Rais Samia ameanzia Mwanza Kujenga Hekalu letu: Tayari kamaliza msingi, kuta na linta, bado kuezeka

Rais Samia ameanzia Mwanza Kujenga Hekalu letu: Tayari kamaliza msingi, kuta na linta, bado kuezeka

Doctor Mama Amon

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
2,089
Reaction score
2,725
1624290570475.png

Rais Samia Suluhu Hassan akiwa Mwanza anatafakari kuhusu Ramani ya Kimkakati (Strategy Map) iliyo muhtasari wa ukurasa mmoja wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26 (uk. 70)

Tangu serikali ya wamu ya sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, ilipoanza kazi nimekuwa najiuliza maswali yafuatayo, kama sehemu ya kazi yangu ya utafiti wa kawaida kuhusu ujasiriadola nchini Tanzania:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba sisi kama nchi tunao utambulisho gani wa kijiografia, kihistoria na kikatiba?
  2. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi?
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025?
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka kuchukua hatua gani ili sisi kama Taifa tuweze kufika huko?
  5. Serikali ya awamu ya sita inataka kutekeleza kazi gani ndani ya kila hatua ya safari yetu?
  6. Serikali ya awamu ya sita inataka nani achukue hatua gani na lini?
  7. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu ya miaka 5 inahitaji fedha kiasi gani?
  8. Serikali ya awamu ya sita inafikiri kwamba tutajuaje kuwa tumefika mwisho wa safari yetu ya miaka 5?
Nilikuwa nasubiri kwa hamu ukamilishwaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 21/22 hadi 25/26 ili kuona kama nitapata majibu ya maswali haya.

Lakini, kabla mpango huo haujakamilishwa wala kuzinduliwa, naona maswali haya yameanza kujibiwa kwa kina kupitia hotuba za Rais.

Tayari Rais Samia amemaliza ziara ya kikazi mkoani mwanza alikokaa kwa siku tatu. Alisema kuwa Kanda ya Ziwa ni Ukanda wa Kiuchumi utakaoitumia Mwanza kama kituo kikubwa cha biashara katika nchi za Maziwa Makuu.

Akiwa huko alizindua miradi na mikakati kadhaa inayoakisi hatua za kimkakati zilizotajwa kwenye Rasimu ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (21/22-25/26). Miradi na mikakati husika iliyozinduliwa ni pamoja na:

  • Mradi wa maji wa Misungwi;
  • Mradi wa reli ya kimataifa katika ukanda wa Ziwa Viktoria;
  • Mradi wa chelezo ya kukarabati meli;
  • Mradi wa ujenzi wa daraja la Ziwa Viktoria;
  • Mkakati wa kuwawezesha vijana kunufaika na fursa za ajira 8,000,000 zinazotengenezwa na serikali kwa ajili yao;
  • Mkakati wa kufuta pengo la kidijitali kati ya wanaume na wanawake (gender digital divide) kwa kujenga shule moja ya kuendeleza Tekinolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na Sayansi, Ubunifu, Tekinolojia, na Hisabati (SUTH) katika kila mkoa; na
  • Mkakati wa kuzalisha ajira kwa vijana wa kike na kiume kupitia miradi mbalimbali ya kitaifa.
Rais alisema kuwa, mkakati wa kufuta pengo la kidijitali kati ya wanaume na wanawake kwa kujenga shule moja ya kuendeleza TEHAMA na SUTH, ni sehemu ya mpango wa serikali wa kuingia katika awamu ya nne ya zama za viwanda kwa kujenga mazingira wezeshi ya kitekinolojia.

Kuhusu ajira, Rais alitaja sekta zifuatazo kama vyanzo vya ajira za vijana hawa: mradi wa umeme wa mwalimu Nyerere, Miradi ya Ujenzi wa Barabara, na Mradi wa bomba la mafuta. Pia alitaja miradi ya kilimo, miradi ya ufugaji, miradi ya uvuvi, na miradi ya TEHAMA inayotekelezwa kupitia ubia wa serikali na sekta.

Aidha, kuhusu suala la ajira, RC David Kafulira alimwahidi Rais Samia kwamba mkoa wake wa Simiyu unakusudia kuchangia 2.5% ya ajira zote, yaani ajira 200,000, kutokana na kuzalisha ajira kupitia minyororo ya ongezeko la thamani ya huduma na bidhaa zilizoko katika sekta mbalimbali mkoani humo.

Kwa mujibu wa hotuba ya jana ya Waziri wa Tamisemi, Ummy Mwalimu,
asilimia baki ya ajira itazalishwa nchini kote katika maeneo yafuatayo: wilaya 126, halmashauri 184, kata 3,956, vijiji 12,319, vitongoji 64,384, na mitaa 4,263.

Na kwa mujibu wa
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, katika mwaka 2019, pato la Kanda ya Ziwa lilikuwa TZS bilioni 34, sawa na 25.9% ya Pato la Taifa.

Aidha, Luoga anasema kuwa Kanda ya Ziwa huzalisha zaidi ya 90% ya dhahabu yote nchini, 50% ya pamba na kahawa na zaidi ya 95% ya mauzo ya samaki ndani na nje ya nchi.

Ziara ya Rais Samia huko Kanda ya Ziwa Viktoria ni mwendelezo wa pilika zake za kujipambanua kama mjasiriadola wa kike kwa kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii ili kuwaeleza ndoto aliyo nayo kuhusu Tanzania mpya chini ya serikali ya awamu ya sita.

Kwanza alikutana na wazee kupitia wazee wa Dar es Salaam, kisha akakutana na kina mama kupitia kina mama wa Dodoma, na leo amekutana na vijana kupitia vijana wa Mwanza.

Nimesikiliza hotuba zake zote tangu Dar es Salaam, Dodoma hadi Mwanza. Ni hotuba nzuri kwa ajili ya kueleza ndoto aliyo nayo juu ya Tanzania mpya.

