Rais Samia, jaribio lolote la kuipa Zanzibar mamlaka kamili ndilo litakuwa anguko lako

Rais Samia, jaribio lolote la kuipa Zanzibar mamlaka kamili ndilo litakuwa anguko lako

Anaongelea mipaka. Use eyes.
Tunavunja muungano. Machogo yarudi bara na makomwe yaende Zanzibar. Enough should be enough. Tutaheshimiana tu. Mazereu na kelele zenu ni nyingi wakati Tanganyika inagharamia vitu vingi huko mchamba wima

Mtanganyika kajaa huku majeshi Na mpaka wamasai eti wamekuja kuchunga samaki , mradi wakimbie Tanganyika imewachosha
 
Kwani sasa hivi ipoje?

Nimekuambia Zanzibar wana 3 branches tayari. Tanganyika wana 3 branches tayari, ila ya JMT imefichwa ndani ya Tanganyika. Kwa maana kwamba Tanganyika imebeba gharama za branches zake na ile ya JMT

Kukiwa na serikali 3 kutakuwa na Tanganyika itakayokuwa na branches zake na gharama zake. Zanzibar tayari wanazo zao. Ile ya JMT itachangiwa na itakuwa na majukumu machache sana ndivyo federal system inavyofanya kazi

Rasimu ya arioba ina mfano mzuri sana. Kutakuwa na Mabunge ya Tanganyika na Zanzibar ambayo yapo hadi sasa

Lile la JMT litakuwa na wajumbe 75 tu ambao ni wachache kuliko Wabunge wa Zanzibar waliopo Dodoma leo
Kama sikosei rasimu inasema 45 ni Wabunge wa Tanganyika watakaohudumiwa na Tanganyika
30 ni Wabunge wa Zanzibar watakaohudumiwa na Zanzibar. Kwasasa hao 30 ni mzigo wa Tanganyika

Tuonyeshe gharama zinaongezeka wapi?

Una shida kubwa mahali. Three branches za federal government ukiongeza three branches za Tanganyika government bado unakuwa na three branches, eh?

Jielimishe zaidi kuhusu federal governing system.
 
Zanzibar inamamlaka kamili , ndo mana Ina rais wake , Tz na Z tunashirikiana kwenye mambo ya muungano tu
 
Sijui nini sasa, si nimekuambia kuwa ni nchi inayoundwa na visiwa ? Kwa nini yenyewe isambaratike ila Zanzibar isambaratike?

Wewe uliyeleta hoja ya Zanzibar itasambaratika ndio unatakiwa ueleze kwani Zanzibar ina utofauti na nchi nyingine za visiwa hadi isambaratike huku nyingine hazisambaratiki

Zanzibar tayari kuna dangerous political rivalry isiyofichika kati ya Pemba na Unguja. Wale kugawana mbao ni asubuhi tu!
 
Zanzibar inamamlaka kamili , ndo mana Ina rais wake , Tz na Z tunashirikiana kwenye mambo ya muungano tu
Raisi huyo Si wa Zanzibar ni kijana aliyewekwa Na Mvamizi Tanganyika kulinda maslahi ya Tanganyika
 
Una shida kubwa mahali. Three branches za federal government ukiongeza three branches za Tanganyika government bado unakuwa na three branches?
Hapana! huwezi kueleza kwanini gharama zinaongezeka. Unapotosha tu kwa kuweka namba

Eleza kwani sasa hivi gharama zinapunguaje ikiwa tuna serikali 3 mbili zikiwa pamoja?

Bunge la Dodoma ni la Tanganyika kiuhalisia. Bunge lina wabunge 393 kati ya hao
Ukiondoa Wabunge takribani 80 wa Zanzibar unabaki na 313 wa Tanganyika

Bunge la JMT kwa mujibu wa Rasimu litakuwa na Wabunge 75 , wachache kuliko wa Zanzibar waliopo Dodoma
Tanganyika itakuwa na 45 wachache kuliko waliopo Dodoma kutoka Zanzibar.
Hivi hapo gharama zinaongezeka au zinapungua?

