Rais Samia aagiza waliokuwa wanaishi Bonde la Mto Msimbazi kinyume na sheria kulipwa Tsh. Milioni 4 kila mmoja

Rais Samia aagiza waliokuwa wanaishi Bonde la Mto Msimbazi kinyume na sheria kulipwa Tsh. Milioni 4 kila mmoja

Attachments

  • 20231116_203111.jpg
    20231116_203111.jpg
    227.1 KB · Views: 5
Hiyo milioni nne na kazi za uyaya hakuna tofauti.

Awamu hii raia wanadharaulika mno.
 
Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa amesema kuwa Serikali itaanza kuwalipa wakazi wa Bonde la Mto Msimbazi Tsh. Mil 4 kila mmoja kama sehemu ya fidia ili wahame eneo hilo. Malipo haya yataanza kufanyika kuanzia Novemba 16, 2023.

===


Hisia mchanganyiko za wakazi wa bonde la Mto Msimbazi kufuatia tamko la Serikali kuwa watalipwa fidia ya ardhi ya Sh4 milioni kwa kila mwenye eneo, imeibuka huku wengine wakiunga mkono uamuzi huo, na wengine wakiupinga.

Awali kulikuwa na malalamiko ya wakazi hao baada ya kuonekana kuwa watafidiwa nyumba zao na si vinginevyo. Kassim Said amehoji iweje wananchi wa Loliondo wao walilipwa vizuri na kujengewa hadi nyumba lakini wao wanaokaa mjini wanapewa kiasi hicho kidogo cha fedha?

"Kwa mfano mimi nyumba yangu ya vyumba vitatu nimelipwa Sh11 milioni nikichanganya na hiyo Sh4 milioni ina maana nina Sh15 milioni, niambie naweza kujenga nyumba ya kiwango hicho hapa mjini? Ngoja tumwachie Mungu yeye ndio anajua," amesema Said.

Lakini hali ni tofauti kwa Siasa Mtambo, ambaye ameridhishwa na uamuzi huo, kwani kwa muda wa miaka 30 amekuwa akiishi kwa tabu katika eneo hilo kutokana na ukweli kuwa hakuwa na uwezo wa kwenda kujenga sehemu nyingine, pengine kwa hicho kidogo walichopewa ataweza hilo kulifanya.

Aisha Sharif mmoja wa wananchi waliokataa fidia kutokana na kutoridhishwa na tathimini, amesema kilichomfurahisha ni kitendo cha Waziri huyo kuahidi kuwasikiliza wote waliokataa pendekezo hilo.

"Hao waliokubali waachwe walipwe kwa kuwa kila mtu anajua thamani ya nyumba yake wengine kuliko tulipwe hiyo hela ni bora tuendelee kubaki hapa mjini," amesema Aisha.

Haya yote yanajiri baada Waziri wa Tamisemi, Mohammed Mchengerwa alipokutana na wananchi hao leo Jumatano Novemba 15, 2023 katika viwanja vya jangwani jijini humo, na kutangaza kuwa kesho (Alhamisi) Serikali itaanza kulipa fidia ya Sh4 milioni kwa kila mwenye ardhi itaanza kulipwa kesho.

Kimsingi, wananchi hao walikuwa na malalamiko wakitaka aina mbili za fidia kufanyika, ile ya nyumba pamoja na hiyo ya ardhi, jambo ambalo awali Serikali ilikubali kuwafidia nyumba pekee.

"Tulisikia malalamiko yenu kupitia nyie wenyewe, viongozi wenu akiwemo Mkuu wa Mkoa, Madiwani na Wabunge, nami nikalifikisha kwa Rais Samia Suluhu Hassan na kwa kuwapenda jana ameridhia kila mwananchi anayepisha mradi huu alipwe Sh4 milioni kama kifuta jasho kwa ardhi aliyoimiliki.

"Kwani kama mlivyosikia wataalam wetu hili walisema ni eneo la ardhi owevu hivyo kisheria halikupaswa kulipwa fidia kwa kuwa sio salama kwa makazi, lakini kwa huruma ya mama amemua mlipwe hiyo Sh4 mlioni,” amesema Mchengerwa.

