba ya mama yake na nyumba ya baba yake unamwezeshaje?
Kuna watu huwa wanaamua kuwa upande wa ubishi bila sababu yoyote. Hata mtoto mdogo anayepewa huduma zote bado anahitaji uhuru wa kuwa na nguvu ya fedha. Kwangu mimi rais wa nchi lkama Tanzania hata kama atalipwa milioni 30 kwa mwezi ni reasonable kabisa.
 
Hawawezi kulitungia sheria; ni mpaka wabadili Katiba. Na mchakato wa kubadili Katiba sidhani kama utakuwa rahisi kivile kwa jambo moja isipokuwa kama wanataka kufanya kwa ujumla

..Raisi ni ccm.

..spika ccm.

..majority ya wabunge ni ccm.

..sasa Nani atawazuia hata kama wakiamua kubadili katiba?
 
Aya sawa!!!
Raisi analipwa kidogo kuliko wakurugenzi wa mashirika ya umma sawaa!!
Ila katika kubana matumizi kama vipi adake milioni mbili tu😉😉😉

Happy fools day
Kwa kazi yote anayoifanya kama kiongozi wa nchi,alipwe 2m au sasa mnataka kumfanya afisa mtendaji wa kijiji na sio raisi tena,tuanze basi na pensheni ya ''aliye jiuzuru''
 
Wewe unaweza fanya kazi bila kulipwa? Sio yeye tu anayewezeshwa, hata majeneral wa jeshi wamewezeshwa.
Kwa hiyo akitaka jenga nyumba ya mama yake na nyumba ya baba yake unamwezeshaje?
ndugu yangu ingawa mimi siyo mkatoliki niliwahi kusikia kitu kama hiki, naomba uchukulie kama mfano, mapadri wa kikatoliki hawalipwi mishahara ila husaidia sana familia zao!. Mimi nipo tayari kufanya kazi "bila malipo" kama ntapewa kila kitu cha kuniwezesha kuhishi na kunihakikishia maisha baada ya kustaafu hadi kufa kwangu. Neno bila malipo hapo juu nime liweka kwenye inverted comma kwani si sahii kusema silipwi wakati napewa kila kitu! na hicho kitu nitakacho pewa ndo ujira wenyewe!!!!, kwahiyo ndugu yangu mshahara wa rais ni jumla ya gharama zoote anazo gharamiwa na selekali kwa mwezi + na hizo miloni tisa na nusu.
 
Muvi yetu imefika epsode ya ngapi?

#Ngoma ikivuma sana mwisho hupasuka.
 
ndugu yangu ingawa mimi siyo mkatoliki niliwahi kusikia kitu kama hiki, naomba uchukulie kama mfano, mapadri wa kikatoliki hawalipwi mishahara ila husaidia sana familia zao!. Mimi nipo tayari kufanya kazi "bila malipo" kama ntapewa kila kitu cha kuniwezesha kuhishi na kunihakikishia maisha baada ya kustaafu hadi kufa kwangu. Neno bila malipo hapo juu nime liweka kwenye inverted comma kwani si sahii kusema silipwi wakati napewa kila kitu! na hicho kitu nitakacho pewa ndo ujira wenyewe!!!!, kwahiyo ndugu yangu mshahara wa rais ni jumla ya gharama zoote anazo gharamiwa na selekali kwa mwezi + na hizo miloni tisa na nusu.

.. William Lukuvi alidai gharama za kumtunza Raisi ni sawa na bajeti ya mikoa mitano.

..madai hayo aliyatoa wakati akipinga hoja ya serikali 3 ktk hotuba ili maarufu aliyoitoa kanisani.

...lazima sasa tupate ufafanuzi wa kina na uwazi kuhusu matumizi ya serikali, ikiwemo mishahara, posho, na marupurupu, ya watumishi wote wa serikali.
 
Back
Top Bottom