Rais Samia ahutubia taifa leo Agosti 22, 2022. Ametoa wito na kuwasihi Watanzania wote kujitokeza kuhesabiwa

Rais Samia ahutubia taifa leo Agosti 22, 2022. Ametoa wito na kuwasihi Watanzania wote kujitokeza kuhesabiwa

Huyu mama ni mkatili sana,Itakuwa anmsokiliza yule makamu wake anayeongea Kama ameweka mkaa wa moto mdomoni.
Mama yetu mh Rais Ni kiongozi mwenye huruma na upendo mkubwa Sana kwetu watanzania, ndio maana unaona akihangaika huku na kule kutatua kero za wananchi, ndio maana unaona akifanya juhudi za kusogezwa huduma muhimu karibu na wananchi, ndio maana unaona akifikia hatua ya kutoa Ruzuku ili kumsaidia mwananchi asielemewe na mzigo kichwani

Ndio maana kila sent inayopatikana anaipeleka kupunguza au kumaliza kero kwa wananchi, ndio maana unaona akifuta ada na kuweka Elimu bure Hadi kidato Cha sita ili hata watoto wa wananchi wanyonge wapate Elimu sawa na wale watokao katika familia zenye kipato kikubwa

Ndio maana unaona akiendelea kuboresha huduma mbalimbali zinazogusa maisha ya mwananchi, ndio maana unaona akiwasihi wasaidizi wake kuwa wanyenyekevu na wenye upendo kwa wananchi hasa wanyonge

Ndio maana unaona Hataki mtu yoyote Yule aonewe au kudhulumiwa haki yake, ndio maana unaona akifuta kesi za kisiasa ili watu walejee kwenye familia zao Hataki kuongoza nchi ambayo Kuna familia zinakesha usiku kucha zikilia machozi kwa kuwa Kuna mpendwa wao kafungwa kwa kuonewa
 
Hakuna sheria inayomlinda huyo raia ,yaani hakuna privacy kama kuna mtu anayo naomba aweke hapa
 
We dogo acha ujinga. Usidhani humu kila mtu mtoto mwenzako.

Mode fungieni hawa watoto. Huyu tangu asubuhi anatuma vitu vya ajabu tu
Wote ni Maboya kasoro wasio na vyama. Kwani CCM wamefanya nini? Wapinzani wamefanya nini?
 
Rais Samia wa JMT atalihutubia Taifa saa 3 00 usiku huu

Usikose

Chanzo: ITV

Updates;

Rais Samia amewaomba watanzania wote watoe ushirikiano kwa makarani wa Sensa katika zoezi litakaloanza das 6:00 usiku huu
Hiyo sio hotuba ni tangazo tu.

Hatuna rais wa kuhutubia taifa ilikuwaga Mkapa tu
 
Mama yetu mh Rais Ni kiongozi mwenye huruma na upendo mkubwa Sana kwetu watanzania, ndio maana unaona akihangaika huku na kule kutatua kero za wananchi, ndio maana unaona akifanya juhudi za kusogezwa huduma muhimu karibu na wananchi, ndio maana unaona akifikia hatua ya kutoa Ruzuku ili kumsaidia mwananchi asielemewe na mzigo kichwani

Ndio maana kila sent inayopatikana anaipeleka kupunguza au kumaliza kero kwa wananchi, ndio maana unaona akifuta ada na kuweka Elimu bure Hadi kidato Cha sita ili hata watoto wa wananchi wanyonge wapate Elimu sawa na wale watokao katika familia zenye kipato kikubwa

Ndio maana unaona akiendelea kuboresha huduma mbalimbali zinazogusa maisha ya mwananchi, ndio maana unaona akiwasihi wasaidizi wake kuwa wanyenyekevu na wenye upendo kwa wananchi hasa wanyonge

Ndio maana unaona Hataki mtu yoyote Yule aonewe au kudhulumiwa haki yake, ndio maana unaona akifuta kesi za kisiasa ili watu walejee kwenye familia zao Hataki kuongoza nchi ambayo Kuna familia zinakesha usiku kucha zikilia machozi kwa kuwa Kuna mpendwa wao kafungwa kwa kuonewa
Nani amekwambia Watanzania tunataka huruma?

Tunataka rais wa kutimiza majukumu yake kama mkuu wa nchi.

Atuhurumie kwasababu gani?

Tunalipa kodi tunataka return basi.
 
