Rais Putin aamuru kikosi maalum cha Nyuklia kuwa katika tahadhari maalum "kiwango cha juu cha tahadhari"

Rais Putin aamuru kikosi maalum cha Nyuklia kuwa katika tahadhari maalum "kiwango cha juu cha tahadhari"

Putin alitoa Offer ya mazungumzo toka ijumaa tena kwa masharti. Na Ukraine ikakubali masharti hayo. Angekuwa na uwezo angekubali masharti hayo? Mbona kabla ya kuchapwa alikuwa akishupaza shingo kuwa watajiunga NATO lakini baada ya kuchapwa kakubali kutojiunga?

Sielewi una uhusiano gani na Putin kiasi cha kumtetea hivyo bila hata kutumia akili. Yaani unaamini Putin alitoa ofa ya kufanya mazungumuzo ya amani baada ya yeye mwenyewe kuwa ameshavamia na kuvunja amani hiyo? Hivi wewe unajua sababu ya Putin kuivamia Ukraine? Uvamizi huu umesababisha Ukraine itajiunga na NATO haraka sana; ilikuwa inacheleweshwa na sababu za rushwa, na Putin amechukia sana kwa rais wa sasa wa Ukraine kusifiwa kwa kukomesha rushwa, ambayo ndiyo ilikuwa kikwazo kikubwa. Unaona sasa hivi Sweden na Norway nazo zinajiunga na NATO, eti nazo anazitishia. Huyu jamaa kapungukiwa sana akili.

Mtu akikaa madarakani muda mrefu tena kwa mabavu, huwa hapati habari sahihi nje ya anavyotaka kusikia, na hilo ndilo tatizo lake. hata kwenye ule mkutano wako na wana usalama wake walikuwa wakitaka kumpinga ila wakamkubalia kwa shingo upande kwa vile hilo ndilo alilokuwa anataka kuskia, na limekuwa ni kosa kubwa sana.

 
Kwa hiyo watu wasikilize porojo zako au maelezo ya rais wa Ukraine aliyosema kuwa wapo tayari kutojiunga na NATO (baada ya kupokea kichapo cha mwizi)?


kumbe hata kiingereza hujui kwa hiyo unadakiza dakiza maneno tu. Kwenye hiyo video umesikia wapi hayo unayotetea
 
Hivi wewe unajua sababu ya Putin kuivamia Ukraine?
Sababu ya Putin kuivamia Ukraine anaifahamu Colonel Macgregor wa jeshi la Marekani (wewe Mmarekani wa Tandahimba huwezi kuelewa)

Colonel Macgregor, afisa mstaafu wa jeshi la Marekani anakujibu hivi Marekani ina nafasi ya kuepusha vita na Putin (Russia). Jambo la kwanza wanalopaswa kufanya Wamarekani ni kukiri na kukubaliana na nukta ya msingi ya Putin (Russia), ambayo serekali ya Russia imeiweka wazi kwa zaidi ya miaka 25 sasa. Nukta yenyewe ni kuwa Russia hawataki majeshi ya Marekani, mizinga ya Marekani, na majeshi ya NATO kwenye mpaka wake na Ukraine (Mashariki ya Ukraine kwenye majimbo yaliyotangazwa huru na Putin).

Colonel Douglas akaendelea kusema: Kiukweli kabisa hata sisi Wamarekani hatukuyataka majeshi ya Russia na mizinga yake ndani ya Cuba, Putin naye hataki mambo hayo mashariki mwa Ukraine. Lazima tukubali madai hayo. Tuache kujifanyisha kuwa madai hayo hayana maana (ni ya kipuuzi).
======



