Rais Samia awarejesha kazini Watumishi zaidi ya elfu nne (4,000+) walioondolewa kipindi cha Magufuli kwa madai ya kugushi vyeti

Uanapotosha makusudi magufuli wakati anahutubia watumishi kule bandarini aliwaambia kama wee ni lasaba ni umejaza lasaba hamna mwenye shida naye ila mtu la saba anafoji ni form four uki mwambia alete cheti cha form anaruka ruka
Ni kweli waliondolewa la Saba kimakosa ndo hao walisharuhusiwa kurudi na wengi walikuwa kwenye kustaafu hivyo walirudi Ili kuchukua mafao yao.
 
Tz hakuna sheria hata Machinga waachwe watakavyo, kuwatoa ni uonevu tu maana hakuna sheria inayoongoza nchi ni Siasa tu za kijingajinga
 
Kweli! Huyu kama aliingia kwa kufoji lazima alikua ashtakiwe na afungwe jela.
Enzi za nyerere kununua jina na kurudia darasa la saba kwa jina la mtu ilikuwa kawaida kwani mfumo ulikuwa hauruhusu mtu kujiendeleza kivingine iwapo utafeli darasa la saba,, ilikua either uwe mwalimu wa UPE au uapply kwenda polisi, sasa kwa mtu mwenye ndoto kubwa, labda kuwa doctor, injinia, meneja, mkurugenzi, etc, walipofeli la saba, option iliyobaki ilikuwa kununua jina na kurudia shule,, hapakuwa na shule nyingi za private eti mtu angeweza kujiunga na kuendelea na masomo ya sekondari,
Tatizo lilikuwa la kimfumo zaidi,, miaka ya sasa mtu hawezi kutumia jina la mtu, wakati kuna options nyingi mno,,
So SSH kuamua hao warudi kazini ni Reasonable na ubinaadamu pia,,
 
Kuna watu wengi mfano bashite, bagaile, etc hii amri haikuwagusa,, huwezi ku cherry pick hivi vitu
 
Kumbe Salary Slip HUJUI kati ya kuku na yai kipi kilianza? FYI Mungu hakuumba yai bali kuku. Kuku ndiye aliyeanza na yai ni mchakato tu wa kiendeleza kizazi cha kuku!
Usishangae tena eti kipi kilianza.
 
Vizuri. Cheti cha form IV hakumuondolei mtu ujuzi alioupata akiwa chuoni plus uzoefu.
 
Hao watu kabla ya kutolewa kazini walikuwa wanafanya kazi Serikalini mbona nchi haikuwa Shimoni? Fine, kabla na baada ya the so called vyeti feki kutoka nchi ilipiga hatua gani?
 
Hakuna jema hapa kwetu, kila analofanya mtu wengine watalalamika
 
Vizuri. Cheti cha form IV hakumuondolei mtu ujuzi alioupata akiwa chuoni plus uzoefu.
Hao watu kabla ya kutolewa kazini walikuwa wanafanya kazi Serikalini mbona nchi haikuwa Shimoni? Fine, kabla na baada ya the so called vyeti feki kutoka nchi ilipiga hatua gani?
Acheni kutete ujinga aisee, mtu kaghushi cheti huyo hana utofauti na jambazi kisheria
 
Nimeipenda, mtu hawezi kufanya kazi miaka 10 halafu unamtoa kirahisi tu...
Mwizi wa cheti au mtumia cheti cha kugushi ni mhalifu anatakiwa kufikishwa mahakamani. Serikali ihalalishe kugushi na kutumia vyeti vya watu wengine.
 
Unachosema ni kweli mama nasikia ana vikozi vya kuunga unga balaa ndo maana naye anashadadia ujjnga .mtu anafoji chei then anarudishwa
Wewe unaemponda mama umetoka hata la saba kweli
 
Duu ina maana wamejiendeleza kuanzia march mwaka huu hadi leo November? ina maana walifanya mitihani wapi na lini? hahahahahaha
Waache wazee wastaafu kwa amani
 
Binafsi hawa walistahili kupewa mafao yao tu na hizi ajira 4000 ziwe ajira mpya haswa kwa vijana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…