Serikali za nchi husika zitahudumia wananchi wake kama ilivyo sasa. Tanganyika inayoitwa Tanzania ina 41T na Zanzibar ina 2.5T. Kwa mambo 7 ya muungano nchi husika zitachangia. Hapo gharama zinaongezeka au zinapungua?
Kumbuka sasa hivi Tanganyika inabeba gharama hizo 100%

Mahakama nayo ni hivyo hivyo, tayari kuna Tanganyika na Zanzibar. Ile ya JMT itakuwa ndogo sana ikiachangiwa na nchi washirika. Hapo gharama zinapungua au zinaongezeka? Kwasasa gharama zote anabeba Mtanganyika

Unaelewa japo kidogo
 
Mi kwa mawazo yangu muungano huu uvunjwe. Uje mwingine. Utakaotunufaisha wote. Haiwezekani kuwa na kitu kinacholalamikiwa na kila mtu halafu kipo kwa ajili ya hao hao watu.
Najua kuna wengine wana hofu na usalama wa nchi mbili zitakazo tokea. Kwamba kunaweza kukawa na uadui utakaochagizwa na maadui wa nje. Wengine wana hofu na mali, undugu, ujirani na utamaduni. Haya yote yawekwe ktk majadiliano kabla ya kuuvunja muungano uliopo ili kusiwe na loop hole ya kuingiza hila.

Sasa hivi bara nao hawataki muungano. Zanzibar wao tangu tunazaliwa wanataka kuvua "koti".

Mbona Mombasa ilipotengwa Na Zanzibar hakujatokea hayo uliyoyaandika ?
 
Narudia tena hakuna mtanzania mpumbavu wa kupigia kura mwanamke tena asiye na akili timamu ,kuwa rais 2025 ...shika sana haya maneno yangu
Rais 2025-30 ni Samia suluhu Hasan note my words, ameshapata kura zote na ameshashinda kwa asilimia 80,trust me anasubiri kuapishwa tu.
#Tanzania haitaweza kurudi kwenye ubinafsi, umimi, Ukabila and in poor international relationship never ever!
 
Hapana! huwezi kueleza kwanini gharama zinaongezeka. Unapotosha tu kwa kuweka namba

Eleza kwani sasa hivi gharama zinapunguaje ikiwa tuna serikali 3 mbili zikiwa pamoja?

Bunge la Dodoma ni la Tanganyika kiuhalisia. Bunge lina wabunge 393 kati ya hao
Ukiondoa Wabunge takribani 80 wa Zanzibar unabaki na 313 wa Tanganyika

Bunge la JMT kwa mujibu wa Rasimu litakuwa na Wabunge 75 , wachache kuliko wa Zanzibar waliopo Dodoma
Tanganyika itakuwa na 45 wachache kuliko waliopo Dodoma kutoka Zanzibar.
Hivi hapo gharama zinaongezeka au zinapungua?

Serikali za nchi husika zitahudumia wananchi wake kama ilivyo sasa. Tanganyika inayoitwa Tanzania ina 41T na Zanzibar ina 2.5T. Kwa mambo 7 ya muungano nchi husika zitachangia. Hapo gharama zinaongezeka au zinapungua?
Kumbuka sasa hivi Tanganyika inabeba gharama hizo 100%

Mahakama nayo ni hivyo hivyo, tayari kuna Tanganyika na Zanzibar. Ile ya JMT itakuwa ndogo sana ikiachangiwa na nchi washirika. Hapo gharama zinapungua au zinaongezeka? Kwasasa gharama zote anabeba Mtanganyika

Unaelewa japo kidogo

Kutakuwa na Bunge la Tanganyika na, kwa ukubwa wa Tanganyika, haliwezi kuwa dogo; kutakuwa na mahakama za Tanganyika na kutakuwa na executive branch ya Tanganyika.

Kwenye federal level, napo kutakuwa na Bunge la federal, ambalo lazima liwe na ukubwa wa kutosheleza mahitaji ya uwakilishi; kutakuwa na mahakama za federal na kutakuwa na executive branch ya federal.

Rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ina weakness moja kubwa sana. Federal government haiwezi kuendeshwa kwa michango ya Tanganyika na Zanzibar. Federal government lazima iwe na full taxing authority. Vinginevyo, federal government will collapse kufumba na kufumbua, ukiibuka mgogoro wa kikatiba baina ya Tanganyika government, federal government na Zanzibar government.

Sijawahi kuona federal government isiyokuwa na taxing authority. Na taxing authority ndiyo itakayosababisha kuwe na ulazima wa federal legislative branch kuwa na uwakilishi mpana.
 
Mzigo upi kiongozi? Zanzibar watakuwa na serikali yao kwa gharama zao, Tanganyika watakuwa kwao na Serikali yao halafu Serikali shirikishi wakikubaliana itakuwepo kwa gharama za pande zote kwa mujibu wa makubaliano kama hamtataka kila nchi itabeba uhuru wake.,

Ni jambo jema kutakuwa na Passport ya Zanzibar, tanganyika mtarudia jina lenu muache kujivisha koti la Muungano kama ndio jina la nchi yenu., jisikieni fakhari kwa Tanganyika yenu kama wazanzibar wanavyojivunia kuwa na jina la Zanzibar
Sema jamaa unachuki sana na Tanganyika
 
Kuna kila dalili Zanzibar ikajitenga na kuwa nchi kamili kwa maslahi ya Viongozi wetu wa awamu hii.

