Rais Samia ameanzia Mwanza Kujenga Hekalu letu: Tayari kamaliza msingi, kuta na linta, bado kuezeka

Rais Samia ameanzia Mwanza Kujenga Hekalu letu: Tayari kamaliza msingi, kuta na linta, bado kuezeka

Practicality ikiwa wazi mtaani na kwa wananchi wala haitahitaji nguvu na theory nyingi kuwaaminisha watu kwamba we are okay.... Hizi Theory za kwenye makaratasi ni nyingi ila impact yake ni ndogo kwa wengi...

Ila ndio siasa siku hizi world wide (fanya vitu minor / short term vya kuonekana, piga propaganda za hapa na pale punde si punde miaka kumi imepita anakuja mwingine) huyo mwingine analaumu aliyetoka na kufanya yale yale ya muda mfupi..., Ila tunakoelekea kwa hizi fikra za vijana wajiajiri na wajijue wenyewe wakati keki inaliwa na wachache.... Amini, Amini ninakwambia...., Generations zijazo watateseka kwa upuuzi uliofanywa / ulioachwa uendelee na generation hii...
Kwa hiyo ushauri wako ni upi kuhusu namna ya kusonga mbele?
 
Nimechukua machache kutoka kwenye uzi wako hapo juu, ambayo ni haya hapa chini yaliyosababishwa na serekali zilizoongozwa na Chadema kuanzia awamu ya 1 hadi ya 5.
CCM wamechukua awamu ya 6, na sasa ndiyo wanataka kurekebisha madudu ya Chadema ya miaka 60 iliyopita!

View attachment 1820668

Nimeelewa sentensi za kwanza isipokuwa sentensi hii: "CCM wamechukua awamu ya 6, na sasa ndiyo wanataka kurekebisha madudu ya Chadema ya miaka 60 iliyopita!" Hata hivyo nitakujibu kama ifuatavyo:

Ibara ya 9(i) ya Katiba ya Tanzania (1977) inasema kuwa kazi ya serikali ni kutumia kila tone la rasilimali za nchi kuwahudumia wajinga, wagonjwa, na maskini kusudi siku moja Tanzania isiwe na wajinga, wagonjwa, na maskini.

Hii ni ndoto. Ni sawa na nyota ya alfajiri inayowaongoza mabaharia. Hawawezi kuifikia lakini inawafikisha mwaloni wanakotaka kwenda. Ni vivyo hivyo katika kuendesha nchi.

Kwa hiyo, ukitaka kukosoa utendaji wa serikali iliyo marakani kwa kuanzia kwenye ujinga, ugonjwa na umaskini, unapaswa kuonyesha kwamba kuna RETARDATION badala ya ACCELLERATION. Hujaonyesha lolote kati ya haya mawili.

Kwa hiyo, bado hujafanikisha kusanifu hoja yako.
 
Kwa hiyo ushauri wako ni upi kuhusu namna ya kusonga mbele?
Kwanza Kabisa..., kuendelea kama nchi tusiwe na nchi ya Samia, Mwendazake, Jakaya, au Yoyote atakayekuja kesho au keshokutwa.....

Kama taifa na kwa kuhusisha wadau na wataalamu lazima tujue ni wapi tunataka kwenda na kwa kutumia njia gani Sio kwa miaka kumi tu..., bali kwa miaka 50 mpaka 100 inayokuja..., yoyote atakayekuja madarakani ni kuhakikisha ile master plan ya nchi tuliyopanga inafuatwa (kwa mujibu wa wataalamu na sio wanasiasa) na kuendelezwa... Vipaumbele vidogo vidogo viwe ni kuweka nyufa na kuimarisha long term plans...

Kilichopo sasa ni muendelezo wa bandika bandua anzisha, acha kila kukicha... Siasa zinakuwa nyingi..., ukiangalia hata kero hazijabadilika ni zile zile miaka nenda rudi.., ila kila mtu akija ni kupapasa papasa tu... ili aonekane mimi nilifanya hiki au kile...

Na hii tabia ya kuhusisha maendeleo ya nchi na mtu au Chama fulani ( ni kuwatenga baadhi ya watu ambao nao ni nguvu kazi) Maendeleo yawe inclusive na yawahusishe wadau wote no matter Chama chao au itikadi zao....
 
