Rais Samia amvaa Ndugai. Asema, "Huwezi kuamini mtu mzima ana-argue tozo na mkopo wa Trilioni 1.3"

Rais Samia amvaa Ndugai. Asema, "Huwezi kuamini mtu mzima ana-argue tozo na mkopo wa Trilioni 1.3"

Rais Samia Suluhu Hassan amesema ni Uhuru wa Mtu kusema chochote, lakini inashangaza Mtu anayetegemewa kushirikiana na Serikali kwenye safari ya maendeleo 'kuargue' kuhusu Tozo na Mkopo wa Trilioni 1.3 kwasababu taarifa zote za Uchumi zinapita kwake akisema, "Ni homa (fever) ya 2025, wasameheni"

Ameongeza, "Huwezi kuamini mtu mzima na unaenda kuargue tozo na mkopo wa Trilioni 1.3 kama kwamba ndio kwamba inatokea Tanzania wakati toka tunapata Uhuru ni Mikopo kwenda mbele. Na katika Mikopo yote huu ni mkopo mzuri zaidi"
Ningekuwa mmiliki wa gazeti kesho lingetoka hivi. "NDUNGAI MTU MZIMA HOVYO" by...
 
Sijaona sababu ya maneno yote haya yaliyomtoka mama, mtu ameomba msamaha tena hadharani lkn bado amemkalia kooni tu, mie sio mfuasi wa Ndugai lkn kikawaida mtu akiomba msamaha asamehewe, Samia alipaswa kutangaza msamaha ila kama kuna mengine waliapswa wayamalize ndani huko kwenye vikao vyao......
 
  • Thanks
Reactions: nao
Sio lazima spika wa bunge awe kibaraka wa rais.
Nchi inaweza kusonga mbele vizuri kama bunge likiacha urafiki na serikali.
Bunge lipi unazungumzia? Tanzania kuna vikao vya CCM hakuna bunge nchi hii. Madhara ya kuuminya upinzani ndio haya sasa nyama zinatokea mbavuni.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Mwanzoni kabisa niliwasikia watu wakisema bunge ni dhaifu.


Spika kaongea kidogo tu watu wamemvaa tena.


Kwahiyo mnataka nini??


Halafu suala la Rais wa nchi kuendelea na hili suala la mikopo ni ufinyu wa akili.

Mtu ameshaomba radhi.

Yeye bado kashikilia bango.

Poor thinking capacity.
Ulifikiria kuwa kwa kuomba tu msamaha ule lingeweza kuisha?kwanza anasema kuwa hiyo clip ilitengenezwa!!tayari heshima yake ndio imeisha potea, na kuanzia hapa wale waliokuwa wameanza kumpogeza kwa kuomba msamaha, kwa msimamo huu wa leo wa mama, hutawasikia tena!!na sasa ameahakuwa mzee wa GUNDU!!mungu anatisha sana yaani ni huyu Ndugai ambaye miaka 6, nyuma alikuwa anajifanya ni mungu mtu??
 
Ndugai sio serikali kaka
Mama anapaswa kuwa na kifua na sio mtu mmoja anamkimbiza hivi
Inavoonekana yawezekana hata alilolifanya leo haikuwa kwenye ratiba zake

Kaitisha ili tuu kumjibu ndugai.
Anapotaka kumwadhibu ndugai aangalie asije kimbiza mwizi wa mitego akaacha mlango wazi

Najua anatambua kabisa ccm ishakuwa chakavu ndio maana haya yanatokea
Asilimia kubwa ya walio mzunguka wote ni wachumia tumbo na wanafiki. Asifikiri katika uadui wa mmoja tuu
 
Sijaona sababu ya maneno yote haya yaliyomtoka mama, mtu ameomba msamaha tena hadharani lkn bado amemkalia kooni tu, mie sio mfuasi wa Ndugai lkn kikawaida mtu akiomba msamaha asamehewe, Samia alipaswa kutangaza msamaha ila kama kuna mengine waliapswa wayamalize ndani huko kwenye vikao vyao......
Hii nafikiri hufanywa kuwatisha wengine wasijaribu kufanya Ndugai
 
  • Thanks
Reactions: ram
Masikini unaepukaje aibu?
Kipi bora…kukosa kabisa madarasa na tundu la choo au kuwa nayo kwa pesa za kukopa?

Bora kujenga sisi wenyewe. Sio gharama kubwa kivile. Tukiamua, tunaweza Itasaidia kulipa Mshahara wako na wapambe wenzako gharama tutakazoziokoa.
 