Ni zaidi ya hatari endapo Zanzibar itaruhusiwa kuwa na mamlaka kamili kwa usalama wa Tanganyika!

Na hapa nisipepese macho NAONA KILA DALILI RAIS WETU WA SASA ANATAKA ZANZIBAR IWE NCHI HURU.

Kwenu Tiss.

Pelekeni hii kwenye uzushi😂😂 Watanzania wanaoenda kutunga uongo😂😂
 
Ni vizuri awape tu na kila mtu aende kwao.
Na faida za Muungano hata sijawahi elewa.
 
Kutakuwa na Bunge la Tanganyika na, kwa ukubwa wa Tanganyika, haliwezi kuwa dogo; kutakuwa na mahakama za Tanganyika na kutakuwa na executive branch ya Tanganyika.
Kwani sasa hivi hakuna Bunge la Tanganyika? Lile lililopo Dodoma ni la Tanganyika kwasababu asilimia 98 ni mambo ya Tanganyika. Ukubwa wa Bunge la sasa ambalo ni la Tanganyika ni uwepo wa gharama zaidi za Wabunge wa Zanzibar wasiokuwa na kazi yoyote palekwasababu mengine hayawahusu

Gharama gani zimeongezeka? Nimekueleza Bunge la sasa lina wabunge 393 ambao wanatosheleza Tanganyika. Ukiondoa 80 waliobaki ni 313 wa Tanganyika. Nionyeshe hesabu itakayoongeza Wabunge wa sasa pale Dodoma

Pili, idadi ya wabunge haikuandikwa katika msahafu au Bibilia. Tanganyika inaweza kupunguza majimbo.
Nimekupa mfano wa Zanzibar kwenye BLW wapo 50 tu wakiogopa gharama.
Kwavile wanaleta Wazanzibar kwa gharama za Tanganyika Dodoma wapo zaidi ya 80

Nonyeshe kwa namba kipi kitaongeza Wabunge wa Tanganyika tofauti na sasa? Kipi kitaongeza gharama tofauti na sasa. Ni hesabu si Hisia na hapa ndipo uonyeshe
Kwenye federal level, napo kutakuwa na Bunge la federal, ambalo lazima liwe na ukubwa wa kutosheleza mahitaji ya uwakilishi; kutakuwa na mahakama za federal na kutakuwa na executive branch ya federal.
Rasimu imeweka 75, 45 Tanganyika , 30 Zanzibar. Bunge litajadili mambo 7 tu . Hivyo Bunge la shirikisho halkitakaa mieizi mitatu kama la sasa. Kuna 7 items ambazo zinajadilika kwa muda mfupi sana. Gharama zinatoka wapi?

Huwezi kuniambia Tanganyika haiwezi kuhudumia Wabunge 45 ikiwa sasa hivi imebeba Wabunge 80 wa Zanzibar ambao uwepo wao ni kusikiliza mada za Tanganyika zisizowahusu.
Rasimu ya Katiba ya Tume ya Warioba ina weakness moja kubwa sana. Federal government haiwezi kuendeshwa kwa michango ya Tanganyika na Zanzibar. Federal government lazima iwe na full taxing authority. Vinginevyo, federal government will collapse kufumba na kufumbua, ukiibuka mgogoro wa kikatiba baina ya Tanganyika government, federal government na Zanzibar government.
Yes naubaliana nawe, lakini kwasasa JMT inaendeshwa na kodi za Tanganyika, kwanini basi kusiwe na % ya kodi kila upande ili iwe ya Federal. Wewe unadhani hiyo kodi haipo sasa hivi, ipo na anayeilipia ni Tanganyika

Bajeti ya Zanzibar ni 2.5T, kodi wanazokusanya TRA NI 400B na ZRB ni 500B. Hakuna hata senti moja inayovuka bahari kuja katika muungano. Shughuli za muungani zinahudumiwa % na kodi za Watanganyika katika bajeti ya 41.T

Maana yake ni moja ,gharama unazosema zimebebwa na Tanganyika, usichotaka ni kuona Zanzibar inawajibika
Watanganyika wanasema hapana! Zanzibar inabebwa kuliko eneo lolote ikiwa na mchango 0 kwa Tanzania
Sijawahi kuona federal government isiyokuwa na taxing authority. Na taxing authority ndiyo itakayosababisha kuwe na ulazima wa federal legislative branch kuwa na uwakilishi mpana.
Federal itakuwa na tax authority ambayo ni % ya kodi za washirika. Kwa maana kwamba kila mshirika atatoa sehemu ya mapato kwa Federal, ndivyo ilivyo sasa hivi kwa bahati mbaya Tax ya JMT inalipwa na Tanganyika peke yake. Zanzibar hawana mchango wowote wanashindwa na mkoa kama Simiyu lakini wanapata shea kubwa sana ya mapato ya JMT ambayo ni mapato ya Tanganyika

Tuonyeshe kwa hesabu si Hisia gharama zipo wapi? zitaongezekaje ?

