Rais Samia atangaza mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu
Mkuchika

IMG_20220108_202826.jpg
 
Kuna watu wajinga sana eti mataga tumeumizwa na huu uteuzi kwani ungekuwa wewe ungemwacha mwanao?
Anyway alichokifanya cha maana ni kumtoa hiyo wizara ndalichako, maana dah na kingereza chake kama changu
Wasukuma hoyeeeee
 
Makuwadi wa ardhi wanachekelea!! Siyo siri. wizara ya ardhi ni wizara ya kimkakati kwa mafisadi!! Kapenyezewa hapo mtoto wa mjini Riz 1 kimkakati!! Hapo mama kapigwa!! inabidi ashtuke mapema!! Pale ardhi ni mahali pagumu sana!! ni sehemu ya rushwa kubwa kubwa!! Ni sehemu yenye presha kubwa ya vimemo vya wakubwa!! Lukuvi alivishinda vyote!! Lukuvi aliwanyoosha maafisa wa ardhi wapenda rusha!! Nina hakika leo wanashangilia sana!! Ila Mungu anaona!!
 
Hiki ulichoandika hapa ni zile tabia za kiafrika za chuki dhidi ya mwenye nacho although yule tayari ameshakuzidi na huwezi kulingana naye hasilani!.
Juzi juzi hapa eti kalienda Arusha kwa kuunguza kodi za wananchi kukagua nauli stendi akidhan katamfurahisha mHama. Kamepigwa chini Sasa. Hakuna tena drama za kisoro.
Bwahaha hahaha hahaha.
Kammmmonnn
 
Nacho kumbuka kipindi Cha Jpm kina nape, Makamba na Ridhiwani Wasinge pewa hizi nafasi za uwaziri.......

Natafakari Sana haya maisha Yanatufunza Sana kweny hizi up & down.....

Nacho kumbuka Nidhamu ya Kazi ilishamili sana serikarini enzi zile kwa Hofu na Woga......

Pole nyingi sana kwa wote ambao tulikua tuna Amini kwenya baadhi ya mambo kwenye UMAGUFULISM...

Jana nimeshuhudia Raia wa kigeni anatengenezewa DRIVING LECENCE ya MCHONGO.....Easy.

Ili ufanikiwe sometimes....ni lazima uwe na timu nzuri....Tena ya watu ambao una wafahamu vizuri na kuwa amini.....tena wanao endana na mifumo yako...

Naona Nchi yenye Amani na furaha tele mikononi mwa mama.....
 
Kuna kisa JPM alikisema alipomtumbua Ubalozi wa Kenya Dr Pindi Chana. Kuna mwenye kumbukumbu vizuri.

Binafsi namuona anafaa sana ila sijajua kasi yake ya kutenda mambo.
 
Wateuliwa nendeni mkatafune nchi nawatakia utafunaji mwema
Huo ndio ukweli, hasa kwenye ardhi!! Lukuvi alionekana kuwa amewawekea kauzibe sana mafisadi na wala rushwa!! ?eo watakesha wanashangilia!! Namhurumia sana Mabula kuwekwa pale!!! Lazima afunikwe na Riz 1, akigoma anaondolewa!! mlengwa hapo ni Riz 1. Mabula hana ubavu wa kustahimili presha ya vimemo kama vya kina Kassimu, Mkwere wa msoga, Kina sa100 nk!! Kosa la Lukuvi ni kuwa hakuwa anaingilika!!! wala siyo mambo ya 2025!!!
 
Bado tuna safari ndefu sana kama taifa, CCM baada ya kututawala kwa miaka 60 wanaonesha dhahiri jinsi akili zao zilivyofika mwisho wa kufikiri. Sasa wanashindwa hata jambo dogo tu la kutafuta sura mpya zenye weledi zije kufanya kazi ya wananchi licha ya wasomi wengi waliopo.

Ni aibu kwa taifa la watu zaidi ya milioni 60 kuongozwa na sura zile zile kila awamu, huu mchezo wa kurithishana madaraka unatengeneza taifa la watawala na watawaliwa. Nawashangaa zaidi wale jamaa zangu wanaoitwa ikulu wakaimbe mipasho wakati hata wao keki ya taifa haiwahusu, hawa ndio watumwa haswa.
Hata huko Marekani kina Bush waliongoza. Kunywa Maji tu mkuu utulie.
 
Back
Top Bottom