Rais Samia kaniangusha na kunisononesha sana ripoti ya CAG 2021-2022

Rais Samia kaniangusha na kunisononesha sana ripoti ya CAG 2021-2022

Tatizo wala si SSH. Bali ni mfumo uliomfikisha hapo. Wengine wanadai Bora JPM lakini Mimi nasema mfumo kwenye Taifa la mamilioni ya watu haubadilishwi na mtu mmoja.
Fanyeni overhaul ya mfumo mzima uliotengenezwa na ccm.
Otherwise mtawalaumu sana wezi na Rais wenu.
Kwa hii mifumo iliyopo hata akija malaika mkuu Gabriel baada ya miezi kadhaa atakuwa mpiga Dili zaidi ya hawa waliopo!
Sasa mwenye maamuzi na mamlaka juu ya Mfumo huo ni nani?
 
Nchi inaendeshwa kwa kufuata katiba. Rais akiamua kutumia madaraka yake unavyotaka si tutarudi kwenye mambo ya awamu ya 5? Vyombo vya dola ndo vinatakiwa viwakamate wahusika na kuwapeleka mahakamani. Tukisema Mama aanze kutumia ubabe hakutakalika. Tumshukuru sana kwa kuamua kufuata utawala wa kisheria.
Good point
 
Tatizo wala si SSH. Bali ni mfumo uliomfikisha hapo. Wengine wanadai Bora JPM lakini Mimi nasema mfumo kwenye Taifa la mamilioni ya watu haubadilishwi na mtu mmoja.
Fanyeni overhaul ya mfumo mzima uliotengenezwa na ccm.
Otherwise mtawalaumu sana wezi na Rais wenu.
Kwa hii mifumo iliyopo hata akija malaika mkuu Gabriel baada ya miezi kadhaa atakuwa mpiga Dili zaidi ya hawa waliopo!
JPM wa ile 1.5t au
 
Kwahio katiba inamtaka raisi asiwachukulie hatua wabadhirifu wa mali za umma au sio? 🤣
Kwamba kila mtu aibe awezavyo tusishikane mikono tu.
Ahahahaha
Kwenye kikao si kulikuwa na wakuu wa vyombo pendwa.
Kila mmoja akafanye kazi yake, hapo wa kufungwa atafungwa, wa kufukuzwa kazi atafukuzwa
 
KUONDOA Mfumo wa kishenzi ni kufukuza wachache kama mfano. Mbona nchi ilitulia na hospitali watu walipokelewa kama hotelini.
Ila kitendo cha yule bwana kufa tu sahizi pharmacy zote za hospitalini hazina dawa hadi ukanunue nje.
You determine how serious people are based on how they solve pressing challenges. Mkuu uendeshaji wa serikali ni mifumo. In short serikali ni protocols na systems na siyo mtu mmoja mmoja. Uozo wa mifumo ndo chanzo Cha mpenda sifa JPM kuwa aliko leo. Mifumo imeoza. Inanuka like huwezi kupambana nayo peke yako! Utaondolewa tu!

Wananchi tuamke Sasa. Wasitubemende na propaganda za ushoga ushoga tunashadidia kumbe waandamizi wapo bize kupishana kukwapua mabilioni ya fedha!
 
You determine how serious people are based on how they solve pressing challenges.
Mkuu uendeshaji wa serikali ni mifumo. In short serikali ni protocols na systems na siyo mtu mmoja mmoja. Uozo wa mifumo ndo chanzo Cha JPM kuwa aliko leo. Mifumo imeoza. Inanuka like huwezi kupambana nayo peke yako! Utaondolewa tu!
Sasa who can rectify zaidi ya raisi. Sababu if everyone hates clean money how can the president survive. Huo mfumo nahisi hata raisi ambaye atataka kubadilisha katiba hii iwape nguvu raia hataweza kumaliza mchakato kabla hajaenda futi 6 ardhini.
 
KWANZA HIVI NDIO VYEO VYAKE

1) Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
2) Mkuu wa nchi na kiongozi namba moja kwa pande zote mbili za Muungano.
3) Amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama.

Hivyo ni vyeo ambavyo vinamruhusu mheshimiwa raisi kuchukua hatua kwa mtu yoyote wa serikalini ambae anafanya kazi yake kinyume na sheria za nchi, aidha kwa yule anaeiibia serikali, anaetoa rushwa, anaepokea au kuchelewesha mipango ya serikali hasa inayohusu maendeleo nk.

Inasikitisha sana mtu mwenye vyeo hivyo anashindwa, au anasita kuwachukulia hatua kali za kuagiza wakamatwe na kufunguliwa mashtaka wale wote waliopatikana na tuhuma za ubadhilifu wa fedha za umma serikalini na badala yake raisi eti anawaomba tu waachie nafasi zao bila kufungwa au kurudisha fedha hizo.

Hata wale aliosema kwamba kila report zinapofika watu hao hao hukutwa na tuhuma zile zile ilitakiwa wakamtwe kwa tuhuma ile ile ya kwanza na kubanwa vizuri walipozipeleka fedha zetu, badala ya kutaka eti washushwe vyeo au kuhamishwa ofisi.

Yani mwizi wa ndala akamatwe na kufungwa huku mwanasheria wa serikali akitafuna kodi zetu kwa kuendesha kesi yake, afu yule anaeiibia serikali mabilioni ya shilingi ahamishwe tu kituo ili akaendelee na utafunaji wa fedha zetu huko katika ofisi nyingine. Ni kwanini asifukuzwe kazi ili nafasi yake ichukuliwe na mtu mungine na ukizingatia kuna watu wengi wana elimu zao mitaani lakini kazi hawana?

Lakini pia sio aishie kufukuzwa tu bali afunguliwe kesi ya uhujumu uchumi na mali zake zote zitaifishwe.

China imeweza kupiga hatua duniani baada ya viongozi wa nchi kusimamia vyeo kodi za wananchi wao kwa kutoa adhabu kali kwa yeyote atakaejaribu kugusa fedha za serikali.
Pia hata Rwanda ipo vizuri baada ya raisi wa nchi hiyo kukitumia vyema cheo chake.

Raisi na amiri jeshi mkuu ukibaki kulalamika, unafikiri mawaziri na viongozi wengine wa kawaida wataweza kuwa na uwezo wa kujiamini kuchukua hatua kweli.

Kama kulalamika umeshalalamika kwa zaidi ya miaka miwili sasa lakini upigaji ni ule ule. Sasa kabla ya kuwaambia watu na hili mkalitizame, tunakuomba na wewe kwanza ujitizame kwamba hiyo ndio njia sahihi ya kuendelea ku deal na mafisadi.

Ukicheka na nyani shambani usishangae kuvuna mabua.
Achukue hatua muanze kumuita diktekta uchwara?
 
Mh. Rais ametoa agizo washughilikiwe haraka, Najua wahusika tumbo joto huko....sidhani Kama wizara/waziri husika atakubali apoteze kazi kwa kutotekeleza.
 
Vyombo vya usalama vinashindwa au naweza kusema vinaogopa kuwakamata kwa sababu havina watu madhubuti wa kuwalinda.

Kwahiyo acha raisi mwenyewe achukue maamuzi yanayowashinda wa chini yake. Yeye ndio bosi wa serikali na mwenye maamuzi ya mwisho kwa mtu yoyote mwenye tuhuma za wizi au ufisadi.
Magu alifanya hivyo na unajua matokeo yake
 
Back
Top Bottom