Kiongozi,

Nimekusoma. Naifahamui Ilani ya CCM vizuri katika sura zote mbili--uimara na udhaifu. Hivyo niseme yafuatayo:

1. Sehemu kubwa ya udhaifu wa Ilani ilizibwa kwa njia ya kauli za jukwaani wakati wa kampeni.

2. Ilani inajibu maswali matatu ya kwanza hapo juu, haina majibu kwa maswali baki matatu.

3. Bajeti iliyopitishwa Bungeni inahusu mpango wa maendeleo wa mwaka mmoja (2021/2022) pekee. Hii ni picha ndogo.

4. Ujenzi wa nchi unaanzia kwenye picha kubwa, kama ambavyo ujenzi wa nyumba unaanzia kwenye blue print yake.

Kwa sababu hizi, kuna umuhimu na uharaka wa kukamilisha mpango wa maendeleo wa miaka mitano ambao unafafanua ilani, na kuweka msingi wa mipango ya mwaka mmoja mmoja na bajeti zake.
Tatizo ni kwamba ujenzi wa maendeleo ya nchi yetu kupitia ccm, yanaishia kwenye hiyo blue print yalipo anzia!
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Tatizo ni kwamba ujenzi wa maendeleo ya nchi yetu kupitia ccm, yanaishia kwenye hiyo blue print yalipo anzia!
Naona umeweka chumvi (hyperbole) hapa: "maendeleo ya nchi yetu kupitia ccm, yanaishia kwenye hiyo blue print yalipo anzia."

Ukiangalia performance metrics za nchi tangu uhuru hadi leo kuna mabadiliko yametokea. Sio kweli kwamba nchi inafanya mark-timing.

Kwa hiyo, kusudi uaminike inabidi uongee kwa takwimu zenye uhalisia.
 
Kwanza Kabisa..., kuendelea kama nchi tusiwe na nchi ya Samia, Mwendazake, Jakaya, au Yoyote atakayekuja kesho au keshokutwa.....

Kama taifa na kwa kuhusisha wadau na wataalamu lazima tujue ni wapi tunataka kwenda na kwa kutumia njia gani Sio kwa miaka kumi tu..., bali kwa miaka 50 mpaka 100 inayokuja..., yoyote atakayekuja madarakani ni kuhakikisha ile master plan ya nchi tuliyopanga inafuatwa (kwa mujibu wa wataalamu na sio wanasiasa) na kuendelezwa... Vipaumbele vidogo vidogo viwe ni kuweka nyufa na kuimarisha long term plans...

Kilichopo sasa ni muendelezo wa bandika bandua anzisha, acha kila kukicha... Siasa zinakuwa nyingi..., ukiangalia hata kero hazijabadilika ni zile zile miaka nenda rudi.., ila kila mtu akija ni kupapasa papasa tu... ili aonekane mimi nilifanya hiki au kile...

Na hii tabia ya kuhusisha maendeleo ya nchi na mtu au Chama fulani ( ni kuwatenga baadhi ya watu ambao nao ni nguvu kazi) Maendeleo yawe inclusive na yawahusishe wadau wote no matter Chama chao au itikadi zao....
Umeandika mawazo murua.
Lakini yako katika ngazi ya swali hili: what have we to do?
Hujasema kitu kuhusu swali: how do we do it?
Unaweza kuongeza nyama kidogo kwenye skeleton hiyo hapo juu kwa kujibu swali la pili?
 
Naona umeweka chumvi (hyperbole) hapa: "maendeleo ya nchi yetu kupitia ccm, yanaishia kwenye hiyo blue print yalipo anzia."

Ukiangalia performance metrics za nchi tangu uhuru hadi leo kuna mabadiliko yametokea. Sio kweli kwamba nchi inafanya mark-timing.

Kwa hiyo, kusudi uaminike inabidi uongee kwa takwimu zenye uhalisia.
Ni kweli tumesogea sogea, Lakini kama ulivyo mjibu jamaa hapo juu, kuhusu mabaharia kuongozwa na nyota ambayo ipo kusiko fikika, nikubalie kwamba mipango mingi ya maendeleo ipo kwenye makaratasi na haitafsiriki kwenye uhalisia wa maisha ya kila siku, na maendeleo!
Pia, Mama Amoni, tupo nyuma ya maendeleo tuliyo paswa kuifikia kwa miongo kadhaa!
 
Umeandika mawazo murua.
Lakini yako katika ngazi ya swali hili: what have we to do?
Hujasema kitu kuhusu swali: how do we do it?
Unaweza kuongeza nyama kidogo kwenye skeleton hiyo hapo juu kwa kujibu swali la pili?
Siyo swali langu, lakini msingi wa how to do it, mama Amoni, upo wazi, KATIBA! South Korea mwaka 1978 walikuwa nyuma yetu kiuchumi, kupaa kwao kiuchumi kupo kwenye msingi wa ubora wa katiba yao!
 
