Rais Samia: Bodaboda ni watoto wangu nitakwenda nao 2025

Rais Samia: Bodaboda ni watoto wangu nitakwenda nao 2025

Mama is trying kuwapa moyo

Hata kama ni kazi mbaya si vyema kuponda njia ambazo mtu anaingiza kipato ilihali ni halali

Ndo anachojaribu kukisema.mama
 
Akipanda watamwangusha, petrol Ina madhara makubwa kwenye UBONGO wa mwanadamu,

Tanks za mafuta kwenye boda zingerudishwa nyuma kuwanusuru boda na Mawenge.

CCM wamezoea cheap politics.

..machinga na bodaboda sio ajira ni kujikimu.

..sera mbaya za Ccm kuhusu ajira, viwanda, na usafiri, ndio zimezalisha machinga na bodaboda.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema anatambua kundi la vijana waliojiajiri kupitia bodaboda na yuko tayari kwenda nao mpaka 2025. Rais Samia Suluhu alizungumza hayo aliposimama kuzungumza na wakazi wa Usa River wilaya ya Arumeru mkoani Arusha.

Vijana hao wa Bodaboda walionyesha kumuunga mkono Rais Samia na kusindikiza Msafara wake kuelekea Usa River kwa ajili ya kuzungumza na Wananchi, baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Faragha wa Mawaziri, Naibu Mawaziri. Aidha bodaboda .

Madereva bodaboda wamesisitiza kazi yao sio ya laana lakini pia wameishukuru serikali ya Rais Samia kwa kuendelea kuwapa mikopo inayowawezesha kuwekeza kwenye shughuli nyingine kama kilimo na biashara.

FqdPZRCXgAEBpec

Image
20230305_212921.jpg
 
Daaah hivi hawa watu wa kuwashikisha mabango namna hiyo huwa wanawaokota wapi? Hao watu huwa wako timamu kichwani?
Hamna sio watu, bodaboda wana umoja yaani chama cha bodaboda kama vile cha.cha walimu, chama cha wafanyakazi

So ni maelewano huko kwenye cha chao kubeba hizo bango
 
Nakuuliza boda ni laana? Kipato halali unaitaje laana. Siwezi kuacha kwa vile nina kazi, nisingekuwa na ajira rasmi ningefanya boda.
Huna kazi,huwezi kufanya hata siziso rasmi kwa sababu mtu mwenye kazi hafanyi?

Mbona umechukua content ya laana tu ukaacha mengine?
Wewe unaweza fanya kazi ya bodaboda ikawa ajira yako ya kudumu?
Je mwanao?Anaweza fanya hii kazi?

Lema anakosea tu jinsi ya kujenga hoja lkn ana points hai
 
CCM saivi wapo kunywa juice tu huku wakichekea tumboni, mama yao kawang'ong'a wao wanachekelea.
 
..machinga na bodaboda sio ajira ni kujikimu.

..sera mbaya za Ccm kuhusu ajira, viwanda, na usafiri, ndio zimezalisha machinga na bodaboda.
Tupambanie KATIBA mpya Ili tuirudishe nguvu KAZI shambani ktk KILIMO Cha kisasa Cha kiviwanda na kibiashara.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema anatambua kundi la vijana waliojiajiri kupitia bodaboda na yuko tayari kwenda nao mpaka 2025. Rais Samia Suluhu alizungumza hayo aliposimama kuzungumza na wakazi wa Usa River wilaya ya Arumeru mkoani Arusha.

Vijana hao wa Bodaboda walionyesha kumuunga mkono Rais Samia na kusindikiza Msafara wake kuelekea Usa River kwa ajili ya kuzungumza na Wananchi, baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Faragha wa Mawaziri, Naibu Mawaziri.

Aidha madereva bodaboda wamesisitiza kazi yao sio ya laana lakini pia wameishukuru serikali ya Rais Samia kwa kuendelea kuwapa mikopo inayowawezesha kuwekeza kwenye shughuli nyingine kama kilimo na biashara.

FqdPZRCXgAEBpec

Image
Kwa mara ya kwwnza ndani ya miaka mingi sana hatimaye CCM tunapiga propaganda nzuri
 
CCM saivi wapo kunywa juice tu huku wakichekea tumboni, mama yao kawang'ong'a wao wanachekelea.
Anakoipeleka CCM kunafikirisha.