Zanzibar kuwajibika si kuongeza gharama ni kushiriki badala ya kuning'inia katika mbeleko wakilipiwa bill za kila kitu
Tanganyika wamechoka ! wanataka ushirika au watue zigo


JokaKuu Pascal Mayalla
 
Kwani sasa hivi hakuna Bunge la Tanganyika? Lile lililopo Dodoma ni la Tanganyika kwasababu asilimia 98 ni mambo ya Tanganyika. Ukubwa wa Bunge la sasa ambalo ni la Tanganyika ni uwepo wa gharama zaidi za Wabunge wa Zanzibar wasiokuwa na kazi yoyote palekwasababu mengine hayawahusu

Gharama gani zimeongezeka? Nimekueleza Bunge la sasa lina wabunge 393 ambao wanatosheleza Tanganyika. Ukiondoa 80 waliobaki ni 313 wa Tanganyika. Nionyeshe hesabu itakayoongeza Wabunge wa sasa pale Dodoma

Pili, idadi ya wabunge haikuandikwa katika msahafu au Bibilia. Tanganyika inaweza kupunguza majimbo.
Nimekupa mfano wa Zanzibar kwenye BLW wapo 50 tu wakiogopa gharama.
Kwavile wanaleta Wazanzibar kwa gharama za Tanganyika Dodoma wapo zaidi ya 80

Nonyeshe kwa namba kipi kitaongeza Wabunge wa Tanganyika tofauti na sasa? Kipi kitaongeza gharama tofauti na sasa. Ni hesabu si Hisia na hapa ndipo uonyeshe

Rasimu imeweka 75, 45 Tanganyika , 30 Zanzibar. Bunge litajadili mambo 7 tu . Hivyo Bunge la shirikisho halkitakaa mieizi mitatu kama la sasa. Kuna 7 items ambazo zinajadilika kwa muda mfupi sana. Gharama zinatoka wapi?

Huwezi kuniambia Tanganyika haiwezi kuhudumia Wabunge 45 ikiwa sasa hivi imebeba Wabunge 80 wa Zanzibar ambao uwepo wao ni kusikiliza mada za Tanganyika zisizowahusu.

Yes naubaliana nawe, lakini kwasasa JMT inaendeshwa na kodi za Tanganyika, kwanini basi kusiwe na % ya kodi kila upande ili iwe ya Federal. Wewe unadhani hiyo kodi haipo sasa hivi, ipo na anayeilipia ni Tanganyika

Bajeti ya Zanzibar ni 2.5T, kodi wanazokusanya TRA NI 400B na ZRB ni 500B. Hakuna hata senti moja inayovuka bahari kuja katika muungano. Shughuli za muungani zinahudumiwa % na kodi za Watanganyika katika bajeti ya 41.T

Maana yake ni moja ,gharama unazosema zimebebwa na Tanganyika, usichotaka ni kuona Zanzibar inawajibika
Watanganyika wanasema hapana! Zanzibar inabebwa kuliko eneo lolote ikiwa na mchango 0 kwa Tanzania

Federal itakuwa na tax authority ambayo ni % ya kodi za washirika. Kwa maana kwamba kila mshirika atatoa sehemu ya mapato kwa Federal, ndivyo ilivyo sasa hivi kwa bahati mbaya Tax ya JMT inalipwa na Tanganyika peke yake. Zanzibar hawana mchango wowote wanashindwa na mkoa kama Simiyu lakini wanapata shea kubwa sana ya mapato ya JMT ambayo ni mapato ya Tanganyika

Tuonyeshe kwa hesabu si Hisia gharama zipo wapi? zitaongezekaje ?

Zanzibar kuwajibika si kuongeza gharama ni kushiriki badala ya kuning'inia katika mbeleko wakilipiwa bill za kila kitu
Tanganyika wamechoka ! wanataka ushirika au watue zigo


JokaKuu Pascal Mayalla

Draft ya Katiba ya Tume ya Warioba ina serious flaws katika uendeshaji wa federal government. Serikali haiwezi kutegemea michango ya kodi kutoka kwa constituent states. Federal government lazima iwe na direct taxing authority, na tax rates zake inevitably huwa zinakuwa kubwa kuliko za states.

