Rais Samia anasema 'hili tunalichukua'. Hayati John Magufuli aliamua pale pale jukwaani

Rais Samia anasema 'hili tunalichukua'. Hayati John Magufuli aliamua pale pale jukwaani

So linahitaji Rais wa kuuliza wananchi nitumbue au nisitumbueeee
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hauko serious au wew ni walewale

Ni mwendo huo huo unaowafaa watanzania kwa sasa baadaye huko wakikaa sawa tunaweza kushift tu automatically...

Sasa kiongozi mpumbavu anayeisababishia nchi hasara kwa upumbavu wake unategemea aachwe bila naye kudhalilishwa kama alivyowakosea na kuwadhalilisha mamilioni ya watanzania....? abembelezwe, afichwefichwe, anyenyekewe nk HAPANA aisee, kuna mijitu mijinga inahitaji adhabu kali sana..
 
So linahitaji Rais wa kuuliza wananchi nitumbue au nisitumbueeee
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hauko serious au wew ni walewale

kiongozi aliyezembe au kuiba hela za mradi wa hospitali huku mamilioni wakikosa huduma za hospitali utaka alembwelembwe baadala ya kudhalilishwa naye baada ya kusababishia maelfu kukosa huduma za hospitali..
 
kiongozi aliyezembe au kuiba hela za mradi wa hospitali huku mamilioni wakikosa huduma za hospitali utaka alembwelembwe baadala ya kudhalilishwa naye baada ya kusababishia maelfu kukosa huduma za hospitali..
So Rais anafanya maamuzi based on taarifa za kusikia kwa wananchi bila kujiridhisha! Vp kama wanamdanganya au ni chuki zao? Refer yule mama tapeli.
 
Uongozi ni kuamua tu kuchukua njia unayopita, unapita unaenda zako bila ya kujali kelele za kutoridhika au vigelegele vya kuridhika.....,miaka yenyewe mingapi ya uongozi ya kuridhisha wote!!

Maamuzi ya papo kwa papo yana uwezekano mkubwa wa kukosea kunakotokana na kukosa taarifa sahihi na mwisho wa siku mtu anaonewa (nina uhakika katika kila maamuzi natano ya papo kwa papo, mawili yanakuwa sivyo). Faida ya hii ni kuwa watu ni kweli wanakuogopa na hujitahidi kuwa 'sio wao' ili kubaki salama

Style ya mama ya 'kulichukua' ina uwezekano wa kutenda haki lakini ina shida ya kuchelewa na......nchi ni kubwa sana yatachukuliwa mangapi miaka yenyewe mitano au 10 tu!

Suluhisho: nenda tu na unachoamini ni sahihi!
Kuna wengine ni nyoka wa mdimi mbili, wanalike kila hoja mpaka wanazozipinga, yaani huku kwako wapo kwenye kuamini njia ya kupita vyovyote maana kote kuna Pros and cons lakini hapo hapo wapo kwa yule aliyechagua upande wa “tutakwenda tutarudi”, yaani mavichochoro ya nchi yenye square kilometers milioni moja kasoro ukafanye maamuzi ya stahili hii ambayo hata kagame na kamkoa kake hawezi kufanya hivyo ni utopolo…

Ajabu zaidi ni kuwa Magufuli before kufanya maauzi hayo ya papo kwa papo alikuwa akizishirikisha pande zote kujitetea hadharani, wakati mwingine kuwahisisha mpaka viongozi wengine wa ngazi mbalimbali.

Narudia tena, masikini sio wakupiganiwa hata siku moja, Bible yenyewe inaeleza namna Mungu alivyokuwa akiwatelekeza wana wa Israel wapigike mpaka wakubali kuwa walibugi step…. Eti ni mtumbue nisimtumbue! Kwani Bossi wa Raisi ni nani kiuhalisia?