Kutokana na kauli zake nilizozisikia mpaka sasa, Rais anayo majawabu yafuatayo, kwa maswali yaliyotajwa hapo juu:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba sisi kama nchi utambuliko wetu wa Kikatiba na Kihistoria ni upi? Serikali inakiri kwamba sisi ni:
    • Nchi moja iliyotokana na muungano wa nchi mbili,
    • ambayo haifungamani na dini yoyote,
    • inayoongozwa kwa mujibu wa kanuni za Jamhuri
    • yenye kuhesimu misingi ya demokrasia,
    • na yenye kuongozwa na serikali inayopata madaraka kutoka kwa watu.
  2. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi? Serikali inasema kuwa hapa tulipo kuna
    • magonjwa,
    • ujinga,
    • ikolojia duni,
    • ofisi za utawala zinazosuasua katika kutoa huduma kwa watu,
    • na uchumi usiojali maslahi ya pamoja kwa ajili ya makundi yote ya watu.
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025? Serikali inataka kuona kila Mtanzania akiwa na maisha yanayoendana na kipato cha uchumi wa kati , kwa maana ya kipato kinachoweza kuchochea upatikanaji wa
    • afya bora,
    • elimu bora,
    • ikolojia bora,
    • ofisi zinazotoa huduma kwa kasi, kwa usawa na kwa wote, katika namna inayoendana na imani ya jamii ya kitaifa ambayo ni msingi wa ujenzi wa jamii ya amani.
    • na uchumi unaojali maslahi ya pamoja kwa ajiliya makundi yote ya watu.
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka kuchukua hatua gani ili tuweze kufika huko? Serikali inasema kuwa hatua zifuatazo lazima zichukuliwe:
    • Kuchochea maendeleo ya rasilimali watu, usawa wa kijinsia, uwezeshaji wa makundi yote ya watu wakiwemo vijana, wanawake, wazee, watoto, wajane, yatima na walemavu;
    • Kuchochea utajiri wa Taifa kupitia uvunaji wa maliasili, uzalishaji mali, kubuni na kukuza kanda za kiuchumi;
    • Ujenzi wa taasisi za kiuchumi, kisiasa na kijamii zinazotoa huduma bora kwa kasi, kwa usawa na kwa wote ;
    • Kuimarisha usalama wa nchi na mahusiano ya kimataifa yaliyo bora zaidi;
    • Kutunza mazingira na kufanya menejimenti ya mabadiliko ya tabianchi;
    • Kujenga imani ya jamii na jamii ya amani kwa kukuza na kuhami mila, maadili na tunu za Taifa;
    • Kuweka mipango ya maendeleo yenye kuonyesga bayana vigezo vya ufanisi, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake.
  5. Serikali ya awamu ya sita inataka kutekeleza kazi na majukumu gani ndani ya kila hatua ya safari yetu? Serikali inataka kuchukua hatua hizi kwa
    • kusimika uongozi bora,
    • kujenga mfumo wa sheria unaoruhusu utoaji wa haki,
    • kujihusisha na ujenzi wa miundo mbinu wezeshi kama vile upatikanaji wa nishati na maji,
    • kukusanya rasilimali fedha,
    • kuchochea ushirikishwaji wa makundi yote ya kijamii, na
    • kusimamia uwajibika wenye tija na kasi.
  6. Serikali ya awamu ya sita inataka nani achukue hatua gani na lini? Kwa kuzingatia kalenda ya kazi za serikali, watekelezaji ni:
    • Mawaziri na makatibu wakuu,
    • Wakurugenzi wa Idara na wakala za serikali,
    • Ma-RC na ma-RAS,
    • Ma-DC na ma-DAS,
    • Ma-DED na wafanyakazi wa halmashauri,
    • Ma-DEO, ma-WEO, ma-VEO, ma-MEO, na ma-KEO,
    • Wadau wa sekta binafsi yakiwemo makampuni, NGOs, FBO, na Vyombo vya habari,
    • Mahakimu, majaji, wasajili wa mahakama, na wanasheria,
    • Spika, Katibu wa Bunge, na wabunge,
    • Na wadau wa maendeleo wa kimataifa.
  7. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu ya miaka 5 inahitaji fedha kiasi gani? Kiasi cha rasilimali zinazohitajika ni Shilingi trilioni 115 ambazo ni
    • bajeti za miaka 5,
    • Bajeti za wizara zote,
    • Bajeti za Halmashauri zote,
    • na bajeti za mawakala wote wa serikali.
  8. Serikali ya awamu ya sita inafikiri kwamba hatimaye tutajuaje kwamba tumefika mwisho wa safari yetu? Kuna vipimo vya ufanisi vinaandaliwa kwa ajili ya kupima kasi na ufanisi wa
    • kila wizara,
    • kila Halmashauri,
    • kila wakala wa serikali,
    • na kwa kila mwaka.
Hivyo, kusudi kauli za Rais zipate msingi imara wa usimamizi na ufuatiliaji, namwalika Waziri wa Fedha kufanya haraka ya kukamilisha maandalizi ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26.

Mpango huu ndio andiko pekee linaloweza kujibu maswali yote hapo juu kwa kina. Hivyo, kwa sasa ni muhimu zaidi kuliko Ilani ya Uchaguzi kwani utafafanua mambo haya kwa kina katika njia inayoruhusu usimamizi na ufuatiliaji. Ilani ya chama ni muhimu, lakini inapaswa kubaki kama "kiambatanisho" kwenye andiko hili muhimu.

Kwako Waziri Mwigulu Lameck Nchemba: Kasi ya Rais Samia ni kubwa kuliko kasi ya Ofisi yako. Kuna kitendeakazi muhimu kinakosekana mikononi mwa Rais--Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (21/22-25/26). Huu ndio waraka pekee unaopaswa kujibu maswali yote hapo juu kwa urefu na upana wake.

1623836260567.png

Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango

Kwa hiyo basi, changamka kuziba pengo hili ambalo ni kinyume cha mazoea bora ya kiutendaji yanayotutaka kuanza utekelezaji baada ya kukamilisha mipango.

