Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Huwezi kuondoa dhana ya umungu mtu kwenye nchii hii bila kuunda mifumo inayojiendesha kama katiba, sheria na taratibu za kuongoza nchi na taasisi zake. Hata yeye hapo alipo kimadarak/kikatiba ni Mungu mtu kwa mujibu wa katiba yetu ni kwamba tu hajaguswa vizuri na vitu vizito. Magufuli hakuwa mungu mtu kwa sababu ya mapenzi yake bali katiba letu bovu ndilo linamfanya kiongozi hasa rais awe mungu mtu. Kama kweli huyu mama anamaanisha anayoyasema na si chuki kwa Magufuli aruhusu mchakato wa kupata katiba mpya na moja wapo ya kuondoa huo umungu mtu mnaousema ni kuondoa kinga ya rais kutokushtakiwa (katiba iruhusu rais aliyoko madaraka/mstaafu ashitakiwe/aondolewe madarakani itakapobainika amekwenda kinyume na katiba ya nchi au maslahi mapana ya nchi). REMEMBER THAT... GREAT MINDS DISCUSS IDEAS WHILE WEAK MINDS DICSCUSS PERSONALITY/PEOPLE.
 
Samia ni Rais Bora,huwezi kumfananisha na yule shetani muuaji
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mungu mtu by virtue of the Consititution of URT. Hatuwezi karne hii kutegemea utashi wa mtu kuongoza nchi ndiyo maana akija huyu tunasifu akija mwingine tunalaumu ni kwa sababu nchi hii inaongozwa kwa utashi wa rais aliyoko madarakani (mungu mtu) na si mifumo ambayo hata raisi anawajibika kuifuata. Wanatofautiana tu style za kuongoza ila rais yoyote wa JMT ni mungu mtu. Haya mengine ni mbwembwe tu. Tunahitaji katiba itakayoondoa uungu mtu wa urais wa JMT na viongozi wengine waliyovalishwa madaraka kupita kiasi na katiba letu bovu.
 
Wewe unamuonaje CAG wa sasa.


Bado naendelea kumsoma, sijajua kama msimamo wake kiweledi , kimaadili na kiuwajibikaji na kiutendaji ukoje kwa kiasi gani iwapo ni wa kuridhisha au namna gani?
 
Nae si alikuwa humo humo kwenye awamu ya 5 na yeyeyndiemnufaika namba 1 wa hiyo awamu, dada anaupiga mwingi hadi anasahau mpira kaucha wapi
 
Kuhamisha serikali kutoka magogoni kwenda Dodoma vipi?
Wilaya zilizokuwa sugu hazikuwa na ofisi, vipi na hao?
 

Dhalimu hakukuta nidhamu ya woga, bali akapandikiza nidhamu ya woga, nidhamu hiyo ilipelekea watu aliokuwa na chuki nao kunyanyaswa, na kufanyiwa ukatili wa wazi. Sisi huku mitandaoni tulikuwa tunampa ukweli wake toka akiwa hai, na hata baada ya kufariki tunaweka ukweli wake wazi, ili kuepusha upotoshaji na sifa za kinafiki. Yaani hatupati tabu since hatujawahi kumkubali alivyokuwa mzima, au akiwa huko ahera madukani. Hatuhitaji msaada wowote maana hii kwetu ndio inatufanya tuwe na nguvu za kiume za kutosha.
 
Shida ni kwamba waliopo sasa wapo kwa ajili ya kulinda interest zao tu.

Wanaoumia ni wengi kuliko wanaonufaika.

That is wrong.
Kwani wale wa awamu ya 5:
1. Hawakuumiza watu?
2. Hawakuwa na interest zao?
 

Amekuambia anategemea kura kupata madaraka? Dhalimu alitangazwa na tume isiyo huru ya uchaguzi kuwa alipata kura 12.5m, je alipata hizo kura Kweli?
 
Nimepitia comments humu kujaribu kuangalia kama Kuna aliye mshauri Huyu mama afanye nini ili kuleta nidhamu kwenye utumishi wa ummma lakiki wapi!!

Magufuli sawa alitishia, Ila nidhamu tuliona,. Je, huyu mama yeye anafanya nini ili kuleta nidhamu hyo. Au yupo haunted na fact kwamba nidhamu kwa Sasa ime dwindle.

Halafu eti anataka nidhamu ya kutoka moyoni eh! Kwa wabongo aliokwisha waruhusu wale kwa urefu wa kamba zao, eh! Jamani,!!

Kwa hapa namheshim tu Kiti Cha urais.

Sema akili pia za wabongo ni mtihani kung'amua hizi twists of words.

Mimi naomba nisamehewe tu. Huyu mama najitahidi kweli kweli kumuelewa lakini wapi?! Naishia kupata 'F'

Nilifurahi alipozungumzia mabadiriko ya elimu, Ila Sasa mengine haya, napata taaabu kwelikweli.

Emwenyezi Mungu nijalie hekima.
 
Nae si alikuwa humo humo kwenye awamu ya 5 na yeyeyndiemnufaika namba 1 wa hiyo awamu, dada anaupiga mwingi hadi anasahau mpira kaucha wapi
Yetu macho na masikio
 
Umenena ukweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…