Rais Samia amsimamisha kazi Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake

Avumaye baharini papa, kumbe wengine wapo. Kama yaliyokuwa yanasemwa na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii ni ya kweli, kumsimamisha tu kazi hakutoshi, inabidi apelekwe mahakamani akajibu tuhuma zinazomkabili.
Huyu ni jambazi apelekwe mahakamani tu akajibu alichofanya. Alifikiri Magufuri ni Mungu na ndiyo iwe mfano kwa viongozi wote
 
Tunamuhitaji mama asiangalie wale viongozi waliowakorofisha matajiri pekeyao ndioanawachukulia hatuwa nasisi wavuvi ziwa tanganyika wa kata yakalya tumefanyiwa uonevu mkubwa hatuja sikia nanikawajibishwa kwa kuharibu malizetu halali ilatunaona waliowakorofisha matajiri ndiohatua zinachukuliwa sasa tuambiwe tujuwe nini hatma yetu ?
 
Wanaosema mama asipewe pressure ni kwasababu maamuzi yoyote atakayoyafanya yana impact kubwa kwa taifa,, hivyo subira na umakini vinahitajika.
Fikiria uteuzi wa yule jaji ulivyolalamikiwa. Lakini naamini mama anafanya moves zenye umakini kuliko baadhi wanavyodhani.
Kwenye football kuna wakati mpira wa kushambulia unaurudisha nyuma kabisa kwa kipa ili kupanga mashambulizi upya.
 
Ana dharau sana huyu dogo
Juzi kwenye clouds alimkebehi sana Mbowe eti 'alizaliwa 1961 umri sawa na mamake '
Utaishi kwa shida sana utazeeka kumzidi Mh Mbowe
Shida wengi wao huwa wanajisahau sana kuwa haya mambo ni ya ulimwengu. Ishi vizuri na watu heshimu wakubwa na wadogo.
Leo Sabaya umedhalilika
Pesa hainunui kila kitu
Umeiba umepora umenyasasa hizo pesa hutazifurahia
Kiama kiko hapa duniani....
Wengine mliobakia muanze kutia maji
Kelele za mitandao kiko wapi?
Kila mtu abebe msalaba wake
 
Wanaochunguza na kupata taarifa za maovu mbalimbali ndio hao wanaoleta taarifa mitandaoni labda uwakataze hao, wakati mwingine wala ahitaji uchunguze matamshi yako na matendo yako yanaonekana wazi, mfno yule aliyesema "Maaskofu wafunge midomo yao" hivi unahitaji uchunguzi kujua kuwa huyo kijana anautovu wa nidhamu.
 


Mvinyo hapana, ila utapata maji baridi tu.
 
Akina mbow wanahistoria ya kuendesha mambo na siasa zao kibabe na kihuni. Akitokea mhun na mbabe mwenzao wanapata wepesi wa kulialia
 
 
Amesimamishwa kupisha Uchunguzi daadeki[emoji23]
View attachment 1783580
Na akionekana hana hatia atarejeshwa kazini na kulipwa stahiki zake zote zilizosimamishwa.

Lakini ninavyoelewa tuhuma yoyote dhidi ya viongozi wa kariba yake huwa ndiyo mwisho wa uteuzi.

Sasa kwa barua hiyo ya ikulu, inamaanisha kibarua bado anacho uchunguzi ukimsafisha, vinginevyo angelikuwa kateuliwa mwingine kushika nafasi yake.
 
Kuwa serious na mambo, acha ujinga
Hamna siri dunia hii. Ukweli usemwe hivyohivyo ulivyo

Uwizi, uhuni, ubabe vyote visemwe kama vilivyo.

Huwa inatokea wengne wakifanya mambo ya kijinga, ya ovyo, ya kihuni, ya kibabe na nk haiandikwi au kutangazwa au kuonekana kama mambo yasiyofaa. Lakin wakifanyiwa wao sasaaaa, dunia nzima itajua. Utafikiri wao ndo binadamu wengine nusu binadamu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…