Rais Samia awarejesha kazini Watumishi zaidi ya elfu nne (4,000+) walioondolewa kipindi cha Magufuli kwa madai ya kugushi vyeti

Rais Samia awarejesha kazini Watumishi zaidi ya elfu nne (4,000+) walioondolewa kipindi cha Magufuli kwa madai ya kugushi vyeti

Tatizo inaonekana zoezi liliendeshwa bila haki, sina hata uhakika kama walioachishwa walipewa nafasi ya kujitetea, nina uhakika kuna watu wengi walionewa tuu maana records zetu ni za kuunga unga tu,

kama imegundulika kuna walioonewa na hakuna namna ya kufanya verifications 100%, rudisha wote kazini zoezi lianze upya, na hata kama walifoji kulikuwa hakuna haja ya kumfukuza dereva au tarishi kwa kufoji cheti cha form four (ubinadamu kidogo), tuanze kujenga mifumo yetu vizuri kuzuia haya matatizo
 
Huu ni utumbo kabisa basi na afute sitisho la ajira kwa wahitimu wa Ualimu na wote wapewe ajira kuanzia mwaka 2015 alipositsha Jiwe na pia iwe kama zamani wakitoka chuoni mojamoja wapangiwe vituo vya kazi.
 
Wadau Hayati RAIS MAGUFULI Aliwaondoa Makazini WATUMISHI wote WalioGHUSHI Vyeti na Nyaraka mbalimbali.
Kitendo cha Kughushi CHETI au NYARAKA yoyote ni KOSA la JINAI
Inakuwaje SERIKALI inawarudisha Makazini WATUMISHI waliotenda huo UHARIFU?
Nilitarajia kama WAHARIFU WENGINE Wangeshtakiwa na Kuwafikisha MAHAKAMAMI sio MAKAZINI
 
Wadau Hayati RAIS MAGUFULI Aliwaondoa Makazini WATUMISHI wote WalioGHUSHI Vyeti na Nyaraka mbalimbali.
Kitendo cha Kughushi CHETI au NYARAKA yoyote ni KOSA la JINAI
Inakuwaje SERIKALI inawarudisha Makazini WATUMISHI waliotenda huo UHARIFU?
Nilitarajia kama WAHARIFU WENGINE Wangeshtakiwa na Kuwafikisha MAHAKAMAMI sio MAKAZINI
Naamini tasisi imeona utendaji wao
 
Kuna uhalifu mzuri na wenye faida wa kulisaidia Taifa lako mkuu. Kuna kipindi inatakiwa mtu auwae ili Taifa Kama Taifa lipone ama lijiokoe.
Wameshakata uzoefu wa kazi acha wafanye kazi. Atakuja raisi mwingine watarudi majumbani tena atakuja mwingine atawarudisha. Nchi yetu inaendeshwa kwa utashi mtu alivyopata raha ama hasira tokea kwa mwenza wake.
 
Tanzania ni Nchi Ngumu Sana

Tanzania ni Tajiri

Ndugu Zangu Tuchape Kazi Tukimtanguliza Mungu Mbele
 
Kuna familia ya mbunge mmoja wa kanda ya ziwa waliliwa vichwa wana ndugu 5 kwa kutumia cheti kimoja watu 6! Ngoja nijifanye kuwatembelea nione kama wote wamerudi kazini!

Mwenye nacho ataongezewa na asiye nacho ata kile kidogo atanyanganywa na kupewa aliyenacho.
Korosho zimekosa wanunuzi, hakika tutamkumbuka!
 
Hapo ni mkakati unasukwa wa kuwatengeneza watumishi hewa ili pesa ipigwe.
 
HONGERA na SHUKRANI nyingi kwa rais Samia kwa huruma ya kiuzazi. Kughushi vyeti ni kosa kisheria lakini katika mazingira ambapo waliofukuzwa walifanyiwa kibaguzi inatosha kuharamisha zoezi. Kwa mfano MAJESHI yote, Makonda Bashite , Mwigulu, Kingwangala nk hawakufukuzwa. Lakini pia hilo kosa lilifanyika kati ya waajiriwa na waajiri kwa maana ya shared responsibilities. Kisha mtu amekufanyia kazi vizuri kwa miaka 30, 20, 10 nk leo unamkanaje?

The best solution ilikuwa kuwastaafisha na kuwalipa, au kuwaacha wastaafu kwa hiari au wastaafu umri ukifika. Muhimu zaidi KUZUIA walioghushi kuajiriwa kwa maana ya kuwa makini wakati wa kuajiri.

Kisiasa, zoezi hili linapunguza negative effects za kufukuzwa wamachinga. Ni siasa nzuri mama Samia. Ukimwachia huru na Mbowe na wale wengine wote mnaowaonea kwa kuwa tu ni wapinzani , (tena upinzani ulioko kisheria)utapata kura nyingi pamoja na yangu.

Diffuse political temperature isiyokuwa ya lazima wala tija. Nyie mnaorudishwa kazini mshukuruni MUNGU kwa kumng'oa JPM , kwa kuleta SSH kama Rais na mzidi kumwombea ili aukatae UOVU, uonevu, ubaguzi, ubadhirifu ili nchi ipate maendeleo na baraka. Mwombeeni afuate na aheshimu Katiba na sheria za nchi moyoni na kimatendo. Mchape kazi msahau yaliyopita huku mkiganga madhara mliyopata. Maisha ni safari ndefu.
 