1624290334737.png

Mnyumbulisho wa Mchoro Unaoonyesha Nadharia ya Mabadiliko katika FYDP III, uk. 70

1624067106513.png


1624067055874.png
 
View attachment 1819542
Rais Samia Suluhu Hassan akiwa Mwanza akitafakari juu ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26

Tangu serikali ya wamu ya sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, ilipoanza kazi nimekuwa najiuliza maswali yafuatayo, kama sehemu ya kazi yanguya utafiti:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi?
  2. Serikali ya awamu ya sita inataka tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025?
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze kazi/miradi gani ili tuweze kufika huko?
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze vipi kazi/miradi husika ili tuweze kukamilisha safari yetu?
  5. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu tangu 2021 hadi 2025 inahitaji rasilimali/fedha kiasi gani?
  6. Serikali ya awamu ya sita inataka tujueje kwamba tumefika mahali ambako serikali inataka kutufikisha?
Nilikuwa nasubiri kwa hamu Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26 ili kuona majibu ya maswali haya. Lakini, kabla mpango huo haujazinduliwa, naona maswali haya yameanza kujibiwa kwa kina kupitia hotuba za Rais.

Tayari Rais Samia amemaliza ziara ya kikazi mkoani mwanza alikokaa kwa siku tatu. Akiwa huko alizindua miradi kadhaa ikiwemo mradi wa maji, mradi wa reli ya kimataifa, mradi wa chelezo ya meli, mradi wa daraja la Ziwa Viktoria na mradi wa kuwaamsha vijana ili wachangamkie fursa zinazotengenezwa na serikali kwa ajili yao.

Ziara hii ni mwendelezo wa pilika zake za kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii ili kuwaeleza ndoto aliyo nayo kuhusu Tanzania mpya chini ya serikali ya awamu ya sita. Kwanza alikutana na wazee kupitia wazee wa Dar es Salaam, kisha akakutana na kina mama kupitia kina mama wa Dodoma, na leo amekutana na vijana kupitia vijana wa Mwanza.

Nimesikiliza hotuba zake zote tangu Dar es Salaam hadi Mwanza. Ni hotuba kwa ajili ya kueleza ndoto aliyo nayo juu ya Tanzania mpya.

Kutokana na kauli zake nilizozisikiliza, Rais anayo majawabu yafuatayo, kwa maswali yaliyotajwa hapo juu:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi?
    • Serikali inasema kuwa hapa tulipo kuna magonjwa,
    • ujinga,
    • ikolojia duni,
    • ofisi za utawala zinazosuasua katika kutoa huduma kwa watu,
    • na uchumi usiojali maslahi ya watu wote.
  2. Serikali ya awamu ya sita inataka tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025?
    • Serikali inataka kuona kila Mtanzania akiwa na maisha yanayoendana na kipato cha uchumi wa katia , kwa maana ya afya bora,
    • elimu bora,
    • ikolojia bora,
    • ofisi zinazotoa haki sawa kwa wote,
    • na uchumi unaojali maslahi ya watu wote.
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze kazi/miradi gani ili tuweze kufika huko? Serikali inasema kuwa kazi zifuatazo lazima zitekelezwe:
    • Kuchochea maendeleo ya rasilimali watu, usawa wa kijinsia, ustawi wa vijana na uwezeshaji wa watu,
    • Kuchochea uzalishaji mali, uvunaji wa rasilimali, na ukuzaji wa kanda za kiuchumi,
    • Ujenzi wa taasisi za kiuchumi, kisiasa na kijamii zinazotoa huduma bora,
    • Usalama na mahusiano ya kimataifa yaliyo bora zaidi,
    • Utunzaji wa mazingira na menejimenti ya mabadiliko ya tabianchi,
    • Ujenzi wa imani ya jamii na jamii ya amani kwa kukuza na kuhami tunu za Taifa,
    • Kuweka mipango ya maendeleo, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake.
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze vipi kazi/miradi hii ili tuweze kukamilisha safari yetu?
    • Kwa kuweka uongozi bora,
    • kujenga mfumo wa sheria unaoruhusu utoaji wa haki,
    • kujihusisha na ujenzi wa miundo mbinu wezeshi,
    • kukusanya rasilimali fedha,
    • kuchochea ushirikishwaji wa umma mpana, na
    • kusimamia uwajibika wenye tija na kasi.
  5. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu tangu 2021 hadi 2025 inahitaji rasilimali/fedha kiasi gani?
    • Kwa kuandaa bajeti ya kila mwaka,
    • Bajeti ya kila wizara,
    • Bajeti ya kila Halmashauri,
    • na bajeti ya kila wakala wa serikali.
  6. Serikali ya awamu ya sita inataka tujueje kwamba tumefika mahali ambako serikali inataka kutufikisha?
    • Kuna vipimo vya ufanisi kwa kila wizara,
    • kila Halmashauri,
    • na kwa kila wakala wa serikali.
Hivyo, kusudi kauli za Rais zipate msingi imara wa usimamizi na ufuatiliaji, namwalika Waziri wa Fedha kufanya haraka ya kukamilisha uandaaji na uzinduzi wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26.

Waraka huu unapaswa kujibu maswali yote haya kwa kina, Hivyo ni muhimu zaidi kuliko Ilani ya Uchaguzi kwani utafafanua mambo haya kwa kina katika njia inayoruhusu usimamizi na ufuatiliaji. Ilani ya chama ni muhimu, lakini inapaswa kubaki kama "kiambatanisho" kwenye andiko hilo muhimu.

Kwako Waziri Mwigulu Lameck Nchemba.
Utapiga mapambio sana mwisho wa siku kumekucha na hakuna lolote uliloahidiwa lililotekelezwa utalia, utahamaki auutafanyaje?

The time bombshell is about to explode and devour your soul
 
View attachment 1819542
Rais Samia Suluhu Hassan akiwa Mwanza akitafakari juu ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26...

