Rais Samia: Katiba mpya hadi watu wasome waelewe maana ya katiba hata hii tuliyonayo

Rais Samia: Katiba mpya hadi watu wasome waelewe maana ya katiba hata hii tuliyonayo

..suala la " kuijua " katiba iliyopo sasa hivi ni subjective.

..kwa mfano, Rais ametumia mbinu, utaratibu, na njia gani, kutambua kiwango cha uelewa wa wananchi kuhusu Katiba?

..Ni wakati gani Raisi atatoa tamko kwamba wananchi wanaijua katiba iliyopo, na wakati gani atatoa tamko kuwa wanaufahamu na katiba inayopendekezwa?

..Naamini wakati muafaka wa kutoa elimu ya Katiba ni kipindi cha KAMPENI ZA KURA YA MAONI kuhusu Katiba pendekezwa.

..Kwa msingi huo wakati wa kuandika Katiba Mpya ni sasa.
Hawa watu wasipoangalia watasababisha vurugu nchi hii
 
Umejitahidi kupotosha mkuu,

Alichosema ni kuwa, watu wapewe shule vizuri ya katiba hii tulionayo, na pia kasema vizuri kabisa, katiba ni ya watanzania, hatuwez sema tuchukue maoni ya wanasiasa tu ndio tuunde katiba, lazima kila mtu atoe maoni, na ili kila mtu atoe maoni ni lazima watu waijue hii katiba iliyopo, na yupo sahihi.
Watu so walishatoa maoini Yao? Kwani Ile rasimu ya Warioba ilipatikanaje kama siyo maoni ya wananchi? Acheni usanii....Rais amesema amesomeshwa dini yake vizuri, sasa kwanini anataka kumkosea Mungu wake hadharani mchana kweupe?
 
Dude linaloitwa katiba Raisi wa jamhuri ya muungano wa tanzania Samia Suluhu hassan amesema kwamba watu wa nchi hii hakuna anaejuwa maana ya katiba kwa hiyo ni vizuri watu kwanza wafundishwe waelewe maana ya katiba kwani hata tuliyonayo hakuna anayeifahamu.

kuhusu katiba mpya jambo hilo litafanyika hadi pale watu watakapo kuwa wanaelewa hata hii tuliyonayo hii maana yake ni kwamba vyama vya upinzani ingawa vimeendelea kusisitiza kuwepo umhimu wa katiba mpya wajue kuwa kwa sasa hilo suala halipo.

Jambo pekee ambalo serikali inaenda kulifanya ni kuwepo kwa somo la katiba mashuleni na vyuoni pamoja na taasisi zote za dini na serikali kuelemishwa maana ya katiba kwani watanzania hawana uelewa na katiba hiyo.

Ndugu zangu vyama vya upinzani mjue kuwa tunaenda kufanya uchaguzi mkuu bila kuwepo kwa tume huru wala katiba mpya! je mko tayari kwenye mashindano? [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
Hawa maraisi kila tunayemchagua anatumiaga techniques hizihizi za kusema wananchi hawaielewi katiba ya sasa[emoji3]jiulize huo utafiti waliufanya lini! hii ni mbinu ya kutumia panadol kwa mgonjwa wa malaria.
 
Elimu ya katiba bado sana nchi hii wanasiasa uchwara na wanaharakati wanadai katiba ili iwawezeshe kuingia ikulu wakati mambo ya muhimu mengi hakuna mwenye habari nayo. Namuunga mkono rais bado elimu inahitajika sana.
Tume huru isiyokuwa na manipulation ya mgombea yeyote (Kutokana na ukweli kwamba, asiwepo mgombea anayeitisha tume kwa namna yoyote Ile. Na hili nalo linahitaji elimu).
By the way, washindani kuwa na nafasi sawa, halihitaji MAONI ya wananchi( Hii ni OBJECTIVE APPROACH).
 
Kumbe na Samia anaiogopa Katiba Mpya akidhani ndio itamuondoa ikulu?!