Allency samurai sayoo Drifter
 
So Rais anafanya maamuzi based on taarifa za kusikia kwa wananchi bila kujiridhisha! Vp kama wanamdanganya au ni chuki zao? Refer yule mama tapeli.
Reference ya mama Tapeli iko wapi? Weka chanzo cha habari na nini kilifuata baada ya kubainika kufanya utapeli? Usiongee kwa hisia na mihemko ya hearsay bro.
 
Siyo kweli kuwa JPM alikuwa anakurupuka kutoa uamuzi bali alikuwa anatembelea sehemu akiwa na data za kutosha kuhusu sehemu anayotembelea. Kwa mfano alipompandisha Mbuge kutoka Kanali hadi kuwa Brigadier general papo kwa papo alishailiongelea jambo hilo na CDF, na ndiyo maana CDF akamvika Mbuge nyota zile siku hiyo hiyo kwani alikuwa anajua. Alipomfukuza DAS wa Kisarawe, alikuwa ana taarifa zote na alisema aliwahi kumuonya mara kadhaa. Hata hivyo wanachi walipoomba barabara ya kwenda Kibaha, hakutoa amri ya papo kwa papo bali aliwaambia hilo analibeba na atalifanyia kazi.

Alipomfukuza yule marehemu mkurugenzi aliyechongewa na Makonda, alishakuwa na taarifa zaidi juu ya ubadhirifu ulikokuwa unafanywa naye hata kabla ya Makonda kuzungumza, na ni kutokana na msukumo wa kutaka maelezo ya taarifa hizo za ubadhilifu ndipo Makonda akatoa lawama hizo. Alipoamuru ATCL iwe ina mmbeba Mapunda na mke wake bure, ni swala ambalo lililkuwa limeshaongelewa na bodi ya wakurugenzi wa ATCL na ndiyo maana siku hiyo Mapunda akawa amepewa kiti pale high table.

Kudhani kuwa alikuwa anakurupuka kutoa maamuzi siyo sahihi, alikuwa anafanya homework yake vizuri sana kabla ya kwenda ziarani na alipokuwa huko alikuwa data za kutosha sana. Ni mtu aliyekuwa na uwezo wa kujua idadi ya samaki kwenye ziwa asingeshindwa kujua matukio ya kwenye sehemu alizokuwa anatembelea kabla hajafika.
 
Ndio maana kwa kukurupuka aliingizwa chaka mara nyingi mfano mmojawapo ni yule mama wa Tanga (alipachikwa jina mjane wa Magufuli) Mtu mwenye hekima hutafakaribjambo na hupata kusikiliza pande zote mbili ili kujiridhisha.

Usilazimishe kila unachokitaka kiwe uoendavyo maisha hayako hivyo. Kwa hiyo hamkukioenda chama chenu mlimpenda mti au mlipenda kabila???
 
Reference ya mama Tapeli iko wapi? Weka chanzo cha habari na nini kilifuata baada ya kubainika kufanya utapeli? Usiongee kwa hisia na mihemko ya hearsay bro.
Ina maana hukuwepo??? Ukipewa reference ndo utaamini mzee baba alikuwa hakurupuki??? Alikurupuka sana kwenye maamuzi na ndio maana wengi aliowatumbua aliwarudisha kwa mlango wa nyuma kimyakimya
 
Yote ni sawa tu hata mahakamani maamuzi huchukua muda lakini badi hukumu inaweza kukosewa mmuzi shihi kwako ni pale utavyoyapokea wewe. Mfano mtu kadulumiwa ng'ombe na polisi halafu kaha kushitaki kwako wew kama kiongozi halafu unawaachia polis wachunguze.

Maamuzi ya papo kwa papo yanahitaji umakini wa hali ya juu na hofu ya Mungu ni sawa na kuibu maswali ya papo kwa papo. Hii njia ndio aliyikuwa anaitumia mfalme Suleman enzi hizo.
 