COL. DOUGLAS MACGREGOR: Let me just reiterate something. I, like you and millions of Americans, would prefer that the troops headed to Eastern Europe right now were headed to the Mexican border. But I’m also very concerned that we find a way to avoid a conflict with Russia. The first thing we have to do is acknowledge that Putin’s basic point, not just his point, the Russian government’s point, which they’ve made for 25 years, is valid. They don’t want U.S. forces and missiles and NATO troops immediately across the border in eastern Ukraine. Absolutely. We didn’t want them in Cuba, he doesn’t want them in eastern Ukraine. We should acknowledge that. Stop pretending it’s a nonissue. It is a major issue for them. Let’s acknowledge it and then let’s get down to business and tell them fine, our concern at this point is we don’t want you to proceed west towards the polish border over the Dnieper River in Ukraine.
 
kumbe hata kiingereza hujui kwa hiyo unadakiza dakiza maneno tu. Kwenye hiyo video umesikia wapi hayo unayot
Wewe utakuwa mzito sana kuelewa, hebu soma hapa (kama kingereza chapanda lakini)
 
Wewe utakuwa mzito sana kuelewa, hebu soma hapa (kama kingereza chapanda lakini)
Unarudia yale yale. Hilo la mazungumzo lilikuwapo siku nyingi sana kabla ya vita; siyo kuwa limekuja baada ya vita. Putin ndiye liyekuwa anajifanya yeye ataimaliza Ukraine kwa siku moja tu na hivyo kulikuwa hakuna haja ya maongezi tena, halafu leo anataka mazungumzo.
 
Unarudia yale yale. Hilo la mazungumzo lilikuwapo siku nyingi sana kabla ya vita; siyo kuwa limekuja baada ya vita. Putin ndiye liyekuwa anajifanya yeye ataimaliza Ukraine kwa siku moja tu na hivyo kulikuwa hakuna haja ya maongezi tena, halafu leo anataka mazungumzo.
Acha uzushi. Ukraine walishupaza shingo kuwa watajiunga NATO

Pia wakatiwa upepo na NATO kuwa Ukraine itapewa fursa hiyo (NATO wakijaribu kumchokonoa Putin)


Ila sasa hivi wamefunzwa na Putin kwa lugha ngumu, wamekubali kutojiunga.

 
View attachment 2133223

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameamuru jeshi la Urusi kuweka vikosi vyake vya nyuklia katika "tahadhari maalum" - kiwango cha juu cha tahadhari kwa Vikosi vya Kimkakati vya Kombora vya Urusi.

Akizungumza na maafisa wakuu wa kijeshi, akiwemo Waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu, alisema mataifa ya Magharibi yamechukua "hatua zisizo za kirafiki" kwa Urusi na kuweka "vikwazo visivyo halali".

Rais wa Urusi Vladmir Putin ameamuru usimamizi wa jeshi kuweka kikosi maalum cha nyuklia katika hali "maalum" ya tahadhari.

Hii ni baada ya kile ambacho Moscow inakiita "taarifa za uchokozi" za nchi za muungano wa Nato.
Source:BBC
huo mkwara tu hana lolote
 
Lete link ya maelezo hayo ya Putin ya kuimaliza Ukraine kwa siku 1 sio watia porojo zako tu.
Kwa nini alikataa mazungumzo na kuamua kuanzisha vita kama hakuwa na confidence ya kushinda haraka tu. Ukiangalia deployement plan yake ya kuizingira ukraine kutokea pande tatu, ni wazi alitegemea vita ya siku moja tu. Ndiyo maana akajikuta baada ya siku mbili vifaru havina mafuta, kwani hakutegemea kuvihitaji baada ya muda huo.
 
Kwa nini alikataa mazungumzo na kuamua kuanzisha vita kama hakuwa na confidence ya kushinda haraka tu. Ukiangalia deployement plan yake ya kuizingira ukraine kutokea pande tatu, ni wazi alitegemea vita ya siku moja tu. Ndiyo maana akajikuta baada ya siku mbili vifaru havina mafuta, kwani hakutegemea kuvihitaji baada ya muda huo.
Lete kwanza link ya maelezo (porojo zako) uloandika kuwa Putin aliahidi kuimaliza Ukraine kwa siku 1.