Tuongelee hii sentensi hapo juu.
Unaweza kuweka mkeka wa ushahidi hapa?
Ukifanya hivyo mjadala utanoga haswa!
Elimu yetu kwa mfano; Tupo kwenye kukariri kama tulivyo kopi kwa Wakomunisti! Mwalimu ana majibu yote, wanafunzi wana mkariri kwa lengo la final exams kisha cheti, ili uajiriwe!
 
Nimeelewa sentensi za kwanza isipokuwa sentensi hii: "CCM wamechukua awamu ya 6, na sasa ndiyo wanataka kurekebisha madudu ya Chadema ya miaka 60 iliyopita!" Hata hivyo nitakujibu kama ifuatavyo:

Ibara ya 9(i) ya Katiba ya Tanzania (1977) inasema kuwa kazi ya serikali ni kutumia kila tone la rasilimali za nchi kuwahudumia wajinga, wagonjwa, na maskini kusudi siku moja Tanzania isiwe na wajinga, wagonjwa, na maskini.

Hii ni ndoto. Ni sawa na nyota ya alfajiri inayowaongoza mabaharia. Hawawezi kuifikia lakini inawafikisha mwaloni wanakotaka kwenda. Ni vivyo hivyo katika kuendesha nchi.

Kwa hiyo, ukitaka kukosoa utendaji wa serikali iliyo marakani kwa kuanzia kwenye ujinga, ugonjwa na umaskini, unapaswa kuonyesha kwamba kuna RETARDATION badala ya ACCELLERATION. Hujaonyesha lolote kati ya haya mawili.

Kwa hiyo, bado hujafanikisha kusanifu hoja yako.
Umejibu vyema.

In fact, kuna retardation across the board and I can prove that all day long.

Mathalani, vita dhidi ya ujinga chini ya awamu ya 1 (ambayo walau ilijitahidi kuwa na dira ya kiuongozi kupita awamu zote zilizofuata) ilikuwa ni kuwaondoa watu kutoka kwenye illiteracy - ulikuwa mkakati sahihi kwa wakati sahihi.

Baada ya Mwalimu (RIP baba yetu) kuondoka madarakani, tumeshuhudia downward trajectory kwenye eneo hili ambayo imekuja kuji manifest zaidi kwenye awamu ya 5 ambapo tumeshuhudia hadi maprofesa wana behave as if hawajawahi kuona chumba cha darasa hata siku moja. No wonder hata yule mbunge Musukuma amekuwa na audacity ya kuwakejeli hadi maprofesa ambao hata kumjibu wameshindwa - si kwa kumpuuza bali they are fully aware kwamba Musukuma has a point!

Ujinga mwingine ni ule wa mtu aitwaye "msomi" ambaye anatarajiwa kuwa na ufahamu wa kutosha kuwa mathalani yeye akiwa ni mgonjwa wa vidonda vya tumbo, anapaswa kuvikwepa kabisa vyakula vyenye asili ya tindikali (acid) na kwamba akiviendekeza vinaweza kumdhuru hadi kumletea umauti. Tuna "msomi" mmoja tena "kiongozi mkuu" akafanya kinyume chake - akaishia kufa kwa ujinga wake pamoja na "usomi" wake. This is just one of the so many examples of RETARDATION chini ya serekali ya Chadema kwa miaka 60 iliyopita!
 
Katiba ya Chadema iliyovunjwa imedhulumu Watanzania wangapi? Imewabambikia kesi Watanzania wangapi na kuwafunga au kuwapora billions kama faini? Katiba ya Chadema iliyovunjwa imeua Watanzania wangapi nchini? Hebu jaribu kutafakari kwa kina badala ya KUKURUPUKA.
Ubaya wa itikadi ya kuthamini matokeo bila kujali uharamu wa mbinu iliyotumika haubadiliki kwa sababu tu kwamba kuna madhara kidogo au madhara makubwa. Kimaadili na kisheria, kifo cha mtu mmoja ni sawa na kifo cha watu 100.

Hivyo, uovu wa kuvunja Katiba ya Chama cha siasa unabeba uzito ule ule sawa na kuvunja Katiba ya nchi.

