Rais Samia: Fedha ambazo zingegharamia Sherehe za miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, zigawanywe sawa

Rais Samia: Fedha ambazo zingegharamia Sherehe za miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, zigawanywe sawa

Kwanini Tanganyika pamoja na udogo wa Zanzibar lakini ilikubali kuungana?? Kwanini mchonga meno hakuiunganisha Tanganyika na Algeria ama Nigeria nchi kubwa mwenzake??
Kwanini jamaa aliitwa mchonga meno? Nataka kujua asili ya hilo jina mkuu tafadhali!
 
huyu mama muambieni Tanganyika haiwezi kupelekeshwa na Urojo. she is where she is because of Katiba and we respect that. short of that she is not even a presidential material.
 
Madam president kaamua kwa busara

Maana kuna jamaa hapa wengipiga mpunga mrefu
Kkkkk
JamiiForums-460750266.jpg
 
Ahsante mama, ujumbe mzuri kabisa. Muungano wa equals -hamna juniour partner au seniour partner wa muungano. Tanganyika Zanzibar wote hadhi sawa kwenye muungano.
 
Hivi kuna mfuko Wa muungano ambao hizi fedha zinatoka bara na visiwani? Kama haupo basi itakuwa ni kama kuchukua hela za bara na kuzipeleka visiwani. Au fungu hili linapatikanaje?
 
Hatamu za muungano zipo Tanganyika, Zanzibar kote kumetapakaa vichogo/majeshi kutoka Tanganyika, kama 50-50 imekuwa nongwa basi vunjeni muungano mkaungane na Algeria nchi kubwa mwenzenu.,

Unapokuja kwenye mgao na faida ya muungano huwezi kumuangalia mshiriki mwenza wako kwa udogo wake sababu nchi 2 huru ziliungana.
Hoja yangu siyo 50/50 hilo wala sina shida nalo. Hujanijibu swali langu huu muungano mumelazimishwa? Na kama mnaona huu muungano si wa Haki mnashindwa nini kama serikali na wananchi kuanzisha petition ya kujiondoa kama ilivyofanyika kwa Brexit? Nachelea kusema wazanzibari wengi wenu unafiki umewajaa mnaposhindwa kutatua changamoto zenu lawama zote kwa serikali ya Tanganyika.
 
Dodoma!

Akizungumza Leo katika kongamano la Muungano jijini Dodoma, Makamu wa Raisi Dr . Philip Mpango amesema Raisi Samia Suluhu Hassan ameelekeza Fedha zilizotakiwa kutumika katika shughuli za maadhimisho ya miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zigawanywe pande hizo mbili (Tanganyika na Zanzibar) ili zikafanye shughuli za maendeleo!

Dk. Philip Mpango ametumia takribani dakika 20 kuhutubia wanakongamano na Kisha kuondoka ili aendelee na shughuli zake za Kila siku za kulijenga taifa!
View attachment 1764536
TAREHE 26 Aprili, 1964 Mataifa mawili haya ya Jamuhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar yalioungana na kuunda Taifa jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo badae ikabadilishwa na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hivyo kila mwaka ifikapo Aprili 26, tunakumbuka siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambapo mwaka huu Muungano huu unatimiza miaka 57, huku ukiwa ni Muungano wa mfano na imara katika Bara la Afrika na ulimwenguni pote.
View attachment 1764577
Ni kiasi gani kilitakiwa kugharamia shughuli za sherehe za muungano?

Kwa nini sherehe hizo zimeahirishwa (pawepo na sababu)

Hakuna popote kwenye katiba, sheria au makubaliano ya muungano yanayosema mgawanyo uwe sawa kwa sawa.