Hili la sensa mkawape ushirikiano kina ngoswe wote ~ alisikika malkia wa nyuki mmiliki wa asali
 
Nani amekwambia Watanzania tunataka huruma?

Tunataka rais wa kutimiza majukumu yake kama mkuu wa nchi.

Atuhurumie kwasababu gani?

Tunalipa kodi tunataka return basi.
Ndio hayo majukumu mh Rais wetu Anaya tekeleza kwa weledi mkubwa Sanaa, mh Rais wetu anatanguliza mbele maslahi ya Taifa, ndio maana unaona namna anavyokubalika na kuungwa mkono na watanzania wengi
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewasihi Watanzania kujitokeza kuhesabiwa na kutoa ushirikiano wa kutosha kwa zoezi la Sensa linalotarajiwa kufanyika tarehe 23 Agosti 2022 ikiwa ni sensa ya Sita kufanyika katika Tanzania huru huku akieleza kuwa matokeo ya awali yatatolewa mwezi Oktoba mwaka huu.

Katika ujumbe wake kwa watanzania alioutoa kupitia vvyombo vya habari usiku wa leo Jumatatu tarehe 22 Agosti 2022 (Saa chache kabla ya zoezi la Sensa) Rais Samia amewakumbusha Watanzania umuhimu wa kutoa taarifa sahihi kwani taarifa hizo ni muhimu kwa mipango ya maendeleo ya taifa na amewatoa hofu watanzania akieleza kuwa kila taarifa inayokusanywa itatunzwa kwa mujibu wa sheria kwani ni kosa kisheria kwa karani wa Sensa kutoa taarifa yoyote aliyoikusanya.

Rais Samia ameeleza kuwa kutokana na ukubwa wa nchi yetu, makarani hawatoweza kuwafikia watu wote kwa siku moja hivyo amewasihi wale wote ambao hawatofikiwa siku ya kwanza ya Sensa (23 Agosti 2022) kutunza kumbukumbu za wale wote watakaolala katika kaya usiku wa kuamkia siku ya sensa ili kuwezesha taarifa hizo kutolewa kwa usahihi pale ambapo makarani watafika.

Kwa mara ya kwanza Sensa ya mwaka huu itajumuisha ukusanyaji wa takwimu za majengo yote nchi nzima hivyo kuwezesha upatikanaji wa taarifa sahihi juu ya ubora wa makazi ya wananchi. Kukamilika kwa zoez hili kutaifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuunganisha sensa ya watu na makazi.

Rais Samia pia amewasisitiza wananchi kutowaficha watu wenye ulemavu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mila potofu kwani kufanya hivyo kutaikwamisha Serikali kupanga kwa usahihi namna ya kuwahudumia watu hao.

Kwa kawaida sensa hufanyika kila baada ya miaka 10, ambapo kwa miaka ya nyuma imewahi kufanyika mwaka 1967, 1978, 1988, 2002, 2012 na kumbukumbu zaidi zinaonesha kuwa kabla ya uhuru, kwa upande wa Tanganyika Sensa ilifanyika mara 5 (Mwaka 1913, 1921, 1931, 1948 na 1957 huku Zanzibar wakifanya sensa mara moja tu mwaka 1958 ingawa sensa za kabla ya uhuru zilikosa vigezo vingi vya kisayansi.
View attachment 2331605
Asante kwa taarifa, tunamfuatilia
P
 
Akimaliza muda wake 2030, watanzania tutamtaka atusubiri Tuamue juu ya katiba yetu kuhusu ukomo, maana tunampenda Sana Rais wetu na tunamhitaji ili aendelee kututumikia watanzania, tumeridhishwa na kulizika na utendaji kazi wake mh Rais wetu
Hahaha watu washachoka dadadeki, huyu raisi siku anamaliza muda wake nadhani watu watacheza barabarani kwa maana duh!
 
Hiyo sio hotuba ni tangazo tu.

Hatuna rais wa kuhutubia taifa ilikuwaga Mkapa tu
Kwako ndio labda Tangazo lakini mh Rais wetu ukisikika tu atazungumza au kuhutubia muda fulani au kuwa mahali fulani unakuta hata kazi zinasimama ili kuweza kupata na kutoa muda wa kumsikiliza mh Rais wetu, anakubalika Sana Rais wetu na anapendwaa Sana mh Rais, hii yote inatokana na namna anavyofanya kazi kwa juhudi na maarifa katik kuwatumikia watanzania
 
Back
Top Bottom