Try to study established federal governing systems around the world; you’ll gain a better understanding of how they operate.

Consider, kwa mfano, Marekani:
[emoji3578]Bunge la Marekani ni kubwa kuliko la state yoyote ya Marekani. Na hii ni kwasababu ya federal taxing authority. Huwezi kulipisha watu kodi halafu ukawanyima uwakilishi wa kutosha Bungeni.
[emoji3578]Marekani kuna 1 US Supreme Court na lower federal courts throughout the country, including 13 federal circuit (appellate) courts na 94 federal district courts.
[emoji3578]Marekani ina federal law enforcement agencies. Kwa kiasi kikubwa, FBI ndiyo police wa federal. Marekani pia ina federal bureau of prisons.
[emoji3578]Marekani pia ina wizara zote zinazopatikana kwenye level ya state na zile ambazo ni za federal pekee yake (i.e., defense, foreign affairs, citizenship and immigration) pamoja na federal reserve (central bank).
[emoji3578]Marekani kuna federal land ambayo usimamizi wake unagharamiwa na federal government.

Turudi kwetu Bongo. Kwa muundo wetu wa sasa, government institutions tulizonazo huku Bara, kimsingi, ni za JMT, lakini zimekuwa pia zikifanya kazi kama za Tanganyika. Tukiwa na federal government, hizi zote inabidi zikome kufanya kazi kama taasisi za Tanganyika. Kwa hiyo, Tanganyika itabidi itunge Katiba na sheria zake na kisha iunde taasisi zake yenyewe. Kama taasisi zilizopo zitarithiwa rasmi na Tanganyika, basi federal government itabidi iunde taasisi zake yenyewe. There’s no sharing, kwasababu Katiba na sheria zinazozisimamia lazima ziwe tofauti.

Draft ya Katiba ya Warioba haikupi picha kamili ya gharama ya uendeshaji wa federal governing system. Hata kama ingepitishwa leo, Tanganyika bado itakuwa na kibarua cha kupata at least Katiba yake yenyewe, assuming itaamua kurithi sheria zilizopo. Hata hivyo, bado italazimika kuzifanyia tweaking za hapa na pale hizo sheria ili kuondoa migongano na masharti yaliyomo kwenye Katiba ya Tanganyika. Kingene ni kwamba federal government itabidi itunge sheria zake yenyewe. Kumbuka, hili jukumu ni ya Bunge la federal, sio la Bunge Maalumu la Katiba!

Kufikiri kwamba hakuna tofauti ya gharama kati ya gharama za muundo wa sasa na za muundo wa federation ni sawa na ujanja wa mbuni kuficha kichwa kwenye mchanga!
 
Kuna kila dalili Zanzibar ikajitenga na kuwa nchi kamili kwa maslahi ya Viongozi wetu wa awamu hii.

Ni zaidi ya hatari endapo Zanzibar itaruhusiwa kuwa na mamlaka kamili kwa usalama wa Tanganyika!

Na hapa nisipepese macho NAONA KILA DALILI RAIS WETU WA SASA ANATAKA ZANZIBAR IWE NCHI HURU.

Kwenu Tiss.

iking’oka si tutaboresha mafia
 
Kwanza ahsante, kuna kitu ulichoshindwa kuthibitisha, ongezeko la gharama! hujaweza kuthnitsha bali una hisia

Nimekuwekea wazi kwamba Tanganyika inabeba 100% ya gharama za kinachoitwa Tanzania

Kuna gharama gani itakayoongezeka? Kugawana gharama kunapunguza au kuongeza?

Zanzibar inasimama na taasisi zake, na Tanganyika ina zake kwa jina la Tanzania. Unapokuwa na federal government Tanganyika inaathirika vipi ikiwa sasa hivi imebeba zigo la Zanzibar yenyewe.
Draft ya Katiba ya Tume ya Warioba ina serious flaws katika uendeshaji wa federal government. Serikali haiwezi kutegemea michango ya kodi kutoka kwa constituent states. Federal government lazima iwe na direct taxing authority, na tax rates zake inevitably huwa zinakuwa kubwa kuliko za states.

Try to study established federal governing systems around the world; you’ll gain a better understanding of how they operate.

