Rais Samia chagua upande wa Haki au Dhuluma, huwezi kwenda na vyote

Rais Samia chagua upande wa Haki au Dhuluma, huwezi kwenda na vyote

Magufuri aka jiwe was indeed a dictator, no question about that, and kuhusu kumsema rais ili afuate katiba ni lazima na wala sio ombi, hilo hatutaacha na ndio kwanza kumekucha,
mtakuwa hamna kazi za kufanya endeleeni mwishowe atawachoka sasahivi anawasihi mtulie mwisho atawanyoosha kuliko hata mtangulizi wake si mlikoma eee?
 
lugha ngumu nitafsilie siyo wote tumesoma wengine tumesoma tukapata zero kama mbowe tu

hujajibu hoja nimekuuliza nani aliyekuambia anaytaka mabadiriko sema wewe unataka mabadiriko uchaguzi ulifanyika kama wewe unaona ni uchafuzi kwakuwa hukupata madaraka mbona wapinzani wengine walipata walikuwa na katiba yao pekeyao?
Anatujumuisha tu 😂😂😂 eti tunataka!
 
Tuliwaambia JPM ni the best president, mkabishi. Haya sasa mnajinyatua kurudi taratiiiiibu
Hivi maana ya neno Best imebadilika siku hizi?

Magufuli alikuwa ni kichaa tu ambaye akina Kikwette na Mkapa walipuuza ushauri wa Mama yake mzazi. Magufuli alikuwa ni kichaa, mwongo, mwizi, muuaji na DIKTETA
 
Magufuri aka jiwe was indeed a dictator, no question about that, and kuhusu kumsema rais ili afuate katiba ni lazima na wala sio ombi, hilo hatutaacha na ndio kwanza kumekucha,
Kila la heri boss! Wacha nikoleze mkaa hapa nichome mahindi na mishkaki ya paka!
 
Kwa hiyo wananchi wote walioshiriki kwenye mchakato wa kutoa maoni kwa ajili ya Katiba Mpya miaka ya 2012, walikuwa wote ni Chadema!

Uvccm hamjawahi kabisa kumiliki akili!
Wote wako hivi
JamiiForums313878302.jpg
 
Muda si mrefu na yeye atakuwa kama mtangulizi wake tu. Kwa mbaali madaraka yameshaanza kumlevya.

Ukiwa Kiongozi, halafu ukashindwa kutambua mahitaji ya wale unao waongoza kwa wakati huo, maana yake umeshakuwa failure tayari
Huyu mama hamna kitu kabisa.
Ni bora angetoa sababu nyingine kuliko hii ya kusema eti tuinue uchumi kwanza. Kwani nani aliua uchumi?
 
Si ndio waliochagua CCM ikashinda law kishundu au??

Pamoja na wananchi wengine lakini wana CCM ndio walioiachagua ilani ya CCM na kupenda sera zao na ndio maana ikashinda na sasa mama ndio anafanyia kazi ilani hiyo

Hakukuwa na uchaguzi boss, bali kulikuwa na maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
Kwa kuwa mama alisema tumkosoe na tumuoneshe njia,
Katiba ni muhimu na huna budi kuifanya kipaumbele kwa taifa letu pia waache watu wafanye siasa freely na uchumi utapanda.

Tengeneza marafiki na washauri wazuri mama utanishukuru baadae.
 
Tatizo ninaloliona kwa sasa ni kuwa SSH anashindwa kujipambanua kama mtenda haki moja kwa moja,
kuna maslahi ya ccm wenzake,wananchi wa kawaida na wapinzani,SSH hajajua au kuamua asimame wapi,
Tatizo katika nchi hii kitu cha kwanza kinacholindwa ni maslahi ya wana ccm,sio wananchi(wanasiasa wa chama tawala)
 
Haujambo mwana JF mwenzangu wa jukwaa letu pendwa la siasa. Ni matumaini yangu unaendelea kupigana vizuri na changamoto za maisha hasa kwenye uchumi huu ulio dorora kutokana na changamoto za UVIKO. Pambana mwana jamvi, usikate tamaa, maisha ni kuishi kwa matumaini kila iitwayo leo mpaka pale pumzi zetu zitakapo katika.

