Rais Samia akutana na kufanya mazungumzo mfanyabiashara Alhaj Aliko Dangote

Msemaji wa serikali Bwana Gerson Msigwa aposti katika ukurasa wake wa twitter kauli hiyo ambayo imezua maswali mengi kwa wananchi.Ametoa kauli hii hivi leo baada ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mazungumzo na mwekezaji Dangote.

Wengi wamejiuliza kwani hali ilikuwaje kabla?Wengine wakijiuliza ni nani huyo ambae aliharibu nchi kiasi hicho?
 
M
Msigwa mnafiki sana ana maana Magufuli alikuwa anakwaza wawekezaji!
 
... huyu Mama PR iko juu sana kuliko mtangulizi! Chama kingekuwa makini, kama ilikuwa ni lazima wawili hawa washike madaraka ya juu, basi mtangulizi aliitakiwa awe msaidizi wa Mama toka mwanzo kabisa.
EeenHee Heee!

Mkuu nimecheka kwelikweli nilipo'visualize' picha hiyo uliyoiweka katika maneno na mimi nikajaribu kuifanya kuwa picha halisi!
 
Ukitaka manufaa ya cement iwe Tshs. 10,000 kwa mfuko lazima kazi zingine zifanyike na macontractors waliopewa kazi kama za usafirishaji, payroll iwe sub contracted kwa watu wengine n.k ili menejimenti ya Dangote Cement ijikite katika core duties uzalishaji na kuhakikisha mashine mitambo ya viwanda inakwenda sawa.

Masuala mengi ya human resources, maduka ya cement waachiwe wengine wafanye. Huu ndiyo mtindo wa kisasa wa ku - run operesheni za viwanda vikubwa ktk dunia hii ya mapinduzi ya viwanda ya nne.

Hutakiwi kufuatilia sijui likizo, off ya kuumwa, kutazama watoto, kufiwa / msiba, mishahara ya madereva na wafanyakazi wengine wasio wataalamu wa cementi au wa uendeshaji kiwanda haya yote unawapatia ma contractor waumize vichwa masuala yasiyohusisha uzalishaji.

Hapa inatakiwa serikali izibane kampuni hizi zinazofanya kazi ya u contract wa madereva , payroll n.k kuwapa wafanyakazi wake wote wanaopelekwa kufanya kazi za Dangote Cement mishahara, stahili, likizo, mikataba na marupurupu, posho kufuatana na sheria za kazi za Tanzania.

Kuilaumu kampuni ya Dangote Cement ambayo haihusiki na uajiri wa hawa madereva na wafanyakazi wengine wa agency ni kupoteza muda. Serikali iwabane ma contractor waliobeba majukumu ya ajira za wafanyakazi hawa.
 
Kuna uwezekano mkubwa, Ikulu ya Chamwino haitaendelea kutumika.
Ifungwe kabisa ina nuksi hiyo. Serikali irudi DSM majengo yanaharibika. Kule Dodoma Wizara nyingi zililazimika kujenga temporary shelter eti majengo ya kudumu ni baadaye. Utopolo huo. Wahamie Dodoma kwa awamu. Business Tycoons wako DSM. Mama Rudisha jiji letu la Kibiashara.

Lile jitu liliharibu kila kitu hasa mahusiano na wachangiaji maendeleo makubwa ya nchi. Dangote Dereva tu ni zaidi ya 1,000 bado wafanyakazi wengine technical na support. Halafu dubwasha moja linacheza naye.

Big up ok beloved Madam President. Umerejesha matumaini Tanzania. Umerejesha kicheko kwenye nyuso zetu. Mungu akupe miaka karne na ushee.
 
Huyu Dangote wakati anapigania kupata gas ya Mtwara, ni Magufuli aliyempigania mpaka kuagiza ajengewe bomba lake mpaka kiwandani,

alipoona vile vile wanamzingua kuhusu makaa ya mawe alimruhusu mpaka awe na eneo lake mwenyewe achimbe,

leo mnamsema kwamba alikuwa anamfanyie mizengwe,?!

kweli kama umemchoka mbwa mpe jina baya.

nyie watu man roho mbaya sana.
 
" Things have changed dramatically, and I will be the champion for Tanzania that the business enviroment has chnged and that please come and invest in Tanzania!"
---Aliko Dangote


Asante Mama Samia, tunaona mwanga!
Bibie SASHA once again..

Good move..wawekaji waje vijana tupate ajira japo tuoe..ubabe na ushamba hauwezi kuendesha nchi karne hii.
 
Unadhani ni kwanini Dangote amesema kuna mabadiliko Tanzania,na watu waje kuwekeza wakati alipokuwa ikulu leo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…