Sasa hivi visingizio vyenu vya mpaka tufundishwe Katiba ya 1977 leo 2023, vina maana gani?
Hata katiba idondoke kutoka mbinguni kama ccm wakigoma kuachia madaraka hakuna chama cha upinzani kitachukua nchi
 
🤣🤣🤣🤣🤣
2025 inamtesa. Kama yeye tu hana uhakika wa kushinda 2025 bila kuiba uchaguzi je hao watakaomfuata 2030 wataweza? Watakubali abadilishe katiba baada ya 2025 ambapo yeye hatokuwa na cha kupoteza?

Aache hadaa. Na hao mabeberu washaanza kumsoma. Maneno matupu hakuna concrete action. Mwakani kuna uchaguzi serikali za mitaa kampeleka mkwe TAMISEMI kwenda kusimamia. Chaguzi ndogo zinafanyika kupoteza hela tu hakuna demokrasia yoyote. Hiyo 2025 kutakuwa na tofauti gani?
Ni kweli kabisa. 2025 inamtesa sana anajaribu Kuja fix zake. Hivi tuambie ni nchi gani ambayo wananchi wake wanajua katiba tofauti na Wananchi wa Bongo.

Anajidai kalelewa vizuri... Hivi kuelewa vizuri unaweza Kuja na uongo, hadaa na wizi wa aina hii. Please, God forbid.
 
Hapo maana yake, ianzishwe topic ya katiba kwenye masomo shuleni na vyuoni. Na kizazi hiko kinachosoma topic hiyo hadi kikue kifikie umri wa mtu mzima.
Hapo wanalenga kizazi cha mwaka 2055 hadi 2070. Wakati huo kizazi hiki kinacho simamia serkali, kitakua kishakwisha, uamuzi utabaki kwa vijana wa kipindi hiko.

Kazi kwelikweli..!!
Hicho kizazi Cha 2050-2070 sipati picha
 
Dude linaloitwa katiba Raisi wa jamhuri ya muungano wa tanzania Samia Suluhu hassan amesema kwamba watu wa nchi hii hakuna anaejuwa maana ya katiba kwa hiyo ni vizuri watu kwanza wafundishwe waelewe maana ya katiba kwani hata tuliyonayo hakuna anayeifahamu.

kuhusu katiba mpya jambo hilo litafanyika hadi pale watu watakapo kuwa wanaelewa hata hii tuliyonayo hii maana yake ni kwamba vyama vya upinzani ingawa vimeendelea kusisitiza kuwepo umhimu wa katiba mpya wajue kuwa kwa sasa hilo suala halipo.

Jambo pekee ambalo serikali inaenda kulifanya ni kuwepo kwa somo la katiba mashuleni na vyuoni pamoja na taasisi zote za dini na serikali kuelemishwa maana ya katiba kwani watanzania hawana uelewa na katiba hiyo.

Ndugu zangu vyama vya upinzani mjue kuwa tunaenda kufanya uchaguzi mkuu bila kuwepo kwa tume huru wala katiba mpya! je mko tayari kwenye mashindano? [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
Raisi yupo sahihi kabisa kuhusu uelewa wa Watanzania bila ya Kusahau kwamba naye ni Mtanzania. Itoshe, imepita miaka miwili na ushee toka ashike dola na Bado haijaielewa.

Ikumbukwe au izangatiwe pia, kuwa, mwaka wake watatu wa kuisoma na kuilelewa Katiba utakuwa ndio mwaka wake wa kuingia kinyang'anyiro cha Uraisi- Je atafaa kuwa Rais wa JMT kama haonyeshi nia ya kulinda Katiba hiyo ya Jamhuri, asiyoielewa? Haijalishi....wabobezi wa sheria wanadai "ignorantia legis neminem excusat"

Kwamba," kwamba mtu asiyejua sheria hawezi kukwepa dhima kwa kukiuka sheria hiyo kwa kutojua maudhui yake"

SSH hawezi kujifunika katika wingu la kutokuwa na Uelewa wa Maudhui ya Katiba yetu, kwani yeye amekuwa ni miongoni mwa viongozi walioapa Kutii na Kuilinda katiba hiyo, unaapa kufanya hivyo bila ya Uelewa wa unachokiapia? Je, anataka kusema kuwa Watanzania wengine hawana akili ya kung'amua yaliyomo kwenye Katiba yao? Kwamba hawana uelewa wa Katiba yao?
Tunapozingatia SSH ni miongoni mwa Watanzania na tunapozingatia hayo aliyoyasema ni kweli, basi Yeye binafsi hana pakutokea, narudia, haya kwamba mtu asiyejua sheria hawezi kukwepa dhima kwa kukiuka sheria hiyo kwa kutojua maudhui yake


Akemewe kwa Vijembe vyake, akemewe kwa kuwatukana Watanzania

2025 apumzishwe.
 