Nianze kwa kumpongeza Mhe. Rais SSH kwa kufikisha siku 100 akiwa kama rais wa kwanza mwanamke kuongoza taifa letu. Pongezi zangu pia zielekezwe kwenye utendaji wa serikali yake kwa siku hizi za awali, amejipambanunua kama mtu wa haki na anayechukia dhuluma kwa matendo. Wote ni mashahidi, kesi mbalimbali zilizokosa ushahidi zimefutwa, wafungwa kadhaa wameachiwa huru, wafanya biashara wako huru, wanasiasa kwa sehemu wanapumua na zaidi uchumu bado umetengamaa japo sio kwa ubora sana.

Tar. 28/06/2021 wakati anasheherekea siku 100, Mhe. Rais SSH alitumia mwanya huu kuongea na wahariri na waandishi wa vyombo vya habari. Mhe. Rais alipokea maswali na maoni kutoka upande wa waandishi, baadae akapata wasaa wa kujibu maswali hayo na kutoa neno kwenye baadhi ya maoni. Kwa kweli alijitahidi sana kuwa muungwana na kuongea ukweli katika mambo mengi. Naomba nijikite kumshauri Mhe. Rais Katika hoja mbili tu, nazo ni katiba mpya na mikutano ya kisiasa ya hadhara.

Kuhusu katiba mpya
, Mhe. Rais hili ni hitaji la kisheria. Mwaka 2012, ilitungwa sheria na Bunge la JMT kuruhusu mchakato wa katiba mpya kuanza mpaka ukamilifu wake. Bahati mbaya mchakato huo uliishia njiani bila mwafaka wala consensus ya kisiasa. Hakuna sheria mpya iliyotungwa kubatilisha sheria hii ya mwaka 2012, hivyo sheria hii bado iko valid mpaka sasa.

Mhe. Rais, Hoja zako za kuweka pending mchakato wa katiba mpya ni kuhusu utengamavu wa uchumi na utulivu wa kisiasa ili kuvutia uwekezaji.

Mosi, mchakato wa katiba mpya kama utafanywa kwa matakwa ya sheria bila kubakwa na wanasiasa, utakuwa bora sana na kufanya hali ya siasa nchini kutengamaa hivyo kuvutia wawekezaji (kulingana na hoja zako).

Pili, katiba mpya ni hitaji la watanzania, sio hitaji la wawekezaji. CCM imekuwa madarakani kwa miaka 60 mpaka leo bado mnahitaji muda kuboresha uchumi? Nadhani ni wakati muafaka sasa kama taifa tukatunga katiba ya wananchi, katiba itakayo ungwa mkono na walio wengi. Hivyo basi kama wawekezaji hawawezi kuwekeza kwa sababu ya mchakato wa katiba mpya, and so be it.

Kenya matharani, wanatuzidi kwa uwekezaji na wawekezaji nchini kwao, mwaka 2011 walifanikiwa kupata katiba mpya, hatukuona mahala popote uchumi wao ukiteteleka wala uwekezaji kushuka kwa sababu ya mchakato ule.

Mhe. Rais, kuepusha lawama na masimango kwa viongozi wanaojifanya miungu watu pindi waingiapo madarakani, na ili kuleta utengamano wa kisiasa katiba mpya haikwepeki.

Kuhusu Mikutano ya Kisiasa,
Mhe. Rais, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 18, 20 na 21 zinatoa uhuru wa watu kukutana na kutoa maoni yao bila kuingiliwa na mtu yeyote ila kwa kufuata sheria za JMT. Pia, sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992, inavipa haki vyama vya siasa vilivyosajiliwa au vilivyo kwenye mchakato wa kusajiliwa kufanya mikutano ya hadhara mahali popote ndani ya JMT.

Mhe. Rais, hakuna sheria yoyote hapa nchini, inayoruhusu wabunge wenye majimbo tu kufanya mikutano ya hadhara, na kukataza wanasiasa wengine kufanya hivyo. Hakuna kitu kama hicho.Hayo yalikuwa maoni yako binafsi, na tunayachukua kama maoni ya rais, ila sio kama sheria za JMT.

