Steven Joel Ntamusano
JF-Expert Member
- Jun 17, 2023
- 5,203
- 3,913
Siku za uhuru kuna marudio ya matukio yale yale ya kila mwaka, wanapoamua kuahirisha wanakuwa wameshapima hasara zozote (kama zipo) zinazoweza kutokea baada ya kufanya hayo maamuzi...Ni taifa la ajabu lisiloenzi uhuru wake.
Siku za uhuru kuna marudio ya matukio yale yale ya kila mwaka, wanapoamua kuahirisha wanakuwa wameshapima hasara zozote (kama zipo) zinazoweza kutokea baada ya kufanya hayo maamuzi.
Ni masuala yale yale ya makomandoo kuvunja mawe vifuani mwao na zile show za kutua na kamba kutoka kwenye helikopta.
Wajanja wanapiga pesa kupitia bajeti zinazotengwa kwa ajili ya shughuli zote za halaiki za siku ya uhuru.
Najua umeamua kupinga kwa sababu ni maamuzi ya Rais Samia ambaye upo uwezekano haumpendi, kwa hiyo unapinga sio kwa sababu unaipenda sana siku ya uhuru bali ni siasa tu za chuki.
Ndio Rais keshaamua, tujadili mada nyingine za muhimu zaidi...i'm on the record kupinga maonyesho ya vijana wetu kupasua matofali vichwani au miilini mwao.
kwanini haka kabiinti kanataka kufuta historia ya Tanganyika huku kanatapanya Mali za Tanganyika kama kamelewa mnazi?Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kufuta sherehe za miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara na badala yake fedha zilizotengwa zitumike kusaidia huduma za kijamii.
Amesema fedha zilizotengwa katika kila taasisi kwa ajili ya maadhimisho hayo zielekezwe katika kutoa huduma za kijamii, huku akieleleza kila mkoa uhakikishe wilaya zake zinafanya shughuli za kijamii, ikiwemo upandaji miti, usafi wa mazingira kwenye maeneo ya kijamii kama masoko, hospitali, kumbi za wazee na wenye mahitaji maalumu.
Hayo yameelezwa leo Jumatano, Desemba 4, 2024 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kikao kazi cha mawaziri kilichofanyika ukumbi wa Hazina jijini Dodoma. "Sherehe za mwaka huu hazitakuwa na gwaride na shughuli nyingine za kitaifa".
Amesema Serikali inatoa wito kwa wananchi kushiriki katika shughuli hizo, ili kujivunia sifa za kipekee ambazo zimetokana na Uhuru wetu.
"Ninatoa rai kwa wakuu wote wa mikoa ya Tanzania Bara, kuzingatia na kufuata ipasavyo maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha maadhimisho haya yanafanyika kwa ufanisi kwa lengo la kuuenzi Uhuru wetu."
View attachment 3168740
Sherehe za uhuru wa Tanganyika zinaamuliwa vipi jinsi ya kufanyika na mtu asiye Mtanganyika?Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kufuta sherehe za miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara na badala yake fedha zilizotengwa zitumike kusaidia huduma za kijamii.
Amesema fedha zilizotengwa katika kila taasisi kwa ajili ya maadhimisho hayo zielekezwe katika kutoa huduma za kijamii, huku akieleleza kila mkoa uhakikishe wilaya zake zinafanya shughuli za kijamii, ikiwemo upandaji miti, usafi wa mazingira kwenye maeneo ya kijamii kama masoko, hospitali, kumbi za wazee na wenye mahitaji maalumu.
Hayo yameelezwa leo Jumatano, Desemba 4, 2024 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kikao kazi cha mawaziri kilichofanyika ukumbi wa Hazina jijini Dodoma. "Sherehe za mwaka huu hazitakuwa na gwaride na shughuli nyingine za kitaifa".
Amesema Serikali inatoa wito kwa wananchi kushiriki katika shughuli hizo, ili kujivunia sifa za kipekee ambazo zimetokana na Uhuru wetu.
"Ninatoa rai kwa wakuu wote wa mikoa ya Tanzania Bara, kuzingatia na kufuata ipasavyo maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha maadhimisho haya yanafanyika kwa ufanisi kwa lengo la kuuenzi Uhuru wetu."
View attachment 3168740
Hiyo ndiyo inayomuhusu, ya Tanganyika haimuhusu kabisa.Aondoe na ile ya mapinduzi Zanzibar
At least yule dikteta alikuwa chembechembe za Utanganyika wa kuchovya.Huu upuuzi uliusema mwaka 2015 Desemba wakati hayati JPM alipofuta sherehe za uhuru na wote nchi nzima tukafanya usafi?.
