Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Ila kuitwa Mungu ilikuwa sahihi!?
Aliyemwita Mungu alikuwa hai na aliyeitwa Mungu alikuwa hai.Ilikuwa kazi yake kukubali kuwa yeye ni Mungu.
Huyu hakumsema usiwaralue,Bali alisema umetunyosha kwelikweli.
Akasema walikuwa kitu kimoja
 
Ila kuitwa Mungu ilikuwa sahihi!?
Nami nasubiri akujibu hapa maana duu Magu walimuita mungu na hawakuhiji ila neno simba wa yuda ni la kawaida kabisa maana hata katibu wa simba aliyestaafu ndugu Mwina Kaduguda anaitwa Simba wa yuda.
 
kauli ya kusema vitu vitapanda sana alikosea sana mama yetu

aombe radhi na aikemee maana wafanyabishara wameitumia kama fursa kupandisha vitu ovyo
 
Khaaa Wewe una shida mahali na urudie kusoma ulichoandika.

Nani alikwambia kuwa mtu akifa matendo yake yasiongelewe?

Lazima mtu akifa kinachoongelewa zaidi ni matendo aliyoyafanya hapa duniani. Na kwako liwe somo kubwa na uanze kutenda mema kwa watu la sivyo watoto wako watakuwa wanapata tabu kama unayoipata kwa kusikia yale aliyoyatenda Kipenzi Chako.

Lakini kumbuka Magu naye alifanya hivyo kwa watangulizi wake na mbaya zaidi walipotaka kujitetea akawaimbia waache "kuwashwa washwa" au ndugu umesahau? Duu kweli Mkuki kwa nguruwe ila kwa binadamu.....
Aliyemwita Mungu alikuwa hai na aliyeitwa Mungu alikuwa hai.Ilikuwa kazi yake kukubali kuwa yeye ni Mungu.
Huyu hakumsema usiwaralue,Bali alisema umetunyosha kwelikweli.
Akasema walikuwa kitu kimoja
 
Uliwahi lalamika wapi kabudi alipomuita Magufuli Mhe. Mungu?
Miungu ipo mingi ila hilo jina ni jina la Mungu wa wakristo. Ambao hawajafundishwa kupigana vita vya damu na nyama, ila siyo kwamba watabaki kimya. Kwenye ulimwengu wa roho tutadondosha madhabahu yote yaliyosababisha hii confusion tupate kujenga upya...Tunatuma moto wa roho mtakatifu kuangamiza kila aina ya roho inayosababisha mikanganyiko ndani ya viongozi wetu, tuna mwaga damu ya Yesu kila sehemu ya ardhi ya Tanzani kuunguza uovu wote ili hatimaye amani irejee katika mioyo yetu, Katika Jina Kuu la Yesu, Simba wa Yuda, Mungu asiye shindwa Bwana wa vita Mzee wa Siku nyingi, Amen
 
Yes! The best kwa ukatili na uuaji na utejaji na ubabe wa kishamba
Acheni kusema vitu ambavyo havina ushahidi. Hebu tutajie watu waliouwawa ama kutekwa. Acheni kuchuma Dhambi, mnahukumu utafikiri ninyi ni Mungu ama mlikuwepo wakati anauwa watu. Acheni kuhukumu.

Yesu akawaambia, Basi na asiye na dhambi awe wa kwanza kumpigia mawe mwanamke huyu.
 
Lini aliwahi kuitwa mungu,taahira wewe,hivi watu mna mavi kichwani? Ni lini jpm aliwahi kusema yeye ni mungu?
Wewe una matatizo ama ya kumbukumbu au mhemko umekuzidi,

Wewe ulikuwa nchi gani ambapo haukuisikia kauli ya Kabudi aliyesema Magu ni kama mungu?

Au kwa kuwa sasa kibao kimegeuka ndipo unaanza kuhamaki.

Kipindi kile tulipiga kelele kwamba mnadhihaki imani za watu tuliambiwa tutulie kwani Hadi ameiponya nchi kwa korona , wewe ulikuwa nchi gani?
 
Nchi yetu haina dini, ila watu wake wana dini zao ambazo kila kiongozi anapaswa kuziheshimu na kuzitambua pale wanapokuwa ndani ya utaratibu. Si hekima kabisa kwa kiongozi yeyote kubagaza dini ya raia ambao wanalindwa na katiba kwa haki yao ya ibaada...