Mhe. Rais, mikutanoo ya hadhara sio hisani kutoka kwako, na wala sio ombi. Ni jukumu lako na serikali yako kusimamia kwa ukamilifu taratibu, Katiba na sheria zote za JMT bila kujali zina kupa favor wewe au wapinzani wako.

Mhe. Rais, uliupata Urais kwa kurithi kulingana na matakwa ya Katiba na sheria za nchi yetu. Embu fikiria wasingefuata katiba na sheria kwenye eneo hilo, labda sasa hivi usingekuwa rais.

Naomba nikukumbushe, kama unachagua kuwa Rais mwema, basi kuwa mwema kwa kila kitu. Usichagua baadhi ya mambo tu ili kufurahisha kundi fulani la watu. Kama unataka kuacha legacy ya kweli katika taifa hili, anza kwa kutenda haki kwa kufuata katiba na sheria zetu.

Lakini kama utaamua kuminya katiba (dictatorship) basi fanya kweli kweli. Usiume na kupuliza, usiwe moto halafu ukawa baridi kwa wakati mmoja. hakuna vuguvugu, hakuna katikati.

Mwisho ila sio kwa umuhimu
, Mhe. Rais, washauri wako wa karibu wanaweza kukujenga au kukubomoa. Kwa sasa una mamlaka makubwa sana, kila utakalofanya utasifiwa na washauri wako. Watu wa kukwambia ukweli kuhusu taifa hili, ni wapinzani wako wa kisiasa na wananchi wasio na mamlaka ya kisiasa. Ukisahau hili na wewe utaanza kuililia hiyo katiba mpya na uhuru wa kisiasa pindi hayo mamlaka yatakapo kutoka, mimi na wewe sio Mungu, hakuna aijuaye kesho zaidi ya Mungu, tenda mema kana kwamba hakuna kesho, tenda haki ili ujipalilie maisha yako ya baadae, usifurahishe kundi dogo la walaji, furahisha umma kwa ujumla.
Kwa kuwa SSH = JPM; mbegu ya wazo lako imetua mwambani. Kwa hiyo ninapayuka tena na tena: KATIBA MPYA!!!?
 
Mama SASHA kawakata mdomo jana.

CCM ni ile ile ..

Ooohhhh ni ile ile.
 
Kuruhusu michakato ya katiba mpya ambayo kwa kiasi kikubwa ni ile yenye mashiko ya tume ya Warioba kwa CCM ni sawa na mtu anayejipa sumu huku akijua kuwa inakwenda kumuua.

Kisaikolojia kukubaliana na mabadiliko ya katiba kwa sasa itaifanya serikali isiwe na morali ya kutekeleza yote wanayoahidi bungeni kwa ilani ya CCM. Uwepo wa ukimya kama vile hakuna madai ya katiba mpya unaipa serikali amani ya kufanya kazi.

Ndio ugumu wa JPM na SSH kukubaliana na michakato ya katiba mpya kwamba sio tu wanajikuta wakishindwa kueleweka miongoni mwa wanachama wa chama tawala bali wanaiyona gharama ya kubadilika kulingana na ukweli wa muda kwamba kuna udhaifu mwingi wa kiutendaji unaoonekana miongoni mwa watu wanaoiangalia serikali na inaonekana suluhisho ni uwepo wa katiba mpya.

Marais wanaununua muda, ingawa mategemea ni kuona zile sababu za kuununua muda zinakuwa na mafanikio ya hicho kinachofanyika kwa maana ya utekezaji wa majukumu ya kukuza uchumi.
 
Haujambo mwana JF mwenzangu wa jukwaa letu pendwa la siasa. Ni matumaini yangu unaendelea kupigana vizuri na changamoto za maisha hasa kwenye uchumi huu ulio dorora kutokana na changamoto za UVIKO. Pambana mwana jamvi, usikate tamaa, maisha ni kuishi kwa matumaini kila iitwayo leo mpaka pale pumzi zetu zitakapo katika.

