Rais Samia aipa Zambia ardhi hekari 20 katika bandari kavu Kwala mkoa wa Pwani

Rais Samia aipa Zambia ardhi hekari 20 katika bandari kavu Kwala mkoa wa Pwani

Mnatia aibu kwa hizi comment zenu hivi mnaelewa kwamba hiyo ni kwa faida ya Tanzania.
Yani kule kwenye bandari kavu ya kwala kila nchi inayopitisha mizigo kupitia bandari yetu imetengewa hekali kadhaa kwaajili ya kuhifadhi mizigo kabla ya kwenda kwenye nchi husika mfano hiyo Zambia.
Kifupi ni kwa faida yetu ni si vinginevyo.
 
Wewe ni mgeni na jf? Hili ni jukwaa la Wapinzani Sasa hivi wamepata wafuasi wao ambao ni Sukuma gang wote ni hater wa Samia
Mimi sifikirii hata kama ni wapinzani bali ni uelewa mdogo miongoni mwetu mfano angalia kwenye post ya Millardayo instagram na twitter kuhusu hii habari ndio utashangaa zaidi.
Kila mtu ni Samia kauza kipande cha ardhi kwa wazambia.
 
Naona kama watu wameelewa tofauti na maana iliyokusudiwa au pengine mimi ndio nimeachwa solemba na hii habari...

Ukisoma kichwa cha habari, ni rahisi kuelewa ya kwamba ndani ya ardhi ya Tanzania kumemegwa hekari 20 na kukabidhiwa nchi ya Zambia kuendesha shughuli za bandari kavu...

Lakini ukiisoma habari zaidi, binafsi nimeelewa ya kwamba ndani ya bandari kavu ya Kwala kutatengwa zone maalumu ambayo itashughulikia forodha ya mizigo ya Zambia peke yake na hii ni kutokana na sababu ya wingi wa mizigo iendayo Zambia na ile ijayo toka Zambia, pia mchango mkubwa wa kibiashara...
Je Ina tofauti na mwalimu alipotoa eneo la kunenepeshea ng'ombe kwa hayati Jumbe, mwenyekiti wa serikali ya mapinduzi?

Sent from my TECNO CI6 using JamiiForums mobile app
 
Wewe huwajui hawa watu wanavyopotosha mambo, Zambia wametengewa eka 20 ndani ya bandati kavu kwa mizigo yao, malipo ya huduma watazopatiwa kama kawaida.
Afadhali umenielewesha sasa nimeelewa maan Post haikuwa na maelezo ya kujitosheleza Ili mtu kuelewa kilichofanyika.
 
Mnatia aibu kwa hizi comment zenu hivi mnaelewa kwamba hiyo ni kwa faida ya Tanzania.
Yani kule kwenye bandari kavu ya kwala kila nchi inayopitisha mizigo kupitia bandari yetu imetengewa hekali kadhaa kwaajili ya kuhifadhi mizigo kabla ya kwenda kwenye nchi husika.
Kifupi ni kwa faida yetu ni si vinginevyo.
Tulia dada,wewe ndio unajua leo?
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania imetenga eneo la hekari 20 za ardhi katika Bandari kavu eneo la Kwala Mkoa wa Pwani kwa ajili ya kuhudumia mizigo kutoka Zambia ambapo amesema hiyo ndio zawadi ya Tanzania kwa Zambia katika wakati huu wa sherehe za Uhuru wa Zambia.

Rais Samia amesema hayo kwenye hotuba yake akiwa ni Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka 59 ya Uhuru wa Zambia iliyofanyika Ikulu ya Lusaka, Zambia.

“Kwa nia ya kuwaweka Watu wa Zambia kama kipaumbele katika mipango yetu na kutokana na azma yetu ya kurahisisha biashara kati ya Nchi hizi mbili, Serikali yangu imefanya maamuzi ya kutenga eneo la hekta 20 katika Bandari kavu ya Kwala katika ukanda wa pwani ya Tanzania kwaajili ya shehena maalum kwaajili ya Zambia”

“Zambia itakuwa na uwezo wa kuhifadhi bidhaa kwa muda mrefu na pia hatua hii itaondoa msongamano, ucheleweshaji na kupunguza gharama za kufanya biashara nchini Zambia ikipelekea kukuza biashara kati ya Nchi zetu mbili na kutengeneza fursa za kibiashara kwa Wananchi kutokea Zambia na Tanzania na hii ni zawadi yetu kutoka Tanzania katika wakati huu wa sherehe za uhuru wa Taifa lenu”

Zambia ni Mteja mkubwa wa Bandari ya Dar es Salaam, ikichukua asilimia 34 ya mizigo yote inayopitia Bandari hiyo kwenda nje ya Tanzania.

Millard Ayo

----
Maoni yangu

Hadi tukifika mwaka 2030 Tanganyika itabidi kuomba uhuru upya ili tujikomboe kwa sababu nchi nzima itakuwa mikononi mwa wachache.

Je, kwanini hakutoa bure eneo la zanzibar!
Ingekuwa heri Kwa Mbeya ingejengwa hiyo bandari kavu. Mimi na wanakijiji wenzangu tuko tayari kuwapa eneo Kwa fidia ndogo.
 
Simuelewi huyu rais. Nani kampa kibao cha kugawa ardhi ya watanzania kwa Zambia?
Miaka ya 70 Tanzania kila kona tulishuhudia kambi za wapigania uhuru hasa wa kusini mwa Afrika wakipewa ardhi na hata hivi karibuni Malawi walikuwa na bandari kavu maarufu kama Malawi cargo pale Mbeya.Hivi waliorudi makwao waliondoka na ardhi yetu?Au kuna vitu kama majengo walituachia kama nchi?Tuache siasa uchwara kwenye mambo yenye tija
 
Ndiyo mnavyojidanganya eeh? sisi tunasema Zanzibar siyo nchi na wala haitokua nchi, mlikubali wenyewe kuingia kwenye muungano au mlilazimishwa?
Sasa mbona sisi Wabara haturuhusiwi kumiliki ardhi Zanzibar.
 
Bahati mbaya baadhi yenu hamjui hali au changamoto za biashara duniani. Kwani hizo hekta zilizotolewa kwa Zambia si ni kwa manufaa ya Tanzania pia ? Tafakari.
Wasikusumbue hawa. Wengi wao humu ni washamba hawajui chochote kuhusu biashara na ufanisi wa biashara duniani
 
Sasa mbona sisi Wabara haturuhusiwi kumiliki ardhi Zanzibar.
Shida kubwa ni kwamba ardhi yenyewe tu hawana! lakini hawana ubavu wa kutuzuia kumiliki ardhi kwa anaetaka kwenda kuishi huko. Nakumbuka wakati wa bunge la katiba mbunge mmoja wa ZANZIBAR kwa jina SYLVESTER MASELE MABUMBA aliwahi kulalamika kwamba kule wanaonewa, Mama samia akamuuliza 'mbona wewe unamiliki shamba kubwa zaidi ya mimi?' inaonekana wapo baadi ya wadau wa huku wanaomiliki ardhi, ila siwezi kujua zaidi, nyinyi mnaojua sheria za huko inabidi mtujuze!
 
Acha gubu na nongwa! Kwani umeambiwa wamepewa waondoke na hiyo ardhi?
Sasa kama hawaondoki na hiyo Ardhi, kwanini nchi yetu iligomea ardhi kuingizwa kwenye jumuiya ya Africa mashariki? Au ndio mambo ya bendera fuata upepo?
 
Na hiki ndio anchoweza KIZIMKAZI. Watanganyika tujipange.
 
Back
Top Bottom