Rais Samia: Bei ya mafuta Tanzania ni rahisi kuliko Marekani

Rais Samia: Bei ya mafuta Tanzania ni rahisi kuliko Marekani

Msisahau hata kama kipato cha USA kipo juu pia ni wazalishaji ilipaswa hii bidhaa iwe chini zaidi kwa USA compared to Tanzania.

Au sababu kipato kipo juu ndo mtu anunue pipi ya TZS 50 kwa TZS 50,000?
Inategemea na kipato, hata hiyo pipi ya 50 iliwahi kuuzwa senti 50 pia.
 
Mama hana washauri ama aliokuwa nao wanamuogopa, anatakiwa asiwe anaongea sana maana matamshi yake mengi yanazua utata alafu naona siku hizi anapanic sana hata kwa vitu vidogo tu
 
Naanza Kuelewa move ya tumia akili kwenye uzi wa FDR…
Kiutaratibu haya mahojiano kuna maswali yanapangwa na majibu anapangiwa Rais namna ya kujibu ina maana ameshindwa kujiongeza kweli na kutoa jibu jepesi hivi?…
Acha tuendelee kuangalia mpira magoli baadae
 
N

Njia ni nyingi ndugu, No1.kubwa zaidi ni kupunguza au kufuta baadhi ya Kodi ktk Bei ya mafuta. Ktk kila Lita moja ya mafuta Kuna Kodi zaidi ya 15. No.2. Ni bulk purchasing. Au kuinunua mafuta Kwa wingi na kutunza ktk maghala kudhibiti mfumuko na kudhibiti uhaba. No 3. Ni kuinunua mafuta crude au mazito na kuja kuyasafisha huku, mafuta hayo ni Bei mdogo. No.4 Ni kuzuia viongozi wa Serikali kumiliki vituo vya mafuta. Hapa tunavyolalamika nakuhakikishia Kuna watu pesa kwao zinaingia Kwa mabilioni. Kuna kiongozi mmoja ana vituo vya mafuta Nchi nzima havina idadi. Unadhan Bei itapoa? KATIBA MPYA ndo inaandikwa hivyo maana ndo itatatua hayo.
Nilikwambia huna akili utabisha?

Ufute Kodi harafu yakipanda tena utafuta nini?

Pili ukifuta Kodi kwa hiyo tuache kujenga barabara(Tarura na Tanroads via Road Fund),tuache kujenga mashule na tuache kujenga vituo vya afya Ili wewe ununue mafuta Kwa bei rahisi? 😁😁😁😁..

Hiyo bulk purchase umekuta haifanyiki? Kwani sasa hivi yananunuliwa kwa utaratibu upi? Eti kutunza kwenye maghala kwani saizi yanatunzwa wapi? Na kama hayatoshi kwani kujenga maghala unadhani ni sawa na kujenga madarasa ya covid 19?

Kwa hiyo mitambo ya kusafisha mafuta ni kama vile mitambo ya kutengenezea boflo na slace sio? Unatumia akili au?

Viongozi kumiliki vituo vya mafuta inahusianaje na kupanda bei Kwa mafuta? Wameanza kumiliki vituo vya mafuta awamu ya 6? Sheria inakataza viongozi kumiliki biashara na mali?

Huo ujinga ulioujaza huko Kichwani ni mzigo tosha,kwamba kwenye Nchi zenye Katiba mpya na Bora bei za mafuta ziko chini sio? Mburula hamtakaa muishe Tzn hii.

Na hizo mbinu zako ni za kutatua kupanda bei Kwa mda mfupi au mda mrefu? Kama ni za mda mrefu utakuwa huna akili na hujajubu swali la unataka nini kifanyike at this moment Ili bei zishuke.
 
Mama hana washauri ama aliokuwa nao wanamuogopa, anatakiwa asiwe anaongea sana maana matamshi yake mengi yanazua utata alafu naona siku hizi anapanic sana hata kwa vitu vidogo tu
Watu wapo kazini wanajua wanachofanya yani kama sisi tunaona yupo tofauti wenye nchi nao wanajua wapo wrong lakini wanatarget yao
 
Rais Samia katika kuwajibu wale wanaolalamika kua bei ya mafuta ni kubwa sana amesema hiyo bei ni ndogo sana hasa ukilinganisha na bei ya mafuta Marekani.

Rais anasema juzi alikua Marekani akakuta bei ya mafuta iko juu sana kuliko Tanzania.

Hayo Rais ameyasema leo hii kwenye kipindi cha mahojiano na Tido Mhando.

Juzi pia Rais akiwa Arusha alisema kua watu wanapenda kulalamika umeme ukikatika kidogo tu wakati hata New York umeme unakatika tu hata kuliko Tanzania.


Hapo Mama kaupga mwingi!
Hivi Mama anataka kulinganisha maisha ya Marekani na Bongo kweli??? US Dollar 1 ni sawa Tshs. 2300~2500. Leo bei ya mafuta imetangazwa ni Tshs 3100~3300 ni sawa na US Dollar 1 na senti kadhaa!!

Mama namshauri akomalie kuondoshwa kwa TOZO ZAIDI YA 11 KWENE MAFUTA NDIZO ZINAFANYA BEI YA MAFUTA IWE KUBWA!!!
Tunajua gharama ya kuingiza Lita 1 ya Petrol au Diesel HAIZIDI TSHS 1200: Sasa hii nyongeza ya ya zaidi ya 1500~2000 inatoka wapi kama siyo TOZO ZA SERIKALI ZINAZOTOZWA PASI NA ULAZIMA WOWOTE??
EWURA WAMEWEKA UTITIRI WA KODI ILI WALIPANE MISHAHARA MIZURI!!!HUU NI UNYONYAJI ULOPITILIZA!
 
Msisahau hata kama kipato cha USA kipo juu pia ni wazalishaji ilipaswa hii bidhaa iwe chini zaidi kwa USA compared to Tanzania.

Au sababu kipato kipo juu ndo mtu anunue pipi ya TZS 50 kwa TZS 50,000?
Akili zako na za mama ni zile zile au anakuzidi kidogo. Ukiwa mzalishaji ndo bei inashuka? Gesi mbona tunazalisha lkn zinapanda bei kila kukicha? Au unahis marekani anakusambazia kwako huku kwa hyo bei ya chini kuliko huko kwake?? Kuna factors nyingi za bei kutofautiana. Order ya msosi (ugali samaki) kwa mbunge huko serena hoteli bei yake ni tofauti na ya mzibua vyoo kwa mama ntilie wa buza. Japo wote wameagiza msosi wa ugali samaki.
 
Back
Top Bottom