Hamna mabadliko ya sheria hadi zilizopo wananchi waache kuzivunja, mitaala ibaki ilivyo hadi pasiwepo na watoto wanaofeli, tusipitishe mabadiliko ya kodi mpaka wananchi waelewe zilizopo, na DP world wangoje wale wa Mpitimbi wasowahi kuagiza hata t-shirt wajue kuendesha bandari.
 
Hicho kizazi Cha 2050-2070 sipati picha
Watakuwa kama hawa waliopo sasa au watakuwa even worse kuliko hawa wanaimba honeeeey honeeey 😅🙏
Watu wanaogopa hata kukanyaga matope huko mashambani unategemea watazaa vizazi vya aina gani ??!
 
Dude linaloitwa katiba Raisi wa jamhuri ya muungano wa tanzania Samia Suluhu hassan amesema kwamba watu wa nchi hii hakuna anaejuwa maana ya katiba kwa hiyo ni vizuri watu kwanza wafundishwe waelewe maana ya katiba kwani hata tuliyonayo hakuna anayeifahamu.

kuhusu katiba mpya jambo hilo litafanyika hadi pale watu watakapo kuwa wanaelewa hata hii tuliyonayo hii maana yake ni kwamba vyama vya upinzani ingawa vimeendelea kusisitiza kuwepo umhimu wa katiba mpya wajue kuwa kwa sasa hilo suala halipo.

Jambo pekee ambalo serikali inaenda kulifanya ni kuwepo kwa somo la katiba mashuleni na vyuoni pamoja na taasisi zote za dini na serikali kuelemishwa maana ya katiba kwani watanzania hawana uelewa na katiba hiyo.

Ndugu zangu vyama vya upinzani mjue kuwa tunaenda kufanya uchaguzi mkuu bila kuwepo kwa tume huru wala katiba mpya! je mko tayari kwenye mashindano? [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
Maana yake hata yeye haijui katiba
 
Raisi yupo sahihi kabisa kuhusu uelewa wa Watanzania bila ya Kusahau kwamba naye ni Mtanzania. Itoshe, imepita miaka miwili na ushee toka ashike dola na Bado haijaielewa.

Ikumbukwe au izangatiwe pia, kuwa, mwaka wake watatu wa kuisoma na kuilelewa Katiba utakuwa ndio mwaka wake wa kuingia kinyang'anyiro cha Uraisi- Je atafaa kuwa Rais wa JMT kama haonyeshi nia ya kulinda Katiba hiyo ya Jamhuri, asiyoielewa? Haijalishi....wabobezi wa sheria wanadai "ignorantia legis neminem excusat"

Kwamba," kwamba mtu asiyejua sheria hawezi kukwepa dhima kwa kukiuka sheria hiyo kwa kutojua maudhui yake"

SSH hawezi kujifunika katika wingu la kutokuwa na Uelewa wa Maudhui ya Katiba yetu, kwani yeye amekuwa ni miongoni mwa viongozi walioapa Kutii na Kuilinda katiba hiyo, unaapa kufanya hivyo bila ya Uelewa wa unachokiapia? Je, anataka kusema kuwa Watanzania wengine hawana akili ya kung'amua yaliyomo kwenye Katiba yao? Kwamba hawana uelewa wa Katiba yao?
Tunapozingatia SSH ni miongoni mwa Watanzania na tunapozingatia hayo aliyoyasema ni kweli, basi Yeye binafsi hana pakutokea, narudia, haya kwamba mtu asiyejua sheria hawezi kukwepa dhima kwa kukiuka sheria hiyo kwa kutojua maudhui yake


Akemewe kwa Vijembe vyake, akemewe kwa kuwatukana Watanzania

2025 apumzishwe.
Apumzishwe na nani ??!!😅😅🙏
 
Back
Top Bottom