Rais Samia ikikupendeza muongezee muda CDF General Mabeyo

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Rais wangu Samia Suluhu Hassan nitafurahi mno kama ukikataa CDF General Mabeyo asistaafu sasa bali nakuomba muombe umuongezee muda mpaka 2025 na ikiwezekana pia nenda nae hadi 2030 ikikupendeza.

Ameliheshimisha JWTZ na ni Jemedari sahihi, makini na aliyetukuka kabisa.

Tafadhali usiiache hii Hazina bali endelea nae kwani ni Mtu Makini hasa Kimedani na Kiutendaji.

Namkubali mno na hata Sisi Wananchi pamoja na 99% ya Wanajeshi tunamkubali sana CDF General Mabeyo.
 
Wakati ule mlitaka Magufuli aongezewe muda atake asitake, Sasa mmehamia kwa Mabeyo.

Hivi Tanzania tuna matatizo gani?
 
Upuuzi mtupu. Ina maana kwenye jeshi yeye tu ndio anauwezo wa kuliongoza jeshi. Sheria kanuni na taratibu za kazi zifuatwe.

Ni ujinga kuamini kwamba mtu kwa kuwa kafanya vizuri basi hakuna mtu mwingine anayeweza kufanya vizuri pia.

Kama umri wa kustaafu umefika akae pembeni apishe wengine waendelee.
 
Kwa njinsi alivyofanikisha misheni kali ya kuwanasa magaidi bila kutumia hata kiwembe; Commando Lt. Urio afikiriwe.

Au mnataka kumtupa kama toilet paper? Hamna utu kabisa ninyi.
 
Wazanzibar wanahitaji hiyo nafasi mkuu
Akipewa Mtu wa Zanzibar hiyo nafasi ya CDF itakuwa si vyema sana kwa sababu zangu ambazo kwa sasa naomba nizihifadhi.

CDF atokee Tanzania Mainland tu sawa?
 
Wee unasema wakati waliopo chini yake wanatamani hata kesho atoke.
Nawajua baadhi na Mmoja wapo yuko Mbweni ndiyo Bingwa wa Majungu kwa CDF General Mabeyo kwakuwa tu kuna Maslahi fulani kayabana na hicho Cheo alikuwa akikitaka sana Yeye.
 
Namkubali sana jenerali akifika miaka 75 ya umri ndio wamstaafishe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…