Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Kachemka wakati akiwa na mamlaka kamili ya kuwajibisha ila kawapa wakajikague na kujitolea hukumu.

Ukiona rais anakwepa majukumu yake basi waziri wa fedha alikuwa sahihi kutoa ile kauli kule bungeni.

Wana buy time, wameona mijadala imepamba moto, kwaiyo njia ya kupunguza mijadala ndio huo aliokuja nao.
 
 
Daaah kuna maamzi yanafanyika unajiuliza hivi kweli kuna kiongozi wa nchi hii?
Yaani honestly hapa report ya TAKUKURU ukiisikia ni ujinga ujinga tu lakini bado kiongozi anaisifia!
Inasikitisha sana,labda hawa viongozi wetu,tuna wa-overrate sana,ukute upeo wao baadhi yao ni mdogo.
Waache ujinga,hawajitolei kufanya kazi,tunawalipa kwa kodi zetu.
 
Nchi hii ni kichwa cha mwenda wa zimu! Mtuhumiwa wa wizi ajichunguze na kujipa adhabu!
 
Wana buy time, wameona mijadala imepamba moto, kwaiyo njia ya kupunguza mijadala ndio huo aliokuja nao.
Hapa si ndiyo wamevuruga kabisa.!!!
===
Wanunue muda kwa staili ya Zumalidi na Simba Bob!
 
Waungwana,
Naomba mwenye taarifa nzima ya CAG aliyoitoa kwa kiswahili mara baada ya kuwasilisha Bungeni.
 
Nchi inachekesha sana
Kwa hayo Madudu ilipaswa kwamza Mawaziri Mbarawa, Mwigulu, January,Nape,Ummy na Diblo Dibala wapigwe chini maana ndiyo wasimazi Wakuu wa sera bila kuwasahau Makatibu Wakuu wao.Sasa kuvunja Bodi ya Shirika kunasaidia nini?inamaana Wizara zao hazihusiki?
 

kama nimeelewa vibaya utanisahihisha
Ina Maana Makatibu wakuu+Wakurugenzi waisome report na kuifanyia kazi!
Ina Maana Kama kuna Makosa/Mapungufu ambayo yanefanya say na Afisa A,Au Meneja fulani,Afisa fulani,Mkuu wa Idara,Mhasibu,Engineer,Afisa ugavi,Mwanasheria,nk nk
hao wakuu waliotajwa wamepewa Rungu wamuwajibishe!
Kwani Kuna Makosa hapo?
Nisahihishe kama Nitakuwa nimekosea kiutendaji!(Protocol)
Instead ya Kuwawajibisha Mawaziri/Makatibu wakuu au wakurugenzi.
Wewe Una mawazo gani na Kwa nini?
 
Kwa uhalisia ni kama twachezewa tusahau
 
Mkuu hiyo nayo ni hatua pia huwezi.mchukulia mtu hatua bila kuwa n evidences za kutosha. Tukae tusubiri makatibu wakuu ni wataalam kwenye wizara zao so wao wanajua vizuri zaidi kuliko raisi
Kwaiyo anawaagiza Makatibu Wakuu gani,kwani wao hawahusiki na huo uwizi?
 
Kwa mazingira yaliyopo hao waliotajwa kuisoma report na kuchukua hatua kwa wabadhirifu wengi wao ni wahusika! ndo maana kuna matukio polisi hawezi kujichunguza inaundwa tume!
Huyu mama Kashindwa hata kuielekeza TAJUKURU na taasisi yake ya Urais kulifanyia kazi?
 
Huu usanii Mkuu,hamna kitu hapo,wanatuhadaa!
Nikwambie tu nchi hii kwa sasa haina Rais kuna mtu tu tunamwita Rais lakini kwa anayoshauriwa na kushindwa kupembua pumba na mchele matokea ndo haya tunayoyaona kwenye barua ya Ikulu!!
 
Tangu ripoti ya CAG ilivyo toka na Rais

kuonyeaha kukerwa ilitakiwa tuone baadhi ya

Viongozi wakijiuzulu lakini wapi wamejilausha

kama vile sio wao!!!!

Wanasubiri hadi wafukuzwe
Wakati wa Magufuli nani alichukuliwa hatua? Kuna ripoti safi imewahi kutoka nchi hii?
 
Hi ofisi ilishaanza kudharaulika
 
Safi sana mh.rais hii ndio watanzania wengi walikuwa wanaisubili kwa hamu na nina imani wezi wote watafikishwa mahakamani,pia tunahitaji katiba mpya itayoweka bayana kuwa mwizi wa mali za umma atashughulikiwa vilivyo.
Ni kweli kama mama anasitasita jibu ni Katiba mpya tu kila mtu atawajibika kivyake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…