Waraka huu unapaswa kujibu maswali yote haya kwa kina, Hivyo ni muhimu zaidi kuliko Ilani ya Uchaguzi kwani utafafanua mambo haya kwa kina katika njia inayoruhusu usimamizi na ufuatiliaji. Ilani ya chama ni muhimu, lakini inapaswa kubaki kama "kiambatanisho" kwenye andiko hilo muhimu.

Kwako Waziri Mwigulu Lameck Nchemba.



Kwa kuitaja Ilani naamini umeisoma kwa undani. Imerejea hali ya Kijamii, Kisiasa na Kiuchumi hadi 2020. Baada ya mrejeo huo imeeleza Sera hadi 2025.

Serikali imepanga kutekeleza yaliyomo kwenye kupitia mikakati mbalimbali. Baadhi ya mikakati hiyo iko kwenye bajeti inayoendelea kujadiliwa bungeni.

Ili baadhi ya Sera ziweze kutekelezwa, Serikali imeanza kuandaa Sheria. Km sheria ambayo itafikishwa bungeni hivi karibuni, baada ya kujadiliwa na wananchi ni Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2021 (The Finance Bill, 2021)
 
Baada ya Kilimo Kwanza, Big Results Now, Uchumi wa Viwanda kufa na bila kuacha matokea sasa kuna mpango mwingine!!

Kwanini nisiamini hata mipango hii itashindwa??? Tumekuwa watu wa mipango tuuuu - hata isiyoweza kutekelezwa. Hatuna mfumo wa kuhoji utekelezaji - hatutakuja kuona mipango hii ikitekelezwa!!
 
Utapiga mapambio sana mwisho wa siku kumekucha na hakuna lolote uliloahidiwa lililotekelezwa utalia, utahamaki auutafanyaje? The time bombshell is about to explode and devour your soul
Kauli zako hazina ushahidi wa kuzitetea.
Kwa hiyo nazikanusha bila kuweka ushahidi wa utetezi hivi: Kauli hizi sio za kweli.
 
Kwa kuitaja Ilani naamini umeisoma kwa undani. Imerejea hali ya Kijamii, Kisiasa na Kiuchumi hadi 2020. Baada ya mrejeo huo imeeleza Sera hadi 2025.

Serikali imepanga kutekeleza yaliyomo kwenye kupitia mikakati mbalimbali. Baadhi ya mikakati hiyo iko kwenye bajeti inayoendelea kujadiliwa bungeni.

Ili baadhi ya Sera ziweze kutekelezwa, Serikali imeanza kuandaa Sheria. Km sheria ambayo itafikishwa bungeni hivi karibuni, baada ya kujadiliwa na wananchi ni Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2021 (The Finance Bill, 2021)
Kiongozi,

Nimekusoma. Naifahamui Ilani ya CCM vizuri katika sura zote mbili--uimara na udhaifu. Hivyo niseme yafuatayo:

1. Sehemu kubwa ya udhaifu wa Ilani ilizibwa kwa njia ya kauli za jukwaani wakati wa kampeni.

2. Ilani inajibu maswali matatu ya kwanza hapo juu, haina majibu kwa maswali baki matatu.

3. Bajeti iliyopitishwa Bungeni inahusu mpango wa maendeleo wa mwaka mmoja (2021/2022) pekee. Hii ni picha ndogo.

4. Ujenzi wa nchi unaanzia kwenye picha kubwa, kama ambavyo ujenzi wa nyumba unaanzia kwenye blue print yake.

Kwa sababu hizi, kuna umuhimu na uharaka wa kukamilisha mpango wa maendeleo wa miaka mitano ambao unafafanua ilani, na kuweka msingi wa mipango ya mwaka mmoja mmoja na bajeti zake.
 
Baada ya Kilimo Kwanza, Big Results Now, Uchumi wa Viwanda kufa na bila kuacha matokea sasa kuna mpango mwingine!! Kwa nini nisiamini hata mipango hii itashindwa??? Tumekuwa watu wa mipango tuuuu - hata isiyoweza kutekelezwa. Hatuna mfumo wa kuhoji utekelezaji - hatutakuja kuona mipango hii ikitekelezwa!!
Mashaka yako yanayo nafasi yake katika "mfumo wa kuhoji utekelezaji." Lakini pia, hata bandiko hili linayo nafasi yake katika mfumo huo. Ninaandika kwa sababu naamini kuwa maandiko haya yatakuwa na mchango wake katika kurekebisha tatizo unaloliongelea.

Na kwa hakika, nasubiri kwa hamu "Mpango wa Maendeleo ya Miaka Mitano Ijayo" ili kuangalia kama kuna "mfumo wa kuhoji utekelezaji." TDV 2025 haikuwa na mfumo huu. Dosari hii ilizibwa baadaye kupitia andiko liitwalo TLTPP, baada ya watu kama vile Prof Luhanga kupiga kelele kwa njia ya hoja. Kwa hiyo, tusichoke.
 
Yote hayo ni UPUUZI MTUPU kama Mama hatahakikisha Katiba na Tume huru ya uchaguzi vinapatikana kabla ya uchaguzi wa October 26, 2025 ili kuhakikisha uchaguzi huo ni wa HAKI na HURU na siyo utakaojaa, wizi na mauaji.
View attachment 1819542
Rais Samia Suluhu Hassan akiwa Mwanza akitafakari juu ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26

Tangu serikali ya wamu ya sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, ilipoanza kazi nimekuwa najiuliza maswali yafuatayo, kama sehemu ya kazi yangu ya utafiti:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi?
  2. Serikali ya awamu ya sita inataka sisi kama Taifa tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025?
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze kazi/miradi gani ili sisi kama Taifa tuweze kufika huko?
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze vipi kazi/miradi husika ili sisi kama Taifa tuweze kukamilisha safari yetu?
  5. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu sisi kama Taifa tangu 2021 hadi 2025 inahitaji rasilimali/fedha kiasi gani?
  6. Serikali ya awamu ya sita inafikiri kwamba sisi kama Taifa tutajuaje kuwa tumefika mwisho wa safari yetu ya miaka 5?
Nilikuwa nasubiri kwa hamu Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26 ili kuona majibu ya maswali haya. Lakini, kabla mpango huo haujazinduliwa, naona maswali haya yameanza kujibiwa kwa kina kupitia hotuba za Rais.