Nianze kwa kumpongeza Mhe. Rais SSH kwa kufikisha siku 100 akiwa kama rais wa kwanza mwanamke kuongoza taifa letu. Pongezi zangu pia zielekezwe kwenye utendaji wa serikali yake kwa siku hizi za awali, amejipambanunua kama mtu wa haki na anayechukia dhuluma kwa matendo. Wote ni mashahidi, kesi mbalimbali zilizokosa ushahidi zimefutwa, wafungwa kadhaa wameachiwa huru, wafanya biashara wako huru, wanasiasa kwa sehemu wanapumua na zaidi uchumu bado umetengamaa japo sio kwa ubora sana.

Tar. 28/06/2021 wakati anasheherekea siku 100, Mhe. Rais SSH alitumia mwanya huu kuongea na wahariri na waandishi wa vyombo vya habari. Mhe. Rais alipokea maswali na maoni kutoka upande wa waandishi, baadae akapata wasaa wa kujibu maswali hayo na kutoa neno kwenye baadhi ya maoni. Kwa kweli alijitahidi sana kuwa muungwana na kuongea ukweli katika mambo mengi. Naomba nijikite kumshauri Mhe. Rais Katika hoja mbili tu, nazo ni katiba mpya na mikutano ya kisiasa ya hadhara.

Kuhusu katiba mpya
, Mhe. Rais hili ni hitaji la kisheria. Mwaka 2012, ilitungwa sheria na Bunge la JMT kuruhusu mchakato wa katiba mpya kuanza mpaka ukamilifu wake. Bahati mbaya mchakato huo uliishia njiani bila mwafaka wala consensus ya kisiasa. Hakuna sheria mpya iliyotungwa kubatilisha sheria hii ya mwaka 2012, hivyo sheria hii bado iko valid mpaka sasa.

Mhe. Rais, Hoja zako za kuweka pending mchakato wa katiba mpya ni kuhusu utengamavu wa uchumi na utulivu wa kisiasa ili kuvutia uwekezaji.

Mosi, mchakato wa katiba mpya kama utafanywa kwa matakwa ya sheria bila kubakwa na wanasiasa, utakuwa bora sana na kufanya hali ya siasa nchini kutengamaa hivyo kuvutia wawekezaji (kulingana na hoja zako).

Pili, katiba mpya ni hitaji la watanzania, sio hitaji la wawekezaji. CCM imekuwa madarakani kwa miaka 60 mpaka leo bado mnahitaji muda kuboresha uchumi? Nadhani ni wakati muafaka sasa kama taifa tukatunga katiba ya wananchi, katiba itakayo ungwa mkono na walio wengi. Hivyo basi kama wawekezaji hawawezi kuwekeza kwa sababu ya mchakato wa katiba mpya, and so be it.

Kenya matharani, wanatuzidi kwa uwekezaji na wawekezaji nchini kwao, mwaka 2011 walifanikiwa kupata katiba mpya, hatukuona mahala popote uchumi wao ukiteteleka wala uwekezaji kushuka kwa sababu ya mchakato ule.

Mhe. Rais, kuepusha lawama na masimango kwa viongozi wanaojifanya miungu watu pindi waingiapo madarakani, na ili kuleta utengamano wa kisiasa katiba mpya haikwepeki.

Kuhusu Mikutano ya Kisiasa,
Mhe. Rais, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 18, 20 na 21 zinatoa uhuru wa watu kukutana na kutoa maoni yao bila kuingiliwa na mtu yeyote ila kwa kufuata sheria za JMT. Pia, sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992, inavipa haki vyama vya siasa vilivyosajiliwa au vilivyo kwenye mchakato wa kusajiliwa kufanya mikutano ya hadhara mahali popote ndani ya JMT.

Mhe. Rais, hakuna sheria yoyote hapa nchini, inayoruhusu wabunge wenye majimbo tu kufanya mikutano ya hadhara, na kukataza wanasiasa wengine kufanya hivyo. Hakuna kitu kama hicho.Hayo yalikuwa maoni yako binafsi, na tunayachukua kama maoni ya rais, ila sio kama sheria za JMT.

Mhe. Rais, mikutanoo ya hadhara sio hisani kutoka kwako, na wala sio ombi. Ni jukumu lako na serikali yako kusimamia kwa ukamilifu taratibu, Katiba na sheria zote za JMT bila kujali zina kupa favor wewe au wapinzani wako.