Consider, kwa mfano, Marekani:
[emoji3578]Bunge la Marekani ni kubwa kuliko la state yoyote ya Marekani. Na hii ni kwasababu ya federal taxing authority. Huwezi kulipisha watu kodi halafu ukawanyima uwakilishi wa kutosha Bungeni.
[emoji3578]Marekani kuna 1 US Supreme Court na lower federal courts throughout the country, including 13 federal circuit (appellate) courts na 94 federal district courts.
[emoji3578]Marekani ina federal law enforcement agencies. Kwa kiasi kikubwa, FBI ndiyo police wa federal. Marekani pia ina federal bureau of prisons.
[emoji3578]Marekani pia ina wizara zote zinazopatikana kwenye level ya state na zile ambazo ni za federal pekee yake (i.e., defense, foreign affairs, citizenship and immigration) pamoja na federal reserve (central bank).
[emoji3578]Marekani kuna federal land ambayo usimamizi wake unagharamiwa na federal government.
Nadhani umeuelewa mfumo wa federal tofauti. Marekani ina federal na states, lakini katika federal ni ndogo kuna mambo ukiachilia zile za ulinzi.

Tunapozungumzia federal kwa Tanzania tuna maana ya mambo 7 ambayo ni Ulinzi na usalama, Mambo ya ndani, mambo ya nje, Fedha, Katiba na vyama vya siasa. sehemu kubwa ni Ulinzi na usalama, mambo ya ndani na nje.

Iwepo mechanism ya kupata kodi za ku run federal government kutoka kwa washirika tofauti na sasa ambako ''federal' inalipiwa na Tanganyika peke yake. Weka % katika kodi za washirika kutoka pande zote

Unajaribu kukuza tu kwamba kutakuwa na mahakama kubwa ya federal, si kweli, kwasababu hata sasa mahakama kuu haifanyi kila kazi za mahakama zingine kama ilivyo US kwa circuit courts.

Kutakuwa na Bunge kubwa , nimekuonyesha kwamba wapo 393 hadi sasa , Zanzibar inapeleka wasikilizaji 80+ wengi kuliko Bunge la rasimu ya Warioba ambapo Zanzibar italeta 30 tu.
Tanganyika itapunguza mzigo wa kuwa na wasikilizaji tu kwa ajili ya ajira

Wewe unadhani kuhudumia Wabunge 80+ wa Zanzibar pale Dodoma ni nafuu kuliko Wabunge 45 wa Tanganyika katika ' federal parliament', hesabu hizi ni kutoka wapi.?


Turudi kwetu Bongo. Kwa muundo wetu wa sasa, government institutions tulizonazo huku Bara, kimsingi, ni za JMT, lakini zimekuwa pia zikifanya kazi kama za Tanganyika. Tukiwa na federal government, hizi zote inabidi zikome kufanya kazi kama taasisi za Tanganyika. Kwa hiyo, Tanganyika itabidi itunge Katiba na sheria zake na kisha iunde taasisi zake yenyewe. Kama taasisi zilizopo zitarithiwa rasmi na Tanganyika, basi federal government itabidi iunde taasisi zake yenyewe. There’s no sharing, kwasababu Katiba na sheria zinazozisimamia lazima ziwe tofauti.
Tatizo lipo wapi? Kutunga sheria au kurithi na kufanyia marekebisho tena sehemu kubwa ni kuondoa jina Zanzibar kuna taabu gani. Taasisi zote zinazoitwa za muungano ni za Tanganyika, zinakuwa za Tanzania pale tu Zanzibar inapohitaji manufaa si kugharamia wala kuwajibika.

Swali muhimu kwako, nitajie taasisi ambayo haina mbadala Zanzibar! moja tu!

Taasisi za muungano ni kwa ajili ya ajira kwa Wazanzibar na Wazanzibar hawawajibiki wala hawajui gharama.

Bajeti yao ya 20/23 ni 2.5T hakuna mahali wameonyesha ghamara zozote za muungano! hata senti moja
Bajeti yao ni maji, elimu, afya ! gharama zingine zote zinalipwa kwa kodi za Watanganyika.

Soma bajeti yao! utaelewa kwanini Tanganyika inabeba mzigo kwa serikali 2.
Draft ya Katiba ya Warioba haikupi picha kamili ya gharama ya uendeshaji wa federal governing system. Hata kama ingepitishwa leo, Tanganyika bado itakuwa na kibarua cha kupata at least Katiba yake yenyewe, assuming itaamua kurithi sheria zilizopo. Hata hivyo, bado italazimika kuzifanyia tweaking za hapa na pale hizo sheria ili kuondoa migongano na masharti yaliyomo kwenye Katiba ya Tanganyika. Kingene ni kwamba federal government itabidi itunge sheria zake yenyewe. Kumbuka, hili jukumu ni ya Bunge la federal, sio la Bunge Maalumu la Katiba!
Mwaka 1964 kulikuwa na katiba ya mpito ambayo ile ya Tanganyika ilifanywa ya JMT.
Kufanya tweaking haina tatizo ni kuondoa jina Zanzibar au Tanzania! period. Hakuna kitu kingine chochote

Federal government itatunga sheria si za kila jambo bali mambo ya federal.