Sambamba na hilo la ulipaji fidia hiyo ya ardhi ambayo kimsingi ni tofauti ile fidia ya jengo, Waziri huyo aliagiza pia Mradi wa uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP), kuanza mara moja ujenzi wa mradi huo huku malipo ya fidia yakiendelea ili kupunguza adha ya mafuriko katika eneo hilo yanayoathiri shuguli za kila siku za wananchi.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila alisema anachojua mkoa huo hauna mafuriko isipokuwa watu ndio wameziba njia zinazopitisha maji kwa kujenga na kuishi maeneo ambayo maji yanapaswa kupita.

Chanzo: Mwananchi
Hapa kuna upigaji unaenda kutokea.
 
Lineup tayari kupata pesa

View: https://www.instagram.com/p/CztYIWjvScj/?igshid=MTc4MmM1YmI2Ng==

Amewahurumia kama binadamu ila wangekutana na mtu kama Jiwe wangeisoma namba 😂😂

Jiwe angewakurupusha tu, mbiombio, aliselema alija, "tulisha waambia kitambo maeneo haya ni ya hatari na serekali yenu ilishakutengeeni maeneo pale mabwepande matokeo yake mkayauza, sasa ondokeni hakuna cha lelemama, hatuwezi kuongea na watu ambao pengine ni wakorofi, nakupeni siku 3,muwe mmeondoka!
 
Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa amesema kuwa Serikali itaanza kuwalipa wakazi wa Bonde la Mto Msimbazi Tsh. Mil 4 kila mmoja kama sehemu ya fidia ili wahame eneo hilo. Malipo haya yataanza kufanyika kuanzia Novemba 16, 2023.

===


Hisia mchanganyiko za wakazi wa bonde la Mto Msimbazi kufuatia tamko la Serikali kuwa watalipwa fidia ya ardhi ya Sh4 milioni kwa kila mwenye eneo, imeibuka huku wengine wakiunga mkono uamuzi huo, na wengine wakiupinga.

Awali kulikuwa na malalamiko ya wakazi hao baada ya kuonekana kuwa watafidiwa nyumba zao na si vinginevyo. Kassim Said amehoji iweje wananchi wa Loliondo wao walilipwa vizuri na kujengewa hadi nyumba lakini wao wanaokaa mjini wanapewa kiasi hicho kidogo cha fedha?

"Kwa mfano mimi nyumba yangu ya vyumba vitatu nimelipwa Sh11 milioni nikichanganya na hiyo Sh4 milioni ina maana nina Sh15 milioni, niambie naweza kujenga nyumba ya kiwango hicho hapa mjini? Ngoja tumwachie Mungu yeye ndio anajua," amesema Said.

Lakini hali ni tofauti kwa Siasa Mtambo, ambaye ameridhishwa na uamuzi huo, kwani kwa muda wa miaka 30 amekuwa akiishi kwa tabu katika eneo hilo kutokana na ukweli kuwa hakuwa na uwezo wa kwenda kujenga sehemu nyingine, pengine kwa hicho kidogo walichopewa ataweza hilo kulifanya.

Aisha Sharif mmoja wa wananchi waliokataa fidia kutokana na kutoridhishwa na tathimini, amesema kilichomfurahisha ni kitendo cha Waziri huyo kuahidi kuwasikiliza wote waliokataa pendekezo hilo.

"Hao waliokubali waachwe walipwe kwa kuwa kila mtu anajua thamani ya nyumba yake wengine kuliko tulipwe hiyo hela ni bora tuendelee kubaki hapa mjini," amesema Aisha.

Haya yote yanajiri baada Waziri wa Tamisemi, Mohammed Mchengerwa alipokutana na wananchi hao leo Jumatano Novemba 15, 2023 katika viwanja vya jangwani jijini humo, na kutangaza kuwa kesho (Alhamisi) Serikali itaanza kulipa fidia ya Sh4 milioni kwa kila mwenye ardhi itaanza kulipwa kesho.

Kimsingi, wananchi hao walikuwa na malalamiko wakitaka aina mbili za fidia kufanyika, ile ya nyumba pamoja na hiyo ya ardhi, jambo ambalo awali Serikali ilikubali kuwafidia nyumba pekee.

"Tulisikia malalamiko yenu kupitia nyie wenyewe, viongozi wenu akiwemo Mkuu wa Mkoa, Madiwani na Wabunge, nami nikalifikisha kwa Rais Samia Suluhu Hassan na kwa kuwapenda jana ameridhia kila mwananchi anayepisha mradi huu alipwe Sh4 milioni kama kifuta jasho kwa ardhi aliyoimiliki.