Tayari Rais Samia amemaliza ziara ya kikazi mkoani mwanza alikokaa kwa siku tatu. Alisema kuwa Kanda ya Ziwa ni Ukanda wa Kiuchumi utakaoitumia Mwanza kama kituo kikubwa cha biashara katika nchi za Maziwa Makuu.

Akiwa huko alizindua miradi kadhaa ikiwemo mradi wa maji, mradi wa reli ya kimataifa, mradi wa chelezo ya meli, mradi wa daraja la Ziwa Viktoria, na miradi ya kuwawezesha vijana kunufaika na fursa za ajira 8,000,000 zinazotengenezwa na serikali kwa ajili yao.

Rais alitaja sekta zifuatazo kama vyanzo vya ajira za vijana hawa: mradi wa umeme wa mwalimu Nyerere, Miradi ya Ujenzi wa Barabara, na Mradi wa bomba la mafuta. Pia alitaja miradi ya kilimo, miradi ya ufugaji, miradi ya uvuvi, na miradi ya TEHAMA inayotekelezwa kupitia ubia wa serikali na sekta.

Kuhusu suala la ajira, RC Kafulira alimwahidi Rais Samia kwamba mkoa wake wa Simiyu unakusudia kuchangia 2.5% ya ajira zote, yaani ajira 200,000, kutokana na kuzalisha ajira kupitia minyororo ya ongezeko la thamani ya huduma na bidhaa zilizoko katika sekta mbalimbali mkoani humo.

Kwa mujibu wa hotuba ya jana ya Waziri wa Tamisemi, Ummy Mwalimu,
asilimia baki ya ajira itazalishwa nchini kote katika maeneo yafuatayo: wilaya 126, halmashauri 184, kata 3,956, vijiji 12,319, vitongoji 64,384, na mitaa 4,263.

Na kwa mujibu wa
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, katika mwaka 2019, pato la Kanda ya Ziwa lilikuwa TZS bilioni 34, sawa na 25.9% ya Pato la Taifa.

Aidha, Luoga anasema kuwa Kanda ya Ziwa huzalisha zaidi ya 90% ya dhahabu yote nchini, 50% ya pamba na kahawa na zaidi ya 95% ya mauzo ya samaki ndani na nje ya nchi.

Ziara ya Rais Samia huko Kanda ya Ziwa Viktoria ni mwendelezo wa pilika zake za kujipambanua kama mjasiriadola wa kike kwa kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii ili kuwaeleza ndoto aliyo nayo kuhusu Tanzania mpya chini ya serikali ya awamu ya sita.

Kwanza alikutana na wazee kupitia wazee wa Dar es Salaam, kisha akakutana na kina mama kupitia kina mama wa Dodoma, na leo amekutana na vijana kupitia vijana wa Mwanza.

Nimesikiliza hotuba zake zote tangu Dar es Salaam, Dodoma hadi Mwanza. Ni hotuba nzuri kwa ajili ya kueleza ndoto aliyo nayo juu ya Tanzania mpya.

Kutokana na kauli zake nilizozisikia mpaka sasa, Rais anayo majawabu yafuatayo, kwa maswali yaliyotajwa hapo juu:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi? Serikali inasema kuwa hapa tulipo kuna
    • magonjwa,
    • ujinga,
    • ikolojia duni,
    • ofisi za utawala zinazosuasua katika kutoa huduma kwa watu,
    • na uchumi usiojali maslahi ya pamoja kwa ajili ya makundi yote ya watu.
  2. Serikali ya awamu ya sita inataka tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025? Serikali inataka kuona kila Mtanzania akiwa na maisha yanayoendana na kipato cha uchumi wa kati , kwa maana ya kipato kinachoweza kuchochea upatikanaji wa
    • afya bora,
    • elimu bora,
    • ikolojia bora,
    • ofisi zinazotoa huduma kwa kasi, kwa usawa na kwa wote, katika namna inayoendana na imani ya jamii ya kitaifa ambayo ni msingi wa ujenzi wa jamii ya amani.
    • na uchumi unaojali maslahi ya pamoja kwa ajiliya makundi yote ya watu.
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze kazi/miradi gani ili tuweze kufika huko? Serikali inasema kuwa kazi zifuatazo lazima zitekelezwe:
    • Kuchochea maendeleo ya rasilimali watu, usawa wa kijinsia, uwezeshaji wa makundi yote ya watu wakiwemo vijana, wanawake, wazee, watoto, wajane, yatima na walemavu;
    • Kuchochea utajiri wa Taifa kupitia uvunaji wa maliasili, uzalishaji mali, kubuni na kukuza kanda za kiuchumi;
    • Ujenzi wa taasisi za kiuchumi, kisiasa na kijamii zinazotoa huduma bora kwa kasi, kwa usawa na kwa wote ;
    • Kuimarisha usalama wa nchi na mahusiano ya kimataifa yaliyo bora zaidi;
    • Kutunza mazingira na kufanya menejimenti ya mabadiliko ya tabianchi;
    • Kujenga imani ya jamii na jamii ya amani kwa kukuza na kuhami mila, maadili na tunu za Taifa;
    • Kuweka mipango ya maendeleo yenye kuonyesga bayana vigezo vya ufanisi, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake.
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze vipi kazi/miradi hii ili tuweze kukamilisha safari yetu? Serikali inataka kutekeleza miradi yake kwa
    • kusimika uongozi bora,
    • kujenga mfumo wa sheria unaoruhusu utoaji wa haki,
    • kujihusisha na ujenzi wa miundo mbinu wezeshi kama vile upatikanaji wa nishati na maji,
    • kukusanya rasilimali fedha,
    • kuchochea ushirikishwaji wa makundi yote ya kijamii, na
    • kusimamia uwajibika wenye tija na kasi.
  5. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu tangu 2021 hadi 2025 inahitaji rasilimali/fedha kiasi gani? Kiasi cha rasilimali zinazohitajika ni Shilingi trilioni 115 ambazo ni
    • bajeti za miaka 5,
    • Bajeti za wizara zote,
    • Bajeti za Halmashauri zote,
    • na bajeti za mawakala wote wa serikali.
  6. Serikali ya awamu ya sita inataka tujueje kwamba tumefika mahali ambako serikali inataka kutufikisha? Kuna vipimo vya ufanisi vinaandaliwa kwa ajili ya kupima kasi na ufanisi wa
    • kila wizara,
    • kila Halmashauri,
    • kila wakala wa serikali,
    • na kwa kila mwaka.
Hivyo, kusudi kauli za Rais zipate msingi imara wa usimamizi na ufuatiliaji, namwalika Waziri wa Fedha kufanya haraka ya kukamilisha uandaaji na uzinduzi wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26.