Kwanini unadhani federal inatakiwa isimamie Tamisemi? Kwasasa Zanzibar hawajui Tamisemi, ukisikia wanazungumzia ujue kuna mafao tu, hawajui gharama zozote zile.
Kufikiri kwamba hakuna tofauti ya gharama kati ya gharama za muundo wa sasa na za muundo wa federation ni sawa na ujanja wa mbuni kuficha kichwa kwenye mchanga!
Tuonyeshe kwa namba gharama zitaongezeka wapi? Hajaweza unahisi tu. Gharama gani zinaongezeka na wapi?

Kwa Serikali 2, unaridhika kwamba Tanganyika ilipe kodi za kuendesha mambo yake na ya muungano hiyo ni sahihi? kwa hesabu gani.

Imefika mahali bill za umeme za Wazanzibar zinalipwa na Watanganyika, huo ndio unafuu!
Madeni ya Zanzibar yanalipwa na JMT ambayo ni Tanganyika
Tunawapa 4.5% ya pato kwajili ya kuendesha nchi yao. Piga hesababu 4.5% ya pato la Tanganyika kila mwezi
Wanapata 21% ya ajira za muungano, hawajui gharama ya hata mtumishi mmoja , ni zigo la Tanganyika

Unawaambia Watanganyika kuna unafuu!! please .
Unafuu upi kwa mchango gani ukilinganisha na Lindi, Singida, Simiyu , Tarime , Handeni au Njombe?

Tuonyeshe kwa kwa namba wa serikali 2 , wapi Zanzibar inachangia kiasi kwamba serikali 3 zitaongeza gharama.

Ikiwa Tanganyika inabeba mzigo wote wa gharama, kugawana majukumu ya federal kuongezaje gharama?

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Kwanza ahsante, kuna kitu ulichoshindwa kuthibitisha, ongezeko la gharama! hujaweza kuthnitsha bali una hisia

Nimekuwekea wazi kwamba Tanganyika inabeba 100% ya gharama za kinachoitwa Tanzania

Kuna gharama gani itakayoongezeka? Kugawana gharama kunapunguza au kuongeza?

Zanzibar inasimama na taasisi zake, na Tanganyika ina zake kwa jina la Tanzania. Unapokuwa na federal government Tanganyika inaathirika vipi ikiwa sasa hivi imebeba zigo la Zanzibar yenyewe.

Nadhani umeuelewa mfumo wa federal tofauti. Marekani ina federal na states, lakini katika federal ni ndogo kuna mambo ukiachilia zile za ulinzi.

Tunapozungumzia federal kwa Tanzania tuna maana ya mambo 7 ambayo ni Ulinzi na usalama, Mambo ya ndani, mambo ya nje, Fedha, Katiba na vyama vya siasa. sehemu kubwa ni Ulinzi na usalama, mambo ya ndani na nje.

Iwepo mechanism ya kupata kodi za ku run federal government kutoka kwa washirika tofauti na sasa ambako ''federal' inalipiwa na Tanganyika peke yake. Weka % katika kodi za washirika kutoka pande zote

Unajaribu kukuza tu kwamba kutakuwa na mahakama kubwa ya federal, si kweli, kwasababu hata sasa mahakama kuu haifanyi kila kazi za mahakama zingine kama ilivyo US kwa circuit courts.

Kutakuwa na Bunge kubwa , nimekuonyesha kwamba wapo 393 hadi sasa , Zanzibar inapeleka wasikilizaji 80+ wengi kuliko Bunge la rasimu ya Warioba ambapo Zanzibar italeta 30 tu.
Tanganyika itapunguza mzigo wa kuwa na wasikilizaji tu kwa ajili ya ajira

Wewe unadhani kuhudumia Wabunge 80+ wa Zanzibar pale Dodoma ni nafuu kuliko Wabunge 45 wa Tanganyika katika ' federal parliament', hesabu hizi ni kutoka wapi.?



Tatizo lipo wapi? Kutunga sheria au kurithi na kufanyia marekebisho tena sehemu kubwa ni kuondoa jina Zanzibar kuna taabu gani. Taasisi zote zinazoitwa za muungano ni za Tanganyika, zinakuwa za Tanzania pale tu Zanzibar inapohitaji manufaa si kugharamia wala kuwajibika.

Swali muhimu kwako, nitajie taasisi ambayo haina mbadala Zanzibar! moja tu!

