Rais Samia awasili Marekani leo Sept 19, 2021 kuhudhuria Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN)

Rais Samia awasili Marekani leo Sept 19, 2021 kuhudhuria Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN)

Aisee namuombea msamaha huyu Mzee wa watu maana umemkomalia kweli kweli, hakuwa malaika alikuwa ni binadamu ambaye si mkamilifu, yapo ambayo alituuzi wengi lakini ndio ubinadamu. Imetosha apumzike kwa amani Mzee wa watu.
Kwanini apumzike kwa amani wakati alitesa wengi?
 
Mkuu 'Mwanambee' hapo juu kakufahamisha vizuri tu, kwa kukutajia hiyo mifano, lakini wewe unaendelea kujitia ujuaji.

Sielewi hapa una maana gani na hiyo "lockdown" ya New York unayoiandika hapa. Unaelewa maana ya 'lockdown'?
Nadhani wewe ndiyo unataka kuleta ujuaji,utajua hujui.
 
m
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JF Kenedi Jijini New York Marekani leo Sept 19,2021 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UN unaotarajiwa kufanyika tarehe 23 Sept 2021...
mara ya mwisho MEKO alihudhuria huu mkutano lini vileeee???
 
Katika watu ambao hawajielewi kabisa kabisa ni watu waliokuwa timu Magufuli. Ni kaputi wa kiwango cha juu kuliko. Wao walidhani ''makamanda'' ndiyo adui yao wasijue kuwa adui yao alikuwa anakula na Magufuli kila siku. Hebu nikupe mfano mmoja. Huyu Mange ni mmoja ya watu waliomtukana na kumdhalilisha Magufuli mno. Leo rais Samia amesimama na kufurahi naye huku anapiga picha...
Wewe ndiyo mjinga magufuli na sisi tulio msapoti tulijua sana ilo tulikuwa tunawajua maadui wote wa uzarendo kuwa wengi ni viongozi wakubwa au waliowai kuwa viongozi ila uwezi kuamrisha jeshi liwapige risasi, kwani waliokuwa wanapanga njama za kumpindua ndani ya chama hakuwajua?

ILA KUSEMA UKWELI WATU WAJINGA NA WAPUUMBAVU KULIKO WOTE NI CHADEMA MAANA HAWAKUJUA KUWA KIFO CHA MAGUFULI MAANA YAKE NINI ,

awakujiuliza kuwa kilitokana na mikono ya watu au la maana ilo swali wangelijua yasinge wakuta yanayo wakuta na yatakayo wakuta siku zijazo .sasa ni hivi kama kifo ni mkono wa mtu wajue swala la katiba ,uchaguzi huru ,democracy, uhuru wa kujieleza ,mikutano ya kisiasa itakuwa ni ndoto kuwepo kuliko kipindi cha magufuli
 
Haya ndiyo majaribu kweli, hivi Samia pale angefanya nini? Ni kweli mange kimambi kaitukana Sana serikali na akija tz sidhani kama ataachwa, ila kule ugenini na kaja Kama watz wengine kumpokea na ghafla ndiyo hivyo tena, je angeonesha chuki zake kwa mange kimambi waziwazi? Na hata akiionesha Kuna msaada gani?
Kwani ujui mafisadi papa walio gawa pesa kwenye rumbesa wameachwa huru huo ni mtandao wa kifisadi serikalini jomba wanafanya yao chini ya samia ,
 
Ubabe wa JPM ulikuwa na tija kwenye Taifa la watu waoga kama letu. Kwa mfano isingekuja tokea watu wahamie Dodoma kama sio ubabe wa mtu mmoja tu!!!
Kuna mengine ametuachia njia panda ili tuhangaike nayo mpaka tunazeeka. Maana pulling yake inataka zaidi ya mbaula kadhaa. Kwa uthubutu tena kwa mifano, JPM ipo siku atakumbukwa sana. Kama haki za binadamu ndio tatizo, mbona mwenyekiti yuko ndani anapambana na hali yake???
Magufuli alikuwa hana shida na raia wema hata kidogo bali waharifu waliopo serikalini na nje ya serikali
Alikuwa very good president kama angefikisha miaka kumi hata wamarekani wangepiga kelele kutaka nchi yao ipate kiongozi kama magufuli
 
Ulitaka akuweke wewe kimada wake akakataa? Mbona unaandika kama bile Magufuli alikutafuna halafu akakutelekeza. Labda hukumvutia
Mother must go[emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957]
FB_IMG_1632123927893.jpg
 
Wewe ndiyo mjinga magufuli na sisi tulio msapoti tulijua sana ilo tulikuwa tunawajua maadui wote wa uzarendo kuwa wengi ni viongozi wakubwa au waliowai kuwa viongozi ila uwezi kuamrisha jeshi liwapige risasi, kwani waliokuwa wanapanga njama za kumpindua ndani ya chama hakuwajua? ILA KUSEMA UKWELI WATU WAJINGA NA WAPUUMBAVU KULIKO WOTE NI CHADEMA MAANA HAWAKUJUA KUWA KIFO CHA MAGUFULI MAANA YAKE NINI ,awakujiuliza kuwa kilitokana na mikono ya watu au la maana ilo swali wangelijua yasinge wakuta yanayo wakuta na yatakayo wakuta siku zijazo .sasa ni hivi kama kifo ni mkono wa mtu wajue swala la katiba ,uchaguzi huru ,democracy, uhuru wa kujieleza ,mikutano ya kisiasa itakuwa ni ndoto kuwepo kuliko kipindi cha magufuli
Kajifunze kwanza kuandika maneno niliyoyaweka kwenye rangi nyekundu, ukishajua basi uje tufanye mjadala.
 