Usirukie vitu vingine kabla ya vile ulivyovitaja hujavithibitisha
 
Lete kwanza link ya maelezo (porojo zako) uloandika kuwa Putin aliahidi kuimaliza Ukraine kwa siku 1.

Usirukie vitu vingine kabla ya vile ulivyovitaja hujavithibitisha
Ndugu yangu, una moyo sana!

Nimegundua kitu kimoja tangu mgogoro wa Ukraine na Russia.

Watanzania wengi sana uwezo wao wa kuchambua mambo na kujenga hoja ni mdogo tena sana!

Aliyesema mtanzania mpe kichwa cha habari taarifa ya yaliyomo atajazilizia mwenyewe hakukosea.

Unajadili na watu ambao hawafuatilii taarifa za habari. Hawafuatilii wachambuzi wa masuala ya kimataifa wanazungimziaje huu mgogoro. Ni changamoto tupu. Yaani mtu anajibu tu yaliyomo kwenye kichwa chake halafu anaona kapatia na yupo safi tu. Nakuona unawawekea uthibitisho na bado watu wanabisha.

Nikupe heko bado unaendelea kuwaelimisha. Kwa sasa mimi nimeshanawa mikono.
 
Ndugu yangu, una moyo sana!

Nimegundua kitu kimoja tangu mgogoro wa Ukraine na Russia.

Watanzania wengi sana uwezo wao wa kuchambua mambo na kujenga hoja ni mdogo tena sana!

Aliyesema mtanzania mpe kichwa cha habari taarifa ya yaliyomo atajazilizia mwenyewe hakukosea.

Unajadili na watu ambao hawafuatilii taarifa za habari. Hawafuatilii wachambuzi wa masuala ya kimataifa wanazungimziaje huu mgogoro. Ni changamoto tupu. Yaani mtu anajibu tu yaliyomo kwenye kichwa chake halafu anaona kapatia na yupo safi tu. Nakuona unawawekea uthibitisho na bado watu wanabisha.

Nikupe heko bado unaendelea kuwaelimisha. Kwa sasa mimi nimeshanawa mikono.
Wajinga wawili mkipeana mikakati ya kijinga
 
Ameshindwa Vita kwa vioi??!! Watanzania a heni ushabiki usio na tija...hi ni siku ya nne ya Vita...Russia haijaingiza kwenye Vita hi main force yake...slichofanya ni kutanguliza special forums kwenye light vehicles...mavifsru yake Kama T 72 hajaingia kabisaa vitani...military strategists wa nchi za magharibi bado hazijagundua military strategies za Russia...hawajua Russia anakusudia kufanya Nini...kinachoendelea kwenye BBC, aljazeera, na kadhalika ni propaganda tu kwa sehdmu kubwa
Hawajagundua ila wewe umegundua sio?
Sasa hizo silaha za nyuklia zinawekwa tayari kwa ajili gani kama hata vita ni rashia rashia tu?
 
Acha uongo na porojo, rais Putin alitoa offa ya mazungumzo toka siku ya ijumaa tena kwa masharti mawili ya Ukraine kutojiunga NATO na kutoweka silaha za NATO/US kwenye ardhi ya Ukraine (ambavyo Ukrainealishavikubali). Na taarifa hiyo tumeipost hapa jf

Btw: Vita yapiganwa ktk ardhi ya Ukraine, Putin keshaharibu miundombinu mbalimbali ya Ukraine, malaki ya waUkraine wamekuwa wakimbizi, halafu waMarekani wa Tandale waona kuwa ati mambo yapo kama yalivyokuwa mwezi jana huko Ukraine. Kwa kifupi kwenye vita hii Ukraine kwa namna yoyote yumo kwenye hasara, huzuni, na majuto

Kwani kabla ya vita si kulikuwa na mazungumzo? Si yeye ndiye aliyeacha mazungumzo na kufanya uvamizi?
 
Back
Top Bottom