Rais Samia ameanzia Mwanza Kujenga Hekalu letu: Tayari kamaliza msingi, kuta na linta, bado kuezeka

Mosi, contextual meaning is always ambiguous.

Hivyo, lazima wewe kama mwandishi uweke bayana unalokusudia pale una=oandika neno "Chadema."

Pili, unasema: "Hizo performance metrics hapo kati pretty much zinaji even out zenyewe, in my opinion there are more negatives than positives."

Katika debate, kauli hii haiwezi kukupa score.

Unapaswa kuweka ushahidi mezani ili kuilinda.
 
Asante kwa kiunganishi cha Rasimu ya FYDP III.
Narudi hapa hapa na review kamili very soon.....
 
Njaa na vilio kila kona , mafuta juu, mchele juu, serikali haina pesa , miradi inajiendea kwa kusua sua, Hakuna shift za 24hr.
 
Nilichojifunza hapa wewe ni meandishi mzuri ila sijaona jipya ni kama risala ilioandikwa kwa ustadi.

Baada ya awamu ya Mkapa na JK CCM haijawahi kuwa na mipango yenye tija ya muda mrefu kwa nchi hii.

Bahati mbaya sana Mwendazake hakuwa muumini wa long vision plan, aliacha makovu ambayo Mama Samia anapambana nayo sasa mpaka yaje yakae sawa itachukuwa muda kidogo
 
Hivi mkuu kweli unaweza kusema Kikwete alikuwa na long term plan kumzidi Magufuli? Yaani katika nchi hii ni rahsi sana kutawala maana wengi ni mazo...bi. Magufuli atabaki kuwa ndo Rais aliyeangalia mbali sana kuliko hao wanaohangaika kufurahisha watu.
 
Hamna kitu mnamahaba tu na mwendazeke, hakuwa na chembe ya sifa za uongozi.
 
Niseme mawili.

Kwanza, hotuba nzuri per se sio kosa. Lakini niongeze kusema kuwa, hapa siongelei hotuba nzuri pekee. Naongelea hotuba na mipango ya utekelezaji inayotekelezwa tangu sasa kwa mujibu wa hotuba husika katika ziara ya Rais Samia.

Sayansi ya matendo yenye ufanisi (praxiology) inatufundisha kuwa nadharia, utendaji, na tathmini (theory, action, review) vinakwenda pamoja. Kwa hiyo, hotuba nzuri ni mwanzo mzuri unaopapswa kusifiwa, labda kama unachuki binafsi na mtoa hotuba. Hivyo, baada ya hotuba nzuri, sasa yafaa tuongelee haya mengine bila kuziponda au kuponda mleta hotuba: utendaji na tathmini.

Pili, unaongelea lengo la "kupewa wadhifa serikalini" kana kwamba hii ni dhambi. Kiu ya madaraka ndiyo kanuni pekee inayosukuma gurudumu la maisha katika sekta zote za maisha ya watu.

Kuna madara ya kiuchumi, madaraka ya kisiasa, madaraka ya kidini, madaraka ya kijamii, madaraka ya kimaarifa, madaraka ya kimapenzi, na orodha inaendelea. kwa hiyo, by itself, lengo la "kupewa wadhifa serikalini" haliwezi kuwa dhambi.

Madaraka ni matamu, na ndio maana wakati mwingine yanatafutwa kwa "kupenyeza rupia," kama unavyojua vizuri. Kinachotofautisha wenye madaraka ni jinsi walivyoyapata na jinsi wanavyoyatumia, basi.
 
Mkuu,
Salama? Ombi lako nimelifanyia kazi, na majibu yangu yanapatyikana hapa: Uhakiki wa Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Serikali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…