Uovu wa kuua mtu mmoja kwa kutumia ajali feki ya barabarani ili kuharibu ushahidi unaoweza kukitia hatiani chama cha siasa ni sawa na uovu wa kitendo cha kuua watu 20 na kutupa miili yao ziwani, etc, etc.

Uovu wa kumdhulumu mtu aliyekukopesha laki moja, wakati wewe ni kiongozi wa chama ngazi ya Kanda, na uovu wa kudhulumu mamilioni vina uzito sawa.

Kwa hakika, hakuna mahali nimekurupuka...
 
This is just one of the so many examples of RETARDATION chini ya serekali ya Chadema kwa miaka 60 iliyopita!
Naona umeteleza tena kwa kuandika "Chadema" pasipo mahali pake.
Mifano yako ni mizuri lakini inapapasa (ni tangential) duara la tatizo tunalolijadili.

Chukua Mipango ya Maendeleo ya miaka kumi na tano iliyopita, angalau.

Humo kuna performance metrics. Awamu kwa awamu onyesha retardation hiyo.
Namna hiyo tutakwenda swa.
 
Tanzania Bora haitakuja kwa hotuba nzuri tu. Kama hotuba nzuri zipo zile za baba wa Taifa. Nchi zote mahitaji vitendo katika kutatua keto zinazowakabili vijana wetu, badala ya maneno matamu ya kisiasa. Wanasiasa waache kukwepa kushughulikia keto muhimu. Idadi kubwa ya vijana hawana ajira, serikali ije na suruhu ya Hilo, badala ya kuhadaa watu eti wanaweza kujiajiri. Wapi? Wapi? Lazima miradi na uwekezaji mkubwa ufanyike kuwapa ajira watu. Nchini Afrika ya kusini, mazingira ya uwekezaji wa kampuni za kichina wanajenga viwanda na kutatua tatizo la vijana kukosa ajira angalau hata Kama haliishi kabisa. Ebu tuache upambe usiosaidia. Labda Kama lengo lako no kupewa wadhifa serikalini
 
Umeandika mawazo murua.
Lakini yako katika ngazi ya swali hili: what have we to do?
Hujasema kitu kuhusu swali: how do we do it?
Unaweza kuongeza nyama kidogo kwenye skeleton hiyo hapo juu kwa kujibu swali la pili?
I Think I have already said it..., If I come with my plans here they will be my plans which are not inclusive (all plans especially long term should involve all stakeholders) How do we do it ? (Involve all the stakeholders na kufanya due dilligence ya pros and cons ya kile kinachotakiwa kufanyika in transparent way) In technical things we needs technicians and not politicians...

Anyway any plans we make should be socially, economically and environmentally viable..., its a shame kwa nchi tajiri watu hawana security wala guarantee ya kesho yao (maziwa matatu makubwa, bahari, vivutio vya wanyama, to name just a few)..., Ili kufanikisha plans zozote zinazotakiwa kufanyika inabidi wananchi waelewe kabisa tupo wapi na wapi tunatakiwa kwenda na tutafika lini, Sio sasa kila mtu anavutia kwake na badala ya kuwa na politics of development tuna politics of survival (Chama kilichopo Madarakani) na Politics of Attack (kwa wale wanaotaka kuingia)...

Kumbuka people don't ask for much..., Just make sure they have guarantee of food on their tables, warmth, clothes, when sick they get looked after their children being educated and their tomorrow (old age) is not a nightmare (which will be with this crop of youngsters whom will have no pensions)..,

To ask people to fend for themselves is just politicking (majority are not made like that) and since our country is rich beyond recognition I think its possible to have majority of middle income people;

Our enemies have not changed; Malazi; Ujinga na Umasikini...., Sasa kama hata kuondoa ujinga mpaka mtu uende uuze shamba ili upate elimu ambayo mwisho wa siku haikusaidii hata kukomboa shamba alilouza babu yako (lazima ujiulize maybe..., just maybe we are going the wrong way AKA Tumepotea...
 
UPUUZI MTUPU!!!! Wewe kufanya ufojaji wa signatures huoni kama ni uovu!!! Na kwa ufinyu mkubwa wa akili uliokuwa nao unataka kufananisha uvunjaji wa katiba wa Chadema ambao haukuathiri Mtanzania yeyote yule kwa senti yake hata moja au uhai wake unataka kufananisha na uvunjanji wa katiba wa mwendazake ambao umegharimu walipa kodi trillions za pesa zao kuchotwa kinyemela bila idhini ya Wabunge, Wafanyakazi, Wakulima na Wafanyabishara kudhulumiwa billions zao kama siyo trillions, watu kubambikiwa kesi, kufungwa na hata kuuawa huku wakiwa hawana hatia yoyote ile.
Itikadi ya kuthamini matokeo bila kujali uharamu wa mbinu iliyotumika haibadiliki kwa sababu tu kwamba kuna madhara kidogo au madhara makubwa. Kimaadili na kisheria, kifo cha mtu mmoja ni sawa na kifo cha watu 100.