Mm nimeshacalculate Kila aina ya hesabu za probability kisiasa bt zinagoma.

Anyway, halipo lisilowezekana chini ya Jua.

Tusubiri.
 
Kwenye maisha jitahidi sana usitafute huruma za watu.

Bodaboda wapige kazi tu, ule ni mtazamo wa mtu mmoja na siyo watu wote. Nina uhakika familia zinazonufaika kupitia ajira ya bodaboda zina mtazamo chanya na tofauti.

Bodaboda waache kutafuta huruma kwa Rais maana hakuna atakachofanya kitaongeza mapato kwenye biashara yao zaidi watatumika kisiasa tu.
 
Mimi sio CCM ila nina akili ya kusema boda ni informal employment. Inasaidia watu kujikimu katika umasikini wao. Huwezi kuita laana.
Alitakiwa kuchunga ulimi wake akajenga hoja kwa tahadhari kubwa. Sasa yeye kasema ni laana? Laaana?!!!!

Ni LAANA. Mtu anapigwa na UPEPO, Anavuta harufu ya PETROL. Je kuna Ndugu au jamaa wa hao Viongozi wa CCM ni dereva wa Bodaboda?
 
Hapana bodoboda sio kazi, ya maana ni kupoteza tu mda.
Inategemea na tafsiri yako ya kazi - kwa ujumla shughuli yoyote halali inayomwingizia mtu kipato ni kazi! Umaskini siyo laana ni mtihani wake Mwenyenzi Mungu. Lazima ikumbukwe kwamba matajiri ni maskini watarajiwa. Unayesema wewe ni maskini inategemea unamlinganisha nani! Mtu huyo huyo unayesema ni maskini sehemu nyingine anaonekana ni tajiri, ukimlinganisha tajiri mkubwa Afrika na Bill Gate huyu wa Afrika kwa akili za ovyo ataoneka maskini. Kusema kuendesha Boda Boda ni laana bila kutoa mbadala wa kazi ya kufanya ni ulimbukeni uliopotiliza inabidi ujitathmini kama unatosha kuwa Kiongozi.
 
Sikutaka sana kutia neno au kushiriki katika huu mjadala wa kauli za Lema kuhusu boda boda. Ila basi ngoja niweke yangu mawazo au maoni kwenye hii makala.
Hivi kweli kuna mtu anamuandaa mtoto wake au kumuombea mtoto wake kua mwendesha boda boda?
Hivi ni kweli kuna shule au chuo kinacho tuandalia vijana kua boda boda?
Nijuavvyo mimi huduma ya boda boda imetokana na ukosefu wa ajira na watu kutokua na usafiri wao binafsi basi ikawa fursa.
Mama Samia ambae ni Rais na Mwenyekiti wetu kusema kua ataenda na boda boda mpaka 2025 sijui kama kweli anawafuraia hao vvijana kufanya kazi hiyo bali anasema hivyo kwakua ni hitaji na tatizo la kisaisa asa kwetu hapa Afrika. Tusiewadanganye vijana kua tupo nao huku tukiwa tunawatumia tu katika kufanikisha mambo yetu.
Hivi ni mtoto wa mbunge,RC,DC,RAS,Mkurugenzi yupi anaendesha boda boda?
Hayati Mao aliyakataa haya ndiyo maana akamuondoa Jiang Kaishek na China ikiwa ya kila mmoja na kunufaika wote.
 
Ila kila kitu kwenye siasa ni fursa, kila kauli ya mmoja inaweza badilishwa na kuwa fursa kwa mwingine. Ila mwisho wa siku mnufaikaji ni mwanasiasa.

Bado watu wa VICOBA nao kuambiwa pia ni watoto wake.

Siku raia watakapoamka na kugundua kuwa wao sio mitaji ya kura za wanasiasa nahisi hapo tutapata kiongozi mzuri. Kinyume na hapo ni mwendo wa kutumiana na kutupana tu.
Wangemobilize na kusajiri chama Cha siasa,

HAKIKA wangetoka hapo walipo.
 
Back
Top Bottom