N

Ndio maana kwa kukurupuka aliingizwa chaka mara nyingi mfano mmojawapo ni yule mama wa Tanga (alipachikwa jina mjane wa Magufuli) Mtu mwenye hekima hutafakaribjambo na hupata kusikiliza pande zote mbili ili kujiridhisha.
Usilazimishe kila unachokitaka kiwe uoendavyo maisha hayako hivyo. Kwa hiyo hamkukioenda chama chenu mlimpenda mti au mlipenda kabila???
Kwa yule mjane alifanya kumsindikiza..lakini suala lake hakulitolea maamuzi...Ila alimuelekeza RPC na wengine kwa sababu wanalifahamu...walifanyie kazi,Ila baadae wakalipotezea..nadhani walimuona yule mama si mkweli.

Sehemu akiingizwa chaka alikuwa anastuka..rejea video aliotembelea gereza la Butimba..kuna diwani alidai kauza shamba lake halali hafu kapewa kesi kuhujumu uchumi...lakini alimsikiliza polisi aliemfungulia mashtaka...hapohapo akagundua yule diwani anachangamoto...akampotezea hapohapo.
 
Ni mwendo huo huo unaowafaa watanzania kwa sasa baadaye huko wakikaa sawa tunaweza kushift tu automatically...

Sasa kiongozi mpumbavu anayeisababishia nchi hasara kwa upumbavu wake unategemea aachwe bila naye kudhalilishwa kama alivyowakosea na kuwadhalilisha mamilioni ya watanzania....? abembelezwe, afichwefichwe, anyenyekewe nk HAPANA aisee, kuna mijitu mijinga inahitaji adhabu kali sana..
So kwa upeo wako nchi haihitaji mahakama bali maamuzi ya hapo kwa hapo kutoka kwa kiongozi? Kweli kuna binadamu wanapenda kuongozwa kidicteta. Nilikiwa najiuliza hawa watu waliokuwa wanasifu yale mambo ya jiwe ni watu wa aina gani, na je wapo kweli au ni propaganda! Ila leo nimeamini kuwa kumbe wapo aisee
 
Reference ya mama Tapeli iko wapi? Weka chanzo cha habari na nini kilifuata baada ya kubainika kufanya utapeli? Usiongee kwa hisia na mihemko ya hearsay bro.
Kama hili hulijui basi wew siyo mfatiliaji wa siasa za Tanzania. Acha uvivu tafuta maarifa mwenyewe mimi nimkupa hints tu.
 
Siyo kweli kuwa JPM alikuwa anakurupuka kutoa uamuzi bali alikuwa anatembelea sehemu akiwa na data za kutosha kuhusu sehemu anayotembelea. Kwa mfano alipompandisha Mbuge kutoka Kanali hadi kuwa Brigadier general papo kwa papo alishailiongelea jambo hilo na CDF, na ndiyo maana CDF akamvika Mbuge nyota zile siku hiyo hiyo kwani alikuwa anajua. Alipomfukuza DAS wa Kisarawe, alikuwa ana taarifa zote na alisema aliwahi kumuonya mara kadhaa. Hata hivyo wanachi walipoomba barabara ya kwenda Kibaha, hakutoa amri ya papo kwa papo bali aliwaambia hilo analibeba na atalifanyia kazi.

Alipomfukuza yule marehemu mkurugenzi aliyechongewa na Makonda, alishakuwa na taarifa zaidi juu ya ubadhirifu ulikokuwa unafanywa naye hata kabla ya Makonda kuzungumza, na ni kutokana na msukumo wa kutaka maelezo ya taarifa hizo za ubadhilifu ndipo Makonda akatoa lawama hizo. Alipoamuru ATCL iwe ina mmbeba Mapunda na mke wake bure, ni swala ambalo lililkuwa limeshaongelewa na bodi ya wakurugenzi wa ATCL na ndiyo maana siku hiyo Mapunda akawa amepewa kiti pale high table.