Hivyo, uovu wa kuvunja Katiba ya Chama cha siasa unabeba uzito ule ule sawa na kuvunja Katiba ya nchi.

Uovu wa kuua mtu mmoja kwa kutumia ajali feki ya barabarani ili kuharibu ushahidi unaoweza kukitia hatiani chama cha siasa ni sawa na uovu wa kitendo cha kuua watu 20 na kutupa miili yao ziwani, etc, etc.

Uovu wa kumdhulumu mtu aliyekukopesha laki moja, wakati wewe ni kiongozi wa chama ngazi ya Kanda, na uovu wa kudhulumu mamilioni vina uzito sawa.

Kwa hakika, hakuna mahali nimekurupuka...
 
Naona umeteleza tena kwa kuandika "Chadema" pasipo mahali pake.
Mifano yako ni mizuri lakini inapapasa (ni tangential) duara la tatizo tunalolijadili.

Chukua Mipango ya Maendeleo ya miaka kumi na tano iliyopita, angalau.

Humo kuna performance metrics. Awamu kwa awamu onyesha retardation hiyo.
Namna hiyo tutakwenda swa.
Hapana, that's a wrong approach. Approach hiyo ndiyo inatufanya tuwe tujisifu hata tusivyostahili.

Bigger picture - linganisha mwaka # 1 tulikuwa wapi na mwaka # 60 tuko wapi. Period.
Hizo "performance metrics" hapo kati pretty much zinaji even out zenyewe (in my opinion there are more negatives than positives).

By the way, ninatumia jina la "Chadema" nilidhani ungeelewa - kama hujaelewa nimeitumia katika context gani then hata hii discussion ni kupotezeana muda tu.
 
UPUUZI MTUPU!!!! Wewe kufanya ufojaji wa signatures huoni kama ni uovu!!! Na kwa ufinyu mkubwa wa akili uliokuwa nao unataka kufananisha uvunjaji wa katiba wa Chadema ambao haukuathiri Mtanzania yeyote yule kwa senti yake hata moja au uhai wake unataka kufananisha na uvunjanji wa katiba wa mwendazake ambao umegharimu walipa kodi trillions za pesa zao kuchotwa kinyemela bila idhini ya Wabunge, Wafanyakazi, Wakulima na Wafanyabishara kudhulumiwa billions zao kama siyo trillions, watu kubambikiwa kesi, kufungwa na hata kuuawa huku wakiwa hawana hatia yoyote ile.
Mawazo haya hayajabadilisha mtazamo wangu hata kwa nukta moja.

Kuhusu habari ya "ufojaji wa signatures," umepotoshwa.

Signature ya Mnyika iliyo kwenye nyaraka zilizopelekwa NEC ni original.

Mwulizeni Mnyika wenu aseme ukweli.

Lakini pili, mie sio muumini wa moral proportionalism.

Nimefundishwa, nikaamini, naamini na nitaendelea kuamini kwamba: one may never violate a negative duty as a means to achieve a good outcome.

Hiyo ndiyo sababu siabudu katika makanisa ambayo viongozi wake wanafundisha itikadi hii ambayo inaitwa Caiaphus Ideology (John 18:13).

Kuelewa sababu za msimamo wangu, soma kiambatanisho kifuatacho.
 

Attachments

Your ability to measure one wrong to another is ZERO therefore I am not surprised at all.
Mawazo haya hayajabadilisha mtazamo wangu hata kwa nukta moja.

Kuhusu habari ufojaji wa signatures, umepotoshwa.

Signature ya Mnyika iliyo kwenye nyaraka zilizopelekwa NEC ni original.

Mwulizeni Mnyika wenu aseme ukweli.

Lakini pili, mie sio muumini wa moral proportionalism.

Nimeamini, naamini na nitaendelea kuamini kuwa one may never violate a negative duty as a means to achieve a good outcome.

Hiyo ndiyo sababu siabudu katika makanisa yanayokumbatia itikadi hii ambayo inaitwa Caiphus Ideology.
 
Back
Top Bottom