Mhe. Rais, uliupata Urais kwa kurithi kulingana na matakwa ya Katiba na sheria za nchi yetu. Embu fikiria wasingefuata katiba na sheria kwenye eneo hilo, labda sasa hivi usingekuwa rais.

Naomba nikukumbushe, kama unachagua kuwa Rais mwema, basi kuwa mwema kwa kila kitu. Usichagua baadhi ya mambo tu ili kufurahisha kundi fulani la watu. Kama unataka kuacha legacy ya kweli katika taifa hili, anza kwa kutenda haki kwa kufuata katiba na sheria zetu.

Lakini kama utaamua kuminya katiba (dictatorship) basi fanya kweli kweli. Usiume na kupuliza, usiwe moto halafu ukawa baridi kwa wakati mmoja. hakuna vuguvugu, hakuna katikati.

Mwisho ila sio kwa umuhimu
, Mhe. Rais, washauri wako wa karibu wanaweza kukujenga au kukubomoa. Kwa sasa una mamlaka makubwa sana, kila utakalofanya utasifiwa na washauri wako. Watu wa kukwambia ukweli kuhusu taifa hili, ni wapinzani wako wa kisiasa na wananchi wasio na mamlaka ya kisiasa. Ukisahau hili na wewe utaanza kuililia hiyo katiba mpya na uhuru wa kisiasa pindi hayo mamlaka yatakapo kutoka, mimi na wewe sio Mungu, hakuna aijuaye kesho zaidi ya Mungu, tenda mema kana kwamba hakuna kesho, tenda haki ili ujipalilie maisha yako ya baadae, usifurahishe kundi dogo la walaji, furahisha umma kwa ujumla.
Huyo rais hana akili ya kuchuja article ya Coronavirus ajue tu hii fake news.

Kaja kuhutubia watu kawaambia wajifukize kwa article ya fake news.

Unategemea nini cha maana hapo?
 
Kuruhusu michakato ya katiba mpya ambayo kwa kiasi kikubwa ni ile yenye mashiko ya tume ya Warioba kwa CCM ni sawa na mtu anayejipa sumu huku akijua kuwa inakwenda kumuua.

Kisaikolojia kukubaliana na mabadiliko ya katiba kwa sasa itaifanya serikali isiwe na morali ya kutekeleza yote wanayoahidi bungeni kwa ilani ya CCM. Uwepo wa ukimya kama vile hakuna madai ya katiba mpya unaipa serikali amani ya kufanya kazi.

Ndio ugumu wa JPM na SSH kukubaliana na michakato ya katiba mpya kwamba sio tu wanajikuta wakishindwa kueleweka miongoni mwa wanachama wa chama tawala bali wanaiyona gharama ya kubadilika kulingana na ukweli wa muda kwamba kuna udhaifu mwingi wa kiutendaji unaoonekana miongoni mwa watu wanaoiangalia serikali na inaonekana suluhisho ni uwepo wa katiba mpya.

Marais wanaununua muda, ingawa mategemea ni kuona zile sababu za kuununua muda zinakuwa na mafanikio ya hicho kinachofanyika kwa maana ya utekezaji wa majukumu ya kukuza uchumi.

..ccm ni chama kikubwa na kikongwe.

..siyo rahisi kuwa swept away na mabadiliko ya katiba.

..kwa upande mwingine naamini ccm ita-gain kwa kuwa mstari wa mbele ktk kuandika katiba mpya, au kuifanyia marekebisho hii iliyopo.

..pia ni vizuri kufanya mabadiliko wakati nchi ina amani, na utulivu, kuliko kufanya mabadiliko under pressure huku kukiwa na rekodi mbaya ya human rights violations.

..Watz huwa hatusubiri mambo yaharibike ndipo tufanye mabadiliko.
 
Tuliwaambia JPM ni the best president, mkabishi. Haya sasa mnajinyatua kurudi taratiiiiibu.
Hapana SSH is the best. JPM alituharibia nchi kabisa ni Mungu tu alituepushia matatizo kutoka kwake maana aliyoyapanga mbele yalikuwa balaa. Tumshukuru sana Mungu.
 
Back
Top Bottom