"Kwani kama mlivyosikia wataalam wetu hili walisema ni eneo la ardhi owevu hivyo kisheria halikupaswa kulipwa fidia kwa kuwa sio salama kwa makazi, lakini kwa huruma ya mama amemua mlipwe hiyo Sh4 mlioni,” amesema Mchengerwa.

Sambamba na hilo la ulipaji fidia hiyo ya ardhi ambayo kimsingi ni tofauti ile fidia ya jengo, Waziri huyo aliagiza pia Mradi wa uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP), kuanza mara moja ujenzi wa mradi huo huku malipo ya fidia yakiendelea ili kupunguza adha ya mafuriko katika eneo hilo yanayoathiri shuguli za kila siku za wananchi.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila alisema anachojua mkoa huo hauna mafuriko isipokuwa watu ndio wameziba njia zinazopitisha maji kwa kujenga na kuishi maeneo ambayo maji yanapaswa kupita.

Chanzo: Mwananchi
Mbona mnapenda kutufanya sisi ng'ombe nyie sio kwamba raisi ameamua watu walipwe mil 4!!?? World Bank ambao ni miongoni mwa watoa fedha za mradi wameagiza watu walipwe fidia no matter what. Hv hii dunia ya information zote bado mnathubutu kutudanganya!!?
 
Mbona mnapenda kutufanya sisi ng'ombe nyie sio kwamba raisi ameamua watu walipwe mil 4!!?? World Bank ambao ni miongoni mwa watoa fedha za mradi wameagiza watu walipwe fidia no matter what. Hv hii dunia ya information zote bado mnathubutu kutudanganya!!?
Waulizwe hao world Bank tujue mbivu na mbichi !!
 
Upigaji na uchaguzi hamna suluhisho la kudumu hapo ni kucheza danadana tu
 
Ila bora Samia, marehemu bichwa angewafukuza kwa kutumia jeshi na hata mia wasingepata
Kwani mbona miaka yote ya utawala wake mbona haliwaacha?hata hivyo hiyo milioni 4 nisawa na bure maana hauwezi pata kiwanja Cha milioni 4 hapa Dar.
 
Anuani zao hao World Bank zipo kwenye Google ni bora wajulishwe kinachoendelea labda itasaidia !
Tutawafikishia taarifa haiwezekani baadhi ya watu wana hati halali alafu umlipe mtu milioni 4 eneo lipo karibu na lami limezungukwa na maduka fidia ya ardhi umlipe mtu milioni 4!!???huo ni uonevu wa mchana kweupe. Serekali hii madeni ya wazungu mabilioni wanalipa haraka haraka fidia ya wanachi wake inawalipa kiduchu tena baada ya mlolongo mrefu!?
 
Kiwanja Dar ni shs ngapi? yeye akipewa 4M anaweza kujenga nyumba ya kuishi na kununu kiwanja Dar? wakati hao wananchi wana nunua na kujenga serikali ya CCM ilikuwa wapi? ni kutafuta sifa za hovyo bila sababu za msingi.
Wengi walivamia... Hivyo hata kulipwa fidia ya ardhi ya 4M + mengineyo ni fadhila kubwa!
 
Mh, hii nchi ngumu sana, ili uweze kuishi ni lazima ujizime data a.k.a usitumie akili! Mpaka leo kimya! Hayo majibu yao sasa!

Wakazi wa Bonde la Mto Msimbazi Kulipwa Fidia Kupisha Uendelezaji wa Bonde hilo​


Hayo yamejiri leo Novemba 15, 2023 wakati Waziri wa Nchi Ofisi Rais TAMISEMI Mhe Mohamed Mchengerwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila alipokutana na wakazi hao katika viunga vya Ofisi za Young African Ilala Jijini Dar es Salaam

Akiongea na Wananchi hao Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI ametoa Kauli ya Serikali ya kuwalipa wakazi hao kuanzia kesho Novemba 16, 2023 ambapo hadi sasa asilimia zaidi ya 92 wameshahakikiwa wanasubiri kulipwa.


Source: Mwanzo › new › wakazi-wa


2400 kulipwa fidia bonde la Msimbazi kesho​


15 Nov 2023 — Amesema “leo hii nimekuja hapa kutoa Tamko ya hatua ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi uanze mara moja kuanzia sasa na hii iende sambamba ...


Source: Timesmajira › 2400-kuli..
 
Huko Kipunguni wametapeliwa na Waziri kabisa yaani ! Hawaamini Macho yao ! usicheze na ccm wewe !
 
Back
Top Bottom