Kudhani kuwa alikuwa anakurupuka kutoa maamuzi siyo sahihi, alikuwa anafanya homewrok yake kabla ya kwenda ziaranai na alipokuwa huko alikuwa data za kutosha sana. Ni mtu aliyekuwa na uwezo wa kujua idadi ya samaki kwenye ziwa asingeshindwa kujua matukio ya kwenye sehemu alizokuwa anatembelea kabla hajafika.
Umejidhalilisha sana uliposema Jiwe alikuwa anajua idadi ya samaki, ajue idadi ya samaki ila hajui hata marais wa nchi maarufu.
 
Wote wanaweza kuwa sawa..
Wote wanaweza wasiwe sawa..
Mmoja anaweza kuwa sawa na mwingine hapa.

Taifa la Tanzania na watu wake kuna mahala linamtaka Marehemu JPM na hulka yake ileile..
Hii nchi kuna baadhi ya watu wajinga sana, narudia tena wajinga sana na ndio wanasababisha hii nchi iwe hapa kwa sasa..

Wakati huu Taifa linahitaji mtu kama marehemu atuvuruge sana na tukija kukaa sawa miaka mingi mbele ndio waje viongozi aina hii ya Mama , pamoja na JK... Style ya uongozi wa mipango na kuamini watu inafaa sana kwenye mataifa yaliyoendelea tayari lakini sio kwa Taifa kama hili lenye baadhi ya watu primitive na wajinga...
😍
 
Kwahakika Mh. Rais Samia anajua leadership na yupo very assertive. Tofauti yangu na yeye ni kwenye kitu kimoja tu, kutokuamini kwenye siasa ya ujamaa na kujitegemea, hapo kwakweli I do not like huo utegemezi na ambao anauongea waziwazi kwa mataifa makubwa, kuwapa indicator kwamba we are subject to them.

Hata kama kweli tutegemezi basi tusipigie mstari kabisa, si tuendelee tu na mambo yetu? Ile kauli yakusema tutumie hizi pesa vizuri ili tupatiwe zingine kwakweli haijanibariki kabisa mpendwa mama yangu, kwanza huo ni mkopo kisha tunaonyesha kama vile tumepewa hisani, daah!

...Ilikuwa ni blend nzuri sana kwa hayati JPM kuwa VP mama Samia, kama ingetokea wangeweza ku blend character zao maana weakness za JPM mama hana na strength za JPM mama kwake ni weaknesses...Thats my personal assessment.
 
Wote wanaweza kuwa sawa..
Wote wanaweza wasiwe sawa..
Mmoja anaweza kuwa sawa na mwingine hapa.

Taifa la Tanzania na watu wake kuna mahala linamtaka Marehemu JPM na hulka yake ileile..
Hii nchi kuna baadhi ya watu wajinga sana, narudia tena wajinga sana na ndio wanasababisha hii nchi iwe hapa kwa sasa..

Wakati huu Taifa linahitaji mtu kama marehemu atuvuruge sana na tukija kukaa sawa miaka mingi mbele ndio waje viongozi aina hii ya Mama , pamoja na JK... Style ya uongozi wa mipango na kuamini watu inafaa sana kwenye mataifa yaliyoendelea tayari lakini sio kwa Taifa kama hili lenye baadhi ya watu primitive na wajinga...
Maamuzi ya haraka siku zote yana matokeo hasi, kiongozi mkubwa km rais lazima awe na mda wa kujiridhisha kwenye kila hatua kinyume chake anakosa sifa, hata wewe mwenyewe nyumbn kwako ukiwa ni mtu wa kuletewa jambo na kulichukua km kilivyo bila kuchakata na kujiridhisha utagombaba na kila mtu, na ndomana marehemu alikuwa na maadui wengi

Kiongozi hatakiwi aogopwe ila aheshimiwe kwa maamuzi yake, ila kwa jiwe ilikuwa kinyume chake, watumishi walikuwa na hofu mda wote, maana wanajua hata akilishwa matangopori hana mda wa kujiridhisha yy ni kutumbua tu
 
Back
Top Bottom