Rais Samia amteua Mavere Tukai kuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD)

Rais Samia amteua Mavere Tukai kuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD)

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
730B7BE0-3F59-4075-9461-2781FFF895DA.jpeg


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi jioni ya Aprili 14, 2022 kama ifuatavyo:

Amemteua Rosemary William Slaa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD), Bi. Slaa ni Afisa Mwandamizi katika Kampuni ya Picenaterhouse Coopers PWC.

Amemteua Mavere Tukai kuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Tukai ni Kiongozi Mkuu wa Mradi wa USAID Global Health Supply Chain Technical Assistance.

Amemteua Raymond William Mndolwa kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Mndolwa ni Mtaalam wa Operesheni, Kampuni ya STC Construction, Dar es Salaam.

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus ni kuwa uteuzi huo unaanza mara moja.
Uteuzi.jpg
 
Huyu ndugu Mavere Tukai ni "kichwa" haswaa.

Ni "pharmaceutical management specialist".

Jamaa yuko FOCUSED na DETERMINED sana.

Alikuwa pale USAID....wamarekani wanamfahamu kwa uwezo mkubwa alionao, watammiss sana.

Imefika muda atutumikie katika MSD.

Kila la heri kwake kamarada Mavere Tukai ,amen🙏

#Siempre JMT🙏
#YetzerHatov🙏
 
Huyu Mavere Tukai ni "pharmaceutical management specialist", amebobea haswa na ana IQ nzuri na anapenda KUSIKILIZA sana.

Mkuu wangu Nyboma kwa heshima ya ulipopita na kufanya kazi kama mzalendo si vema kuwakandia watanzania wenzako.

#Against Bigotry 🙏
#Against Any Form Of Prejudice And Discrimination 🙏

SIEMPRE JMT🙏
 
Mkuu wangu unapinga hata uteuzi wa kichwa Tukai Mavere?!!![emoji1787][emoji1787]
Kichwa maana yake nini weww sema umetumwa kuja kuoamba pamba tu hapa. Kuna vichwa vingapi tz hapa hadi vimepita Harvard lakini hakuna kitu. Akina prof muhongo na chenge sio vichwa? Mbona wameboronga kama kawaida?. Unga wa giningi. Kaa kwa kutulia weae kijana. Kuna watu wenye weredi wengi sana tz lakini uliza wanachofanya maofisini hata form 6 hawezi fanya.
 
Kichwa maana yake nini weww sema umetumwa kuja kuoamba pamba tu hapa. Kuna vichwa vingapi tz hapa hadi vimepita Harvard lakini hakuna kitu. Akina prof muhongo na chenge sio vichwa?.mbona wameboronga kama kawaida?. Unga wa giningi............... Kaa kwa kutulia weae kijana. Kuna watu wenye weredi wengi sana tz lakini uliza wanachofanya maofisini hata form 6 hawezi fanya
Duuh 😳🤣🤣

Mkuu si kwa povu hili usiku mkubwa....

Ok....twende taratibu...

Sasa ulitaka amteue nani hapo MSD?!!!!
 
Huyu Mavere Tukai ni "pharmaceutical management specialist".....amebobea haswa na ana IQ nzuri na anapenda KUSIKILIZA sana......

Mkuu wangu Nyboma kwa heshima ya ulipopita na kufanya kazi kama mzalendo si vema kuwakandia watanzania wenzako....

#Against Bigotry [emoji120]
#Against Any Form Of Prejudice And Discrimination [emoji120]

SIEMPRE JMT[emoji120]
Unamkumbuka Daudi Balali ?
 
Back
Top Bottom