Waraka huu unapaswa kujibu maswali yote haya kwa kina, Hivyo ni muhimu zaidi kuliko Ilani ya Uchaguzi kwani utafafanua mambo haya kwa kina katika njia inayoruhusu usimamizi na ufuatiliaji. Ilani ya chama ni muhimu, lakini inapaswa kubaki kama "kiambatanisho" kwenye andiko hilo muhimu.

Kwako Waziri Mwigulu Lameck Nchemba: Kasi ya Rais Samia ni kubwa kuliko kasi ya Ofisi yako. Kuna kitendeakazi muhimu kinakosekana mikononi mwa Rais--Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (21/22-25/26). Huu ndio waraka pekee unaopaswa kujibu maswali yote hapo juu kwa urefu na upana wake.

Changamka kuziba pengo hili ambalo ni kinyume cha mazoea bora ya kiutendaji yanayotutaka kuanza utekelezaji baada ya kukamilisha mipango.


 
Yote hayo ni UPUUZI MTUPU kama Mama hatahakikisha Katiba na Tume huru ya uchaguzi vinapatikana kabla ya uchaguzi wa October 26, 2025 ili kuhakikisha uchaguzi huo ni wa HAKI na HURU na siyo utakaojaa, wizi na mauaji.
Dah! Mzee wa "UPUUZI" upo?

Ngoja nikuulize swali:

Viongozi wa Chama cha siasa wanaovunja Katiba ya Chama chao, tena baada ya kushauriwa ipapsavyo na Msajili wa Vyama vya Siasa, halafu wakawa wanaendesha "Operesheni Haki" kwa ajili ya kudai "Katiba Mpya" itakayowasaidia kushika dola, wakipata dola hiyo watawezaje kuheshimu Katiba ya Nchi?

Jawabu ni hapana. Kwa hiyo, katika mazingira haya, dawa ya kuhakikisha haki inatawala ni ipi?
 
Kiongozi,

Nimekusoma. Naifahamui Ilani ya CCM vizuri katika sura zote mbili--uimara na udhaifu. Hivyo niseme yafuatayo:

1. Sehemu kubwa ya udhaifu wa Ilani ilizibwa kwa njia ya kauli za jukwaani wakati wa kampeni.

2. Ilani inajibu maswali matatu ya kwanza hapo juu, haina majibu kwa maswali baki matatu.

3. Bajeti iliyopitishwa Bungeni inahusu mpango wa maendeleo wa mwaka mmoja (2021/2022) pekee. Hii ni picha ndogo.

4. Ujenzi wa nchi unaanzia kwenye picha kubwa, kama ambavyo ujenzi wa nyumba unaanzia kwenye blue print yake.

Kwa sababu hizi, kuna umuhimu na uharaka wa kukamilisha mpango wa maendeleo wa miaka mitano ambao unafafanua ilani, na kuweka msingi wa mipango ya mwaka mmoja mmoja na bajeti zake.

Nami Mama Amon naipokea rejea yako ya hoja ulizozitoa kwenye bandiko kuu na hii inayojibu hoja zangu.

Ilani ya CCM inaweza kuwa na mapungufu kwa kuwa inahusu Sera za Chama za kuielekeza Serikali yake mwelekeo wa nchi Kijamii, Kisiasa, Kiuchumi na Kitejnolojia. Ilani hiyo imekuwa ikitayarishwa kutokana na malengo yaliyomo kwenye Dira ya Maendeleo ya Taifa, 2025 (Development Vision 2025). Kwa kuwa hiyo Dira haijarejewa, bado ni mwongozo halali wa maendeleo ya nchi hii.

Serikali uwajibika kuandaa na kutekeleza Mpango unaojibu Sera zilizomo kwenye Ilani ya Uchaguzi. Kabla ya kila bajeti, Wizara ya Fedha na Mipango huandaa mpango wa utekelezaji kwa mwaka wa fedha unaofuata, ambao ndio huwa mwongozo wa bajeti husika.

Umetoa hoja kwamba kuna umuhimu na uharaka wa kukamilisha mpango wa maendeleo wa miaka mitano ambao unafafanua ilani, na kuweka msingi wa mipango ya mwaka mmoja mmoja na bajeti zake. Naamini umepata na kupitia Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2021/22 - 2025/26, nakala ambayo nimeiambatanisha. ITAPENDEZA kupata maoni yako.View attachment 26.pdf
 
Katiba ya Chadema iliyovunjwa imedhulumu Watanzania wangapi? Imewabambikia kesi Watanzania wangapi na kuwafunga au kuwapora billions kama faini? Katiba ya Chadema iliyovunjwa imeua Watanzania wangapi nchini? Hebu jaribu kutafakari kwa kina badala ya KUKURUPUKA.
Dah! Mzee wa "UPUUZI" upo?

Ngoja nikuulize swali:

Viongozi wa Chama cha siasa wanaovunja Katiba ya Chama chao, halafu wakawa wanaendesha "Operesheni Haki" kwa ajili ya kudai "Katiba Mpya" itakayowasaidia kushika dola, wakipata dola hiyo watawezaje kuheshimu Katiba ya Nchi?

