Rais Samia atangaza mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu
Angekuwa Jiwe angetuletea mpaka yale makovidi ndani. Yule mzee kitu kinaitwa busara kwake kilishagafariki dunia tangia akiwa mtoto ila yeye akaja kufariki akiwa mzee.
Nchi hii ilifika mahala ukibembeleza mambo hayaendi!
 
Muda mfupi ujao Mabadiliko ya Baraza la mawaziri yanatarajiwa kutangazwa kutoka Ikulu Jijini Dar es salaam.

======

Rais Samia amebadilisha muundo wa Wizara Tatu, Ameunganisha Wizara ya Uwekezaji iliyokuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Viwanda na Biashara kuwa Wizara Moja ambayo itaitwa Uwekezaji, Viwanda na Biashara.

Ameunda Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na Wizara ya mwisho aliyoifanyia mabadiliko ni Wizara ya Afya

Uteuzi (Mawaziri Wapya):

Nape Moses Nnauye - Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hamad Masauni - Waziri Mambo ya Ndani ya Nchi

Dkt. Pindi Chana - Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu)

Dkt. Angelina Mabula - Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hussein Bashe - Waziri wa Kilimo

Manaibu:
Anthony Mavunde - Kilimo

Jumanne Abdallah Sagini - Mambo ya Ndani

Dr. Lemomo Ole Kiruswa - Madini

Ridhiwani Kikwete - Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Atupele Mwakibete - Ujenzi na Uchukuzi (Upande wa Uchukuzi)


Mabadiliko ya Mawaziri:

Jenista Mhagama - Utawala Bora

Ummy Mwalimu - Afya

George Simbachawene - Katiba na Sheria

Profesa Joyce Ndalichako - Waziri wa Kazi

Innocent Lugha Bashungwa - TAMISEMI

Profesa Adolf Mkenda - Wizara ya Elimu

Dkt. Dorothy Gwajima - Wanawake, Jinsia na Makundi Maalum

Mohammed Mchengerwa - Utamaduni na Michezo

Dkt. Ashatu Kijaji - Uwekezaji


Mawaziri Walioachwa

Palamagamba Kabudi - Alikuwa Wizara ya Katiba na Sheria

William Lukuvi - Alikuwa wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi

Kitila Mkumbo - Alikuwa Wizara ya Viwanda na Biashara

Geoffrey Mwambe - Alikuwa Wizara ya Uwekezaji

=====

Kwa Ufupi;

Ikulu

Mkuchika

Utumishi
Mhagama
Ndejembi

Tamaisemi
Bashungwa
Silinde
Festo

Makamu wa Rais
Jafo
Hamis Hamis


Sera Bunge
Pindi Chana
Nderiananga

Ajira na kazi
Ndalichako
Katambi

Fedha
Mwigulu
Chande

Ulinzi
Tax

Ndani
Masauni
Sagini

Katiba
Simbachawene
Pinda

Mambo ya Nje
Mulamula
Mbaruku

Kilimo
Bashe
Mavunde


Mifugo
Mashimba
Ulega

Ardhi
Mabula
Kikwete

Maliasili
Ndumbaro
Masanja

Nishati
Makamba
Byabato

Madini
Biteko
Kiluswa

Ujenzi
Mbarawa
Atupele Mwakibete
Godtlfrey Kasekenya

Viwanda
Kijaji
Kigahe

Afya
Ummy Mwalimu
Ole Mollel


Elimu
Mkenda
Kipanga

Maendeleo ya kamii
Gwajima dorothy
Mwanaidi Hamis

Maji
Jumaa aweso
Mahundi

Utamaduni
Mchengerwa
Gekul

Habari Mawasiliano
Nape Nnauye
Kundo Mathew
Ni kweli CCM ina wenyewe wa timu Msoga, na sasa imerudi huko kikamilifu. Pamoja na yote, naona mama anaongoza kwa kuangalia 2025 tu, na sijui kwa nini awe anapanicki hivyo ilihali yeye ndiye mwenyekiti wa CCM, na kwa wakati huu CCM haina mpinzani.

Hao wenye CCM ndio waliokuwa wameikwamisha sana mpaka wakaja na sera ya mizigo na kujivua Magamba. Sasa tena sijui itakuwaje huko mbeleni. Ila kama wewe uko CCM na hauna ukaribu na Kikwete, basi imekula kwako. Dili zitapigwa sana serikalini katika miaka hii minne iliyobaki.
 
Juzi juzi hapa eti kalienda Arusha kwa kuunguza kodi za wananchi kukagua nauli stendi akidhan katamfurahisha mama. Kamepigwa chini Sasa. Hakuna tena drama za kisoro.

Bwahaha hahaha hahaha.

Kammmmonnn
Mama hapendi wakristo na watu wa bara!
 
Mkuchika ex spy moja katii ya inner circle ya Tiss protector wa magogoni huyo mzee na umrii alikuwa nao badoo anaweza kulenga shabaha hatari sana
 
So, kumbe Prof. Kitila, Prof. Kabudi, Lukuvi, Mwambe na Waitsra ndio waliokuwa wanampa Samia joto la 2025?

Kabudi arudi jalalani kwake tu sasa
plus ndugai. mama hataki kuucha urais ,aise kuzungukwa na maaskali jeshi ni raha aise, ikulu patamu bwana!! Ila wenye chama sidhani Kama watamuacha aendelee
 
plus ndugai. mama hataki kuucha urais ,aise kuzungukwa na maaskali jeshi ni raha aise, ikulu patamu bwana!! Ila wenye chama sidhani Kama watamuacha aendelee
Na ndo waliomshauri awapumzishe hao
 
Timu Msoga 3: Team Sukuma Gang 0
Dakika ya 90' ya mchezo na hakuna dakika za nyongeza
 
Back
Top Bottom