Rais Samia awarejesha kazini Watumishi zaidi ya elfu nne (4,000+) walioondolewa kipindi cha Magufuli kwa madai ya kugushi vyeti

Rais Samia awarejesha kazini Watumishi zaidi ya elfu nne (4,000+) walioondolewa kipindi cha Magufuli kwa madai ya kugushi vyeti

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Ni wazi kabisa mtu akifoji kitu official huyu ni mualifu na adhabu yake inaweza kuwa kifungo mpaka miaka7.

Hamna kitu kinasikitisha kama mtu unahangaike kusoma kwa bidii pamoja na changamoto zote unakomaa, halafu ajira aje kupewa mtu ambaye kaamua kutumia shortcut ya kufoji vyeti, hii haiko sawa.

Nilitegemea Hawa watu wawe mfano wa onyo la kughushi vyeti lakini ndio kwanza wanarudishwa kazini, ni sawa na mtu aliefungiwa account yake benki alipokamatwa akingiza noti feki ila sasa anasamehewa na zile noti feki zinahesabiwa kuwa orijino.

Vijana kibao wapo mitaani wamesoma kwa shida ili kumaliza degree / masters, kiukweli hawatendewi haki hawa vijana, Binafsi sikuwa fan wa magufuli lakini kuna mambo machache sana aliyoyafanya nilikuwa upande wake likiwemo hili swala la kuchomoa wanao ghushi vyeti,

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora imetangaza kuwarejesha kazini Wafanyakazi zaidi ya elfu nne (4000+) ambao waliondolewa kazini kutokana na kugushi vyeti katika maeneo mbalimbali lakini sasa kwa huruma ya Rais Samia watarejeshwa kazini kwa sharti la kuwa wawe wamejiendeleza kielimu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora Mohamed Mchengerwa amesema "wale walioweza kujiendeleza ambao ni zaidi ya 4100 tayari wamerejeshwa kazini, pia tunao Watumishi 1150 ambao hawakufanikiwa kujiendeleza maana yake hawana sifa za kutosha kuendelea kuitumikia Serikali japo walikua ni Watendaji wazuri”

Rais Samia alishatuagiza kwamba hawa 1150 kutokana na utendaji wao uliotukuka Watumishi hao wote walipwe haki zao na stahiki zao kama vile wapo kazini kwahiyo watalipwa"
 
Utadhani hakuwa kwenye hiyo serikali.

Ipo siku Rais mwingine anaetokana na CCM, atakuja kumuomba radhi Mbowe kwa kesi ya kusingiziwa, na pengine kumlipa fidia, na CCM hawa hawa wanafurahia Mbowe kuwekwa ndani, watampongeza huyo Rais.

Kuwaelewa CCM na akili zao, ni vigumu kama ilivyo vigumu kujua Mungu alitoka wapi au kati ya yai na kuku, kipi kilianza.

Anyway, awalipe fidia na wale waliobomolewa nyumba zao maeneo ya Kimara wakati wa Mwendazake.
 
Mnawarudishaje kazini watu waliofukuzwa Kwa kuwa na vyeti feki? badala ya kuajiri vijana waliohitimu vyuo vikuu kwa bidii na jitihada zao kwanini tuendelee kuwapa moyo ambao hawakusota darasani kwa miaka ila wao wakachakachua vyeti kwa dakika chache,
Halafu walijiendeleza lini na wapi? Sikupenda watu wafukuzwe kazi kama awamu ya 5 ilivyofanya , lakini porojo kwamba walijiendeleza ni uzushi.
 
Kati ya 4000+ waliojiendeleza kielimu watakuwa wangapi?waliofika mda wa kustaafu niwangapi?na zile stress mtu atajiendeleza kweli?
Wanasiasa wana udanganyifu sana
Naomba ushahidi kama walijiendeleza
 
Wamejiendeleza vipi kielimu?
Mtu alitumia jina la ndugu yake akapata kazi sasa leo hii amejiendeleza vipi kupata hivyo vigezo. Au ambaye alikosa cheti cha Form 4 alienda kuwa private candidate akafanya NECTA na kufaulu. Na kwa muda gani imefanyika hiyo wakati SSH hana hata mwaka. Na walijuaje kwamba watarudishwa mpaka wakaenda kusoma ndani ya miezi 6 hii.

Kama mtu anaitwa Mwajuma Jumanne na alifeli darasa la saba mwaka 1990. Akatumia cheti cha Ashura Abdallah na kazini alitumia hilo jina, huyu vigezo vya miaka ile ya 90s kujiunga na chuo amevipataje leo hii. Na sasa ataitwa Mwajuma au Ashura?

Na vipi mtu aliyefoji vyeti vya taaluma naye amejiendeleza au wamesema ana uzoefu. Kwa nini serikali iingie gharama kulipa watu ambao walivunja sheria kwa kughushi, serikali inaungana na waarifu?

Bora ingewalipa mafao yao ila kazini wasirudi. Kuna watu kibao mtaani wenye vigezo visivyo na mashaka wameambiwa wajiajiri
 
L

Lakini hii serekali inatuanaje sisi wavuvi kata ya kalya tulichomewa nyavu zetu na kuchukuliwa machine zetu za boat kimakosa kabisa tunalipwa lini tutendewe haki
Ni wavuta bangi gani walichoma nyavu zenu. Kwamba watu wa serikali walikuja bila kosa lolote mlilofanya au kukiuka masharti yoyote wakachoma nyavu zenu na boti. Serikali ina wehu wa hivyo?
 
Kwahiyo kughushi cheti si kosa kisheria au sijaelewa vzr.

Kutoboa Mwafrika haitakaa itokee.

Kwamba umeghushi umekatwa halafu serikali inakupongeza.

Sasa yule aliyekuwa anatibu watu isivyo kiutaratibu yeye ana mkosi.

Ni kama tunaenda na pweza wa utabiri
 
Back
Top Bottom