Nikitumia kingereza utaelewa
🤣
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣Utumbo wa bata.....Umeshindwa kiswahili kiingereza utakiweza? Baba yako alikuwa na PhD ya Kemia na kilimshinda ije kuwe wewe uliyesoma shule za kata!
 
[emoji1787]
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787]Utumbo wa bata.....Umeshindwa kiswahili kiingereza utakiweza? Baba yako alikuwa na PhD ya Kemia na kilimshinda ije kuwe wewe uliyesoma shule za kata!
Duck's stomach ..... you'll know you don't know. Magufuli was not a stupid president that's why he stops all your nonsense. Tanzanians, we want a careful government that follows in the footsteps of the magufuli legacy
 
Duck's stomach ..... you'll know you don't know. Magufuli was not a stupid president that's why he stops all your nonsense. Tanzanians, we want a careful government that follows in the footsteps of the magufuli legacy
🤣
🤣 🤣 🤣 Tatizo lako ni moja. Unajaribu kutafsiri neno kwa neno kutoka kiswahili kwenda kiingereza. Namna hii utakuwa unaongea kiingereza cha kuchekesha muda wote. Namna nzuri ni kuelewa sentensi halafu unaiandika kwa kiingereza.
 
Rais S. S. H na Mange Kimambi pichani.

Nimeona watu wametoa maelezo yenye hisia tofauti kufuatia Mange Kimambi kuonekana katika picha na Mhe. Rais huko nchini Marekani.

Mimi nlifuatilia video inayoonesha namna Watanzania waishio nchini Marekani walivyojitokeza kumpokea Mhe. Rais kwa mahaba makubwa sana akiwamo huyo dada Mange Kimambi. ( Maarufu mtandaoni). Aidha, nimeona katika video, Watanzania mbalimbali wakihangaika kutaka kupata kumbukumbu ya picha na Rais wao mara baada ya kukutana naye. Mmoja kati yao ni huyo Mange Kimambi ambaye anaoneka akitoa simu yake ili apigwe picha na Mhe. Rais wetu.

Inaeleweka dhahiri kuwa, Rais ni Mkuu wa nchi , Amiri jeshi Mkuu, Mfariji Mkuu wa taifa. Vilevile Rais wetu ni mzazi, mama na ni Mlezi. Sisi Wazaramo tuna msemo usemao ' Bozi jako' yaani ukizaa mtoto asiye akili ( bozi) huyo naye ni wa kwako pia. Mama/ mzazi anaweza kuzaa Imamu au Padri, anaweza kuzaa mchumi, mhandisi, mwalimu, daktari, nk hii ikawa furaha sana kwa mzazi. Kwa mkosi tu, mzazi anaweza kuzaa jambazi , kahaba, gaidi, dikteta hata mkwepakodi, hii ikawa huzuni na fedheha. Hata hivyo, mama/ mzazi aliyetimamu kichwani na moyoni hatamkana mwanawe kwa sababu yoyote ile. Na kwamba akipata majanga mtoto huyo mama ataumia na kusikitika sana. Hii ndiyo imekuwa silka na hulka ya kimama siku zote kwa miaka na mikaka . ( Asiye mama anaweza asiilewe vizuri hali hii). Kwa hiyo, kwa maoni yangu, mama ameitumia ile nadharia ya Kiswahili ya 'kiganja kilichonyewa na mtoto akikatwi' au ile ya Wazaramo ya 'Bozi jako'.

Nadharia nyingine huenda imetumika hata kukubali kupiga picha na Mange Kimambi ni ile ya msemo wa Kiswahili ' Mwiba unapoingilia ndipo unapotokea' Mange Kimambi huko nyuma kidogo alionekana akisema vibaya nchi na baadhi ya viongozi wetu kupitia mtandao. Alifanya vibaya sana. ( Bila kujali sababu gani, alikosea), kwa hiyo, kwa kiasi fulani aliichafua taswira ya nchi yetu. Kwa hiyo, huenda mama alitaka yuleyule aliyeichafua taswira ya nchi yetu ndiye huyohuyo aisafishe. 'Mwiba unapoingilia ndipo unapotokea'.

Aidha, tangu dahari, watu wamekuwa wakifanya makosa makubwa na madogo usoni mwa wanadamu na kujisahihisha, kutubu, kuungama, na kujutia makosa yao. Nani anajua, huenda Mange Kimambi naye ameamua kujirudi, kujisahisha, kuungama na kutubu dhidi ya ujinga wake. Kwa mintarafu hii na kwa kanuni ile ya 'kiganja alichonyea mtoto akikatwi', ndiyo maana kwa maoni yangu mama ameamua kukisafisha kiganja chake na kuendelea na maisha.

Hii pia imekuwa ni Falsafa ya mzee Jakaya Kikwete ya kutorithi maadui bali ni busara kutengeneza rafiki wengi zaidi iwezekanavyo. Jamani, ' Bozi jako, mwiba ulipoingilia ndipo utokepo na kiganya alichonyea mtoto akikatwi! Bila shaka picha ile inasema zaidi kuliko maneno yetu. Tuupe muda wakati uwakatike.

IMG_20210920_184431.jpg
 
Back
Top Bottom