Rais Samia anaweza akastahimili lakini chawa wake anaweza asistahimili

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Rais Samia ameyasema hayo akiwa anawaambia viongozi wa vyama vya siasa wanatakiwa kufanya siasa za kistaarabu kwasababu kutukanana siyo mila za kitanzania.

Akisema kuwa yeye anaweza kuwa na upeo mkubwa wa ustamihilivu kama aliyokuwa nayo, sababu yanampata lakini anakaa kimya lakini chawa wake anaweza asiwe na ustahilivu huo akavaana na chawa wa kiongozi mwingine hivyo kuleta vurugu nchini

Akasema badala ya kushinda wakitukanana wabishane kwenye hoja kama vile kwenye miradi ambayo haijakamilika na kwa kufanya hivyo itachangia kuleta maendeleo na uwajibikaji.

Wadau, kwa kauli hiyo team 'ANAUPIGA MWINGI' sasa wametambulika rasmi?
 
Hawa vyawa ni akina nani?
👇
20230103_144500.jpg
 
Aisee ndugai ana weza elezea vizuri sana.
 
Kwa wale Ambao walikuwa Hawajui nguvu ya Mbowe na Chadema, Sasa Leo wametambulishwa rasimi
 
Sababu za Lema na Lisu kujibanza kwa wazungu zinadhidi kumalizwa, mikutano ya siasa imeruhusiwa, madai yote ya Lisu yamelipwa, kesi yenye kila aina ya ushahidi ya gaidi wa kuuwa viongozi wa serikali imefutwa.
Ngoja tuone kiki mpya watakayokuja nao .
 
Hongera Mama kwa kuwakumbuka chawa wako. Kwa kweli wanafanya kazi nzuri.
 
Hoja ya msingi kwenye kauli ya Rais kuhusu CHAWA ni jinsi ya kukosoa Serikali au mtu yeyote isiwe ya matusi kwa kuwa mkosolewa anaweza akastahimili lakini wafuasi wake (CHAWA) wasistahimili
 
Back
Top Bottom