Ni wazi kabisa mtu akifoji kitu official huyu ni mualifu na adhabu yake inaweza kuwa kifungo mpaka miaka7.

Hamna kitu kinasikitisha kama mtu unahangaike kusoma kwa bidii pamoja na changamoto zote unakomaa, halafu ajira aje kupewa mtu ambaye kaamua kutumia shortcut ya kufoji vyeti, hii haiko sawa.
Kazi na iendelee!
 
Hawa watalipwa mishahara yote pamoja na posho za usumbufu kwa kipindi chote walichokuwa mtaani. Hongera CCM mna tengeneza tatizo then mnalitubu afu mnaomba credit kwa wananchi.
 
Hii itakuwa ni hela ya mtu mkubwa tu inaingiziwa mkwanja wa hao wote wanaojiita vyeti fake wamerudishwa ama wamejiendeleza
 
Ni wazi kabisa mtu akifoji kitu official huyu ni mualifu na adhabu yake inaweza kuwa kifungo mpaka miaka7.

Hamna kitu kinasikitisha kama mtu unahangaike kusoma kwa bidii pamoja na changamoto zote unakomaa, halafu ajira aje kupewa mtu ambaye kaamua kutumia shortcut ya kufoji vyeti, hii haiko sawa.
Kama nimemuelewa vzr Waziri ni kwamba wanaorudishwa kazini niwale walioondolewa kazini kwa kutokuwa na elimu ya kidato cha nne na sasa wameshajiendeleza na sio wale 12,000 waliogushi vyeti.
 
Utadhani hakuwa kwenye hiyo serikali.

Ipo siku Rais mwingine anaetokana na CCM, atakuja kumuomba radhi Mbowe kwa kesi ya kusingiziwa, na pengine kumlipa fidia, na CCM hawa hawa wanafurahia Mbowe kuwekwa ndani, watampongeza huyo Rais.

Kuwaelewa CCM na akili zao, ni vigumu kama ilivyo vigumu kujua Mungu alitoka wapi au kati ya yai na kuku, kipi kilianza.

Anyway, awalipe fidia na wale waliobomolewa nyumba zao maeneo ya Kimara wakati wa Mwendazake.
Kwani Mungu aliumba kuku au yai?
 
Ni wazi kabisa mtu akifoji kitu official huyu ni mualifu na adhabu yake inaweza kuwa kifungo mpaka miaka7.

Hamna kitu kinasikitisha kama mtu unahangaike kusoma kwa bidii pamoja na changamoto zote unakomaa, halafu ajira aje kupewa mtu ambaye kaamua kutumia shortcut ya kufoji vyeti, hii haiko sawa.

Nilitegemea Hawa watu wawe mfano wa onyo la kughushi vyeti lakini ndio kwanza wanarudishwa kazini, ni sawa na mtu aliefungiwa account yake benki alipokamatwa akingiza noti feki ila sasa anasamehewa na zile noti feki zinahesabiwa kuwa orijino.

Vijana kibao wapo mitaani wamesoma kwa shida ili kumaliza degree / masters, kiukweli hawatendewi haki hawa vijana, Binafsi sikuwa fan wa magufuli lakini kuna mambo machache sana aliyoyafanya nilikuwa upande wake likiwemo hili swala la kuchomoa wanao ghushi vyeti,

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora imetangaza kuwarejesha kazini Wafanyakazi zaidi ya elfu nne (4000+) ambao waliondolewa kazini kutokana na kugushi vyeti katika maeneo mbalimbali lakini sasa kwa huruma ya Rais Samia watarejeshwa kazini kwa sharti la kuwa wawe wamejiendeleza kielimu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora Mohamed Mchengerwa amesema "wale walioweza kujiendeleza ambao ni zaidi ya 4100 tayari wamerejeshwa kazini, pia tunao Watumishi 1150 ambao hawakufanikiwa kujiendeleza maana yake hawana sifa za kutosha kuendelea kuitumikia Serikali japo walikua ni Watendaji wazuri”

Rais Samia alishatuagiza kwamba hawa 1150 kutokana na utendaji wao uliotukuka Watumishi hao wote walipwe haki zao na stahiki zao kama vile wapo kazini kwahiyo watalipwa"

Kwahiyo sheria hazifuatwi kwenye haya mambo bali ni utashi wa rais.
 
Wadau Hayati RAIS MAGUFULI Aliwaondoa Makazini WATUMISHI wote WalioGHUSHI Vyeti na Nyaraka mbalimbali.
Kitendo cha Kughushi CHETI au NYARAKA yoyote ni KOSA la JINAI
Inakuwaje SERIKALI inawarudisha Makazini WATUMISHI waliotenda huo UHARIFU?
Nilitarajia kama WAHARIFU WENGINE Wangeshtakiwa na Kuwafikisha MAHAKAMAMI sio MAKAZINI
Kuna baadhi ya wafanyakazi hawakughushi kabisa, kosa lao walikuwa wamefika darasa la saba na baadae wakaendelea kupata vyeti vya (mfano) udereva kwa madaraja tafauti. Hivi vyeti vya udereva vilikuwa sahihi siyo feki, sasa hapo unawaondoa nini?
 
Back
Top Bottom