Rais Samia akishiriki tamasha la Mashindano ya Kuhifadhi Quran kwa Wanawake

Rais Samia akishiriki tamasha la Mashindano ya Kuhifadhi Quran kwa Wanawake

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288

View: https://www.youtube.com/watch?v=dt5CakYo9AA
Leo kutakuwa na mashindano makubwa ya kuhifadhi Quran kwa wanawake katika uwanja wa Mkapa.
Mgeni rasmi atakuwa ni Rasi wa Tanzania - Dr Samia
Mashindano yataonyeshwa Live kupitia channel mbali duniani
Wanawake wameuhifadhi msahafu mzima wakiwemo watoto wadogo
Yaanza saa 12:00 asubuhi mpka saa 7:00 mchana

FAIDA YA KUHIFADHI QURAN
Kuhifadhi Qur'an kuna faida nyingi za kiroho, kijamii, na kimaisha, ikiwemo:

  1. Thawabu za Kiakhera: Kuhifadhi Qur'an ni ibada kubwa ambayo inampatia mhifadhi wake thawabu nyingi kutoka kwa Allah, ikiwa ni pamoja na daraja za juu katika Pepo.
  2. Ulinzi na Baraka: Kuhifadhi Qur'an husaidia kupata ulinzi wa Allah na baraka katika maisha, kwani Qur'an ni chanzo cha nuru na mwongozo.
  3. Kuhifadhi Dini: Kuhifadhi Qur'an ni njia ya kulinda dini na kuhakikisha kuwa maneno ya Allah yanabaki sahihi na safi bila mabadiliko.
  4. Kiongozi wa Maisha: Qur'an ni mwongozo wa maisha ya kila siku. Mtu anayehifadhi Qur'an ana uwezo wa kuzingatia na kutekeleza mafundisho yake kwa urahisi zaidi.
  5. Heshima na Hadhi: Watu wanaohifadhi Qur'an wanapata heshima kubwa katika jamii, kwani wanachukuliwa kama watu wa dini na kiongozi wa kiroho.
  6. Ukaribu na Allah: Mtu anayehifadhi Qur'an anajenga ukaribu na Allah kupitia kujifunza, kuzingatia, na kutafakari maneno Yake.
  7. Faida za Akili: Kuhifadhi Qur'an kunaboresha kumbukumbu, uwezo wa kuelewa mambo, na umakini, kwani inahitaji bidii na uvumilivu.
  8. Mafanikio ya Kijamii: Wanaohifadhi Qur'an mara nyingi wanapata fursa nzuri katika jamii, kama vile kuwa viongozi wa maombi, walimu, na washauri wa kiroho.

Rais Samia Suluhu Hassan,​

Amesema unapomlea binti vizuri kidini, akayasoma na kuyaelewa mafunzo ya kidini, ni dhahiri kwamba atakuja kuwa mama bora katika siku za baadaye na kuja kuwa mlezi mzuri wa familia na jamii yake.

Mashindano haya [kuhifadhi Quran] ni faraja kwa watoto wetu wanaoshiriki na wanaoandaliwa kuwa raia na wazazi wema, kwahiyo ni vema tukaweka nguvu kukuza zaidi mashindano ya aina haya.
 
Knowledge is not what is memorized. Knowledge is what benefits. By imam Shafi'i
hujamfahamu vizuri kakusudia nini au umekusudia kupindisha. kwa maana hio tunakosea vyo kikuu kutoruhusu wanafunzi waingie na madesa siku ya mtihani? Unajua faida utayopata wewe siku ya hesabu kama mzee endapo mtoto wako akihifadhi Quran?
 
hujamfahamu vizuri kakusudia nini au umekusudia kupindisha. kwa maana hio tunakosea vyo kikuu kutoruhusu wanafunzi waingie na madesa siku ya mtihani? Unajua faida utayopata wewe siku ya hesabu kama mzee endapo mtoto wako akihifadhi Quran?
Huna hata jema. Huo ujumbe nilioweka hapo kuna mahali nimekosoa au kupindisha. Udini utakuua ndio maana hata ukiambiwa ibada njema utasema unakejeriwa.
 
Hivi hao wanawake wa kiislam wakifika huko mbinguni wanapewa nini??? Maana wanaume wanatunukiwa nguvu za kushughulikia mabikra 72 na mito ya pombe,,,,au hawa wakienda huko ndo wanakua hao ma bikra wanaopewa wanaume
 
Faida nyingine Quran inapinga Dhuluma katika kudhulumu Uhai wa Watu, kwa njia ya kuzuia Utekaji, Mauaji na kwa namna zingine

Allah alisimamie hili, Amin
Una ujumbe wowote kwa mgeni maalum?
 
Mohammed alisema kuwa wanawake ni wajinga na wengi wa watu walio kuzimu ni wanawake. Ni jambo la kuchekesha, ukizingatia kwamba mlipuaji wa kujitoa muhanga wa kigaidi au mtu aliyeuawa kishahidi katika jihad ameahidiwa mabikira 72 mbinguni.

Pia, kama watu wengi kuzimu ni wanawake, na watu wengi mbinguni ni kama Osama Bin Laden na watu wengine wenye ndevu kama Mohammed, nadhani wanaume wengi wangetamani kwenda kuzimu kuliko mbinguni.
Heheheh
 
Huna hata jema. Huo ujumbe nilioweka hapo kuna mahali nimekosoa au kupindisha. Udini utakuua ndio maana hata ukiambiwa ibada njema utasema unakejeriwa.
Ulikusudia kufanyaje?
 
Back
Top Bottom