Hivi Tanzania bara ilipata uhuru lini
Inatia hasira kwa kweli sijui kizazi kijacho kitajifunza nnYaani nashindwa kuelewa kwanini kusema uhuru wa Tanganyika unaonekana kama mhaini unataka kupindua nchi sasa viongozi wakubwa wa juu kama hawa wanaogopa kusema Tanganyika then wanasema uhuru wa Tanzania bara,sielewi kwanini wanataka kulifuta jina la Tanganyika kwenye history ya hii nchi ya Muungano na kwa masilahi ya nani.
Samia anafanya mengi sana huku Tanganyika kuliko huko kwao Zanzibar, cha muhimu kwako ni kutafuta habari zake nyingi ambazo nina uhakika huzifahamu ndio maana unakimbilia kwenye hoja ya kibaguzi ya utanganyika na uzanzibari.At least yule dikteta alikuwa chembechembe za Utanganyika wa kuchovya.
Waulize tu Tan road madaraja sasa hivi mvua zinanyesha yanavunjika, kama wana hata senti kuyajengea. Pili tunaposema anafanya makubwa Tanganyika, je mkusanyaji mapato mkubwa ni nani kati ya Tanganyika na Zanzibar ? Kwa hiyo ulitaka Tanganyika azalishe na pesa yake atumie mwingine, japo hata hivyo ndivyo inafavyofanyika sasa. Tatu, pesa hata sh 1 ya Zanzibar wanazokusanya inavuka kuja Tanganyika kufanya chochote au ni kinyume chake ?Samia anafanya mengi sana huku Tanganyika kuliko huko kwao Zanzibar, cha muhimu kwako ni kutafuta habari zake nyingi ambazo nina uhakika huzifahamu ndio maana unakimbilia kwenye hoja ya kibaguzi ya utanganyika na uzanzibari.
Wakati Rais wa Kenya aliposema majuzi kwamba Tanzania kwa sasa inaizidi Kenya katika mchango wake kiuchumi alikuwa anaongelea Tanzania Bara au Visiwani?.Waulize tu Tan road madaraja sasa hivi mvua zinanyesha yanavunjika, kama wana hata senti kuyajengea. Pili tunaposema anafanya makubwa Tanganyika, je mkusanyaji mapato mkubwa ni nani kati ya Tanganyika na Zanzibar ? Kwa hiyo ulitaka Tanganyika azalishe na pesa yake atumie mwingine, japo hata hivyo ndivyo inafavyofanyika sasa. Tatu, pesa hata sh 1 ya Zanzibar wanazokusanya inavuka kuja Tanganyika kufanya chochote au ni kinyume chake ?
Aliyetaja Zanzibar ni wewe mkuu. Nimejibu kukuonyesha nani anamnufaisha nani. Usingetaja hiyo Zanzibar au Tanganyika Wala nisingejibu kuvihusu. Yako mengi sana tunyamaze tu ndugu.Wakati Rais wa Kenya aliposema majuzi kwamba Tanzania kwa sasa inaizidi Kenya katika mchango wake kiuchumi alikuwa anaongelea Tanzania Bara au Visiwani?.
Samia anaiboresha hiyo TRA ili iweze kukusanya zaidi ya sasa, Samia kapigana mpaka wakulima wa korosho wamepata bei kubwa kuliko waliyowahi kuipata tangu uhuru wa nchi.
Samia anaimalizia reli ya SGR ili iwe na uwezo sawa na ile ya Lobito kule Angola, anafanya mengi sana na hii hulka ya kuuongelea uzanzibari na utanganyika ni ujinga wetu tu humu jukwaani.
Ni mbinu ya kijinga ya kuja na malalamiko mengine baada ya kushindwa kuyathamini mema anayoyapigania kwa faida ya Tanzania nzima.
Umevamia maongezi haya katikati, kuna mtu nilimjibu kuhusu huo ubaguzi wake.Aliyetaja Zanzibar ni wewe mkuu. Nimejibu kukuonyesha nani anamnufaisha nani. Usingetaja hiyo Zanzibar au Tanganyika Wala nisingejibu kuvihusu. Yako mengi sana tunyamaze tu ndugu.
Hii inatakiwa kamuliwa na waziri mkuu.Tatizo Kassimu haaminiki na nguvu hanaHiyo ndiyo inayomuhusu, ya Tanganyika haimuhusu kabisa.