Rais Samia atuombe msamaha Wakristo, Simba wa Yuda kwetu ni Yesu Kristo peke yake

Discussion siyo kifo bali matumizi ya هيافوs sehemu isiyotakiwa.
Katafute wewe sehemu inayotakiwa, sasa hakuna cha simba wa sharubu. Wacheni uoga wa kijinga. Kwisha wakati wake.
 
Mtabishana sana, Yesu hajawahi kuwa mfalme wa Wayahudi na hakuna aliywahi kuwa mfalme wa Wayahudi. Nani zaidsi ya haile selassie ndiye aliyekwa mfalme na ni simba wa yuda aliyefia kwenye banda la ng'ombe.
 
Kweli kumwita Hayati Magufuli Simba wa Yuda si sawa kabisa. Ni dharau kubwa sana kwa sisi waumini wa dini ya Kikristo.

Maana kwetu sisi Yesu Kristo ndiye Simba wa Yuda.

Rais kweli hapa si sawa kabisa.

Amina, dharau kubwa sana, Asipojirudi basi wacha Simba wa Yuda, Yesu Kristo ashughulike naye.
 
Mtabishana sana, Yesu hajawahi kuwa mfalme wa Wayahudi na hakuna aliywahi kuwa mfalme wa Wayahudi. Nani zaidsi ya haile selassie ndiye aliyekwa mfalme na ni simba wa yuda aliyefia kwenye banda la ng'ombe.

Kweli kabisa kwa akili kama zako za kuvukia road
 
Kweli kabisa kwa akili kama zako za kuvukia road
kwa zako wewe, tuambie lini Yesiu alikuwa mfalme wa Wayahudi? Simba wa Yuda (Wayahudi) ni nembo ya Kifalme wewe. Nembo hiyp wa mwisho kuitumia "official" alikuwa Haile Sellasie wa Ethiopia.

Msitake kujaza watu ujinga mliojazwa nao makanisani huko.
 
Msimlazimishe kuomba msamaha, SIMBA WA YUDA yupo atajitetea mwenyewe. Aliyepita watu walikuwa wanamsujudia na wengine walimwita MUNGU. Mungu aliposhuka nadhani hakuna asiyejua kilichotokea.
Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu.
 
Wewe ni mkristo? Au unadandia treni front. Sisi wenyewe wakristo tumeona poa tu we wa dini ya mataifa unalalamika.
Kama Mkristo na- support kazi anayofanya Mama nchi hii lakini siwezi kusema binadamu kuitwa Simba wa Yuda ni sawa au poa. Binafsi naelewa kafanya hivyo bahati mbaya bila kuujua ukweli.
Ila kwako ni aibu sana kusema Wakristo tumeona poa.
Halafu kajifunze kwenye Biblia wa Wamataifa ni nani ( Gentiles). In short ni wewe na mimi ambao sio uzao wa Israel (Yakobo).
 
Mbona wapambe wa mwenda zake walipo mfananisha mwenda zake na Yesu mliufyata hakusema kitu.
Mbona sabufa aliposema anamfahamu mke wa Yesu tulikaa kimya,Leo hizi kelele zinatoka wapi?
Sisi wafuasi wa hii dini busara yetu ni kunyamaza.
 
Yuda Ni kabila la yuda. Biblia siyo gazeti. Acha kukurupuka.
 
Huyu mbona sijawahi sikia mkilalamika,

King of Kings , Lord of lords, conquering LION OF JUDAH , His Imperial Majesty Haile Sellasie I
 
Kweli kumwita Hayati Magufuli Simba wa Yuda si sawa kabisa. Ni dharau kubwa sana kwa sisi waumini wa dini ya Kikristo.

Maana kwetu sisi Yesu Kristo ndiye Simba wa Yuda.

Rais kweli hapa si sawa kabisa.
Hiyo imeisha

Hata YESU mwenyewe wayahudi walikata pale Herode alipoandika MFALME WA MAYAHUDI

Nisawa na SASA mnavokataa
 
Msisahau Januari na nape ndio walioleta cyber crime law. Na kwa utabiri wa Lema na Lisu mama anaweza akapigisha mchakamchaka nyie mnaocoment vibaya zaidi ya mwendazake.

Anaweza akavua koti mitandao yote ikapigwa pini. Mnapokosoa mjiangalie kidogo. Online kila unapoingi na ku log in huwa unaacha signature yaani IP adress na vinginevyo kwahiyo kukupata ni rahisi sana. Fikiria na chukua hatua.
 
kwa zako wewe, tuambie lini Yesiu alikuwa mfalme wa Wayahudi? Simba wa Yuda (Wayahudi) ni nembo ya Kifalme wewe. Nembo hiyp wa mwisho kuitumia "official" alikuwa Haile Sellasie wa Ethiopia.

Msitake kujaza watu ujinga mliojazwa nao makanisani huko.

Umekaa kibishi, baki hivyo hivyo.
 
Kweli kumwita Hayati Magufuli Simba wa Yuda si sawa kabisa. Ni dharau kubwa sana kwa sisi waumini wa dini ya Kikristo.

Maana kwetu sisi Yesu Kristo ndiye Simba wa Yuda.

Rais kweli hapa si sawa kabisa.
Si sawa kwa nini? Dini huijui unajitia kimbelembele wakati muda wote uko busy kutenda madhambi tuuui!!
 
Mi naomba andiko ndani ya biblia linalo mtaja Yesu kuwa ni simba wa Yuda.
 
Ufunuo 5:5 Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia,Usilie;tazama Simba aliye wa kabila ya Yuda,Shina la Daudi,yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu,na zile muhuri zake saba.
Na mwana Kondoo ni nani kama Simba ni Yesu?
 
yuda si jina tu bali ni kabila pia. Huyo yuda iskariyote ni jina lake la kwanza kulikuwa na yuda wengi ndio maana yule alitambuliwa kama yuda iskariote. Ila simba wa yuda ni moja tu YESU AITWAE KRISTO
Na mwana Kondoo ni yupi kama Yesu ni Simba?.
 
Labda Magufuli ndo alikuwa anajiita hivyo kwa mawaziri wake. Ndo maana wengine wakawa wanamwita mheshimiwa Mungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…