Rais Samia aajiri vijana 18,449 serikalini kukuza ufanisi wa kazi

Rais Samia aajiri vijana 18,449 serikalini kukuza ufanisi wa kazi

Hapo wamejumlisha na zile za sensa zilizoisha.

Porojo nyingi sana.

Hamna kitu wanaweza zaidi ya kuwapa Yanga ndege na milioni 5 kwa kila goli.
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameendeleza juhudi zake za kuwawezesha vijana na kuboresha ufanisi wa kazi katika taasisi za serikali. Ndani ya miezi sita ya kwanza ya mwaka 2023,serikali imeajili vijana 18,449.

Idadi hiyo inajumuisha walimu wapatao 13,130 ambao wamepata nafasi za ajira katika sekta ya elimu. Aidha, kada ya Afya imepokea watumishi wapya 5,319, wanaosaidia kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Licha ya mipango mbalimbali ya kuwawezesha vijana kujiajiri, Rais Samia ameendelea kutoa vibali vya ajira kwa taasisi za serikali zenye uhitaji. Hatua hii inalenga kutoa fursa kwa vijana wenye ujuzi na talanta, wakati huo huo kukuza ufanisi wa kazi katika taasisi hizo.

Rais Samia ameonyesha dhamira yake ya kusaidia vijana kujenga kazi na kuchangia katika maendeleo ya nchi. Utekelezaji wa sera hii ya ajira kwa vijana unaonyesha nia ya serikali ya kujenga taifa lenye nguvu kazi ya vijana wenye ujuzi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi.

Mafanikio haya yanathibitisha jitihada za serikali katika kutoa fursa za ajira kwa vijana na kuboresha sekta muhimu kama elimu na afya. Wananchi wana matumaini kuwa hatua hii italeta mabadiliko chanya katika utoaji wa huduma na kukuza ustawi wa taifa.
Tafuta kazi ya kufanya. Hii imekushinda, me nashauri wale wanaopigaga makelele na mayowe wakitafuta/kuwataka watu waandamane wawatafute majobless. Mapema tu kinaeleweka mbona, watu wamechoka mtaani hapakaliki
 
sasa angekuwa kma mama hivi miaka yake mitano bwam yule Vijaja wengi wengekuwa vizur msongamano ungepungua kuliko uliopo saivi, Jiwe alisababisha umasikini endelefu kidogo kwa vijana wa taifa hili,
Siyo kidogo, ni sana. Jiwe afe tena huko aliko.
 
18,000 baada ya miaka Saba halafu mnajisifia?
Kwani kwa kipindi Cha dark days Hadi Leo Kuna graduate wangapi?
 
Kunakitu naona hakikosawa alitoa kibali lini kuajiri hidadi hiyo ?naona idadi nindogo ya walioajiriwa kulikotulivyo tangaziwa ufafanuzi hapa unatakiwa
 
Ungejua walioomba nafasi izo walikua zaidi ya laki na sabini na waliopata ni karibu ishirini elfu tu usingeandika huu ushubwada hapa
 
Hao vijana hakuna mwenye ujuzi wa kuendesha Bandari yetu ?
Huko vyuoni Siku hizi vijana wanasomeshwa fani gani ?

Maana naona wengi ni Walimu wa shule za Msingi tu.
 
Vijana wanatakiwa wapewe nchi siyo huko kwenye vitu vingine sijui ualimu ,hiyo ni danganya toto
 
Back
Top Bottom