#COVID19 Rais Samia: Ilikuwa ni vigumu kwangu kufanya kazi na Hayati Magufuli hasa alivyokuwa anakabiliana na suala la Covid -19

#COVID19 Rais Samia: Ilikuwa ni vigumu kwangu kufanya kazi na Hayati Magufuli hasa alivyokuwa anakabiliana na suala la Covid -19

Nashukuru huyu Mama hakuwa Rais kipindi cha Corona, bila shaka mpaka leo Tanzania tungekuwa kifungoni.

Huyu Mama taifa likipitia kigumu kama cha Corona na mashinikizo kibao ya wazungu naamini hawezi kuhimili kifupi Mama ni mwepesi sana.

Nilikuwa na imani kidogo na Mama Samia ila sasa imekufa kabisa, kifupi mama hana dira wala mwongozo wa Taifa anaongoza kimazoea tu.

Kama CCM mnalipenda Taifa letu huyu Mama anatakiwa akamilishe tu hii awamu.
Yupo hadi 2030 labda kama Mungu aamue kumchukua.
 
Jiwe walilolikataa waashi ndo jiwe kuu la pembeni, hata wanaomuhoji huyo mama walishagundua kuwa bado matumizi ya akili hamna
 
Labda utueleze amevunja sehemu gani ya kiapo? Kumbuka kiapo kinasema nini kuhusu siri
Pili, Magufuli alipokuwa anasema ''hii nchi imeriwa kweri ...'' hakuwa anavunja kiapo kwa maana yako? Magufuli alipotueleza mkataba wa Bagamoyo walioujadili wenyewe katika Cabinet hakuvunja kiapo?

Well said, ndio maana tukiwasikia watu wanasema wao ni CCM hawataki katiba mpya tunawashangaa sana. Katiba ni mwongozo wa nchi unaomgusa kila mtu bila kujali itikadi dini etc

JokaKuu
Tatizo lenu mmefanya JPM ndiyo benchmark ya nchi...Two wrongs never make a right nchi ni zaidi ya JPM jamani, tukubali kuongozwa na sheria, kanuni, taratinu na miongozo.
 
Hii inatosho kuamini JPM alipumzishwa na bi tozo alilijua hilo na kwa kusagia huku possible alipata msaada wa Us na msoga... atafunguka tu yote.. haka ka bibi kachawi sana
Kwamba kalijua kuwa màgufool anataka kutupwa kwenye ziwa la moto
 
Kama alimshauri nunua magenereta akagoma, Mwamba akaenda kuchimba Bwawa la Nyerere, basi akalifukie watu tujipange kununua majenereta, maana kwa sasa yamejazana kwenye balaza za maduka
 
Uwanja wa taifa waliaga mwili mamilioni na sehemu kibao misongamano mikubwa akiwemo mama Samia wakuu wa vyombo.vyote vya ulinzi na usalama na hakuna aliyekuwa kachanja au kuvaa barakoa uliona walikufa kwa Corona?
Yaani wewe kwa sababu hakuna ndugu zako waliokufa kwa corona kipindi kile unadhani nchi ilikuwa salama na hakuna huo ugonjwa. Kwa taarifa yako watu walikufa kwa ugonjwa huu sana tu. Serikali ilikuwa haitoi taarifa
 
Yaani wewe kwa sababu hakuna ndugu zako waliokufa kwa corona kipindi kile unadhani nchi ilikuwa salama na hakuna huo ugonjwa. Kwa taarifa yako watu walikufa kwa ugonjwa huu sana tu. Serikali ilikuwa haitoi taarifa
Mbona wewe hujafa? Acha woga! Hata wazee wetu wangesema kimbia risasi inaua!, tusingepata uhuru!
 
Acha roho mbaya. Kwa taarifa yako Mama alikuwa anamwambia JPM in black and white mambo aliyokuwa anaona hayaendi sawa hasa miaka miwili ya kwanza ya utawala wao mpaka akataka kujiuzulu. JPM asivyojua katiba akamwambia jiuzulu nitachagua mtu mwingine ndipo alipoambiwa kuwa SSH akijiuzulu tunarudi kwenye uchaguzi upya ndipo ikabidi waendelee tu hivyo hivyo. Siyo kwamba SSH anasema baada ya JPM kufariki
Ila wabongo hizo tetesi unaongea kama unahadithia tamthilia vile.
 
MMzee





Yule ni Hamnazo Kabisa. Ndio shida ya kuongozwa na mtu anaeingia period Kila wakati
Tulia tu rafiki. Kwanza mwanamke mwenye miaka 62 haingii period. Halafu kuingia period siyo ugonjwa. Mama yako angekuwa haingii period wala usingezaliwa mpumbavu wewe. Huyo unaye tu hadi 2030 labda Mungu aamue kumchukua
 
Huyu mama Samia corona ingemkuta Akiwa Raisi angetupiga mi lock down hadi tungekoma

Na tungevaa mibarakoa l hadi machoni double double hadi nyuso zetu tuonekane kama vinyago vya kimakonde
Hata angekuwa Rais kipindi corona imechachamaa asingetoa amri ya lockdown. Watanzania wangekula nini? Yeye alichokuwa anataka ni kukubali kuwa ugonjwa upo na watu kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo kuliko KUKANA kuwa hakuna ugonjwa na ku-pretend kuwa haupo.
 
Acha roho mbaya. Kwa taarifa yako Mama alikuwa anamwambia JPM in black and white mambo aliyokuwa anaona hayaendi sawa hasa miaka miwili ya kwanza ya utawala wao mpaka akataka kujiuzulu. JPM asivyojua katiba akamwambia jiuzulu nitachagua mtu mwingine ndipo alipoambiwa kuwa SSH akijiuzulu tunarudi kwenye uchaguzi upya ndipo ikabidi waendelee tu hivyo hivyo. Siyo kwamba SSH anasema baada ya JPM kufariki
Wewe hujanielewa,
Kwa nini Chato aseme alikuwa anamkubali JPM na wapo njia moja.

Leo hii amekuwa mtu wa mafumbo, mipasho na kama haitoshi amekwenda kumsema hovyo US.

Halafu huo uongozi wake aliokuwa anaona ni bora ndio huu?
 
Mama alikuwa anataka lock down magu alikataa katakata ,watz tushukuru mungu kovidi 8likuja kipindi cha JPM ingekuja kipindi cha huyu pimbi tunge dhalilika sana
COVID ilikuwepo sana kipindi Mama anachukua madaraka. Angekuwa na nia hiyo angefanya. Anafahamu sana kuwa kwa hali halisi ya Watanzania lockdown isingewezekana. Hata kama ana mapungufu yake lakini yeye siyo mjinga kama mnavyotaka kutuaminisha
 
Back
Top Bottom