Rais Samia aongea na Wazee wa Dar: Aahidi kutojali vyama katika teuzi zake. Serikali kutunza Haki, Demokrasia, Uhuru wa Habari

Rais Samia aongea na Wazee wa Dar: Aahidi kutojali vyama katika teuzi zake. Serikali kutunza Haki, Demokrasia, Uhuru wa Habari

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili Ukumbi wa Mlimani City kuongea na Wazee wa Dar es Salaam

Tunakuletea updates hapa

Mwenyekiti wa Wazee wa Dar, Salum Matimbwa
Tumepata kadi za msamaha wa Bima, lakini Wazee hatupati baadhi ya vipimo na Dawa tukifika Hospitalini

Tunaomba Rais Samia tunapokuwa Hospitalini, tupate vipimo na dawa zote kadri ya Magonjwa yanayotusibu

Tunakupongeza kwa kusimamia Sheria na Utawala bora. Tunaomba juhudi ziendelee ili kushughulikia kero za Wananchi

Vyombo vya Ulinzi na Usalama vifanye kazi kwa Sheria, Kanuni na Utaratibu waliojiwekea. Inapobidi Wananchi washirikishwe ili kuondoa manung'uniko

Wazee tunaomba Vyombo vyote vya Usafiri wa Umma vitenge viti maalum vya kukaa wazee

Pia, vihimizwe kuhakikisha vinawabeba wajukuu zetu ambao ni Wanafunzi wanapokwenda na kurudi shuleni

Kuna uwakilishi wa makundi mbalimbali #Bungeni lakini Wazee hatuna uwakilishi

Hivyo tunaomba na sisi ikikupendeza Rais, tupewe nafasi hiyo ili tupate Watu wa kutusemea matatizo yetu kwenye Vyombo vya Mamlaka

Waziri wa Afya - Dkt. Dorothy Gwajima
Wazee wanazidi kuongezeka. Mwaka 2012 kulikuwa na Wazee milioni 2.5 sawa na asilimia 5.6 na hivi sasa wameshafika milioni 2.52.

Mauaji ya wazee yamepungua kutoka 577 mwaka 2014 hadi wazee 34 mwezi Desemba mwaka 2020.

Rais Samia Suluhu Hassan

Tahadhari dhidi ya Corona\uvaaji barakoa ukumbini

Naomba niwaombe radhi kwamba mtindo wa maisha umebadilika. Tumekuja na vikaba midomo ninyi pamoja na sisi

Kwasababu mkusanyiko huu ni mkubwa na Wazee ni rahisi kupata haya maambukizi, hatuwezi kujua nani anayo na nani hana. Sisi wenzenu tunazunguka sana

Wazee wameona mengi na wana uzoefu mkubwa. Ndiyo maana tumeona tuje kuzungumza nanyi ili tuone mnasema nini na mnatuambia nini

Ni utamaduni, toka tumepata Uhuru Viongozi wetu wamekuwa wakikaa na kuongea na Wazee. Mimi sina jambo ila nimekuja kuwasikiliza

Tiba kwa Wazee
Mbali na Sera, Ilani ya CCM inatutaka kufanyia kazi suala la tiba ya Wazee. Waziri wa Afya ametoa ahadi nzuri lakini nataka aisimamie leo na sio kesho.

Dunia ipo kwenye Corona na wahanga wakubwa ni Wazee. Kamati niliyoiunda wanakwenda vizuri na karibu wataleta majibu

Nakubaliana nanyi kuhusu kuwawezesha kiuchumi lakini tuna Mfuko wa TASAF na tutakwenda kwenye Wilaya zote na kuhakikisha kila Mzee mwenye sifa anapata nafasi

Jambo la kutoa pensheni kwa kila Mzee tulipiga hesabu tukaona ni gumu kutokana na hali ya Uchumi

Corona imeshusha Uchumi karibu wa Dunia nzima. Pamoja na kwamba tutajitutumua tukue lakini tuna miradi mikubwa ambayo inahitaji kukamilika

Naomba mnipe muda niangalie hali ya Uchumi inavyokua halafu nitalitolea maamuzi. Tujenge Nchi kwanza halafu tutagawana faida

Wito wa kuwatunza Wazee
Nitoe wito kwa Jamii ya Kitanzania tutunze Wazee, awe amekuzaa au hajakuzaa. Tuna kisingizio cha maisha magumu ila naona ni maadili

Shughuli ya kuchukua Wazee kuwaweka kwenye nyumba maalum inafanywa na wenzetu wa Magharibi, Serikali itawajengea nyumba ila tuwatunze

Onyo dhidi ya uhalifu
Leo nimesoma mtandaoni kwamba Dar kuna Watu wanajaribu kupima kina cha Maji, Viujambazi vimeanza kuja juu - Naomba nitoe meseji wasijaribu kina cha Maji. IGP upo hapa, Mitandaoni wanamtaja Afande mmoja alikomesha ujambazi wanasema Mama turudishie, kaliangalie hilo
 
Tupate maombi kwanza
 
Rais anaongea na wazee wa jiji la Dar es Salaam nje ya jiji la Dar es Salaam!
 
Asante sana kwa taarifa, Safi sana ngoja tusubiri nondo za Mh SSH.
 
Katika mambo yanayoleta baraka tele ni pamoja na kuwathamini wazee.
Nawatakia kila la kheri kwenye mkutano huo.
 
Mimi kijana siruhisiw kuingia ndani? Japo nikae chini.
 
Nimeona watoa hotuba baadhi Yao wakifanya reference ya CCM na si vyama vyote vya siasa kwa ujumla. Rais ni wa Watanzania, atakayoyahutubia yanahusu watanzania wote na siasa za nchi zina ubia Kati ya vyama vya upinzani na chama tawala. Hilo hakipendezi kwa mshikamano wa Taifa na uungwaji mkono wa serikali ya awamu ya sita.
Washereheshai mmefanya kosa kubwa, lirekebishe hilo next time.
 
Back
Top Bottom