Rais Samia, hayupo mchawi, pafahamu ulipotuchanganya

Rais Samia, hayupo mchawi, pafahamu ulipotuchanganya

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kwa hakika ulianza vizuri na sifa za dhati tukakumwagia.

Hauna mtu wa kumlaumu, bali huku ndiko uliko tuchanganya:

1. Kauli yako kuwa katiba mpya isiwe kipaumbele chetu (wakati wewe ni mnufaika wa iliyopo).

2. Kauli yako kuwa kudai katiba mpya ni kuleta chokochoko.

3. Kuongeza kodi na tozo kwa wananchi katikati ya janga la Corona (wakati vigogo kodi haziwahusu).

4. Kuendelea kujikongoja na vita dhidi ya gonjwa la Corona (wakati vigogo mko salama).

5. Kuendeleza sera kandamizi dhidi ya haki za watu kujumuika.

6. Kutokuchukua hatua thabiti kulingana na ripoti za CAG.

7. Kuendekeza uwepo wa takrima kwa vigogo usiokuwa na tija.

8. Kunyamazia ukiukwaji wa katiba bungeni kuliko hata na wabunge kharam.

Haya yanataka matamko yako thabiti yenye kuzingatia sheria na katiba ya nchi ili kuyaweka sawa.

Kwenye majanga yanayo athiri moja kwa moja watu kiuchumi, kodi na tozo hupunguzwa, haziongezwi.

Machungu ya ukweli huu bila shaka ndiyo yaliyomfikisha mzee baba hapa:

IMG_20210719_051952_877.jpg


Vipi anapata kodi katikati ya gonjwa hili? Uamuzi wake wa kukomaa (rudimentary) tu kuwa ugonjwa huu haupo in desperation, mtu anaweza kuuelewa.

Kwa hakika tulipo, hakuna haja ya kumlaumu dobi. Kaniki ni rangi yake.

Ninawasilisha.
 
Umma wa watanzania walikuwa naye kabla ya kauli yake kuhusu katiba mpya.

Angali hajachelewa. Kutereza si kuanguka.
Watanzania wa fb ,tweeter ,jf ,insta vituko ni vingi
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Umma wa watanzania walikuwa naye kabla ya kauli yake kuhusu katiba mpya.

Angali hajachelewa. Kutereza si kuanguka.
Umma wa watanzania unaozungumzia wewe ni wapi. ..wewe wafia chadema ndio unaita Umma. .we unaakili kweli. .?
 
Back
Top Bottom