Rais Samia afuta sherehe za Uhuru, aagiza fedha zitumike kusaidia huduma za kijamii

Rais Samia afuta sherehe za Uhuru, aagiza fedha zitumike kusaidia huduma za kijamii

Sherehe kama hizi za uhuru,muungano angalao kila baada ya miaka mitano.
Ule moto tunaokimbiza kila mwaka upumzishwe makumbusho ya taifa.

Tunachoma fedha nyingi kukimbiza moto eti unaleta maendeleo.Hizo nchi tunazozipigia magoti kila siku kwa habari ya misaada huwa wanakimbiza moto?
 
Tangu awamu iiyopita wanazifuta tu kila mwaka mbona za mapinduzi ya zanzibar hazijawahi kufutwa.Tanganyia ndo basi tena
 
Tukipata Katiba Mpya itakuwa ndio siku ya uhuru wetu. Tutajibamba
Acha wajipe raha za muda karibu tutaelewana
 
Hahahah 😆 ngoja kwanza ncheke tu.
Mbona kachelewa.
All the best
 
vipi asha achakugawa mil 700 kwa kila gori
Hili nalo langoli aachane nalo. Halina faida.
Tutafute mfumo bora kiasi cha kwamba pale timu youote inawakilisha nchi katika mchezo wowote ule serikali inagharamia flights na accomodation. Timu husika ilipe mishahara na hizo bonus za magoli.
 
Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kufuta sherehe za miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara na badala yake fedha zilizotengwa zitumike kusaidia huduma za kijamii.

Amesema fedha zilizotengwa katika kila taasisi kwa ajili ya maadhimisho hayo zielekezwe katika kutoa huduma za kijamii, huku akieleleza kila mkoa uhakikishe wilaya zake zinafanya shughuli za kijamii, ikiwemo upandaji miti, usafi wa mazingira kwenye maeneo ya kijamii kama masoko, hospitali, kumbi za wazee na wenye mahitaji maalumu.

Hayo yameelezwa leo Jumatano, Desemba 4, 2024 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kikao kazi cha mawaziri kilichofanyika ukumbi wa Hazina jijini Dodoma. "Sherehe za mwaka huu hazitakuwa na gwaride na shughuli nyingine za kitaifa".

Amesema Serikali inatoa wito kwa wananchi kushiriki katika shughuli hizo, ili kujivunia sifa za kipekee ambazo zimetokana na Uhuru wetu.

"Ninatoa rai kwa wakuu wote wa mikoa ya Tanzania Bara, kuzingatia na kufuata ipasavyo maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha maadhimisho haya yanafanyika kwa ufanisi kwa lengo la kuuenzi Uhuru wetu."
View attachment 3168740
Mwamba jiwe
 
Which???😀😀naomba nifungue kichwa kwasababu bajeti ya mwaka si IPO inagusa resources
Sasa hapo mwanawane sii kuna pa diem so watu wanasafirisha vimada wazee wa bolt boda boda kama sie hapa tunafaidika ujue.
Wazazi wa vimada nao wanatumiwa japo tujisenti tuwili tutatu.
 
Sasa hapo mwanawane sii kuna pa diem so watu wanasafirisha vimada wazee wa bolt boda boda kama sie hapa tunafaidika ujue.
Wazazi wa vimada nao wanatumiwa japo tujisenti tuwili tutatu.
Daah haya mkuu,naona resources ni nyingi
 
Sawa hizo hela zifanye hicho kilichokusudiwa,sio ziingizwe kwenye mahesabu mengine wajanja wazipige...
Na zitapigwa haswa!
Alitakiwa aseme Jambo lenye kutathminika kwa macho
Kama ujenzi jengo au barabara
Utengenezaji wa vifaa eg madawati, meza, vitanda n.k
 
IGP atakula wapi?
Askari walikuwa wanasota,walaji ni huko juu
 
Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kufuta sherehe za miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara na badala yake fedha zilizotengwa zitumike kusaidia huduma za kijamii.

Amesema fedha zilizotengwa katika kila taasisi kwa ajili ya maadhimisho hayo zielekezwe katika kutoa huduma za kijamii, huku akieleleza kila mkoa uhakikishe wilaya zake zinafanya shughuli za kijamii, ikiwemo upandaji miti, usafi wa mazingira kwenye maeneo ya kijamii kama masoko, hospitali, kumbi za wazee na wenye mahitaji maalumu.

Hayo yameelezwa leo Jumatano, Desemba 4, 2024 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kikao kazi cha mawaziri kilichofanyika ukumbi wa Hazina jijini Dodoma. "Sherehe za mwaka huu hazitakuwa na gwaride na shughuli nyingine za kitaifa".

Amesema Serikali inatoa wito kwa wananchi kushiriki katika shughuli hizo, ili kujivunia sifa za kipekee ambazo zimetokana na Uhuru wetu.

"Ninatoa rai kwa wakuu wote wa mikoa ya Tanzania Bara, kuzingatia na kufuata ipasavyo maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha maadhimisho haya yanafanyika kwa ufanisi kwa lengo la kuuenzi Uhuru wetu."
View attachment 3168740
Hivi amefuta au ameelekeza namna tofauti ya kusherehekea tofauti na ile iliyozoeleka ya magwaride?
Ila Kiswahili kigumu sana.
 
Back
Top Bottom