Taasisi za muungano ni kwa ajili ya ajira kwa Wazanzibar na Wazanzibar hawawajibiki wala hawajui gharama.

Bajeti yao ya 20/23 ni 2.5T hakuna mahali wameonyesha ghamara zozote za muungano! hata senti moja
Bajeti yao ni maji, elimu, afya ! gharama zingine zote zinalipwa kwa kodi za Watanganyika.

Soma bajeti yao! utaelewa kwanini Tanganyika inabeba mzigo kwa serikali 2.

Mwaka 1964 kulikuwa na katiba ya mpito ambayo ile ya Tanganyika ilifanywa ya JMT.
Kufanya tweaking haina tatizo ni kuondoa jina Zanzibar au Tanzania! period. Hakuna kitu kingine chochote

Federal government itatunga sheria si za kila jambo bali mambo ya federal.

Kwanini unadhani federal inatakiwa isimamie Tamisemi? Kwasasa Zanzibar hawajui Tamisemi, ukisikia wanazungumzia ujue kuna mafao tu, hawajui gharama zozote zile.

Tuonyeshe kwa namba gharama zitaongezeka wapi? Hajaweza unahisi tu. Gharama gani zinaongezeka na wapi?

Kwa Serikali 2, unaridhika kwamba Tanganyika ilipe kodi za kuendesha mambo yake na ya muungano hiyo ni sahihi? kwa hesabu gani.

Imefika mahali bill za umeme za Wazanzibar zinalipwa na Watanganyika, huo ndio unafuu!
Madeni ya Zanzibar yanalipwa na JMT ambayo ni Tanganyika
Tunawapa 4.5% ya pato kwajili ya kuendesha nchi yao. Piga hesababu 4.5% ya pato la Tanganyika kila mwezi
Wanapata 21% ya ajira za muungano, hawajui gharama ya hata mtumishi mmoja , ni zigo la Tanganyika

Unawaambia Watanganyika kuna unafuu!! please .
Unafuu upi kwa mchango gani ukilinganisha na Lindi, Singida, Simiyu , Tarime , Handeni au Njombe?

Tuonyeshe kwa kwa namba wa serikali 2 , wapi Zanzibar inachangia kiasi kwamba serikali 3 zitaongeza gharama.

Ikiwa Tanganyika inabeba mzigo wote wa gharama, kugawana majukumu ya federal kuongezaje gharama?

JokaKuu Pascal Mayalla

Usidhani mimi ninapinga Serikali tatu. No, sipingi. Ninachopinga ni argument yako kwamba hakuna gharama itakayoongezeka. That isn’t true. Sijui kwanini umekazana kutaka nikuoneshe ongezeko in numbers. Numbers za kufikirika? Nimekuambia hypothetical setup iliyomo kwenye Draft ya Katiba ya Tume ya Warioba haikupi more realistic picture ya financial burden ya uendeshaji wa Muungano wa Serikali tatu. Ni mzaha mkubwa kusema Tanganyika itakuwa na wabunge 45 kwenye Bunge la federal. Hayo yote yamesababishwa na envisaged federal government isiyokuwa na taxing authority. Niambie, ni federal government ya nchi gani inayoendeshwa kwa michango? Federal government inasimamia ulinzi na usalama wa nchi halafu itegemee michango ya states kweli? Hiyo ni Serikali au NGO? That’s a foolish man’s wisdom! The country can’t safeguard its sovereignty in that manner.

Tukiamua kuwa na federal governing system, government institutions zilizopo haziwezi kuwa shared any more. That said,

[emoji3578]Mahakama za federal ziko wapi? Haiwezekani mtu wa Kagera akivunja federal law aje kujibu mashitaka Dar es Salaam.
[emoji3578]Federal law enforcement agencies ziko wapi? Haiwezekani federal law enforcement responsibilities zibebwe na state law enforcement agencies.
[emoji3578]Federal bureau of prisons iko wapi? Haiwezekani federal prisoners wawe jukumu la state bureaus of prisons.

Sisi hatutakuwa watu wa kwanza kuwa na federation. Time-tested federations zipo za kumwaga duniani. Nipe mfano wa federation yoyote inayoendeshwa kwa style ambayo Draft ya Katiba ya Warioba inapendekeza. Hakuna sababu ya kuamini kwamba sisi ni smarter kuliko nchi ambazo zimekuwa na federation for decades, if not centuries.

Federal government ndiyo baba na mama lao. Hata states zikiteteleka zinakuwa bailed out na federal government. With the proposed federal government setup, states zikiwa insolvent, federal government nayo haitasalimika. Again, that setup is a foolish man’s wisdom!
 
Back
Top Bottom