Sijaona sababu ya maneno yote haya yaliyomtoka mama, mtu ameomba msamaha tena hadharani lkn bado amemkalia kooni tu, mie sio mfuasi wa Ndugai lkn kikawaida mtu akiomba msamaha asamehewe, Samia alipaswa kutangaza msamaha ila kama kuna mengine waliapswa wayamalize ndani huko kwenye vikao vyao......
Tatizo ni kwamba mama mwenyewe hii inshu imekuwa ya kushtukizwa na yeye

Wakati anakimbia alijua yuko nao kumbe wamesimama wanamwangalia tuu

Hajui nyuma ya ndugai kuna kina nani

Asifikiri vita ya siasa za ndani ya chama ni maneno.
Akataka kujisahau na kumshikia kiuono aseee yani alitoka kabisa kwenye mudi


Hapo ndio Ndugai ajue nguvu ya bunge, serikali inaliogopa bunge siku zote
 
Naungana na wewe ; kafanya kosa kubwa snaa kuomba msamaha. Alitakiwa akae kimya asi comment chochote .

Angeonekana mwanaume zaidi . Kuomba msamaha means he is dumb na Hana stand, damn it.

Mwanaume kujiamini na ametoa mawazo yake huru ambayo yalikuwa ni mazuri Tu; hii Mikopo ni ya kipuuzi maana asilimia kubwa ya hii mikopo huliwa kifisadi na Hiyo ni report ya SHIRIKA LA FEDHA LA DUNIA.

Sasa yeye angebaki hapo hapo ; kuwa kama tumekopa , tozo ishushwe zaidi .

Samia Mwenyewe na kundi lake ni fisadi tu na ni Upenyo wa rushwa, unamuomba Samahani ya Nini , kwani yeye nani , atatoka kwenye kiti kama walivyotoka wengine , I can’t pleading for my thoughts and stand , ni upumbavu

Kuweka tozo ni failure ya mama , mbona tuliishi na Ngosha bila tozo

Job sio mwanaume yule , coward , mwanaume misimamo kwa unachoamini , na mwanaume hueshimika kwa misimamo yake. Ndio maana JPM ni rais bora wa maisha.

TISS wamemshauri kuomba msamaha na yeye kaomba kweli , leo mama kamtia kidole cha nyuma na msamaha wake. Haya ndio madhara ya kukosa stand. Mwanaume kujiamini hata ukibaki alone kwenye mawazo yako, poa tu ; ipo siku some people will understand you !

Maana mm najiuliza kaomba msamaha kwa kosa gani? Africa bwana

Yaani ukitoa mawazo yako kinzani, ni kosa Dah

Pole ndungai, kumbe we lofa tu
Nimekudharau sana
sina mahaba na ndugai wala ccm.

ila usimlaumu kwa kukurupuka kwake kuomba msamaha.

pressure kutoka ndani ya ccm ilikuwa kubwa sana na jamaa akawa hana namna. alibanwa kwenye crempu.

na ukute hata kundi lililokuwa nyuma yake lilimuacha apambane kivyake.

shida ni kwamba amemuomba msamaha mwanamke, mbaya zaidi ni mwanamke mwenye asili ya pwani. wanawake wa pwani na vichambo ni pete na kidole.

kichambo alichopewa leo sidhani kama alikitarajia. angalau leo yale maccm yenye tamaa ya kiti cha urais, yamejua rangi halisi ya mama.
 
Huyu mama anapaswa kuelewa nafasi aliyonayo ni nyeti namba moja kitaifa.
Unapoendeleza malumbano ya kike kwa mtu ambaye tayari amejishusha na kuomba msamaha.
Rais wa nchi unapaswa kuonyesha ukomavu wa kisiasa ikiwemo pia kuwavumilia na kuwasamehe wale msioendana kimtizamo.
Mimi binafsi namuona mama kama vile ndie kaingia mtego wa Ndugai.
Vinginevyo siasa ndani ya CCM zitamsumsumbua zaidi, kwani atabaki na kundi la wanafiki kama huyo Mwigulu & wanafiki classics
Hamna nyoka unatakiwa kumponda kichwani ukipiga kiunoni ukajidanganya kafa akikuvizia anakumaliza, hapa wanajaribu kumwekea mama mazingira magumu 2025 sasa kashtuliwa mapema acha awamalize tuu kila mbuzi ale urefu wa kamba yake.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Hii nafikiri hufanywa kuwatisha wengine wasijaribu kufanya Ndugai
Ukumbuke vita ya siasa za kugeukana ni kama vita ya magenge ya uhalifu? Wani misitike minzi dethi

Sasa hapa aone tuu namna waliomzunguka ambao wako nyuma ya ndugai ni akina nani?
 
Kassim majaliwa na ndungai wamepewa ujumbe kuwa wanatakiwa wajiuzulu.

Vita ya 2025 imeipasua CCM vipande-vipande.

Pambaf.
 
Back
Top Bottom