Tumsaidie mama yetu, hili wakristo wengi kama mimi limetugusa na kwakua naamini hakufanya kusudi bali hakujua kama ni blasphemy kwa wakristo, sasa ajue kuwa si neno jepesi na busara ni kutolea ufafanuzi au kuomba radhi kwakua hakukusudia ili tusijegawanyika bure pasipo sababu ya msingi.
 
Two wrongs never make a right, yeye akikosa haitoi haki kwa mwingine kukosea vile vile, bali kujifunza na kama kuna adhabu angekuwa hai basi tunhetakiwa kumwadabisha...Tumeona kupitia kwake umuhimu wa Katiba Mpya so ni bora kuanzia sasa tukarebisha haya makosa kama yake kupitia mifumo yetu ambayo mama ni Katiba iliyompa uhalali wakuwa kama Mungu mtu
 
Mkuu Mmawia , asante kwa hoja hii ya nidhamu ya woga.

Kuna watu humu hili la nidhamu ya woga ndio wamelijua Leo baada ya kusemwa na Mama Samia.

If you have time, angalia tarehe ya bandiko hili na hoja yake muone sisi wengine tulilisema lini.


Kwa wavivu wa kufollow links, hapo niliuliza
Hatukuishia Kwa Number 1 tuu,
ila pia niliendesha somo humu namna ya kutofautisha kuongea Kwa ukali na kufoka foka

hata number 3, yule Kiranja Mkuu wa viranja pia tuliwahi kumshauri

Hata baadhi ya Mawaziri walipokosa utu, akina sisi tuliwasema...

Na hatukuishia viongozi wakuu na Mawaziri pekee, hata ma RC tuliwamulika

Huyu pia

Hivyo hili la nidhamu ya woga lilikuwepo sana kwa JPM, lakini twende nyuma na kurudi mbele,
Kwa hali hii, mfano Mama naye ni binadamu, anaweza kukosea, jee akikosea kibinaadamu, kuna kiongozi yoyote ndani ya serikali anaweza kum correct, au kuna any main stream media that would dare criticize or correct her, or the epitome of cowardice inaendelea?!.

Nasisitiza Mama naye she is a human being, anahitaji kusapotiwa, kusaidiwa, kushauriwa, na akikosea akosolewe kistaarabu kwa lugha ya heshima na staha huku akishauriwa the right thing to do, ushauri wangu wa kwanza, ni Tanzania tunaweza kabisa kusonga mbele na kufanya mazuri bila kunyoosheana vidole and calling names kama "Simba wa Yuda".
Nashauri tufanye tuu mambo tofauti bila kumtaja taja Kwa ubaya!
Aachwe Apumzike!.

Jumapili Njema

Paskali.
 

Kabisa hapo chini samia ashauriwe asidhani magufuli hana wanaompenda au waliompenda, kumnanga hadharani na akidhani watu hawaelewi itamcost na kumtenganisha na baadhi ya wananchi, yeye afanye kuunganisha watu hata kinafiki tu huku akifanya kazi yake vizuri
 
Kwa aina ya Teuzi za Rais samia sidhani na sioni akideliver lolote la maana hapa nchini na naona pesa ikiibwa kama njugu na miradi mingi kutokwisha
 
Acha unafiki hakuna mkristo halisi wa aina yako.

Ok kama Rais wako aliitwa "mungu" na wewe ulinyamaza kama mkristo halisi basi wewe ni wakala wa shetani maana kwetu wakristo halisi hatukubali kuongozwa na "mungu" kwa kuwa huyo ni shetani. Ilikupasa nawe ukemee pale Kabudi alipomuita Rais Magufuli kuwa yeye ni kama mungu.

Pia umesema simba wa yuda ni jina la Mungu wa wakristo, hauoni kuwa hauna maana kwa kumpigia kelele Rais ambaye ametumia jina hilo akiamini kuwa ni jina la kawaida maana yeye SI mkristo na jina hilo ni la kawaida tu kama mchezaji wa yanga anavyoitwa Jesus Moroko. Je hapa ulishawahi kulalamika?

Pia nikueleze kuwa Mzee Mwina Kaduguda anajulikana kwa kuitwa simba wa yuda. Je ulishawahi kulalamika jina hilo?

Acha unafiki na ukatubu kwa kuwa una nia ovu dhidi ya mamlaka na imeandikwa iheshemu mamlaka maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Bwana.
 
Kwa aina ya Teuzi za Rais samia sidhani na sioni akideliver lolote la maana hapa nchini na naona pesa ikiibwa kama njugu na miradi mingi kutokwisha
Unamshauri nini sasa ili asikwame?
 
Jiwe aliharibu kila mahala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…