Serikali ya Zanzibar huwa inachangia kiasi kwenye uendeshaji wa shughuli za muungano? (sharti hili liwekwe wazi)

Utaratibu unaelekeza kuzingatia asilimia sio nusu kwa nusu
 
Hatamu za muungano zipo Tanganyika, Zanzibar kote kumetapakaa vichogo/majeshi kutoka Tanganyika, kama 50-50 imekuwa nongwa basi vunjeni muungano mkaungane na Algeria nchi kubwa mwenzenu.,

Unapokuja kwenye mgao na faida ya muungano huwezi kumuangalia mshiriki mwenza wako kwa udogo wake sababu nchi 2 huru ziliungana.
Halafu jaribu kutumia lugha ya kistaarabu kuwaita watu vichogo maana yake nini.? Nadhani hata mimi nikikuita kwa lugha ya kukukashifu hautafurahia .mna tabia ya kujiona wastaarabu kumbe ushuzi mtupu.
 
Kwa ufupi kila zama na mambo yake.... mwache aijenge zanzibar. Ni sebemu ya Tanzania 🇹🇿. Namsapoti asilimia 100%. Tuache unafki, mpenda kwao hutunzwa, waswahili walisema hivo.

Hili litam - cost..

Viongozi wetu hawa hawajui kuwa Wa - Tanganyika tulio zaidi ya 55,000,000 ukilinganisha na Wazanzibari wasiozidi 2,000,000 hawaoni mantiki ya kuongozwa na Rais raia toka taifa jingine dogo kabisa...

Huu muungano HAPANA. Binafsi mimi huwa sielewi huu ni muungano wa aina gani. Ni muungano wa kulazimishana...

HAYA MAMBO SIYO KABISA. Si ajabu hili lika - speed upya na haraka HISIA ZA UBOVU/KASORO za muungano huu...

I predict kuwa, mambo haya yanayoonekana kuwa madogo dogo, tutambue kuwa, yanaweza ku - speed mwisho wake kabla ya 2025...

Ajifunze kwa marehemu Magufuli. He was selfish President, si msikivu, aliyejidhania ni mtakatifu kuliko Mungu, mwenye kiburi, aliyejiona ana akili kuliko watanzania wote..

Mwisho wake, akafa kifo cha ajabu na çha kusikitisha...

Samoa jifunze kwa tukio hili. Go and follow the right path. I see her, she is almost going through the same way...

Tatizo la viongozi wetu ni ugumu wao au pengine hawataki kusikiliza na pengine kupokea ushauri wa watu "wadogo" na "wapumbavu" kama sisi...
 
Nini mantiki ya kugawana sawa? Upande mmoja wa muungano huo una asilimia 2% na nyingine 98% halafu fedha wagawane 50 kwa 50?? Ni akili ya namna gani hii. Tukianza na nani alikuwa anagharimia sherehe hizo, utakuta swala la kugawana ni kama kuna mmoja anagawiwa. Ikiwa fedha hizo zilichangwa na pande zote za muungano - ni sahihi kusema kila mtu arejeshewe alichochanga - hakutakuwa na sherehe. Nimekuwa nikiamini kuwa sherehe za kijaifa zimekuwa zikigharimiwa na Bara!! Sasa sherehe ni chanzo cha mapato huko Visiwani!

Usawa huwa sio 50/50. Usawa ni kila mmoja kupata fursa kwa kadiri ya uwezo wake (equity vs equality).

Kwa jambo hili mama amenikwaza! Na ameanza na jambo ambalo hata sio moja ya matatizo ya muungano!!
 
Baby here we goooo.... In Marlaw voice
 
Punguza hasira boss, Zanzibar ni miongoni mwa nchi zinazounda muungano
Zanzibar ila ni ndogo so haiwezekani Rwanda na Tanzania mjerumani agawanye sawa raslimali sawa mkuu.objectivity inatakiwa na sio subjectivity
 
Ilatakiwa akajenge nazo hospitali mwanakwerekwe kama mlivyouzutumia nyingine kujenga barabara mwenge na hospitali Dodoma
Kwahiyo fungu moja la fedha zipelekwe Zanzibar na jingine Tanganyika au Tanzania? Kwasababu Tanganyika haina mamlaka ya mapato?
 
Back
Top Bottom