Jawabu ni hapana. Kwa hiyo, katika mazingira haya, dawa ya kuhakikisha haki inatawala ni ipi?
 
View attachment 1819542
Rais Samia Suluhu Hassan akiwa Mwanza akitafakari juu ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26

Tangu serikali ya wamu ya sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, ilipoanza kazi nimekuwa najiuliza maswali yafuatayo, kama sehemu ya kazi yangu ya utafiti:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi?
  2. Serikali ya awamu ya sita inataka sisi kama Taifa tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025?
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze kazi/miradi gani ili sisi kama Taifa tuweze kufika huko?
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze vipi kazi/miradi husika ili sisi kama Taifa tuweze kukamilisha safari yetu?
  5. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu sisi kama Taifa tangu 2021 hadi 2025 inahitaji rasilimali/fedha kiasi gani?
  6. Serikali ya awamu ya sita inafikiri kwamba sisi kama Taifa tutajuaje kuwa tumefika mwisho wa safari yetu ya miaka 5?
Nilikuwa nasubiri kwa hamu Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26 ili kuona majibu ya maswali haya. Lakini, kabla mpango huo haujazinduliwa, naona maswali haya yameanza kujibiwa kwa kina kupitia hotuba za Rais.

Tayari Rais Samia amemaliza ziara ya kikazi mkoani mwanza alikokaa kwa siku tatu. Alisema kuwa Kanda ya Ziwa ni Ukanda wa Kiuchumi utakaoitumia Mwanza kama kituo kikubwa cha biashara katika nchi za Maziwa Makuu.

Akiwa huko alizindua miradi kadhaa ikiwemo mradi wa maji, mradi wa reli ya kimataifa, mradi wa chelezo ya meli, mradi wa daraja la Ziwa Viktoria, na miradi ya kuwawezesha vijana kunufaika na fursa za ajira 8,000,000 zinazotengenezwa na serikali kwa ajili yao.

Rais alitaja sekta zifuatazo kama vyanzo vya ajira za vijana hawa: mradi wa umeme wa mwalimu Nyerere, Miradi ya Ujenzi wa Barabara, na Mradi wa bomba la mafuta. Pia alitaja miradi ya kilimo, miradi ya ufugaji, miradi ya uvuvi, na miradi ya TEHAMA inayotekelezwa kupitia ubia wa serikali na sekta.

Kuhusu suala la ajira, RC Kafulira alimwahidi Rais Samia kwamba mkoa wake wa Simiyu unakusudia kuchangia 2.5% ya ajira zote, yaani ajira 200,000, kutokana na kuzalisha ajira kupitia minyororo ya ongezeko la thamani ya huduma na bidhaa zilizoko katika sekta mbalimbali mkoani humo.

Kwa mujibu wa hotuba ya jana ya Waziri wa Tamisemi, Ummy Mwalimu,
asilimia baki ya ajira itazalishwa nchini kote katika maeneo yafuatayo: wilaya 126, halmashauri 184, kata 3,956, vijiji 12,319, vitongoji 64,384, na mitaa 4,263.

Na kwa mujibu wa
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, katika mwaka 2019, pato la Kanda ya Ziwa lilikuwa TZS bilioni 34, sawa na 25.9% ya Pato la Taifa.

Aidha, Luoga anasema kuwa Kanda ya Ziwa huzalisha zaidi ya 90% ya dhahabu yote nchini, 50% ya pamba na kahawa na zaidi ya 95% ya mauzo ya samaki ndani na nje ya nchi.

Ziara ya Rais Samia huko Kanda ya Ziwa Viktoria ni mwendelezo wa pilika zake za kujipambanua kama mjasiriadola wa kike kwa kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii ili kuwaeleza ndoto aliyo nayo kuhusu Tanzania mpya chini ya serikali ya awamu ya sita.

Kwanza alikutana na wazee kupitia wazee wa Dar es Salaam, kisha akakutana na kina mama kupitia kina mama wa Dodoma, na leo amekutana na vijana kupitia vijana wa Mwanza.

Nimesikiliza hotuba zake zote tangu Dar es Salaam, Dodoma hadi Mwanza. Ni hotuba nzuri kwa ajili ya kueleza ndoto aliyo nayo juu ya Tanzania mpya.

Kutokana na kauli zake nilizozisikia mpaka sasa, Rais anayo majawabu yafuatayo, kwa maswali yaliyotajwa hapo juu:

  1. Serikali ya awamu ya sita inasema kwamba kwa sasa mwaka 2021 sisi kama Taifa tuko wapi? Serikali inasema kuwa hapa tulipo kuna
    • magonjwa,
    • ujinga,
    • ikolojia duni,
    • ofisi za utawala zinazosuasua katika kutoa huduma kwa watu,
    • na uchumi usiojali maslahi ya pamoja kwa ajili ya makundi yote ya watu.
  2. Serikali ya awamu ya sita inataka tuwe tumefika wapi ifikapo mwaka 2025? Serikali inataka kuona kila Mtanzania akiwa na maisha yanayoendana na kipato cha uchumi wa kati , kwa maana ya kipato kinachoweza kuchochea upatikanaji wa
    • afya bora,
    • elimu bora,
    • ikolojia bora,
    • ofisi zinazotoa huduma kwa kasi, kwa usawa na kwa wote, katika namna inayoendana na imani ya jamii ya kitaifa ambayo ni msingi wa ujenzi wa jamii ya amani.
    • na uchumi unaojali maslahi ya pamoja kwa ajiliya makundi yote ya watu.
  3. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze kazi/miradi gani ili tuweze kufika huko? Serikali inasema kuwa kazi zifuatazo lazima zitekelezwe:
    • Kuchochea maendeleo ya rasilimali watu, usawa wa kijinsia, uwezeshaji wa makundi yote ya watu wakiwemo vijana, wanawake, wazee, watoto, wajane, yatima na walemavu;
    • Kuchochea utajiri wa Taifa kupitia uvunaji wa maliasili, uzalishaji mali, kubuni na kukuza kanda za kiuchumi;
    • Ujenzi wa taasisi za kiuchumi, kisiasa na kijamii zinazotoa huduma bora kwa kasi, kwa usawa na kwa wote ;
    • Kuimarisha usalama wa nchi na mahusiano ya kimataifa yaliyo bora zaidi;
    • Kutunza mazingira na kufanya menejimenti ya mabadiliko ya tabianchi;
    • Kujenga imani ya jamii na jamii ya amani kwa kukuza na kuhami mila, maadili na tunu za Taifa;
    • Kuweka mipango ya maendeleo yenye kuonyesga bayana vigezo vya ufanisi, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake.
  4. Serikali ya awamu ya sita inataka tutekeleze vipi kazi/miradi hii ili tuweze kukamilisha safari yetu? Serikali inataka kutekeleza miradi yake kwa
    • kusimika uongozi bora,
    • kujenga mfumo wa sheria unaoruhusu utoaji wa haki,
    • kujihusisha na ujenzi wa miundo mbinu wezeshi kama vile upatikanaji wa nishati na maji,
    • kukusanya rasilimali fedha,
    • kuchochea ushirikishwaji wa makundi yote ya kijamii, na
    • kusimamia uwajibika wenye tija na kasi.
  5. Serikali ya awamu ya sita inasema kuwa safari yetu tangu 2021 hadi 2025 inahitaji rasilimali/fedha kiasi gani? Kiasi cha rasilimali zinazohitajika ni Shilingi trilioni 115 ambazo ni
    • bajeti za miaka 5,
    • Bajeti za wizara zote,
    • Bajeti za Halmashauri zote,
    • na bajeti za mawakala wote wa serikali.
  6. Serikali ya awamu ya sita inataka tujueje kwamba tumefika mahali ambako serikali inataka kutufikisha? Kuna vipimo vya ufanisi vinaandaliwa kwa ajili ya kupima kasi na ufanisi wa
    • kila wizara,
    • kila Halmashauri,
    • kila wakala wa serikali,
    • na kwa kila mwaka.
Hivyo, kusudi kauli za Rais zipate msingi imara wa usimamizi na ufuatiliaji, namwalika Waziri wa Fedha kufanya haraka ya kukamilisha uandaaji na uzinduzi wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa 2021/22 hadi 2025/26.

Waraka huu unapaswa kujibu maswali yote haya kwa kina, Hivyo ni muhimu zaidi kuliko Ilani ya Uchaguzi kwani utafafanua mambo haya kwa kina katika njia inayoruhusu usimamizi na ufuatiliaji. Ilani ya chama ni muhimu, lakini inapaswa kubaki kama "kiambatanisho" kwenye andiko hilo muhimu.

Kwako Waziri Mwigulu Lameck Nchemba: Kasi ya Rais Samia ni kubwa kuliko kasi ya Ofisi yako. Kuna kitendeakazi muhimu kinakosekana mikononi mwa Rais--Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (21/22-25/26). Huu ndio waraka pekee unaopaswa kujibu maswali yote hapo juu kwa urefu na upana wake.

View attachment 1820640
Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha

Kwa hiyo basi, changamka kuziba pengo hili ambalo ni kinyume cha mazoea bora ya kiutendaji yanayotutaka kuanza utekelezaji baada ya kukamilisha mipango.

Nimechukua machache kutoka kwenye uzi wako hapo juu, ambayo ni haya hapa chini yaliyosababishwa na serekali zilizoongozwa na Chadema kuanzia awamu ya 1 hadi ya 5.
CCM wamechukua awamu ya 6, na sasa ndiyo wanataka kurekebisha madudu ya Chadema ya miaka 60 iliyopita!

1623851741986.png
 
Yote hayo ni UPUUZI MTUPU kama Mama hatahakikisha Katiba na Tume huru ya uchaguzi vinapatikana kabla ya uchaguzi wa October 26, 2025 ili kuhakikisha uchaguzi huo ni wa HAKI na HURU na siyo utakaojaa, wizi na mauaji.

Mkuu Jibu la hoja hiyo kutoka kwake Mama Amon linakutosha. Isitoshe yeye ametoa hoja kuhusu Mpango wa Maendeleo wewe unaendelea kucheza ngoma ya hao wanaotaka kuingia madarakani pasipo kueleza watafanya nini wakipata hayo madaraka!!! Au wewe ndio umetoa UPUUZI MTUPU

Dah! Mzee wa "UPUUZI" upo?

Ngoja nikuulize swali:

Viongozi wa Chama cha siasa wanaovunja Katiba ya Chama chao, halafu wakawa wanaendesha "Operesheni Haki" kwa ajili ya kudai "Katiba Mpya" itakayowasaidia kushika dola, wakipata dola hiyo watawezaje kuheshimu Katiba ya Nchi?

Jawabu ni hapana. Kwa hiyo, katika mazingira haya, dawa ya kuhakikisha haki inatawala ni ipi?

Ni sahihi kabisa ulichohoji kuwa wasioheshimu Katiba ya Chama chao ndio hao hao wanadai Katiba mpya ya JMT. Nyuma ya madai yao wana imani kuwa Katiba mpya ndiyo mwarobaini wa kuwaingiza Ikulu.
 
Practicality ikiwa wazi mtaani na kwa wananchi wala haitahitaji nguvu na theory nyingi kuwaaminisha watu kwamba we are okay.... Hizi Theory za kwenye makaratasi ni nyingi ila impact yake ni ndogo kwa wengi...

Ila ndio siasa siku hizi world wide (fanya vitu minor / short term vya kuonekana, piga propaganda za hapa na pale punde si punde miaka kumi imepita anakuja mwingine) huyo mwingine analaumu aliyetoka na kufanya yale yale ya muda mfupi..., Ila tunakoelekea kwa hizi fikra za vijana wajiajiri na wajijue wenyewe wakati keki inaliwa na wachache.... Amini, Amini ninakwambia...., Generations zijazo watateseka kwa upuuzi uliofanywa / ulioachwa uendelee na generation hii...
 
Back
Top Bottom