Rais Samia, jaribio lolote la kuipa Zanzibar mamlaka kamili ndilo litakuwa anguko lako

Mbona DRC wanauwana au Rwanda Wana ukabila ila Tanzania tuna survive bila shida au toka lini Zanzibar ndio iwe threat kuliko Kenya au Msumbiji?? Ingekua hivi nchi nyingi zisingepewa uhuru kisa tu hofu zisizokua na basis.

You’re not serious! Political instabilities kwenye hizo nchi hazijatuathiri? Think again!
 
Usalama wa kitu gani labda? Ni kipi so special hapa bara ambacho Zanzibar ndio inapaswa kuwa kinga yetu? Au ni muungano wa kitambiko kiasi kwamba ukivunjika mizimu itafanya yake?
akikujibu unijulishe. muungano wenyewe huu haueleweki umekaa kichawikichawi tu....
 
Hamna cha maana ambacho Zanzibar inaipatia Tanganyika

Mbona hatujaungana na Comoro upande wa kusini mashariki

All in all kila upande uwe na mamlaka yake, yaani kuwe na Zanzibar huru na Tanganyika huru
Umoja ni nguvu, Jicho lako halioni mbali, hasa katika securty wise #shutup
 
Acheni hoja chonganishi kwa Mhe. Rais. Ni watu wenye akili ndogo tu wanaofikiria Dola ya Tanzania inaweza kuundwa upya. Wewe mleta mada hujui kuvunja Muungano ni uhaini? Halafu unamhusishaje Mkuu wa nchi, Rais na Amiri Jeshi Mkuu? Suala la Dola ya Tanzania siyo la kisiasa. Wala nchi hii haiwezi kuundwa upya. Ilishaundwa na waasisi wetu.#Tulete hoja za kujenga nchi na tumuache Mhe. Rais afanye kazi.🙏🙏🙏
 
Hakuna sehemu nimetaja TISS hapo mkuu, nilichosisitiza ni kwamba SHH hawezi kuuvunja muungano kivyakevyake kwa kutegemea hako ka kiti ka urais, HAWEZI.

Kuna jamaa mmoja angekuwa hai angekusimulia (mnaemuita jiwe)
 

Mbona katiba mlioachiwa na Nyerere mmeshaichoka mnataka mpya? Kwa nini Muungano usiguswe?
 

Imekaliwaje kijeshi?
 
Mupango muzima ni Zanzibar kurejea status yake ya zamani- Jamhuri ya watu wa Zanzibar na mwanchama wa EAC. Zanzibar rightfully and dutifully belongs to EAC. Muungano historical accident.
 
Huyu mama Samia hata kama hamumpendi acheni kurushi yeye hana uwezo wala mamlaka ya kulipa Zanzibar mamlaka kamili

Katiba ndio yenye maamuzi na huo uwezo
Lakini binafsi kwa sasa sioni shida Zanzibar na Tanganyika kuwa na mamlaka kamili kwa sababu kuu mbili moja Zanzibar kwa sasa ina wasomi wengi waweza ongeza nchi bila shida tofauti na enzi za mzee Karume ambaye aliongoza nchi akiwa na elimu ya darasa la pili na waliomxunguka.wengi walikuwa hawana elimu hata wajukuu zake akina Fatuma Karume naona wana tu digrii na wanaongea kingereza kuliko babu yao mzee karume

Kwa Tanganyika nako wasomi wengi sasa na wafanyabiashara watanganyika ni wengi hivyo hata wapemba wakirudi.kwao nchi yenye mamlaka huru ya Zanzibar nafasi zao Tanganyika zitashikwa na wahindi,waarabu ,wachaga ,wakinga nk watakuwa tu kama wawekezaji kama watokao Ulaya nk
 
No problem, mama hajui ubinafsi.
 
Huo ni wasi wasi usio na mashiko, na nitatoa mifano; Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Kongo, Zambia, Malawi na Msumbiji ni nchi huru tumepakana nao kwa ardhi ni mpaka upi wa hatari kuliko mwingine kwangu mimi naona ardhi ni hatari zaidi. Pili kama haya ndio matakwa yao wewe Mtanganyika unazuiaje au uhatarishi unatoka wapi (enzi zile za Cold war umepita kama wao wanataka kuurudisha Usultani sisi unatuhusu nini?) mfano mwingine COMORO ni taifa huru just nearby. Ni bora wakawa na serikali yao kamili na sisi tukawa na yetu na kama kuna haja ya ushirikiano maalum basi uwekwe kwa maslahi ya wote, tunaweza kushirikiana through EAC kwa mfano. Sio kuwaburuza. Kwa Technolojia ya sasa, makombora ya masafa marefu/mafupi ni nani alie salama ukaribu au umbali sio kigezo tena cha usalama. Kigezo kikubwa cha usalama ni kuishi na wengine kwa kuheshimiana bila kuumizana (win win situation).
 
Huyu ni rais ana wajomba zake oman. Kwa kauli yake alipotaka kuingia siasa lengo lake alikua aingie upinzani. Kwa kule zanzibar upinzani inaeleweka wakati huo ilikua cuf. Sio siri cuf na maalim seif lengo lao lilikua ni kuipatia zanzibar uhuru kamili wenye kiti baraza la umoja wa mataifa.
Bila shaka samia alishauriwa aingie ccm aihujumu ndani kwa ndani hatimae kuivunja jamhuri ya muungano wa tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…